< 2 Samuel 20 >

1 Also it bifelde, that a man of Belial was there, Siba bi name, the sone of Bothri, a man of the generacioun of Gemyny; and he sownede with a clarioun, and seide, No part is to vs in Dauid, nether eritage in the sone of Ysai; thou, Israel, turne ayen in to thi tabernaclis.
Basi, kulikuwa na mtu mbaya sana aliyeitwa Sheba mwana wa Bikri, Mbenyamini, aliyekuwako huko. Akapiga tarumbeta na kupaza sauti, “Hatuna fungu katika Daudi, wala hatuna sehemu katika mwana wa Yese! Kila mtu aende hemani mwake, enyi Israeli!”
2 And al Israel was departid fro Dauid, and suede Siba, the sone of Bothri; forsothe the men of Juda cleuyden to her kyng, fro Jordan `til to Jerusalem.
Kwa hiyo watu wote wa Israeli wakamwacha Daudi na kumfuata Sheba mwana Bikri. Lakini watu wa Yuda wakawa karibu na mfalme wao katika safari yote kutoka Yordani mpaka Yerusalemu.
3 And whanne the kyng hadde come in to his hows in Jerusalem, he took ten wymmen, hise secundarie wyues, whiche he hadde left to kepe the hous, and he bitook hem in to keping, and yaf mete to hem; and he entride not to hem; but thei weren closid `til to the dai of her deeth, and lyueden in widewehed.
Daudi aliporudi katika jumba lake la kifalme huko Yerusalemu, aliwachukua wale masuria kumi aliokuwa amewaacha ili kuangalia jumba la kifalme na kuwaweka ndani ya nyumba chini ya ulinzi. Akawapa mahitaji yao lakini hakukutana nao kimwili. Waliwekwa kifungoni wakaishi kama wajane mpaka kifo chao.
4 Forsothe Dauid seide to Amasa, Clepe thou to gidere to me alle the men of Juda in to the thridde dai, and be thou present.
Ndipo mfalme akamwambia Amasa, “Waite watu wa Yuda waje kwangu katika muda wa siku tatu, nawe mwenyewe uwepo hapa.”
5 Therfor Amasa yede, that he clepe to gidere the puple of Juda; and he dwellide ouer the couenaunt, which the kyng hadde set to hym.
Lakini Amasa alipokwenda kuwaita Yuda, alichukua muda mrefu zaidi ya ule mfalme aliokuwa amemwekea.
6 Sotheli Dauid seide to Abisai, Now Siba, the sone of Botri, schal turmente vs more than Absolon dide; therfor take the seruauntis of thi lord, and pursue hym, lest in hap he fynde strengthid citees, and ascape vs.
Daudi akamwambia Abishai, “Sasa Sheba mwana wa Bikri atatuletea madhara zaidi kuliko alivyofanya Absalomu. Wachukue watu wa bwana wako na umfuatie, la sivyo atapata mji wenye ngome na kututoroka.”
7 Therfor the men of Joab yeden out with Abisai, and Cerethi and Ferethi, and alle stronge men yeden out of Jerusalem to pursue Siba, the sone of Bochry.
Hivyo watu wa Yoabu, na Wakerethi na Wapelethi, pamoja na wapiganaji mashujaa wote wakaondoka chini ya uongozi wa Abishai. Wakatoka Yerusalemu ili kumfuata Sheba mwana wa Bikri.
8 And whanne thei weren bisidis the greet stoon, which is in Gabaon, Amasa cam, and ran to hem; forsothe Joab was clothid with a streit coote at the mesure of his abit, and was gird aboue with a swerd, `ether dagger, hangynge doun `til to the entrayls in a schethe, `which swerd maad `craftily myyte go out bi liyt touchyng, and smyte. Therfor Joab seide to Amasa,
Wakati walikuwa kwenye mwamba mkubwa huko Gibeoni, Amasa alikuja kuwalaki. Yoabu alikuwa amevaa mavazi yake ya kijeshi; juu yake alifunga mkanda kwenye kiuno wenye upanga ndani ya ala. Alipokuwa akienda mbele, ule upanga ukaanguka kutoka kwenye ala.
9 Heil, my brother! And he helde with the riyt hond the chyn of Amasa, as kissinge him.
Yoabu akamwambia Amasa, “U hali gani, ndugu yangu?” Kisha Yoabu akamshika Amasa ndevu kwa mkono wake wa kuume ili ambusu.
10 Forsothe Amasa took not kepe of the swerd, `which swerd Joab hadde, and Joab smoot Amasa in the side, and schedde out his entrailis in to the erthe, and Amasa was deed; and Joab addide not `the secounde wounde. Forsothe Joab and Abisai, his brother, pursueden Siba, the sone of Bochri.
Amasa hakuona upanga uliokuwa mkononi mwa Yoabu, naye Yoabu akamchoma nao tumboni, nayo matumbo yake yakamwagika chini. Pasipo kuchomwa mara ya pili, Amasa akafa. Basi Yoabu na Abishai nduguye wakamfuatia Sheba mwana wa Bikri.
11 In the meene tyme whanne `sum men of the children of Dauid, of the felowis of Joab, hadden stonde bisidis the deed bodi of Amasa, thei seiden, Lo! he that wolde be the felowe of Dauid for Joab.
Mmoja wa watu wa Yoabu akasimama kando ya Amasa, akasema, “Yeyote ampendaye Yoabu na yeyote aliye upande wa Daudi, na amfuate Yoabu!”
12 Forsothe Amasa was bispreynt with blood, and lay in the myddil of the weie. Sum man siy this, that al the puple abood to se Amasa, and he remouyde Amasa fro the weie in to the feeld, and he hilide Amasa with a cloth, lest men passynge schulden abide for hym.
