< 2 Samuel 15 >
1 Therfor aftir these thingis Absolon made a chaar to hym, and knyytis, and fifti men, that schulden go bifor hym.
Ikawa baada ya haya Absalomu akaandaa gari la farasi na farasi kwa ajili yake pamoja na watu hamsini wa kwenda mbele zake.
2 And Absolon roos eerli, and stood bisidis the entryng of the yate in the weie; and Absolon clepide to hym ech man, that hadde a cause that he schulde come to the doom of the kyng, and Absolon seide, Of what citee art thou? Which answeride, and seide, Of o lynage of Israel Y am, thi seruaunt.
Absalomu alikuwa akiamka mapema na kusimama kando ya njia iliyoelekea katika lango la mji. Mtu yeyote aliyekuwa na shauri la kuja kwa mfalme kwa ajili ya hukumu, Absalomu alimwita na kumwuliza, “Unatoka mji upi?” Na mtu yule hujibu, Mtumishi wako anatoka mojawapo ya kabila za Israeli.”
3 And Absolon answeride to hym, Thi wordis semen to me good and iust, but noon is ordeyned of the kyng to here thee. And Absolon seide, Who schal ordeyne me iuge on the lond,
Hivyo Absalomu umwambia, “Tazama, shitaka lako ni jema na la haki, lakini hakuna aliyepewa mamlaka na mfalme kusikiliza shitaka lako.
4 that alle men that han cause come to me, and Y deme iustly?
Absalomu uongeza, “Natamani kwamba ningefanywa mwamzi ndani ya nchi ili kwamba kila mtu aliye na shitaka angeweza kuja kwangu nami ningempa haki.
5 But whanne a man cam to Absolon to greete hym, he helde forth the hond, and took, and kisside that man;
Hivyo ikawa kila mtu aliyekuja kumweshimu Absalomu yeye hunyosha mkono na kumshika na kumbusu.
6 and Absolon dide this to al Israel, that cam to doom to be herd of the kyng; and Absolon drow awei the hertis of men of Israel.
Absalomu alifanya hivi kwa Israeli wote waliokuja kwa mfalme kwa ajili ya hukumu. Hivyo Absalomu akaipotosha mioyo ya watu wa Israeli.
7 Forsothe aftir foure yeer Absolon seide to kyng Dauid, Y schal go, and Y schal yelde my vowis, whiche Y vowide to the Lord in Ebron;
Ikawa mwishoni mwa miaka minne Absalomu akamwambia mfalme, “Tafadhari niruhusu niende ili nitimize nadhiri niliyoiweka kwa Yahwe huko Hebroni.
8 for thi seruaunt vowynge vowide, whanne he was in Gessur of Sirie, and seide, If the Lord bryngith ayen me in to Jerusalem, Y schal make sacrifice to the Lord.
Kwa maana mtumishi wako aliweka nadhiri alipokuwako Geshuri katika Shamu akisema, 'Ikiwa Yahwe kweli atanirejesha Yerusalemu, ndipo nitamwabudu yeye.”
9 And the kyng seide to hym, Go thou in pees. And Absolon roos, and yede in to Ebron.
Hivyo mfalme akamwambia, “Nenda kwa amani”. Absalomu akainuka na kwenda Hebroni.
10 Forsothe Absolon sente aspieris in to al the lynage of Israel, and seide, Anoon as ye heren the sown of clarioun, seye ye, Absolon schal regne in Ebron.
Kisha Absalomu akatuma wapelelezi katika jamaa zote za Israeli, kusema, “Mara msikiapo sauti ya tarumbeta semeni, 'Absalomu anatawala katika Hebroni.”
11 Forsothe twei hundrid men clepid of Jerusalem yeden with Absolon, and yede with symple herte, and outirli thei knewen not the cause.
Watu mia mbili waliokuwa wamearikwa kutoka Yerusalemu wakaenda na Absalomu. Wakaenda katika ujinga wao bila kujua Absalomu alichokipanga. Wakati
12 Also Absolon clepide Achitofel of Gilo, the councelour of Dauid, fro his citee Gilo. And whanne he offride sacrifices a strong swerynge togidere was maad, and the puple rennynge togidere was encreessid with Absolon.
Absalomu akitoa dhabihu, alituma watu kwa Ahithofeli katika mji wake huko Gilo. Yeye alikuwa mshauri wa Daudi. Uaini wa Absalomu ukawa na nguvu kwa kuwa watu waliomfuata waliendelea kuongezeka.
13 Therfor a messanger cam to Dauid, and seide, With al herte al Israel sueth Absolon.
Mjumbe akaja kwa Daudi na kusema, “Mioyo ya watu wa Israeli inaambatana na Absalomu.”
