< 2 Kings 25 >

1 Forsothe it was don in the nynthe yeer of his rewme, in the tenthe moneth, in the tenthe dai of the moneth, Nabugodonosor, kyng of Babiloyne, cam, he, and al his oost, in to Jerusalem; and thei cumpassiden it, and bildiden `stronge thingis in the cumpass therof.
Hivyo katika mwaka wa tisa wa utawala wa Sedekia, katika siku ya kumi ya mwezi wa kumi, Nebukadneza mfalme wa Babeli, akiwa na jeshi lake lote, alifanya vita dhidi ya Yerusalemu. Akapiga kambi nje ya mji na kuuzunguka mji pande zote.
2 And the citee was closid, and cumpassid, `til to the eleuenthe yeer of king Sedechie,
Mji ulizungukwa na jeshi mpaka mwaka wa kumi na moja wa utawala wa Mfalme Sedekia.
3 in the nynthe day of the monethe; and hungur `hadde maistrie in the citee, and `breed was not to the puple of the lond.
Ilipowadia siku ya tisa ya mwezi wa nne, njaa ikazidi kuwa kali sana ndani ya mji, hadi hapakuwa na chakula kwa ajili ya watu.
4 And the citee was brokun, and alle men werriours fledden in the niyt bi the weie of the yate, which is bitwixe the double wal, to the gardyn of the kyng; sotheli Caldeis bisegiden the citee `bi cumpas. Therfor Sedechie fledde bi the weie that ledith to the feeldi placis of the wildirnesse;
Kisha ukuta wa mji ukavunjwa, na jeshi lote likakimbia. Wakaondoka mjini usiku kupitia lango lililokuwa kati ya kuta mbili karibu na bustani ya mfalme, ingawa Wakaldayo walikuwa wameuzunguka mji. Wakakimbia kuelekea Araba.
5 and the oost of Caldeis pursuede the king, and it took him in the pleyn of Jerico; and alle the werriours, that weren with him, weren scaterid, and leften him.
Lakini jeshi la Wakaldayo likamfuatia mfalme na kumpata katika sehemu tambarare za Yeriko. Askari wake wote wakatengwa naye na kutawanyika,
6 Therfor thei ledden the king takun to the king of Babiloyne, in to Reblatha, which spak dom with him, `that is, with Sedechie.
naye akakamatwa. Akapelekwa kwa mfalme wa Babeli huko Ribla, mahali ambapo hukumu yake ilitangazwa.
7 Sotheli he killide the sones of Sedechie bifor him, and puttide out his iyen, and boond him with chaynes, and ledde him in to Babiloyne.
Wakawaua wana wa Sedekia mbele ya macho yake. Kisha wakayangʼoa macho yake, wakamfunga kwa pingu za shaba na kumpeleka Babeli.
8 In the fifthe monethe, in the seuenthe dai of the monethe, thilke is the nyntenthe yeer of the king of Babiloyne, Nabuzardan, prince of the oost, seruaunt of the king of Babiloyne, cam in to Jerusalem;
Mnamo siku ya saba ya mwezi wa tano, katika mwaka wa kumi na tisa wa utawala wa Nebukadneza mfalme wa Babeli, Nebuzaradani jemadari wa askari walinzi wa mfalme, afisa wa mfalme wa Babeli, alikuja Yerusalemu.
9 and he brente the hows of the Lord, and the hows of the king, and the housis of Jerusalem, and he brente bi fier ech hows;
Alichoma moto Hekalu la Bwana, jumba la kifalme, na nyumba zote za Yerusalemu. Aliteketeza kila jengo muhimu.
10 and al the oost of Caldeis, that was with the prince of knyytis, distriede the wallis of Jerusalem `in cumpas.
Jeshi lote la Wakaldayo, chini ya jemadari wa askari walinzi wa mfalme, walivunja kuta zilizoizunguka Yerusalemu.
11 Forsothe Nabuzardan, prince of the chyyualrie, translatide the tother part of the puple, that dwellide in the citee, and the fleeris, that hadden fled ouer to the king of Babiloyne, and the residue comyn puple;
Nebuzaradani jemadari wa askari walinzi akawapeleka uhamishoni watu waliokuwa wamebaki katika mji, pamoja na mabaki ya watu wa kawaida, na wale waliojisalimisha kwa mfalme wa Babeli.
