< 2 Kings 21 >

1 Manasses was of twelue yeer, whanne he bigan to regne, and he regnyde fyue and fifti yeer in Jerusalem; the name of his modir was Asiba.
Manase alikuwa na umri wa miaka kumi na mbili wakati alipoanza kutawala; alitawala miaka hamsini na tano katika Yerusalemu. Mama yake alikuwa anaitwa Hefziba.
2 And he dide yuel in the siyt of the Lord, bi the idols of hethene men, whiche hethene men the Lord dide awei fro the face of the sones of Israel.
Alifanya maovu usoni kwa Yahwe, kama machukizo ya mataifa ambayo Yahwe aliyafukuza nje mbele ya wana wa Israeli.
3 And he was turned, and bildide hiye thingis, whiche Ezechie, his fadir, distriede; and he reiside auteris of Baal, and he made woodis, as Achab kyng of Israel hadde do; and he worschipide `with out forth al the knyythod of heuene, and worschipide it in herte.
Kwa kupajenga tena mahala pa juu ambapo Hezekia baba yake alipaharibu, na akajenga madhabahu kwa ajili ya Baali, akafanya Ashera, kama Ahabu mfalme wa Israeli alivyofanya, akasujudu kwa nyota zote za mbinguni na kuwaabudu wao.
4 And he bildide auteris in the hows of the Lord, of which the Lord seide, Y schal sette my name in Jerusalem.
Manase akajenga madhabahu za kipagani kwenye nyumba ya Yahwe, ingawaje Yahwe aliamuru, “Jina langu litakuwa Yerusalemu daima.”
5 And he bildide auteris to al the knyythod of heuene in the twei large places of the temple of the Lord;
Akajenga madhabahu kwa ajili ya nyota zote za mbinguni katika behewa mbili za nyumba ya Yahwe.
6 and he `ledde ouer his sone thorouy the fier; and he vside false dyuynyngis in auteris, on whiche sacrifice was maad to feendis, and he kepte false dyuynyngis bi chiteryng of bryddis; and he made men to haue yuele spiritis spekynge in the wombe, and he multipliede false dyuynours in entraylis of beestis sacrified to feendis, that he schulde do yuel bifor the Lord, and terre hym to ire.
Akamuweka mtoto wake wa kiume kwenye moto; akatazama bao ushirikina na kujishuhulisha pamoja wale ambao wenye pepo wa utambuzi na wale wachawi. Akafanya maovu mengi usoni kwa Yahwe na kuchochea hasira kwa Mungu.
7 And he settide an ydol of wode, which he hadde maad, in the temple of the Lord, `of which temple the Lord spak to Dauid, and to Salomon, his sone, Y schal sette my name withouten ende in this temple, and in Jerusalem which Y chees of alle the lynagis of Israel.
Sanamu ya kuchongwa ya Ashera ambayo aliitnegeneza, akaiweka kwenye nyumba ya Yahwe. Nyumba hii ndiyo ambayo Yahwe alimwambia Daudi na Sulemani mwanawe; alisema: “Ni nyumba hii na katika Yerusalemu, ambayo nimeichagua kutoka makabila yote ya Isaraeli, ambako nitaliweka jina langu milele.
8 And Y schal nomore make the foot of Israel to be moued fro the lond which Y yaf to the fadris of hem; so netheles if thei kepen in werk alle thingis whiche Y comaundide to hem, and al the lawe whiche Moises, my seruaunt, comaundide to hem.
Sintofanya miguu ya Israeli kushindwa tena nje ya nchi ambayo niliwapa babu zao, kama tu watakuwa makini kutii yale yote niliyowaamuru, na kufuata sheria zote ambazo mtumishi wangu Musa aliwaamuru.”
9 Sotheli thei herden not, but weren disseyued of Manasses, that thei diden yuel ouer hethene men, whiche the Lord al to-brak fro the face of the sones of Israel.
Lakini watu hawakusikia, na Manase akawaongoza kufanya maovu zaidi kuliko yale ya mataifa ambayo Yahwe aliyaharibu mbele ya watu wa Israeli.
10 And the Lord spak in the hond of his seruauntis prophetis, and seide,
Basi Yahwe akaongea na watumishi wake manabii, akisema,
11 For Manasses, kyng of Juda, dide these worste abhomynaciouns ouer alle thingis which Ammorreis diden bifor hym, and maden also the puple of Juda to do synne in hise vnclennessis;
Kwasababu Manase mfalme wa Yuda amefanya haya machukizo, na kutenda maovu zaidi kuliko yote waliyoyatenda Waamori ambao walikuwa mbele yake walikubali, na pia aliwafanya Yuda kuasi kwa sanamu zake,
12 therfor the Lord God of Israel seith these thingis, Lo! Y schal brynge in yuelis on Jerusalem and Juda, that who euer herith, bothe hise eeris tyngle;
kwa hiyo Yahwe, Mungu wa Israeli, akasema hivi: Tazama, nakaribia kuleta uovu juu ya Yerusalemu na Yuda ambayo kila mtu asikiapo kuhusu hilo, masikio yake yote yatang'aa.