14 And Dauid seide to hise seruauntis that weren with hym in Jerusalem, Rise ye, and flee we; for noon ascaping schal be to us fro the face of Absolon; therfor haste ye to go out, lest he come, and ocupie vs, and fille on vs fallynge, and smyte the citee bi the scharpnesse of swerd.
Hivyo Daudi akawambia watumishi wake waliokuwa pamoja naye huko Yerusalemu, “Haya na tuinuke na kukimbia kwani hakuna hata mmoja atakayesalimika kwa Absalomu. Jiandaeni kuondoka mara moja asije akatupata mara hata akasababisha madhara juu yetu na kuushambulia mji kwa makali ya upanga.”
15 And the seruauntis of the kyng seiden to hym, We thi seruauntis schulen performe gladli alle thingis, what euer thingis oure lord the kyng schal comaunde.
Watumishi wa mfalme wakamwambia, “Tazama, watumishi wako wapo tiyari kufanya lolote bwana wetu mfalme atakaloamua.
16 Therfor the kyng yede out, and al his hous, on her feet; and the king lefte ten wymmen concubyns, `that is, secundarie wyues, to kepe the hous.
Mfalme akaondoka na familia yake yote pamoja naye, lakini mfalme akawaacha wanawake kumi waliokuwa masuria wa mfalme ili walitunze kasri.
17 And the king yede out, and al Israel, on her feet, and the kyng stood fer fro the hous.
Baada ya mfalme kwenda na watu wote pamoja naye, wakasimama katika nyumba ya mwisho.
18 And alle hise seruauntis yeden bisidis him, and the legiouns of Cerethi and of Ferethi, and alle men of Geth `strong fiyters, sixe hundrid men, that sueden him fro Geth, yeden on foote bifor the kyng.
Jeshi lake lote likaenda pamoja naye na mbele yake wakaenda Wakerethi na Wapelethi, na Wagiti mia sita wote waliokuwa wamemfuata kutoka Gathi.
19 Forsothe the kyng seide to Ethai of Geth, Whi comest thou with vs? Turne thou ayen, and dwelle with the kyng, for thou art a pilgrym, and thou yedist out fro thi place.
Kisha mfalme akamwambia Itai Mgiti, “Kwa nini wewe pia uende nasi? Rudi na ukae na mfalme Absalomu kwa kuwa wewe ni mgeni tena mfungwa. Rudi mahali pako mwenyewe.
20 Thou camest yistirdai, and to dai thou art compellid to go out with vs. Sotheli Y schal go, whidur Y schal go; turne ayen, and lede ayen thi britheren with thee, and the Lord do mercy and treuthe with thee, for thou schewidist grace and feith.
Kwani ni jana tu umeondoka, kwa nini nikufanye uzunguke nasi popote? Hata sijui niendako. Hivyo rudi pamoja na wenzako. Utiifu na uaminifu viambatane nawe.”
21 And Ethai answeride to the kyng, and seide, The Lord lyueth, and my lord the kyng lyueth, for in what euer place thou schalt be, my lord the kyng, ether in deeth ethir in lijf, there thi seruaunt schal be.
Lakini Itai akamjibu mfalme na kusema, “Kama Yahwe aishivyo na kama bwana wangu mfalme aishivyo, kwa hakika mahali popote bwana wangu mfalme aendako, mtumishi wako pia ndipo atakapokwenda, kwamba ni maisha au kifo.”
22 And Dauid seide to Ethay, Come thou, and passe. And Ethai of Geth passide, and the kyng, and alle men that weren with hym, and the tother multitude.
Hivyo Daudi akamwambia Itai, haya tangulia uende pamoja nasi.” Hivyo Itai Mgiti akaenda pamoja na mfalme, pamoja na watu wake wote na familia zao zote.
23 And alle men wepten with greet vois, and al the puple passide; and the kyng yede ouer the strond of Cedron, and al the puple yede ayens the weie of the olyue tree, that biholdith to deseert.
Nchi yote ikalia kwa sauti kadili watu walivyokuwa wakivuka Bonde la Kidroni, mfalme naye pia akavuka. Watu wote wakasafiri kuelekea nyikani.
24 Forsothe and Sadoch the preest cam, and alle the dekenes with hym, and thei baren the arke of boond of pees of God, and thei diden doun the arke of God; and Abiathar stiede, til al the puple was passid that yede out of the citee.
Walikuwepo pia Sadoki pamoja na Walawi wote wamebeba sanduku la Mungu la agano. Wakaliweka sanduku la Mungu chini na kisha Abiathari akaungana nao. Wakasubiri mpaka watu wote walioondoka mjini walipokwisha kupita.