12 and he lefte of the pore men of the lond vyntilieris, and erthe tilieris.
Lakini yule jemadari wa askari walinzi akawaacha baadhi ya wale watu maskini kabisa ili watunze mashamba ya mizabibu na mashamba mengine.
13 Sotheli Caldeis braken the brasun pilers, that weren in the temple, and the foundementis, and the see of bras, that was in the hous of the Lord; and thei translatiden al the metal in to Babiloyne.
Wakaldayo walivunja vipande zile nguzo za shaba, vile vishikilio vya shaba vilivyohamishika, na ile Bahari ya shaba, ambavyo vyote vilikuwa katika Hekalu la Bwana. Hivyo wakaichukua hiyo shaba na kuipeleka Babeli.
14 And thei token the pottis of bras, and trullis, and fleisch hokis, and cuppis, and morteris, and alle brasun vessels, in whiche thei mynystriden;
Wakachukua pia vyungu, masepetu, mikasi ya kusawazishia tambi, sahani na vyombo vyote vya shaba vilivyotumika katika huduma ya Hekalu.
15 also and censeris, and violis. The prince of the chyualrie took tho that weren of gold, and tho that weren of siluer,
Jemadari wa askari walinzi wa mfalme akachukua vile vyetezo na yale mabakuli ya kunyunyizia, vitu vyote vile vilivyokuwa vimetengenezwa kwa dhahabu safi au fedha.
16 that is, twei pileris, o see, and the foundementis, whiche king Salomon hadde maad `in to the temple of the Lord; and no weiyte was of metal of alle the vessels.
Shaba iliyotokana na zile nguzo mbili, ile Bahari na vile vishikilio vilivyohamishika, ambavyo Solomoni alikuwa ametengeneza kwa ajili ya Hekalu la Bwana, ilikuwa na uzito usioweza kupimika.
17 O piler hadde eiyten cubitis of hiyte, and a brasun pomel on it of the heiyte of thre cubitis, and a werk lijk a net, and pomgarnadis on the pomel of the piler, alle thingis of bras; and the secounde piler hadde lijk ournyng.
Kila nguzo ilikuwa na urefu wa dhiraa kumi na nane. Sehemu ya shaba juu ya nguzo moja ilikuwa na urefu wa dhiraa tatu na ilikuwa imepambwa kwa wavu na makomamanga ya shaba kuizunguka kote. Ile nguzo nyingine pamoja na wavu wake ilifanana na hiyo ya kwanza.
18 Also the prince of the chyualrie took Saraie, the firste preest, and Sophony, the secunde prest,
Yule jemadari wa askari walinzi akawachukua kama wafungwa Seraya kuhani mkuu, kuhani Sefania aliyefuata kwa cheo, na mabawabu watatu.
19 and thre porteris, and oon onest seruaunt of the citee, that was a souereyn ouer men werriours, and fyue men `of hem that stoden bifor the king, whiche he foond in the citee; and he took Sopher, the prince of the oost, that preuide yonge knyytis, `ether men able to batel, of the puple of the lond, and sixe men of the comyns, that weren foundyn in the citee;
Miongoni mwa wale watu waliokuwa wamesalia katika mji, alimchukua afisa kiongozi wa wapiganaji, na washauri watano wa mfalme. Akamchukua pia mwandishi aliyesimamia uandikishaji wa watu wa nchi, pamoja na watu wake sitini waliopatikana ndani ya mji.
20 whiche Nabuzardan, prince of the chyualrie, took, and ledde to the king of Babiloyne, in to Reblatha.
Nebuzaradani jemadari akawachukua hao wote na kuwapeleka kwa mfalme wa Babeli huko Ribla.
21 And the kyng of Babiloyne smoot hem, and killide hem in Reblatha, in the lond of Emath; and Juda was translatid fro his lond.
Huko Ribla, katika nchi ya Hamathi, mfalme wa Babeli akaamuru wanyongwe. Hivyo Yuda wakaenda utumwani, mbali na nchi yao.
