< 2 Kings 15 >
1 In the seuenthe and twentithe yeer of Jeroboam, king of Israel, Azarie, sone of Amasie, kyng of Juda, regnede;
Katika mwaka wa ishirini na saba wa Yeroboamu mfalme wa Israeli, Azaria mwana wa Amazia mfalme wa Yuda akaanza kutawala.
2 he was of sixtene yeer, whanne he bigan to regne, and he regnede two and fifti yeer in Jerusalem; the name of his modir was Jecelia of Jerusalem.
Azaria alikuwa na umri wa miaka kumi na sita alipoanza kutawala, na alitawala kwa mda wa miaka hamsini na mbili katika Yerusalemu. Mama yake alikuwa anaitwa Yekolia, na alikuwa anatokea Yerusalemu.
3 And he dide that, that was plesaunt bifor the Lord, bi alle thingis which Amasie, his fadir, hadde do;
Alifanya yaliyo mema machoni pa Yahwe, kama baba yake Amazia alivyofanya.
4 netheles he distriede not hiy thingis; yit the puple made sacrifice, and brente encense in hiye thingis.
Lakini, mahali pa juu hapakuwa pameondolewa. Watu wakaendelea kutoa sadaka na kufukiza ubani katika mahala pa juu.
5 Forsothe the Lord smoot the kyng, and he was leprouse til in to the day of his deeth; and he dwellide in an hous freli bi hym silf. Sotheli Joathas, sone of the kyng, gouernde the palis, and demyde the puple of the lond.
Yhawe akampiga mfalme hivyo basi akawa na ukoma mpaka siku ya kifo chake na alikaa kwenye nyumba ya pekee. Yothamu, mtoto wa mfalme, alikuwa juu ya watu na kuwaongoza watu wa nchi.
6 Forsothe the residue of the wordis of Azarie, and alle thingis whiche he dide, whether these ben not writun in the book of wordis of daies of the kyngis of Juda?
Kama kwa mambo mengine yanayomhusu Azaria, yote aliyoyafanya, je hayajaandikwa kwenye kitabu cha matukio ya wafalme wa Yuda?
7 And Azarie slepte with hise fadris; and thei birieden hym with hise eldre men in the citee of Dauid; and Joathas, his sone, regnede for hym.
Hivyo Azaria alilala pamoja na babu zake katika mji wa Daudi. Yothamu, mtoto wake, akawa mfalme katika mahala pake.
8 In the eiyte and threttithe yeer of Azarie, kyng of Juda, Zacharie, sone of Jeroboam, regnede on Israel in Samarie sixe monethis.
Katika mwaka wa thelathini na nane mwaka wa Azaria mfalme wa Yuda, Zekaria mwana wa Yeroboamu akatawala juu ya Israeli katika Samaria kwa miezi sita.
9 And he dide that, that was yuel bifor the Lord, as his fadris diden; he departide not fro the synnes of Jeroboam, sone of Nabath, that made Israel to do synne.
Alifanya yaliyo maovu usoni mwa Yahwe, kama baba zake waliyoyafanya. Hakuziacha dhambi za Yeroboamu mwana wa Nabeti, ambaye alisababisha Israeli kuasi
10 Forsothe Sellum, the sone of Jabes, conspiride ayens hym in Samarie; and Sellum smoot hym opynli, and killide hym, and regnede for hym.
Shalumu mwana wa Yabeshi akafanya njama dhidi ya Zekaria, akamshambulia katika Ibleamu, na kumuua. Kisha akawa mfalme katika mahala pake.
11 Sotheli the residue of the wordis of Zacharie, whethir these ben not writun in the book of wordis of daies of the kyngis of Israel?
Kama kwa mambo mengine yanayomuhusu Zekaria, yameandikwa kwenye kitabu cha matukio ya wafalme wa Israeli.
12 Thilke is the word of the Lord, which he spak to Hieu, and seide, `Thi sones `til to the fourthe generacioun schulen sitte `of thee on the trone of Israel; and it was doon so.
Hili ndilo lililokuwa neno la Yahwe ambalo aliongea na Yehu, kusema, “Kizazi chako kitakaa katika kiti cha Israeli mpaka kizazi cha nne.” Hiyo ikatokea.
13 Sellum, sone of Jabes, regnede in the nynthe and thritty yeer of Azarie, kyng of Juda; sotheli he regnyde o monethe in Samarie.
Shalumu mwana wa Yabeshi akaanza kutawala katika mwaka wa thelathini na tisa wa Azaria mfalme wa Yuda, na kutawala kwa mwezi mmoja tu katika Samaria.
14 And Manaheu, the sone of Gaddi, styede fro Thersa, and cam in to Samarie; and he smoot Sellum, sone of Jabes, in Samarie, and killide hym, and regnede for hym.