25 And the kyng seide to Sadoch, Bere ayen the arke of God in to the citee; if Y schal fynde grace in the iyen of the Lord, he schal lede me ayen, and he schal schewe to me that arke and his tabernacle.
Mfalme akamwambia Sadoki, “Ulirudishe sanduku la Mungu mjini. Ikiwa nitaona neema machoni pa Yahwe atanirudisha na kunionesha tena sanduku na mahali likaapo.
26 Sotheli if the Lord seith, Thou plesist not me; Y am redi, do he that, that is good bifor hym silf.
Lakini ikiwa atasema, sipendezwi nawe,' tazama mimi nipo hapa, na anitendee yaliyo mema machoni pake.”
27 And the kyng seide to Sadoch, preest, A! thou seere, `that is, profete, turne ayen in to the citee, with pees; and Achymaas, thi sone, and Jonathas, the sone of Abiathar, youre twei sones, be with you.
Pia mfalme akamwambia Sadoki kuhani, “Je wewe siyo mwonaji? Rudi mjini kwa amani na wanao wawili, Ahimaazi mwanao na Yonathani mwana wa Abiathari.
28 Lo! Y schal be hid in the feeldi places of deseert, til word come fro you, and schewe to me.
Tazama nitasubiri katika vivuko vya Araba mpaka nitakapo pata neno kutoka kwenu kunitaarifu.”
29 Therfor Sadoch and Abiathar baren ayen the arke of God in to Jerusalem, and dwelliden there.
Hivyo Sadoki na Abiathari wakalirudish sanduku la Mungu Yerusalemu nao wakakaa humo.
30 Forsothe Dauid stiede on the hil of olyue trees, stiynge and wepynge, with the heed hilyd, and `goynge with nakid feet; but also al the puple that was with hym, stiede with the heed hilid, and wepte.
Lakini Daudi akaenda bila viatu huku akilia hata Mlima wa Mizeituni, naye alikuwa amefunika kichwa chake. Kila mtu miongoni mwao waliokuwa pamoja naye akafunika kichwa chake, nao wakaenda huku wakilia.
31 Forsothe it was teld to Dauid, that Achitofel was in the sweryng togidere with Absolon; and Dauid seide, Lord, Y byseche, make thou fonned the counsel of Achitofel.
Mtu mmoja akamwambia Daudi kusema, Ahithofeli ni miongoni mwa waaini walio pamoja na Absalomu.” Hivyo Daudi akaomba, “Ee Yahwe, tafadhari badili ushauri wa Ahithofeli kuwa upumbavu.”
32 And whanne Dauid stiede in to the hiyenesse of the hil, in which he schulde worschipe the Lord, lo! Cusi of Arath, with the cloth to-rent, and with the heed ful of erthe, cam to hym.
Ikawa Daudi alipofika juu njiani mahala Mungu alipokuwa akiabudiwa, Hushai Mwarki akaja kumlaki vazi lake limeraruliwa na mavumbi kichwani pake.
33 And Dauid seide to hym, If thou comest with me, thou schalt be to me to charge; sotheli if thou turnest ayen in to the citee,
Daudi akamwambia, “Ikiwa utaenda nami utakuwa mzigo kwangu.
34 and seist to Absolon, Y am thi seruaunt, kyng, suffre thou me to lyue; as Y was the seruaunt of thi fadir, so Y schal be thi seruaunt; thou schalt distrye the counsel of Achitofel.
Lakini ukirudi mjini na kumwambia Absalomu, 'Nitakuwa mtumishi wa mfalme kama nilivokuwa mtumishi wa baba yako, ndivyo nitakavyokuwa mtumishi wako,' ndipo utayageuza mashauri ya Ahithofeli kwa ajili yangu.
35 Forsothe thou hast with thee Sadoch and Abiathar, preestis; and `thou schalt schewe ech word, what euer word thou schalt here in the hows of the kyng, to Sadoch and Abiathar, preestis.
Je haunao pamoja nawe Sadoki na Abiathari makuhani? Hivyo chochote ukisikiacho katika kasri, uwaambie Sadoki na Abiathari makuhani.
36 Sotheli twei sones `of hem ben with hem, Achymaas, sone of Sadoch, and Jonathan, sone of Abiathar; and ye schulen sende bi hem to me ech word which ye schulen here.
Tazama wanao pamoja nao wana wao wawili, Ahimaasi, mwana wa Sadoki, na Yonathani mwana wa Abiathari. Mniletee habari juu ya kila mnachokisikia.”
37 Therfor whanne Chusi, freend of Dauid, cam in to the citee, also Absolon entryde in to Jerusalem.
Hivyo Hushai, rafiki wa Daudi, akaja mjini wakati Absalomu anafika na kuingia Yerusalemu.