< 2 Kings 8 >
1 Forsothe Elisee spak to the womman, whose sone he made to lyue, and he seide, Rise thou, and go, bothe thou and thin hows, and `go in pilgrimage, where euer thou schalt fynde; for the Lord schal clepe hungur, and it schal come on the lond bi seuene yeer.
Wakati huu, Elisha alikuwa amemwambia yule mwanamke ambaye mwanawe alikuwa amefufuliwa, “Ondoka wewe na jamaa yako ukaishi mahali popote unapoweza kwa kitambo kidogo, kwa sababu Bwana ameamuru njaa katika nchi hii ambayo itadumu kwa miaka saba.”
2 And sche roos, and dide bi the word of the man of God; and sche yede with hir hows, and was in pilgrimage in the lond of Philistym many daies.
Yule mwanamke akafanya kama vile yule mtu wa Mungu alivyosema. Yeye na jamaa yake wakaondoka na kwenda kuishi katika nchi ya Wafilisti kwa miaka saba.
3 And whanne seuene yeer weren endid, the womman turnede ayen fro the lond of Philisteis; and sche yede out, to axe the kyng for her hows, and hir feeldis.
Baada ya miaka saba, yule mwanamke akarudi kutoka nchi ya Wafilisti, akaenda kwa mfalme kumsihi kwa ajili ya nyumba yake na shamba lake.
4 Sotheli the kyng spak with Giezi, child of the man of God, and seide, Telle thou to me alle the grete dedis whiche Elisee dide.
Mfalme alikuwa anazungumza na Gehazi, mtumishi wa mtu wa Mungu, naye alikuwa amesema, “Hebu niambie mambo yote makuu yaliyofanywa na Elisha.”
5 And whanne he telde to the kyng, hou Elisee hadde reiside a deed man, the womman apperide, whos sone he hadde maad to lyue, and sche criede to the kyng for hir hows, and for hir feeldis. And Giesi seide, My lord the king, this is the womman, and this is hir sone, whom Elisee reiside.
Wakati Gehazi alipokuwa akimweleza mfalme jinsi Elisha alivyomfufua mtu, yule mwanamke ambaye mwanawe alikuwa amefufuliwa na Elisha akaja ili amsihi mfalme kwa ajili ya nyumba yake na shamba lake. Gehazi akasema, “Huyu ndiye huyo mwanamke, bwana wangu mfalme, na huyu ndiye mwanawe ambaye Elisha alimfufua.”
6 And the kyng axide the womman, and sche tolde to hym, that the thingis weren sothe. And the kyng yaf to hir o chaumburleyn, and seide, Restore thou to hir alle thingis that ben hern, and alle fruytis of the feeldis, fro the dai in which she left the lond `til to present tyme.
Mfalme akamuuliza yule mwanamke kuhusu mambo hayo, naye akamweleza. Ndipo akaamuru afisa ashughulikie shauri lake na kumwambia, “Mrudishie huyu mwanamke kila kitu kilichokuwa mali yake, pamoja na mapato yote yaliyotokana na shamba lake tangu siku alipoondoka nchini hadi sasa.”
7 Also Elisee cam to Damask, and Benadab, kyng of Sirie, was sijk; and thei telden to hym, and seiden, The man of God cam hidur.
Elisha akaenda Dameski, naye Ben-Hadadi mfalme wa Aramu alikuwa mgonjwa. Mfalme alipoambiwa, “Mtu wa Mungu ametoka mbali akapanda hadi hapa,”
8 And the kyng seide to Azael, Take with thee yiftis, and go thou in to the meetyng of the man of God, and `counsele thou bi hym the Lord, and seie thou, Whether Y may ascape fro this `sikenesse of me?
mfalme akamwambia Hazaeli. “Chukua zawadi na uende kumlaki huyo mtu wa Mungu. Muulize Bwana kupitia yeye, kwamba, ‘Je, nitapona ugonjwa huu?’”
9 Therfor Azael yede in to the meetyng of hym, and hadde with hym silf yiftis, and alle the goodis of Damask, the burthuns of fourti camels. And whanne he hadde stonde bifor Elisee, he seide, Thi sone, Benadab, kyng of Sirie, sente me to thee, and seide, Whether Y may be helid of this `sikenesse of me?