Menahemu mwana wa Gadi akapanda kutoka Tirza kwenda Samaria. Akamshambulia Shalumu mwana wa Yabeshi hapo, katika Samria. Akamuua na kuwa mfalme katika mahali pake.
15 Sotheli the residue of wordis of Sellum, and his conspirasie, bi which he settide tresouns, whether these ben not writun in the book of wordis of daies of the kyngis of Israel.
Kama kwa mambo mengine yanayomuhusu Shalumu na njama aliyoifanya, yameandikwa kwenye kitabu cha matukio cha wafle wa Israeli.
16 Thanne Manaheu smoot Capham, and alle men that weren thereynne, and the termes therof fro Thersa, for thei nolden opyn to hym; and he killide alle wymmen therof with child, and karf hem.
Ndipo Menahemu akamshambulia Tifsa na wote waliokuwa pale, na mipaka yote kuzunguka Tizra, kwasababu hawakufungua kwenye mji. Hivyo akaushambulia, na akawapasua wanawake wajawazito wote katika hicho kijiji.
17 In the nynthe and thrittithe yeer of Azarie, kyng of Juda, Manaheu, sone of Gaddi, regnede on Israel ten yeer in Samarie.
Katika mwaka wa thelathini na tisa wa Ahazia mfalme wa Yuda, Menahemu mwana wa Gadi akaanza kutawala; alitawala kwa miaka kumi katika Samaria.
18 And he dide that, that was yuel bifor the Lord; he departide not fro the synnes of Jeroboam, sone of Nabath, that made Israel to do synne.
Alifanya yaliyo maovu usoni mwa Yahwe. Katika maisha yake yote, hakuziacha dhambi za Yeroboamu mwana wa Nabeti, ambaye alifanya Israeli kufanya dhambi.
19 In alle the daies of hym Phul, the kyng of Assiries, cam in to Thersa. And Manaheu yaf to Phul a thousynde talentis of siluer, that he schulde be to hym in to help, and schulde make stidefast his rewme;
Kisha Pulu mfalme wa Ashuru akaja kinyume cha nchi, na Menahemu akampatia Pulu talanta elfu moja za fedha, hivyo msaada wa Pulu ungeweza kuwa na yeye kuimarisha utawala wa Israeli katika nchi yake.
20 and Manaheu settide taliage of siluer on Israel to alle myyti men and riche, that he schulde yyue to the kyng of Assiries; he settide fifti siclis of siluer bi alle men; and the king of Assiries turnede ayen, and dwellide not in Thersa.
Menahemu akatoza hii pesa kutoka Israeli kwa kumtaka kila mtu tajiri alipe shekeli hamsini za fedha kwake kumpatia mfalme wa Ashura. Hivyo mfalme wa Ashuru akarudi na hakukaa pale katika ile nchi.
21 Forsothe the residue of wordis of Manaheu, and alle thingis whiche he dide, whether these ben not wrytun in the book of wordis of daies of the kyngis of Israel?
Kama kwa mabo mengine yanayomuhusu Menahemu, na yote aliyoyafanya, je hayajaandikwa kwenye kitabu cha matukio ya waflme wa Israeli?
22 And Manaheu slepte with hise fadris; and Phaceia, his sone, regnyde for hym.
Hivyo Menahemu akalala pamoja na babu zake, na Pekahia mtoto wake akawa mfalme katika mahala pake.
23 In the fiftithe yeer of Azarie, kyng of Juda, Phaceia, sone of Manaheu, regnede on Israel in Samarie twei yeer.
Katika mwaka wa hamsini wa Azaria mfalme wa Yuda, Pekahia mwana wa Menahemu akaanza kutawala juu ya Israeli katika Samaria; alitawala kwa muda wa miaka miwili.
24 And he dide that, that was yuel bifor the Lord; he departide not fro the synnes of Jeroboam, sone of Nabath, that made Israel to do synne.
Alifanya yaliyo maovu usoni pa Yahwe. Hakuziacha dhambi za Yeroboamu mwana wa Nabeti, ambazo kwa hizo alisababisha Israeli kufanya dhambi.
25 Forsothe Phacee, sone of Romelie, duyk of his oost, conspiride ayens hym, and smoot hym in Samarie, in the tour of the kyngis hous, bisidis Argob, and bisidis Arib; `and he smoot hym with fifti men of the sones of Galaditis; and Phacee killide hym, and regnede for hym.
Pekahia alikuwa na afisa aliyekuwa anaitwa Peka mwana wa Remalia, ambaye alifanya njama dhidi yake. Pamoja na watu hamsini wa Gileadi, Peka akamuua Pekahia pamoja na Argobu na Arie katika Samaria, katika ngome ya nyumba ya mfalme. Peka akamuua alipomua Pekahia akawa mfalme katika mahala pake.