22 Sotheli he made souereyn Godolie, sone of Aicham, sone of Saphan, to the puple that was left in the lond of Juda; which puple Nabugodonosor, king of Babiloyne, hadde left.
Nebukadneza mfalme wa Babeli akamteua Gedalia mwana wa Ahikamu, mwana wa Shafani, awe msimamizi wa watu aliowaacha Yuda.
23 And whanne alle the duykis of knyytis hadde herd these thingis, thei, and the men that weren with hem, that is, that the king of Babiloyne hadde ordeyned Godolie, thei camen `to Godolie, in Maspha, Ismael, sone of Nathanye, and Johannan, sone of Charee, and Saraie, sone of Thenameth of Nechophat, and Jeconye, sone of Machati, thei, and Machat, and the felowis of hem.
Maafisa wote wa jeshi na watu wao waliposikia kwamba mfalme wa Babeli amemteua Gedalia kuwa mtawala, wakamjia Gedalia huko Mispa. Hawa walikuwa Ishmaeli mwana wa Nethania, Yohanani mwana wa Karea, Seraya mwana wa Tanhumethi Mnetofathi, na Yezania mwana wa Mmaaka, pamoja na watu wao.
24 And Godolie swoor to hem, and to the felowis of hem, and seide, Nyle ye drede to serue the Caldeis; dwelle ye in the lond, and serue ye the king of Babiloyne, and it schal be wel to you.
Gedalia akaapa ili kuwatia moyo wao na watu wao. Akasema, “Msiwaogope maafisa wa Kikaldayo. Kaeni katika nchi na kumtumikia mfalme wa Babeli, na itakuwa vyema kwenu.”
25 Forsothe it was don in the seuenthe monethe, `that is, sithen Godolie was maad souereyn, Hismael, the sone of Nathanye, sone of Elysama, of the `kyngis seed, cam, and ten men with hym, and thei smytiden Godolie, which diede; but also thei smytiden Jewis and Caldeis, that weren with hym in Maspha.
Hata hivyo, katika mwezi wa saba Ishmaeli mwana wa Nethania mwana wa Elishama, aliyekuwa wa uzao wa mfalme, akaja pamoja na watu kumi, nao wakamuua Gedalia, na pia watu wa Yuda, pamoja na Wakaldayo waliokuwa naye huko Mispa.
26 And al the puple roos fro litil `til to greet, and the prynces of knyytis, and camen in to Egipt, and dredden Caldeis.
Baada ya haya, watu wote kuanzia aliye mdogo sana hadi aliye mkubwa kabisa, pamoja na maafisa wa jeshi, wakakimbilia Misri kwa kuwaogopa Wakaldayo.
27 Therfor it was doon in the seuenthe and threttithe yeer of transmigracioun, `ether passyng ouer, of Joakyn, kyng of Juda, in the tweluethe monethe, in the seuene and twentithe dai of the monethe, Euylmeradach, kyng of Babiloyne, in the yeer in which he bigan to regne, reiside the heed of Joakyn, kyng of Juda,
Katika mwaka wa thelathini na saba tangu Yehoyakini mfalme wa Yuda apelekwe uhamishoni, katika mwaka ule ambao Evil-Merodaki alifanyika mfalme wa Babeli, alimwacha huru Yehoyakini kutoka gerezani siku ya ishirini na saba ya mwezi wa kumi na mbili.
28 fro prisoun, and spak to hym benygneli; and he settide the trone of Joakyn aboue the trone of kyngis, that weren with hym in Babilonye.
Alizungumza naye kwa upole na kumpa kiti cha heshima zaidi kuliko wale wafalme wengine aliokuwa nao huko Babeli.
29 And he chaungide `hise clothis, whiche he hadde in prisoun; and he eet breed euer in the siyt of Euylmeradach, in alle the daies of his lijf.
Hivyo Yehoyakini akayavua mavazi yake ya mfungwa, na siku zote za maisha yake zilizobaki alikula mezani mwa mfalme.
30 Also Euylmeradach ordeynede sustenaunce `to hym with out ceessyng; which sustenaunce also was youun of the kyng to hym bi alle daies, and in alle the daies of his lijf.
Siku kwa siku mfalme alimpa Yehoyakini posho siku zote za maisha yake.

< 2 Kings 25 >