< 2 Peter 3 >

1 Lo! ye moost dereworth britheren, Y write to you this secounde epistle, in which Y stire youre clere soule bi monesting togidere,
Wapenzi wangu, hii ni barua ya pili ninayowaandikia. Katika barua hizo mbili nimejaribu kufufua fikira safi akilini mwenu kwa kuwakumbusheni mambo haya.
2 that ye be myndeful of tho wordis, that Y biforseide of the hooli prophetis, and of the maundementis of the hooli apostlis of the Lord and sauyour.
Napenda mkumbuke maneno yaliyosemwa na manabii watakatifu, na ile amri ya Bwana na Mwokozi mliyopewa na mitume wenu.
3 First wite ye this thing, that in the laste daies disseyueris schulen come in disseit, goynge aftir her owne coueityngis,
Awali ya yote jueni kwamba siku za mwisho watakuja watu ambao mienendo yao inatawaliwa na tamaa zao mbaya. Watawadhihaki ninyi
4 seiynge, Where is the biheest, or the comyng of hym? for sithen the fadris dieden, alle thingis lasten fro the bigynnyng of creature.
na kusema: “Aliahidi kwamba atakuja! Je, sasa yuko wapi? Mambo ni yaleyale tangu babu zetu walipokufa; hali ya vitu ni ileile kama ilivyokuwa mwanzo wa ulimwengu!”
5 But it is hid fro hem willynge this thing, that heuenes were bifore, and the erthe of water was stondynge bi watir, of Goddis word;
Watu hao, kwa makusudi, husahau kwamba zamani Mungu alinena, nazo mbingu na nchi zikaumbwa. Dunia iliumbwa kutoka katika maji na kwa maji;
6 bi which that ilke world clensid, thanne bi watir perischide.
na kwa maji hayo, yaani yale maji ya gharika kuu, dunia ya wakati ule iliangamizwa.
7 But the heuenes that now ben, and the erthe, ben kept bi the same word, and ben reseruyd to fier in to the dai of doom and perdicioun of wickid men.
Lakini mbingu na nchi za sasa zahifadhiwa kwa neno la Mungu kwa ajili ya kuharibiwa kwa moto. Zimewekwa kwa ajili ya Siku ile ambapo watu wasiomcha Mungu watahukumiwa na kuangamizwa.
8 But, ye moost dere, this o thing be not hid to you, that o dai anentis God is as a thousynde yeeris, and a thousynde yeeris ben as o dai.
Lakini, wapenzi wangu, msisahau kitu kimoja! Mbele ya Bwana, hakuna tofauti kati ya siku moja na miaka elfu; kwake yote ni mamoja.
9 The Lord tarieth not his biheest, as summe gessen, but he doith pacientli for you, and wole not that ony men perische, but that alle turne ayen to penaunce.
Bwana hakawii kutimiza yale aliyoahidi kama watu wengine wanavyofikiri kuwa atakawia. Yeye ana saburi kwa ajili yenu, maana hapendi hata mmoja wenu apotee, bali huwavuta wote wapate kutubu.
10 For the dai of the Lord schal come as a theef, in which heuenes with greet bire schulen passe, and elementis schulen be dissoluyd bi heete, and the erthe, and alle the werkis that ben in it, schulen be brent.
Siku ya Bwana itakuja kama mwizi. Siku hiyo, mbingu zitatoweka kwa kishindo kikuu; vitu vyake vya asili vitateketezwa kwa moto, nayo dunia itatoweka pamoja na kila kitu kilichomo ndani yake.
11 Therfor whanne alle these thingis schulen be dissolued, what manner men bihoueth it you to be in hooli lyuyngis and pitees,
Maadamu kila kitu kitaharibiwa namna hiyo, je, ninyi mnapaswa kuwa watu wa namna gani? Mnapaswa kuishi kitakatifu na kumcha Mungu,
12 abidinge and hiyynge in to the comyng of the dai of oure Lord Jhesu Crist, bi whom heuenes brennynge schulen be dissoluyd, and elementis schulen faile bi brennyng of fier.
mkiingojea Siku ile ya Mungu na kuifanya ije upesi—Siku ambayo mbingu zitateketezwa kwa moto na kuharibiwa, na vitu vyake vya asili vitayeyushwa kwa joto.
13 Also we abiden bi hise biheestis newe heuenes and newe erthe, in which riytwisnesse dwellith.
Lakini sisi, kufuatana na ahadi yake, twangojea mbingu mpya na dunia mpya ambayo imejaa uadilifu.
14 For which thing, ye moost dere, abidynge these thingis, be ye bisye to be foundun to hym in pees vnspottid and vndefoulid.
Kwa hiyo wapenzi wangu, mkiwa mnangojea Siku ile, fanyeni bidii kuwa safi kabisa bila hatia mbele ya Mungu, na kuwa na amani naye.
15 And deme ye long abiding of oure Lord Jhesu Crist youre heelthe, as also oure moost dere brother Poul wroot to you, bi wisdom youun to hym.
Mnapaswa kuuona uvumilivu wa Bwana kuwa ni nafasi anayowapeni mpate kuokolewa, kama Paulo ndugu yetu mpenzi alivyowaandikia akitumia hekima aliyopewa na Mungu.
16 As and in alle epistlis he spekith `in hem of these thingis; in which ben summe hard thingis to vndurstonde, whiche vnwise and vnstable men deprauen, as also thei don othere scripturis, to her owne perdicioun.
Hayo ndiyo asemayo katika barua zake zote anapozungumzia suala hilo. Yapo mambo kadhaa katika barua zake yaliyo magumu kuyaelewa, mambo ambayo watu wajinga, wasio na msimamo, huyapotosha kama wanavyopotosha sehemu nyingine za Maandiko Matakatifu. Hivyo wanasababisha maangamizi yao wenyewe.
17 Therfor ye, britheren, bifor witynge kepe you silf, lest ye be disseyued bi errour of vnwise men, and falle awei fro youre owne sadnesse.
Lakini ninyi, wapenzi wangu, mmekwisha jua jambo hili. Basi, muwe na tahadhari msije mkapotoshwa na makosa ya waasi, mkaanguka kutoka katika msimamo wenu imara.
18 But wexe ye in the grace and the knowyng of oure Lord Jhesu Crist and oure Sauyour; to hym be glorie now and in to the dai of euerlastyngnesse. Amen. (aiōn g165)
Lakini endeleeni kukua katika neema na katika kumjua Bwana wetu na Mwokozi Yesu Kristo. Utukufu uwe kwake, sasa na hata milele! Amina. (aiōn g165)

< 2 Peter 3 >

The Great Flood
The Great Flood