< 2 Kings 3 >

1 Forsothe Joram, sone of Achab, regnede on Israel, in Samarie, in the eiytenthe yeer of Josephat, kyng of Juda. And he regnede twelue yeer,
Yehoramu mwana wa Ahabu akawa mfalme wa Israeli katika Samaria mwaka wa kumi na nane wa utawala wa Yehoshafati mfalme wa Yuda, naye akatawala kwa miaka kumi na miwili.
2 and he dide yuel bifor the Lord, but not as his fader and modir;
Akafanya maovu machoni pa Bwana, lakini sio kama baba yake na mama yake walivyokuwa wamefanya. Akaondoa nguzo ya ibada ya Baali ambayo baba yake alikuwa ameitengeneza.
3 for he took awei the ymagis of Baal, whiche his fadir hadde maad, netheles in the synnes of Jeroboam, sone of Nabath, that made Israel to do synne, `he cleuyde, and yede not awei fro tho.
Hata hivyo akashikamana na dhambi za Yeroboamu mwana wa Nebati, ambazo alisababisha Israeli kuzitenda, wala hakuziacha.
4 Forsothe Mesa, kyng of Moab, nurschide many beestis, and paiede to the kyng of Israel an hundrid thousynde of lambren, and an hundrid thousynde of wetheris, with her fleesis.
Basi Mesha mfalme wa Moabu akafuga kondoo, naye akawa ampatie mfalme wa Israeli wana-kondoo 100,000 pamoja na sufu ya kondoo dume 100,000.
5 And whanne Achab was deed, he brak the boond of pees, which he hadde with the kyng of Israel.
Lakini baada ya Ahabu kufa, mfalme wa Moabu aliasi dhidi ya mfalme wa Israeli.
6 Therfor kyng Joram yede out of Samarie in that dai, and noumbride al Israel.
Kwa hiyo wakati ule Mfalme Yehoramu akaondoka kutoka Samaria na kukusanya Israeli yote tayari kwenda vitani.
7 And he sente to Josephat, kyng of Juda, and seide, The kyng of Moab yede awei fro me; come thou with me ayens him to batel. Which Josephat answeride, Y schal stie; he that is myn, is thin; my puple is thi puple; and myn horsis ben thin horsis.
Akapeleka pia ujumbe ufuatao kwa Yehoshafati mfalme wa Yuda: “Mfalme wa Moabu ameasi dhidi yangu. Je, utakwenda pamoja nami kupigana dhidi ya Moabu?” Akajibu, “Nitakwenda pamoja nawe. Mimi ni kama wewe, watu wangu ni kama watu wako, farasi wangu ni kama farasi wako.”
8 And he seide, Bi what weie schulen we stie? And he answeride, Bi the deseert of Ydumee.
Akauliza, “Je, tutashambulia kupitia njia gani?” Akajibu, “Kupitia Jangwa la Edomu.”
9 Therfor the kyng of Israel, and the kyng of Juda, and the kyng of Edom, yeden forth, and cumpassiden bi the weie of seuene daies; and `watir was not to the oost, and to the beestis, that sueden hem.
Hivyo mfalme wa Israeli akaondoka akiwa pamoja na mfalme wa Yuda na mfalme wa Edomu. Baada ya kuzunguka kwa siku saba, jeshi likawa limeishiwa maji kwa matumizi yao na kwa ajili ya wanyama waliokuwa nao.
10 And the kyng of Israel seide, Alas! alas! alas! the Lord hath gaderide vs thre kyngis to bitake vs in the hond of Moab.
Mfalme wa Israeli akamaka, “Nini! Je, Bwana ametuita sisi wafalme watatu ili tu kututia mikononi mwa Moabu?”
11 And Josephat seide, Whether ony prophete of the Lord is here, that we biseche the Lord bi hym? And oon of the seruauntis of the kyng of Israel answeride, Elisee, the sone of Saphat, is here, that schedde watir on the hondis of Elie.
Lakini Yehoshafati akauliza, “Je, hayuko nabii wa Bwana hapa, ili tuweze kumuuliza Bwana kupitia kwake?” Afisa mmoja wa mfalme wa Israeli akajibu, “Elisha mwana wa Shafati yuko hapa. Ndiye alikuwa akimimina maji juu ya mikono ya Eliya.”
12 And Josephat seide, Is the word of the Lord at hym? Whiche seiden, `It is. And the kyng of Israel, and Josephat, kyng of Juda, and the kyng of Edom, yeden doun to hym.
Yehoshafati akasema, “Neno la Bwana liko pamoja naye.” Kwa hiyo mfalme wa Israeli na Yehoshafati pamoja na mfalme wa Edomu wakamwendea.
13 Forsothe Elise seide to the kyng of Israel, What is to me and to thee? Go thou to the prophetis of thi fadir and of thi modir. And the kyng of Israel seide to hym, Whi hath the Lord gaderid these thre kyngis, to bitake hem into the hondis of Moab?
Elisha akamwambia mfalme wa Israeli, “Nina nini mimi nawe? Nenda kwa manabii wa baba yako na manabii wa mama yako.” Mfalme wa Israeli akajibu, “La hasha, kwa sababu ni Bwana ambaye ametuita pamoja sisi wafalme watatu ili atutie mikononi mwa Moabu.”
14 And Elisee seide to hym, The Lord of oostis lyueth, in whos siyt Y stonde, if Y were not aschamed of the cheer of Josephat, king of Juda, treuli Y hadde not perseyued, nethir Y hadde biholde thee.
