< 2 Kings 7 >

1 Forsothe Elisee seide, Here ye the word of the Lord; the Lord seith these thingis, In this tyme to morewe a buschel of flour schal be for a stater, and twei buschels of barli for a stater, in the yate of Samarie.
Elisha akasema, “Sikiliza neno la Bwana. Hivi ndivyo asemavyo Bwana: Wakati kama huu kesho, kipimo kimoja cha unga mzuri kitauzwa kwa shekeli moja ya fedha, na vibaba viwili vya shayiri kwa shekeli moja ya fedha katika lango la Samaria.”
2 And oon of the duykis, on whos hond the kyng lenyde, answeride to the man of God, and seide, Thouy `also the Lord make the goteris of heuene to be openyd, whether that, that thou spekist, mai be? Which Elisee seide, Thou schalt se with thin iyen, and thou schalt not ete therof.
Yule afisa ambaye mfalme alikuwa anauegemea mkono wake akamwambia yule mtu wa Mungu, “Tazama, hata kama Bwana atafungua madirisha ya mbinguni, je, jambo hili litawezekana?” Elisha akajibu, “Utaona kwa macho yako mwenyewe, lakini wewe hutakula chochote kati ya hivyo!”
3 Therfor foure leprouse men weren bisidis the entryng of the yate, whiche seiden togidere, What wolen we be here, til we dien?
Basi kulikuwepo na watu wanne wenye ukoma katika ingilio la lango la mji. Wakaambiana, “Kwa nini tukae hapa mpaka tufe?
4 Whether we wolen entre in to the citee, we schulen die for hungur; whether we dwellen here, we schulen die. Therfor come ye, and fle we ouer to the castels of Sirie; if thei schulen spare vs, we schulen lyue; sotheli if thei wolen sle, netheles we schulen die.
Kama tukisema, ‘Tutaingia mjini,’ mjini kuna njaa, nasi tutakufa humo. Kama tukikaa hapa, tutakufa. Kwa hiyo twende kwenye kambi ya Waaramu na tujisalimishe. Kama wakituacha hai, tutaishi; kama wakituua, basi na tufe.”
5 Therfor thei risiden in the euentide to come to the castels of Sirie; and whanne thei hadden come to the bigynnyng of the castels of Sirie, thei founden not ony man there.
Wakati wa giza la jioni, wakaondoka na kwenda kwenye kambi ya Waaramu. Walipofika mwanzo wa kambi, hapakuwa na mtu,
6 Forsothe the Lord hadde maad a sown of charis, and of horsis, and of ful myche oost to be herd in the castels of Sirie; and thei seiden togidere, Lo! the kyng of Israel hath hirid bi meede ayens vs the kyngis of Etheis and of Egipcians; and thei camen on vs.
kwa kuwa Bwana alilifanya jeshi la Waaramu lisikie sauti kama ya magari ya vita, farasi na jeshi kubwa, kiasi kwamba waliambiana, “Tazama, mfalme wa Israeli ameajiri mfalme wa Wahiti na mfalme wa Wamisri kuja kutushambulia sisi!”
7 Therfor thei risiden, and fledden in derknessis, and leften her tentis, and horsis, and mulis, and assis, in the castels; and thei fledden, couetynge to saue her lyues oonli.
Kwa hiyo wakaondoka na kukimbia wakati wa giza la jioni na kuacha mahema yao, farasi wao na punda wao. Wakakimbia kuokoa maisha yao na kuacha kila kitu ndani ya kambi kama kilivyokuwa.
8 Therfor whanne thilke leprouse men hadden come to the bigynnyng of the castels, thei entriden into o tabernacle, and eetun, and drunken; and thei token fro thennus siluer, and gold, and clothis; and yeden, and hidden; and eft thei turneden ayen to anothir tabernacle, and in lijk maner thei token awei fro thennus, and hidden.
Wale watu wenye ukoma walipofika mwanzoni mwa kambi, wakaingia kwenye mojawapo ya mahema. Wakala na kunywa, na kuchukua fedha, dhahabu na nguo, wakaenda kuvificha. Wakarudi na kuingia katika hema jingine, na kuchukua baadhi ya vitu kutoka ndani yake na kuvificha pia.
9 And thei seiden togidere, We doen not riytfuli, for this is a dai of good message; if we holden stille, and nylen telle til the morewtid, we schulen be repreued of trespassyng; come ye, go we, and telle in the `halle of the kyng.
Kisha wakaambiana, “Hili tunalolifanya sio jema. Hii ni siku ya habari njema, nasi tunakaa kimya. Kama tukisubiri mpaka mapambazuko, maafa yatatupata. Twendeni mara moja tukatoe habari hizi katika jumba la mfalme.”
10 And whanne thei hadden come to the yate of the citee, thei telden to hem, and seiden, We yeden to the castels of Sirie, and we founden not ony man there, no but horsis and assis tied, and tentis fastned.