Hazaeli akaenda kumlaki Elisha, akiwa amechukua zawadi ya kila kitu kizuri kilichopatikana Dameski, mizigo iliyobebwa na ngamia arobaini. Akaingia ndani na kusimama mbele yake, akasema, “Mwanao Ben-Hadadi mfalme wa Aramu amenituma niulize, ‘Je, nitapona ugonjwa huu?’”
10 And Elisee seide, Go thou, and seye to hym, Thou schalt be heelid; forsothe the Lord schewide to me that he schal die bi deth.
Elisha akajibu, “Nenda ukamwambie, ‘Hakika utapona’; lakini Bwana amenifunulia kwamba kweli atakufa.”
11 And he stood with hym, and he was disturblid, `til to the castyng doun of cheer; and the man of God wepte.
Elisha akamkazia Hazaeli macho kwa nguvu mpaka akaona aibu. Kisha mtu wa Mungu akaanza kulia.
12 `To whom Azael seide, Whi wepith my lord? And he answeride, For Y woot what yuelis thou schalt do to the sones of Israel; thou schalt brenne bi fier the strengthid citees of hem, and thou schalt sle bi swerd the yonge men of hem, and thou schalt hurtle doun the litle children of hem, and thou schalt departe the women with childe.
Hazaeli akauliza “Kwa nini bwana wangu analia?” Elisha akajibu, “Kwa sababu najua mabaya utakayowatendea Waisraeli. Utachoma moto ngome zao, utawaua vijana wao kwa upanga, kuwatupa chini kwa nguvu watoto wachanga, na kuwatumbua wanawake wenye mimba.”
13 And Azael seide, What sotheli am Y, thi seruaunt, a dogge, that Y do this grete thing? And Elisee seide, The Lord schewide to me that thou schalt be kyng of Sirie.
Hazaeli akasema, “Itawezekanaje mtumishi wako, aliye mbwa tu, kufanya tendo la ajabu namna hiyo?” Elisha akamjibu, “Bwana amenionyesha kuwa utakuwa mfalme wa Aramu.”
14 And whanne he hadde departid fro Elisee, he cam to his lord; which seide to Azael, What seide Elisee to thee? And he answeride, Elisee seide to me, Thou schalt resseyue helthe.
Kisha Hazaeli akamwacha Elisha na kumrudia bwana wake. Ben-Hadadi akamuuliza, “Elisha alikuambia nini?” Hazaeli akajibu, “Aliniambia kwamba hakika utapona.”
15 And whanne `the tother day hadde come, Azael took the cloth on the bed, and bischedde with watir, and spredde abrood on the face of hym; and whanne he was deed, Azael regnede for hym.
Lakini kesho yake Hazaeli akachukua nguo nzito, akailoweka ndani ya maji, akaitandaza juu ya uso wa mfalme, hivyo akafa. Kisha Hazaeli akaingia mahali pake kuwa mfalme wa Aramu.
16 In the fyuethe yeer of Joram, sone of Achab, kyng of Israel, and of Josephat, kyng of Juda, Joram, sone of Josephat, kyng of Juda, regnede.
Katika mwaka wa tano wa Yoramu mwana wa Ahabu mfalme wa Israeli, wakati huo Yehoshafati akiwa mfalme wa Yuda, Yehoramu mwana wa Yehoshafati akaanza kutawala kama mfalme wa Yuda.
17 He was of two and thretti yeer whanne he bigan to regne, and he regnede eiyte yeer in Jerusalem.
Alikuwa na umri wa miaka thelathini na miwili alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu kwa miaka minane.
18 And he yede in the weies of the kyngis of Israel, as the hows of Achab hadde go; for the douyter of Achab was his wijf; and he dide that, that is yuel in the siyt of the Lord.
Akaenenda katika njia za wafalme wa Israeli, kama nyumba ya Ahabu ilivyokuwa imefanya, kwa kuwa alimwoa binti wa Ahabu. Akatenda maovu machoni pa Bwana.
19 Forsothe the Lord nolde distrie Juda, for Dauid, his seruaunt, as he `hadde bihiyt to Dauid, that he schulde yyue to hym a lanterne, and to hise sones in alle daies.
