< 2 Samuel 6 >

1 Forsothe Dauid gaderide eft alle the chosun men of Israel, thritti thousynde.
Basi kwa mara nyingine Daudi akawakusanya wateuli wa Israeli, elfu thelathini.
2 And Dauid roos, and yede, and al the puple that was with hym of the men of Juda, to brynge the arke of God, on which the name of the Lord of oostis, sittynge in cherubyn on that arke, was clepid.
Daudi akainuka na akaenda na watu wake wote waliokuwa pamoja naye kutoka Baala ulioko Yuda ili alilete sanduku la Mungu, liitwalo kwa jina la Yahwe wa majeshi, akaaye juu ya makerubi.
3 And thei puttiden the arke of God on a newe wayn, and thei token it fro the hows of Amynadab, that was in Gabaa. Forsothe Oza and Haio, the sons of Amynadab, dryueden the newe wayn.
Wakaliweka sanduku la Mungu juu ya mkokoteni mpya. Wakalitoa katika nyumba ya Abinadabu, iliyokuwa juu ya kilima. Uza na Ahio, wanawe, wakauongoza mkokoteni.
4 And whanne thei hadden take it fro the hows of Amynadab, that was in Gabaa, and kepte the arke of God, Haio yede bifor the arke.
Wakautoa mkokoteni na sanduku la Mungu juu yake nyumbani mwa Abinadabu juu ya kilima. Ahio alikuwa ametangulia mbele ya sanduku.
5 Forsothe Dauid and al Israel pleieden byfor the Lord, in alle `trees maad craftili, and harpis, and sitols, and tympans, and trumpis, and cymbalis.
Kisha Daudi na nyumba yote ya Israeli wakaanza kucheza mbele ya Yahwe, wakishangilia kwa vyombo vya mziki, vinubi, vinanda, matari, kayamba na matowazi.
6 Forsothe after that thei camen to the corn floor of Nachor, Oza helde forth the hond to the arke of God, and helde it, for the oxun kikiden, and bowiden it.
Hata walipofika katika shinikizo la Nasoni, wale ng'ombe wakakwama, Uza akanyosha mkono wake na kulikumbatia sanduku la Mungu, naye akalishikilia.
7 And the Lord was wrooth bi indignacioun ayens Oza, and smoot hym on `the foli; and he was deed there bisidis the arke of God.
Kisha asira ya Yahweh ikawaka dhidi ya Uza. Mungu akampiga kwa ajili ya dhambi yake. Uza akafa pale pale kando ya sandaku la Mungu.
8 Forsothe Dauid was sori, for the Lord hadde smyte Oza; and the name of that place was clepid the Smytyng of Oza `til in to this dai.
Daudi akakasirika kwa kuwa Yahwe alimpiga Uza, naye akapaita mahali pale Peresi Uza. Eneo hilo linaitwa Peres Uza hata leo.
9 And Dauid dredde the Lord in that dai, and seide, Hou schal the arke of the Lord entre to me?
Daudi akamwogopa Yahweh siku hiyo. Akasema, “Sanduku la Yahwe lawezaje kuja kwangu?”
10 And he nolde turne the arke of the Lord to hym silf in to the citee of Dauid, but he turnede it in to the hows of Obethedom of Geth.
Hivyo Daudi hakuwatayari tena kulichukua sanduku la Yahwe katika mji wa Daudi. Badala yake, akaliweka kando katika nyumba ya Obedi Edomu Mgiti.
11 And the arke of the Lord dwellide in the hows of Obethedom of Geth thre monethis; and the Lord blessid Obethedom, and al his hows.
Sanduku la Yahwe likakaa katika nyumba ya Obedi Edomu Mgiti kwa miezi mitatu. Kwa hiyo Yahwe akambariki yeye na nyumba yake yote.
12 And it was teld to kyng Dauid, that the Lord hadde blessid Obethedom, and alle `thingis of hym, for the arke of God. And Dauid seide, Y schal go, and brynge the arke with blessyng in to myn hows. Therfor Dauid yede, and brouyte the arke of God fro the hows of Obethedom in to the citee of Dauid with ioye; and ther weren with Dauid seuen cumpanyes, and the slain sacrifice of a calff.
Kisha mfalme Daudi akaambiwa, “Yahwe ameibariki nyumba ya Obedi Edomu na kila kitu alichonacho kwa sababu ya sanduku la Mungu.” Hivyo Daudi akaenda na kulipandisha sanduku la Mungu kutoka katika nyumba ya Obedi Edomu hadi mji wa Daudi kwa furaha.