Hivyo wakaenda mjini na kuwaita walinzi wa langoni, wakawaambia, “Tulikwenda katika kambi ya Waaramu lakini hapakuwepo na mtu huko, hata sauti ya mtu yeyote, ila farasi na punda waliofungwa na mahema yaliyoachwa kama yalivyokuwa.”
11 Therfor the porteris yeden, and telden in the paleis of the kyng with ynne.
Walinzi wa langoni wakatangaza habari ile kwa sauti kuu, na taarifa hii ikatolewa ndani ya jumba la mfalme.
12 Which king roos bi niyt, and seide to hise seruauntis, Y seie to you, what the men of Sirie han do to vs; thei witen, that we trauelen with hungur, therfor thei yeden out of the castels, and ben hid in the feeldis, and seien, Whanne thei schulen go out of the citee, we schulen take hem quyk, and thanne we schulen mowe entre in to the citee.
Mfalme akaamka usiku na kuwaambia maafisa wake, “Nitawaambia kile Waaramu walichotufanyia. Wanajua kwamba tuna njaa, hivyo wameacha kambi yao ili kujificha mashambani, wakifikiri, ‘Kwa hakika watatoka nje ya mji, nasi tutawakamata wakiwa hai na kuingia ndani ya mji.’”
13 Forsothe oon of his seruauntis answeride, Take we fyue horsis, that leften in the citee; for tho ben oonli in al the multitude of Israel, for othere horsis ben wastid; and we sendynge moun aspie.
Mmoja wa maafisa wake akajibu, “Waamuru watu wachache wakawachukue farasi watano kati ya wale waliobaki katika mji. Hatima yao itakuwa kama ya Waisraeli wote walio hapa. Watakuwa tu kama Waisraeli hawa ambao wanangoja kifo. Hivyo tuwatumeni wajue kumetendeka nini.”
14 Therfor thei brouyten forth twei horsis; and the kyng sente in to the castels of men of Sirie, and seide, Go ye, and se.
Ndipo wakachagua magari mawili ya vita pamoja na farasi wake, naye mfalme akawatuma wafuatilie jeshi la Waaramu. Akawaamuru waendeshaji akisema, “Nendeni mkaone ni nini kilichotokea.”
15 Whiche yeden after hem `til to Jordan; lo! forsothe al the weie was ful of clothis, and of vessels, whiche the men of Sirie castiden forth, whanne thei weren disturblid. And the messangeris turneden ayen, and schewiden to the kyng.
Wakawafuatia hadi Yordani, nao wakakuta barabara yote ikiwa imetapakaa nguo na vyombo vya Waaramu walivyokuwa wamevitupa walipokuwa wanatoroka. Basi wale wajumbe wakarudi na kutoa taarifa kwa mfalme.
16 And the puple yede out, and rauyschide the castels of Sirie; and a buyschel of flour was maad for o stater, and twei buyschels of barli for o stater, bi the word of the Lord.
Kisha watu wakatoka na kuteka nyara kambi ya Waaramu. Kwa hiyo kipimo cha unga mzuri kikauzwa kwa shekeli, na vipimo viwili vya shayiri kwa shekeli, kama vile Bwana alivyokuwa amesema.
17 Forsothe the kyng ordeynede at the yate that duyk, in whos hond the kyng lenyde; whom the cumpeny to-trad with her feet, and he was deed, bi the word, which the man of God spak, whanne the kyng cam doun to hym.
Basi mfalme alikuwa amemweka yule afisa ambaye mfalme alikuwa anauegemea mkono wake awe msimamizi wa lango. Nao watu wakamkanyaga walipoingia langoni, naye akafa, kama vile mtu wa Mungu alivyokuwa ametangulia kusema wakati mfalme alipofika nyumbani kwake.
18 And it was doon bi the word of the man of God, which he seide to the kyng, whanne he seide, Twei buyschels of barli shulen be for a statir, and a buyschel of wheete flour for a stater, in this same tyme to morewe in the yate of Samarie;
Ikatokea kama vile mtu wa Mungu alivyokuwa amemwambia mfalme: “Wakati kama huu kesho, kipimo kimoja cha unga mzuri kitauzwa kwa shekeli moja ya fedha, na vibaba viwili vya shayiri kwa shekeli moja ya fedha katika lango la Samaria.”
19 whanne thilke duyk answeride to the man of God, and seide, Yhe, thouy the Lord schal make the goteris in heuene to be openyd, whether this that thou spekist may be? and the man of God seide, Thou schalt se with thin iyen, and thou schalt not ete therof.
Yule afisa alikuwa amemwambia yule mtu wa Mungu, “Tazama, hata kama Bwana atafungua madirisha ya mbinguni, je, jambo hili litawezekana?” Naye yule mtu wa Mungu alikuwa amemjibu, “Utaona kwa macho yako mwenyewe, lakini wewe hutakula chochote kati ya hivyo!”
20 Therfore it bifelde to hym, as it was biforseid; and the puple to-trad hym with feet in the yate, and he was deed.
Ndivyo hasa ilivyotokea kwake, kwa kuwa watu walimkanyaga langoni, naye akafa.

< 2 Kings 7 >