Hata hivyo, kwa ajili ya Daudi mtumishi wake, Bwana hakutaka kuiangamiza Yuda. Alikuwa ameahidi kuidumisha taa kwa ajili ya Daudi na wazao wake milele.
20 In tho daies Edom, `that is, Ydumee, yede awei, that it schulde not be vndur Juda; and made a kyng to it silf.
Wakati wa Yehoramu, Edomu waliasi dhidi ya Yuda na kujiwekea mfalme wao wenyewe.
21 And Joram cam to Seira, and alle the charis with hym; and he roos bi nyyt, and smoot Ydumeis, that cumpassiden hym, and the princis of charis; sotheli the puple fledde in to her tabernaclis.
Basi Yehoramu akaenda Sairi pamoja na magari yake yote ya vita. Waedomu wakamzunguka yeye na majemadari wake wa magari yake ya vita, lakini akaondoka, akapenya usiku na kuwashambulia Waedomu. Hata hivyo, jeshi lake likatorokea nyumbani mwao.
22 Therfor Edom yede awei, that it was not vndur Juda `til to this day; thanne also Lobna yede awey in that tyme.
Hadi leo Edomu wameasi dhidi ya Yuda. Libna pia wakaasi wakati huo huo.
23 Forsothe the residues of wordis of Joram, and alle thingis whiche he dide, whether these ben not writun in the book of wordis of daies of the kingis of Juda?
Kwa matukio mengine ya utawala wa Yehoramu na yote aliyoyafanya, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Yuda?
24 And Joram slepte with hise fadris, and was biried with hem in the citee of Dauid; and Ocozie, his sone, regnede for hym.
Yehoramu akalala pamoja na baba zake, na akazikwa pamoja nao katika Mji wa Daudi. Naye Ahazia mwanawe akawa mfalme baada yake.
25 In the tweluethe yeer of Joram, sone of Achab, kyng of Israel, Ocozie, sone of Joram, kyng of Juda, regnede.
Katika mwaka wa kumi na mbili wa utawala wa Yoramu mwana wa Ahabu mfalme wa Israeli, Ahazia mwana wa Yehoramu mfalme wa Yuda alianza kutawala.
26 Ocozie, the sone of Joram, was of two and twenti yeer whanne he bigan to regne, and he regnede o yeer in Jerusalem; the name of his moder was Athalia, the douyter of Amry, kyng of Israel.
Ahazia alikuwa na umri wa miaka ishirini na miwili alipoanza kutawala, naye akatawala katika Yerusalemu kwa mwaka mmoja. Mama yake aliitwa Athalia, mjukuu wa Omri mfalme wa Israeli.
27 And he yede in the waies of the hows of Achab, and dide that, that is yuel, bifor the Lord, as the hows of Achab dide; for he was hosebonde of a douyter of the hows of Achab.
Akaenenda katika njia za nyumba ya Ahabu, na kutenda maovu machoni pa Bwana, kama nyumba ya Ahabu ilivyokuwa imefanya, kwa kuwa alikuwa ameoa kutoka nyumba ya Ahabu.
28 Also he yede with Joram, sone of Achab, to fiyt ayens Azael, kyng of Sirie, in Ramoth of Galaad; and men of Sirie woundiden Joram.
Ahazia akaenda vitani na Yoramu mwana wa Ahabu kupigana na Hazaeli mfalme wa Aramu huko Ramoth-Gileadi. Waaramu wakamjeruhi Yoramu.
29 Which turnede ayen, to be heelid in Jezrael; for men of Sirie woundiden hym in Ramoth, fiytynge ayens Azael, kyng of Sirye. Forsothe Ocozie, sone of Joram, the kyng of Juda, cam doun to se Joram, sone of Achab, in to Jezrael, that was sijk there.
Hivyo Mfalme Yoramu akarudi Yezreeli ili apate kuuguza majeraha aliyojeruhiwa na Waaramu huko Ramothi alipopigana na Hazaeli mfalme wa Aramu. Ndipo Ahazia mwana wa Yehoramu mfalme wa Yuda akashuka kwenda Yezreeli kumtazama Yoramu mwana wa Ahabu, kwa sababu alikuwa amejeruhiwa.