13 and Y schal holde forth on Jerusalem the corde of Samarie, and the birthun of the hows of Achab, and Y schal do awei Jerusalem, as tablis ben wont to be doon awei; and Y schal do awey and turne it, and Y schal lede ful ofte the poyntel on the face therof.
Nitanyoosha juu ya Yerusalemu kipimo kilichotumika dhidi ya Samaria, na kuangusha msatari utakaotumika dhidi ya nyumba ya Ahabu; Nitaifuta Yerusalemu safi, kama kufuta sahani, kuifuta na kuifunika juu chini.
14 Forsothe Y schal leeue relikis of myn eritage, and Y schal bitake hem in to the hond of enemyes therof; and thei schulen be in distriynge, and in raueyn to alle her aduersaries;
Nitawatupa masalia ya urithi wangu na kuwaweka mikononi mwa maadui zao. Watakuwa nyara na mateka kwa maadui zao wote,
15 for thei diden yuel bifor me, and thei continueden terrynge me to ire, fro the dai in which her fadris yeden out of the lond of Egipt `til to this day.
kwa sababu wamefanya yaliyo maovu usoni kwangu, na kunichochea hasira, tangu siku babu zao walipotoka Misri, hadi leo.”
16 Ferthermore also Manasses schedde ful myche ynnocent blood, til he fillide Jerusalem `til to the mouth, with outen hise synnes bi whiche he made Juda to do synne, to do yuel bifor the Lord.
Aidha, Manase akazimwaga damu nyingi za wasio na hatia, hadi alipoijaza Yerusalemu kutoka upande huu kwenda mwingine kwa kifo. Hii ilikuwa ni kuongeza kwenye dhambi ambayo aliifanya Yuda kuasi, wakati walipofanya uovu mbele za Yahwe.
17 Forsothe the residue of the wordis of Manasses, and alle thingis whiche he dide, and his synne whiche he synnede, whether these ben not writun in the book of wordis of daies of the kyngis of Juda?
Kama kwa mambo mengine yamhusuyo Manase, yote aliyoyafanya, na dhambi ambayo aliyoifanya, je haya hayajaandikwa kwenye kitabu cha matukio cha wafalme wa Yuda?
18 And Manasses slepte with hise fadris, and was biried in the gardyn of his hows, in the gardyn of Azam; and Amon, his sone, regnyde for hym.
Manase akalala pamoja na babu zake na alizikwa kwenye bustani ya nyumba yake, katika bustani ya Uza. Amoni mwanawe akawa mfalme katika sehemu yake.
19 He was of two and twenti yeer, whanne he bigan to regne; and he regnede twei yeer in Jerusalem; the name of his modir was Mesalamech, the douyter of Arus of Gethela.
Amoni alikuwa na miaka kumi na mbili alipoanza kutawala; alitawala miaka miwili katika Yerusalemu. Mama yake alikuwa anaitwa Meshlemethi; alikuwa binti wa Haruzi wa Yotba.
20 And he dide yuel in the siyt of the Lord, as Manasses, his fader, hadde do.
Alifanya yaliyo maovu usoni mwa Yahwe, kama manase baba yake alivyofanya.
21 And he yede in al the weie, bi which his fader hadde go, and he seruide to vnclennessis, to whiche his fadir hadde seruyd, and he worschipide tho; and he forsook the Lord God of hise fadris,
Amoni alifuata njia zote ambazo baba yake alizotembelea na kuabudu sanamu ambazo baba yake aliziabudu, na kuzisujudia.
22 and he yede not in the weye of the Lord.
Akajitenga na Yahwe, Mungu wa baba zake, na hakutembea katika njia ya Yahwe.
23 And hise seruauntis settiden tresouns to hym, and killiden the kyng in hise hows.
Watumishi wa Amoni wakafanya njama dhidi yake na kumuua mfalme kwenye nyumba yake mwenyewe.
24 Sothely the puple of the Lord smoot alle men, that hadden conspirid ayens kyng Amon, and thei ordeyneden to hem a kyng, Josias, `his sone, for hym.
Lakini watu wa nchi wakawaua watu wote waliofanya njama dhidi ya mfalme Amoni, na wakamfanya Yosia mtoto wake kuwa mfalme katika sehemu yake.
25 Forsothe the residue of wordis of Amon, whiche he dide, whether these ben not writun in the book of wordis of daies of the kyngis of Juda?
Kama ilivyo kwa mambo mengine yamhusuyo Amoni yale aliyoyafanya, je hayajaandikwa kwenye kitabu cha matukio ya wafalme wa Yuda?
26 And he slepte with hise fadris, and thei birieden hym in his sepulcre in the gardyn of Azam; and Josias, his sone, regnede for him.
Watu wakamzika kwenye kaburi lake katika bustani ya Uza, na Yosia mwanawe akawa mfalme katika sehemu yake.

< 2 Kings 21 >