26 Sotheli the residue of wordis of Phacee, and alle thingis whiche he dide, whether these ben not writun in the book of wordis of daies of the kyngis of Israel?
Kama kwa mambo mengine yanayomuhusu Pekahia, yote aliyoyafanya, yameandikwa kwenye kitabu cha matukio ya wafalme wa Israeli.
27 In the two and fiftithe yeer of Azarie, kyng of Juda, Phasee, sone of Romelie, regnyde in Samarie twenti yeer.
Katika mwaka wa hamsini na mbili wa Azia mfalme wa Yuda, Peka mwana wa Remalia akaanza kutawala juu ya Israeli katika Samaria; alitawala miaka Ishirini.
28 And he dide that, that was yuel bifor the Lord; and he departide not fro the synnes of Jeroboam, sone of Nabath, that made Israel to do synne.
Alifanya yaliyo maovu usoni mwa Yahwe. Hakuziacha dhambi za Yeroboamu mwana wa Nabati, ambaye alisababisha Israeli kufanya dhambi.
29 In the daies of Phacee, kyng of Israel, Teglat Phalasar, kyng of Assur, cam, and took Aion, and Aibel, the hows of Maacha, and Janoe, and Cedes, and Asor, and Galaad, and Galilee, and al the lond of Neptalym; and translatide hem in to Assiriens.
Katika siku za Peka mfalme wa Israeli, Tiglath Pileseri mfalme wa Ashuru akaja na kuichukua Iyoni, Abel Beth Maaka, Yanoa, Kadeshi, Hazori, Gileadi, na nchi yote ya Naftali. Akawachukua hao watu hadi Ashuru.
30 Forsothe Osee, sone of Hela, conspiride, and settide tresouns ayens Phasee, sone of Romelie, and smoot hym, and killide hym; and he regnyde for hym, in the twentithe yeer of Joathan, sone of Ozie.
Hivyo Hoshea mwana wa Ela akafanya njama dhidi ya Peka mwana wa Remalia. Akaishambulia na kisha kumuua. Kisha akawa mfalme katika mahali pake, katika mwaka wa ishirini wa Yothamu mwana wa Uzia.
31 Forsothe the residue of wordis of Phacee, and alle thingis whiche he dide, whether these ben not writun in the book of wordis of daies of the kyngis of Israel?
Kama kwa mambo mengine yanayomuhusu Peka, yote aliyoyafanya, yameandikwa kwenye kitabu cha matukio ya wafalme wa Israeli.
32 In the secounde yeer of Phacee, sone of Romelie, kyng of Israel, Joathan, sone of Ozie, kyng of Juda, regnyde;
Katika mwaka wa pili wa Peka mwana wa Remalia, mfalme wa Israeli, Yothamu mwana wa Azaria, mfalme wa Yuda akaanza kutawala.
33 he was of fyue and twenti yeer, whanne he bigan to regne, and he regnede sixtene yeer in Jerusalem; the name of his modir was Jerusa, the douyter of Sadoch.
Alikuwa na umri wa miaka ishirini alipoanza kutawala; alitawala kwa muda wa miaka kumi na sita katika Yerusalimu. Mama yake alikuwa anaitwa Yerusha; alikuwa binti ya Sadoki.
34 And he dide that, that was plesaunt bifor the Lord; he wrouyte bi alle thingis, whiche his fadir Ozie hadde do;
Yotahmu alifanya yaliyo sahihi usoni pa Yahwe. Alifuata mfano wa yote baba yake Azaria aliyofanya.
35 netheles he dide not awey hiy thingis; yit the puple made sacrifice, and brente incense in hiy thingis; he bildide the hiyeste yate of the hows of the Lord.
Ila, mahali pa juu hapakuchukuliwa. Watu walikuwa wakitio sadaka na kufukiza ubani katika mahali pa juu. Yothamu akajenga lango la juu la nyumba ya Yahwe.
36 Forsothe the residue of wordis of Joathan, and alle thingis whiche he dide, whether these ben not writun in the book of wordis of daies of the kyngis of Juda?
Kama kwa mambo mengine yanayomuhusu Yothamu, na yote aliyoyafanya, je yameandikwa katika kitabu cha matukio ya wafalme wa Yuda?
37 In tho daies the Lord bigan to sende in to Juda Rasyn, the kyng of Sirie, and Phacee, the sone of Romelie.
Katika zamani hizo Yahwe akaanza kumtuma dhidi ya Yuda Rezini mfalme wa Sahmu, na Peka mwana wa Remalia.
38 And Joathan slepte with hise fadris, and was biried with hem in the citee of Dauid, his fadir; and Achaz, his sone, regnyde for hym.
Yothamu akalala pamoja na babu zake na akazikwa pamoja na babu zake katika mji wa Daudi, babu yake. Kisha Ahazi, mtoto wake, akwa mfalme katika mhali pake.