< 1 Timothy 3 >

1 A feithful word. If ony man desirith a bishopriche, he desirith a good werk.
Hili ni neno la kuaminiwa, kwamba mtu akitamani kazi ya uangalizi, atamani kazi nzuri.
2 Therfor it bihoueth a byschop to be with out repreef, the hosebonde of o wijf, sobre, prudent, chast, vertewous, holdinge hospitalite, a techere;
Basi, imempasa mwangalizi awe mtu asiye na lawama, mume wa mke mmoja, mwenye kiasi, anayejitawala, anayeheshimika, mkarimu, ajuaye kufundisha,
3 not youun myche to wyn, not a smytere, but temperat, not ful of chiding, not coueitouse, wel reulinge his hous,
asiwe mlevi, wala mkali bali awe mpole, asiwe mgomvi wala mpenda fedha.
4 and haue sones suget with al chastite;
Lazima aweze kuisimamia nyumba yake mwenyewe vizuri na kuhakikisha kwamba watoto wake wanamtii na kuwa na heshima kwa kila njia.
5 for if ony man kan not gouerne his house, hou schal he haue diligence of the chirche of God? not new conuertid to the feith,
(Kwa maana kama mtu hajui jinsi ya kusimamia nyumba yake mwenyewe, atawezaje kuliangalia kanisa la Mungu?)
6 lest he be borun vp in to pride, and falle in to doom of the deuel.
Asiwe mtu aliyeokoka karibuni asije akajivuna na kuangukia kwenye hukumu ile ile ya ibilisi.
7 For it bihoueth hym to haue also good witnessing of hem that ben with outforth, that he falle not in to repreef, and in to the snare of the deuel.
Inampasa pia awe na sifa njema kwa watu walio nje, ili asije akalaumiwa na kuanguka kwenye mtego wa ibilisi.
8 Also it bihoueth dekenes to be chast, not double tungid, not youun myche to wyn, not suynge foul wynnyng;
Vivyo hivyo, mashemasi nao wawe watu wanaostahili heshima, wasiwe wenye kauli mbili au wenye kujifurahisha kwa mvinyo, wala wanaotamani faida isiyo halali.
9 that han the mysterie of feith in clene conscience.
Inawapasa kushikamana sana na ile siri ya imani kwa dhamiri safi.
10 But be thei preued first, and mynystre so, hauynge no cryme.
Ni lazima wapimwe kwanza; kisha kama hakuna neno dhidi yao, basi na waruhusiwe kuhudumu kama mashemasi.
11 Also it bihoueth wymmen to be chast, not bacbitinge, sobre, feithful in alle thingis.
Vivyo hivyo, wake zao wawe wanawake wanaostahili heshima, wasio wasingiziaji, bali wawe na kiasi na waaminifu katika kila jambo.
12 Dekenes be hosebondis of o wijf; whiche gouerne wel her sones and her housis.
Shemasi awe mume wa mke mmoja na inampasa aweze kusimamia watoto wake na watu wa nyumbani mwake vyema.
13 For thei that mynystren wel, schulen gete a good degre to hem silf, and myche triste in the feith, that is in Crist Jhesu.
Wale ambao wamehudumu vyema katika huduma ya ushemasi hujipatia msimamo bora na ujasiri mkubwa katika imani yao ndani ya Kristo Yesu.
14 Sone Timothe, Y write to thee these thingis, hopinge that Y schal come soon to thee;
Ingawa ninatarajia kuja kwako hivi karibuni, ninakuandikia maagizo haya sasa ili kwamba,
15 but if Y tarie, that thou wite, hou it bihoueth thee to lyue in the hous of God, that is the chirche of lyuynge God, a pilere and sadnesse of treuthe.
kama nikikawia, utajua jinsi iwapasavyo watu kuenenda katika nyumba ya Mungu, ambayo ndiyo kanisa la Mungu aliye hai, lililo nguzo na msingi wa kweli.
16 And opynli it is a greet sacrament of pitee, that thing that was schewid in fleisch, it is iustified in spirit, it apperid to aungels, it is prechid to hethene men, it is bileuyd in the world, it is takun vp in glorie.
Bila shaka yoyote, siri ya utauwa ni kubwa: Alidhihirishwa katika mwili wa kibinadamu, akathibitishwa kuwa na haki katika Roho, akaonekana na malaika, akahubiriwa miongoni mwa mataifa, akaaminiwa ulimwenguni, akachukuliwa juu katika utukufu.

< 1 Timothy 3 >