< 2 Kings 24 >

1 In the daies of hym Nabugodonosor, kyng of Babiloyne, stiede, and Joachym was maad seruaunt to hym by thre yeeris; and eft Joachym rebellide ayens hym.
Wakati wa utawala wa Yehoyakimu, Nebukadneza mfalme wa Babeli aliishambulia nchi, naye Yehoyakimu akawa mtumwa wake kwa miaka mitatu. Lakini hatimaye akabadili mawazo yake na kuasi dhidi ya Nebukadneza.
2 And the Lord sente to hym theuys of Caldeis, and theuys of Sirie, and theuys of Moab, and theuys of the sones of Amon; and he sente hem `in to Juda, that he schulde destrie it, bi the word of the Lord, which he spak bi hise seruauntis prophetis.
Bwana akatuma wavamiaji wa Wakaldayo, Waaramu, Wamoabu na Waamoni ili kumshambulia. Aliwatuma kuiangamiza Yuda sawasawa na neno la Bwana lililosemwa na watumishi wake manabii.
3 Forsothe this was doon bi the word of the Lord ayens Juda, that he schulde do awei it bifor him silf, for the synnes of Manasses, and alle thingis whiche he dide,
Hakika mambo haya yalitokea Yuda kulingana na agizo la Bwana, ili kuwaondoa kutoka machoni pake kwa sababu ya dhambi za Manase na yote aliyoyafanya,
4 and for the giltles blood which he sched out; and he fillide Jerusalem with the blood of innocentis; and for this thing the Lord nolde do mercy.
ikiwa ni pamoja na kumwaga damu isiyo na hatia. Kwa kuwa aliijaza Yerusalemu kwa damu isiyo na hatia, naye Bwana hakuwa radhi kusamehe.
5 Forsothe the residue of wordis of Joachim, and alle thingis whiche he dide, whether these ben not writun in the book of wordis of daies of the kyngis of Juda?
Matukio mengine ya utawala wa Yehoyakimu na yote aliyoyafanya, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Yuda?
6 And Joachym slept with hise fadris, and Joakyn, his sone, regnyde for him.
Yehoyakimu akalala pamoja na baba zake. Naye Yehoyakini mwanawe akawa mfalme baada yake.
7 And the kyng of Egipt addide no more to go out of hys lond; for the kyng of Babiloyne hadde take alle thingis that weren the kyngis of Egipt, fro the strond of Egipt `til to the flood Eufrates.
Mfalme wa Misri hakutoka tena katika nchi yake, kwa sababu mfalme wa Babeli alikuwa ameitwaa himaya yake yote, kuanzia Kijito cha Misri hadi Mto Frati.
8 Joakyn was of eiytene yeer, whanne he bigan to regne, and he regnyde thre monethis in Jerusalem; the name of his modir was Nahesta, douytir of Helnathan of Jerusalem.
Yehoyakini alikuwa na miaka kumi na minane alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu miezi mitatu. Jina la mama yake aliitwa Nehushta binti Elnathani kutoka Yerusalemu.
9 And he dide yuel bifor the Lord, bi alle thingis whiche hise fadir hadde do.
Akafanya maovu machoni pa Bwana, kama vile baba yake alivyokuwa amefanya.
10 In that tyme the seruauntis of Nabugodonosor, kyng of Babiloyne, stieden `in to Jerusalem, and the citee was cumpassid with bisegyngis.
Wakati huo, maafisa wa Nebukadneza mfalme wa Babeli walikuja ili kuishambulia Yerusalemu, nao wakaizunguka kwa jeshi.
11 And Nabugodonosor, kyng of Babiloyne, cam to the citee with hise seruauntis, that he schulde fiyte ayens it.
Nebukadneza mwenyewe akaupandia mji wakati maafisa wake walipokuwa wameuzunguka kwa jeshi.
12 And Joakyn, kyng of Juda, yede out to the king of Babiloyne, he, and his modir, and hise seruauntis, and hise princis, and hise chaumburleyns; and the king of Babiloyne resseyuede him, in the eiythe yeer of `his rewme.
Yehoyakini mfalme wa Yuda, mama yake, wahudumu wake, wakuu na maafisa wake wote wakajisalimisha kwa Nebukadneza. Katika mwaka wa nane wa utawala wa mfalme wa Babeli, akamchukua Yehoyakini kuwa mfungwa.
13 And he brouyte forth fro thens alle the tresours of the `hous of the Lord, and the tresours of the kingis hous; and he beet togider alle the goldun vessels, whiche Salomon, king of Israel, hadde maad in the temple of the Lord, bi the `word of the Lord.
Kama vile Bwana alivyokuwa amesema, Nebukadneza akaondoa hazina yote kutoka Hekalu la Bwana na kutoka jumba la mfalme, akavichukua vyombo vyote vya dhahabu ambavyo Solomoni mfalme wa Israeli alikuwa amevitengeneza kwa ajili ya Hekalu la Bwana.
14 And he translatide al Jerusalem, and alle the princis, and alle the strong men of the oost, ten thousynde, in to caitiftee, and ech crafti man, and goldsmyyt; and no thing was left, outakun the pore puplis of the lond.
Akawachukua watu wa Yerusalemu wote kwenda uhamishoni: yaani maafisa wote na mashujaa, watu wenye ustadi na ufundi, jumla yao watu elfu kumi. Watu maskini sana ndio tu waliobaki katika nchi.
15 Also he translatide Joakyn in to Babiloyne, and the moder of the king, `the wyues of the king, and the chaumburleyns of the king; and he ledde the iugis of the lond in to caitifte fro Jerusalem in to Babiloyne;
Nebukadneza akamchukua mateka Yehoyakini hadi Babeli. Pia akawachukua utumwani kutoka Yerusalemu hadi Babeli mama yake mfalme, wake zake, maafisa wake, na viongozi wote wa nchi.
16 and alle stronge men, seuene thousynde; and crafti men and goldsmyythis, a thousynde; alle stronge men and werriouris; and the king of Babiloyne ledde hem prisoners in to Babiloyne.
Mfalme wa Babeli pia akawahamishia Babeli mashujaa elfu saba, wenye nguvu na wanaofaa kupigana vita, na watu wenye ustadi na mafundi elfu moja.
17 And he ordeynede Mathanye, the brother of his fadir, for hym; and puttide to hym the name Sedechie.
Akamfanya Matania, ndugu wa baba yake Yehoyakini, kuwa mfalme mahali pake, na akalibadilisha jina lake kuwa Sedekia.
18 Sedechie hadde the oon and twentithe yeer of age, whanne he bigan to regne, and he regnyde eleuene yeer in Jerusalem; the name of his modir was Amychal, douyter of Jeremye of Lobna.
Sedekia alikuwa na umri wa miaka ishirini na mmoja alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu miaka kumi na mmoja. Jina la mama yake aliitwa Hamutali binti Yeremia, kutoka Libna.
19 And he dide yuel bifor the Lord, bi alle thingis which Joachym hadde do.
Alifanya maovu machoni pa Bwana, kama alivyofanya Yehoyakimu.
20 For the Lord was wrooth ayens Jerusalem, and ayens Juda, til he caste hem awey fro his face; and Sedechie yede awei fro the king of Babiloyne.
Ilikuwa ni kwa sababu ya hasira ya Bwana haya yote yalitokea Yerusalemu na Yuda, naye mwishoni akawaondoa mbele zake. Basi, Sedekia akaasi dhidi ya mfalme wa Babeli.

< 2 Kings 24 >