Amasa alikuwa akigaagaa katika damu yake katikati ya barabara; mtu mmoja akaona kwamba vikosi vyote vilikuwa vinasimama pale. Huyo mtu alipotambua kwamba kila aliyefika pale Amasa alipokuwa alisimama, alimburuta Amasa kutoka barabarani mpaka kwenye shamba na kutupia nguo juu yake.
13 Therfor whanne he was remouyd fro the weie, ech man passide suynge Joab to pursue Siba, the sone of Bochri.
Baada ya Amasa kuondolewa kutoka barabarani, watu wote walienda pamoja na Yoabu kumfuatia Sheba mwana wa Bikri.
14 Forsothe Siba hadde passide bi alle the lynagis of Israel til in to Habela, and in to Bethmacha; and alle chosun men weren gaderid to hym.
Sheba akapita katika makabila yote ya Israeli hadi Abel-Beth-Maaka na kupitia eneo lote la Waberi ambao walijikusanya pamoja na kumfuata.
15 Therfor thei camen, and fouyten ayens hym in Habela, and in Bethmacha, and cumpassiden the citee with strengthingis; and the citee was bisegid. Sotheli al the cumpany, that was with Joab, enforside to distrie the wallis.
Vikosi vyote vya Yoabu vikaja na kumhusuru Sheba mwana wa Bikri huko Abel-Beth-Maaka. Wakauzingira mji kwa kuweka vikosi vya askari, ili kukabiliana na ngome ya mji. Walipokuwa wanagongagonga ukuta ili kuubomoa na kuuangusha chini,
16 And a wijs womman of the citee criede an hiy, Here ye! here ye! seie ye to Joab, Neiye thou hidur, and Y schal speke with thee.
mwanamke mmoja mwenye busara akaita kutoka ndani ya mji, akisema, “Sikilizeni! Sikilizeni! Mwambieni Yoabu aje hapa ili niweze kuzungumza naye.”
17 And whanne he hadde neiyed to hir, sche seide to hym, Art thou Joab? And he answeride, Y am. To whom sche spak thus, Here thou the wordis of thin handmayde. Which Joab answeride, Y here.
Yoabu alikwenda mbele yake, akamuuliza, “Wewe ni Yoabu?” Akamjibu, “Ndiye mimi.” Yule mwanamke akamwambia, “Sikiliza kile mtumishi wako atakachokuambia.” Akamwambia, “Ninasikiliza.”
18 And eft sche seide, A word was seid in eld prouerbe, Thei that axen, axe in Habela; and so thei profitiden.
Huyo mwanamke akaendelea kusema, “Zamani za kale walikuwa wakisema, ‘Wakaulize ushauri huko Abeli,’ hivyo kulimaliza lile shauri.
19 Whethir Y am not, that answere treuthe to Israel? and sekist thou to distrie a citee, and to distrie a modir citee in Israel? whi castidist thou doun the eritage of the Lord?
Sisi ni watu wa amani na waaminifu katika Israeli. Wewe unajaribu kuharibu mji ambao ni mama katika Israeli. Kwa nini unataka kumeza urithi wa Bwana?”
20 And Joab answeride, and seide, Fer be, fer be this fro me; Y `caste not doun, nether Y distrye.
Yoabu akajibu, “Hilo liwe mbali nami. Hilo liwe mbali nami kumeza au kuharibu.
21 The thing hath not so it silf; but a man of the hil of Effraym, Siba, sone of Bochri, bi surname, reiside his hond ayens kyng Dauid; bitake ye him aloone, and we schulen go awei fro the citee. And the womman seide to Joab, Lo! his heed schal be sent to thee bi the wal.
Hivyo sivyo ilivyo. Mtu mmoja jina lake Sheba mwana wa Bikri, kutoka nchi ya vilima vya Efraimu, ameinua mkono wake dhidi ya mfalme, dhidi ya Daudi. Nikabidhini mtu huyu mmoja, nami nitajiondoa katika mji huu.” Huyu mwanamke akamwambia Yoabu, “Kichwa chake mtatupiwa kupitia juu ya ukuta.”
22 Therfor the womman entride to al the puple, and sche spak to hem wiseli; whiche `castiden forth to Joab the heed of Siba, sone of Bochri, gird of. And Joab sownede with a trumpe, and thei departiden fro the citee, ech man in to hise tabernaclis; forsothe Joab turnede ayen to Jerusalem to the kyng.
Ndipo huyo mwanamke akaenda kwa watu wote akiwa na ushauri wake wa busara, nao wakakata kichwa cha Sheba mwana wa Bikri na kumtupia Yoabu. Kwa hiyo Yoabu akapiga tarumbeta, na watu wake wakatawanyika kutoka mjini, kila mmoja akirejea nyumbani kwake. Naye Yoabu akarudi kwa mfalme huko Yerusalemu.
23 Therfor Joab was on al the oost of Israel; forsothe Benanye, sone of Joiada, was on Cerethi and Ferethi;
Yoabu alikuwa jemadari wa jeshi lote la Israeli; Benaya mwana wa Yehoyada alikuwa juu ya Wakerethi na Wapelethi;
24 forsothe Adhuram was on tributis; forsothe Josaphat, sone of Achilud, was chaunceler; forsothe Siba was scryueyn;
Adoramu alikuwa kiongozi wa wale waliofanya kazi ya kulazimishwa; Yehoshafati mwana wa Ahiludi alikuwa mweka kumbukumbu;
25 forsothe Sadoch and Abiathar weren preestis;
Sheva alikuwa mwandishi; Sadoki na Abiathari walikuwa makuhani;
26 forsothe Hira of Hiarith was preest of Dauid.
na Ira, Myairi, alikuwa kuhani wa Daudi.

< 2 Samuel 20 >