13 And whanne thei, that baren the arke of the Lord, hadden stied six paaces, thei offriden an oxe and a ram. And Dauid smoot in organs boundun to the arm;
Ikawa waliolibeba sanduku la Yahwe walipochukua hatua sita, akatoa sadaka ng'ombe na ndama aliyenona.
14 and daunside with alle strengthis bifor the Lord; sotheli Dauid was clothid with a lynnun surplis.
Daudi akacheza mbele ya Yahwe kwa nguvu zake zote; alikuwa amevaa naivera ya kitani pekee.
15 And Dauid, and al the hows of Israel, ledden forth the arke of testament of the Lord in hertli song, and in sown of trumpe.
Hivyo Daudi na nyumba yote ya Israeli wakalipandisha sanduku la Yahwe kwa vifijo na sauti za tarumbeta.
16 And whanne the arke of the Lord hadde entride in to the citee of Dauid, Mychol, the douytir of Saul, bihelde bi a wyndow, and sche siy the kyng skippynge and daunsynge bifor the Lord; and sche dispiside hym in hir herte.
Hata ikawa sanduku la Yahwe lilipofika mjini mwa Daudi, Mikali, binti Sauli, alichungulia dirishani. Akamwona mfalme Daudi akiruka na kucheza mbele ya Yahwe. Akamdharau moyoni mwake.
17 And thei brouyten in the arke of the Lord, and settiden it in his place, in the myddis of tabernacle, which tabernacle Dauid hadde maad `redy therto; and Dauid offride brent sacrifices and pesible bifor the Lord.
Wakaliingiza sanduku la Yahwe na kuliweka mahali pake, katikati ya hema ambayo Daudi alikuwa ameliwekea. Kisha Daudi akatoa sadaka ya kuteketezwa na matoleo ya amani mbele za Yahwe.
18 And whanne Dauid hadde endid tho, and hadde offrid brent sacrifices and pesible, he blesside the puple in the name of the Lord of oostis.
Ikawa Daudi alipomaliza kutoa sadaka za kuteketezwa na sadaka za amani, akawabariki watu kwa jina la Yahwe wa majeshi.
19 And he yaf to al the multitude of Israel, as wel to man as to womman, to ech `o thinne loof, and o part rostid of bugle fleisch, and flour of wheete fried with oile; and al the puple yede, ech man in to his hows.
Kisha akawagawia watu wote, umati wote wa Israeli, wanaume kwa wanawake, kipande cha mkate, nyama na keki ya zabibu. Kisha watu wote wakaondoka; kila mmoja akarudi kwake.
20 And Dauid turnede ayen to blesse his hows, and Mychol, the douytir of Saul, yede out in to the comyng of Dauid, and seide, Hou glorious was the kyng of Israel to day vnhilynge hym silf bifor the handmaidis of hise seruauntis, and he was maad nakid, as if oon of the harlotis be maad nakid?
Kisha Daudi akarudi ili aibariki familia yake. Mikali, binti Sauli, akatoka ili akutane na Daudi naye akasema, “Jinsi gani mtukufu mfalme wa Israeli alivyokuwa leo, aliyejiacha uchi mbele ya macho ya vijakazi miongoni mwa watumishi wake, kama mmoja wa wapumbavu ambaye bila aibu hujifunua yeye mwenyewe!”
21 And Dauid seide to Mychol, The Lord lyueth, for Y schal pley bifor the Lord, that chees me rathere than thi fadir, and than al the hows of hym, and comaundide to me, that Y schulde be duyk on the puple `of the Lord of Israel;
Daudi akamjibu Mikali, “Nilifanya hivyo mbele ya Yahwe, aliyenichagua juu ya baba yako na juu ya familia yake yote, aliyeniweka kuwa kiongozi juu ya watu wa Yahwe, juu ya Israeli. Mbele ya Yahwe nitafurahi!
22 and Y schal pleie, and Y schal be maad `vilere more than Y am maad, and Y schal be meke in myn iyen, and Y schal appere gloriousere with the handmaydys, of whiche thou spakist.
Nitakuwa nisiye na heshima hata zaidi ya hapa, na nitajishusha mbele za macho yangu mwenyewe. Lakini kwa hawa vijakazi uliowasema, nitaheshimiwa.”
23 Therfor a sone was not borun to Mychol, the douytir of Saul, til in to the dai of hir deeth.
Hivyo Mikali, binti Sauli, hakuwa na watato hata alipokufa.

< 2 Samuel 6 >