< 2 Chronicles 27 >
1 Joathan was of fyue and twenti yeer, whanne he bigan to regne, and he regnede sixtene yeer in Jerusalem; the name of his modir was Jerusa, the douyter of Sadoch.
Yothamu alikuwa na umri wa miaka ishirini na mitano alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu miaka kumi na sita. Mama yake aliitwa Yerusha binti Sadoki.
2 He dide that, that was riytful bifor the Lord, bi alle thingis whiche Ozie, his fadir, hadde do; outakun that he entride not in to the temple of the Lord, and the puple trespasside yit.
Akafanya yaliyo mema machoni pa Bwana kama Uzia baba yake alivyokuwa amefanya, lakini tofauti na yeye, hakuingilia huduma za hekaluni mwa Bwana. Lakini hata hivyo, watu wakaendelea na desturi zao mbaya.
3 He bildide the hiy yate of the hous of the Lord, and he bildide manye thingis in the wal of Ophel;
Yothamu akajenga upya Lango la Juu la Hekalu la Bwana na kufanya kazi kubwa kwenye ukuta katika kilima cha Ofeli.
4 also he bildide citees in the hillis of Juda, and he bildide castels and touris in forestis.
Akajenga miji katika vilima vya Yuda pamoja na ngome na minara mwituni.
5 He fauyt ayens the kyng of the sones of Amon, and ouercam hym; and the sones of Amon yauen to hym in that tyme an hundrid talentis of siluer, and ten thousynde choris of barli, and so many of wheete; the sones of Amon yauen these thingis to hym in the secounde and in the thridde yeer.
Yothamu akafanya vita na mfalme wa Waamoni na kumshinda. Mwaka ule Waamoni wakamlipa talanta 100 za fedha, kori 10,000 za ngano na kori 10,000 za shayiri. Waamoni wakamletea kiasi hicho hicho mwaka wa pili na wa tatu.
6 And Joathan was maad strong, for he hadde dressid hise weies bifor `his Lord God.
Yothamu akaendelea kuwa na nguvu kwa sababu alienenda kwa ukamilifu mbele za Bwana Mungu wake.
7 Forsothe the residue of wordis of Joathan, and alle hise batels, and werkis, ben writun in the book of kyngis of Israel and of Juda.
Matukio mengine ya utawala wa Yothamu, pamoja na vita vyake vyote na vitu vingine alivyofanya, vimeandikwa katika kitabu cha wafalme wa Israeli na Yuda.
8 He was of fyue and twenti yeer, whanne he bigan to regne, and he regnede sixtene yeer in Jerusalem.
Alikuwa na umri wa miaka ishirini na mitano alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu miaka kumi na sita.
9 And Joathan slepte with hise fadris, and thei birieden hym in the citee of Dauid; and Achaz, his sone, regnede for him.
Yothamu akalala na baba zake na akazikwa katika Mji wa Daudi. Naye Ahazi mwanawe akawa mfalme baada yake.