Elisha akasema, “Hakika, kama Bwana Mwenye Nguvu Zote aishivyo ambaye ninamtumikia, kama si kuheshimu Yehoshafati mfalme wa Yuda, nisingekutazama wala hata kukutupia jicho.
15 Now forsothe brynge ye to me a sautrere. And whanne the sautrere song, the hond of the Lord was maad on hym, and he seide, The Lord seith these thingis,
Lakini sasa, nileteeni mpiga kinubi.” Mpiga kinubi alipokuwa akipiga, mkono wa Bwana ukaja juu ya Elisha,
16 Make ye the wombe, ether depthe, of this stronde dichis and dichis.
naye akasema, “Hivi ndivyo asemavyo Bwana, ‘Chimbeni bonde hili lijae mahandaki.’
17 For the Lord seith these thingis, Ye schulen not se wynd, nethir reyn, and this depthe schal be fillid with watris, and ye schulen drynke, and youre meynees, and youre beestis.
Kwa kuwa hivi ndivyo asemavyo Bwana: Hamtaona upepo wala mvua, lakini bonde hili litajaa maji, nanyi pamoja na ngʼombe wenu na wanyama wenu wengine mtakunywa.
18 And this is litil in the siyt of the Lord. Ferthermore also he schal bitake Moab in to youre hondis;
Hili ni jambo rahisi machoni pa Bwana. Pia ataitia Moabu mikononi mwenu.
19 and ye schulen smyte ech strengthid citee, and ech chosun citee, and ye schulen kitte doun ech tre berynge fruyt, and ye schulen stoppe alle the wellis of watris, and ye schulen hile with stonys ech noble feeld.
Mtaushinda kila mji wenye ngome na kila mji mkubwa. Mtakata kila mti ulio mzuri, mtaziba chemchemi zote, na kuharibu kila shamba zuri kwa mawe.”
20 Therfor it was doon eerli, whanne sacrifice is wont to be offrid, and, lo! watris camen bi the weie of Edom, and the lond was fillid with watris.
Kesho yake asubuhi, karibu na wakati wa kutoa dhabihu ya asubuhi, tazama, maji yakawa yanatiririka kutoka upande wa Edomu! Nayo nchi ikajaa maji.
21 Sotheli alle men of Moab herden, that kyngis hadden stied to fiyte ayens hem; `and men of Moab clepiden togidere alle men, that weren gird with girdil aboue, and thei stoden in the termes.
Basi Wamoabu wote walikuwa wamesikia kuwa wale wafalme wamekuja kupigana dhidi yao. Hivyo kila mtu, kijana na mzee, ambaye angeweza kushika silaha akaitwa na kuwekwa mpakani.
22 And men of Moab risiden ful eerli, and whanne the sunne was risun thanne euen ayens the watris, thei sien the watris reed as blood euene ayens.
Walipoamka asubuhi na mapema, jua likawa linamulika juu ya maji. Wamoabu waliokuwa upande wa pili wakaona maji ni mekundu, kama damu.
23 And thei seiden, It is the blood of swerd, `that is, sched out bi swerd; kyngis fouyten ayens hem silf, and thei ben slayn togider; now go thou, Moab, to the prey.
Wamoabu wakasema, “Ile ni damu! Lazima hao wafalme wamepigana na kuchinjana wao kwa wao. Sasa Moabu, twendeni tukateke nyara!”
24 And thei yeden in to the castels of Israel; forsothe Israel roos, and smoot Moab, and thei fledden bifor men of Israel. Therfor thei that hadden ouercome, camen, and smytiden Moab, and destrieden cytees;
Lakini Wamoabu walipofika kwenye kambi ya Israeli, Waisraeli wakainuka na kuwapiga mpaka wakakimbia. Nao Waisraeli wakaivamia nchi na kuwachinja Wamoabu.
25 and alle men sendynge stoonys filliden ech beste feeld, and stoppiden alle the wellis of watris, and kittiden doun alle trees berynge fruyt, so that oneli `wallis maad of erthe weren left; and the citee was cumpassid of men settinge engynes, and was smytun bi greet part.
Wakaiharibu miji, kila mtu akatupa jiwe juu ya kila shamba zuri mpaka likafunikwa. Wakaziba chemchemi zote na kukata kila mti mzuri. Kir-Haresethi peke yake ndio uliobaki na mawe yake yakiwa mahali pake. Lakini hata hivyo watu waliokuwa na makombeo wakauzunguka na kuushambulia vilevile.
26 And whanne the kyng of Moab hadde seyn this, that is, that the enemyes hadden the maistrie, he took with hym seuene hundrid men drawynge swerdis, that thei shulden breke in to the kyng of Edom; and thei myyten not.
Mfalme wa Moabu alipoona kuwa vita vimekuwa vikali dhidi yake, akachukua watu 700 wenye panga ili kuingia kwa mfalme wa Edomu, lakini wakashindwa.
27 And he took his firste gendrid sone, that schulde regne for hym, and offride brent sacrifice on the wal; and greet indignacioun was maad in Israel; and anoon thei yeden awei fro hym, and turneden ayen in to her lond.
Ndipo akamchukua mwanawe mzaliwa wake wa kwanza, ambaye angekuwa mfalme baada yake, akamtoa kama dhabihu ya kuteketezwa juu ya ukuta wa mji. Ghadhabu ikawa kubwa dhidi ya Israeli; wakajiondoa kwake na kurudi katika nchi yao wenyewe.

< 2 Kings 3 >