< 1 Samuel 30 >

1 And whanne Dauid and hise men hadden come `in to Sichelech in the thridde dai, men of Amalech hadden maad asauyt on the south part in Sichelech; and thei smytiden Sichelech, and brenten it bi fier.
Daudi na watu wake wakafika Siklagi siku ya tatu. Basi Waamaleki walikuwa wamevamia Negebu na Siklagi. Wakawa wameshambulia mji wa Siklagi na kuuteketeza kwa moto,
2 And thei ledden the wymmen prisoneris fro thennus, fro the leeste `til to the grete; and thei hadden not slayn ony, but thei ledden with hem, and yeden in her weie.
nao wakawa wamewachukua mateka wanawake pamoja na wote waliokuwamo humo, vijana na wazee. Hawakuua yeyote, bali waliwachukua wakaenda zao.
3 Therfor whanne Dauid and hise men hadde come to the citee, and hadden founde it brent bi fier, and that her wyues, and her sones, and douytris weren led prisoneris,
Daudi na watu wake walipofika Siklagi, wakakuta mji umeangamizwa kwa moto na wake zao pamoja na wana wao na binti zao wamechukuliwa mateka.
4 Dauid and the puple that was with hym reisiden her voices, and weiliden, til teeris failiden in hem.
Hivyo Daudi na watu wake wakapiga yowe mpaka wakaishiwa na nguvu za kulia.
5 Forsothe also twei wyues of Dauid weren led prisoneris, Achynoem of Jezrael, and Abigail, the wijf of Nabal of Carmele.
Wake wawili wa Daudi walikuwa wametekwa: yaani Ahinoamu wa Yezreeli, na Abigaili, mjane wa Nabali wa Karmeli.
6 And Dauid was ful sori; forsothe al the puple wold stone hym, for the soule of ech man was bittir on her sones and douytris. Forsothe Dauid was coumfortid in his Lord God.
Daudi alihuzunika sana kwa sababu watu walikuwa wakisemezana juu ya kumpiga kwa mawe. Kila mmoja alikuwa na uchungu rohoni kwa sababu ya wanawe na binti zake. Lakini Daudi akajitia nguvu katika Bwana, Mungu wake.
7 And he seide to Abiathar, preest, the sone of Achymelech, Bringe thou ephoth to me. And Abiathar brouyte ephoth to Dauid; and Dauid councelide the Lord,
Kisha Daudi akamwambia kuhani Abiathari mwana wa Ahimeleki, “Niletee kisibau.” Abiathari akamletea,
8 and seide, Schal Y pursue, ether nay, `these theues? and schal Y take hem? And the Lord seide to hym, Pursue thou; for with out doute thou schalt take hem, and thou schalt take awey the prey.
naye Daudi akamuuliza Bwana, “Je, nifuatie kundi hili la wavamizi? Je, nitawapata?” Bwana akajibu, “Wafuatie. Hakika utawapata na utafanikiwa kuwaokoa.”
9 Therfor Dauid yede, he and sixe hundrid men that weren with hym, and thei camen `til to the stronde of Besor; and sotheli the wery men abididen.
Daudi pamoja na watu wake 600 wakafika kwenye Bonde la Besori, mahali ambapo wengine waliachwa nyuma,
10 Forsothe Dauid pursuede, he and foure hundrid men; for twei hundrid abididen, that weren weeri, and myyten not passe the stronde of Besor.
kwa kuwa watu 200 walikuwa wamechoka sana kuweza kuvuka hilo bonde. Lakini Daudi pamoja na watu 400 wakaendelea kufuatia.
11 And thei founden a man of Egipte in the feeld, and thei brouyten hym to Dauid; and thei yauen `breed to hym, that he schulde ete, and `schulde drynke watir;
Wakamkuta Mmisri katika shamba fulani, nao wakamleta kwa Daudi. Wakampa huyo Mmisri maji ya kunywa na chakula;
12 but also thei yauen to hym a gobet of a bundel of drye figis, and twei byndyngis of dried grapis. And whanne he hadde ete tho, his spirit turnede ayen, and he was coumfortid; for he hadde not ete breed, nether hadde drunk watir in thre daies and thre nyytis.
kipande cha andazi la tini na andazi la zabibu zilizokaushwa. Akala naye akapata nguvu, kwa kuwa hakuwa amekula chakula chochote wala kunywa maji kwa siku tatu usiku na mchana.
13 Therfor Dauid seide to hym, Whos man art thou, ethir fro whennus and whidur goist thou? And he seide, Y am a child of Egipt, the seruaunt of a man of Amalech; forsothe my lord forsook me, for Y bigan to be sijk the thridde dai ago.
Daudi akamuuliza, “Wewe ni wa nani, na umetoka wapi?” Akajibu, “Mimi ni Mmisri, mtumwa wa Mwamaleki. Bwana wangu alinitelekeza nilipougua siku tatu zilizopita.
14 Sotheli we braken out to the south coost of Cerethi, and ayens Juda, and to the south of Caleb, and we brenten Sichelech bi fier.
Tulivamia Negebu ya Wakerethi, na nchi ya Yuda, na Negebu ya Kalebu. Nasi tulichoma moto Siklagi.”
15 And Dauid seide to hym, Maist thou lede me to this cumpeny? Which seide, Swere thou to me bi God, that thou schalt not sle me, and schalt not bitake me in to the hondis of my lord; and Y schal lede thee to this cumpeny. And Dauid swoor to hym.
Daudi akamuuliza, “Je, unaweza kuniongoza kufikia kundi hili la uvamizi?” Akajibu, “Niapie mbele ya Mungu kwamba hutaniua wala kunikabidhi mikononi mwa bwana wangu, nami nitakupeleka hadi waliko.”
16 And whanne the child hadde ledde hym, lo! thei saten at the mete, on the face of al the erthe, etynge and drynkynge, and as halewynge a feeste, for al the prey and spuylis whiche thei hadden take of the lond of Filisteis, and of the lond of Juda.
Akamwongoza Daudi mpaka mahali walipokuwa, nao walikuwa wametawanyika eneo lote, wakila, wakinywa na wakifanya karamu kwa sababu ya nyara nyingi walizochukua kutoka nchi ya Wafilisti na kutoka Yuda.
17 And Dauid smoot hem fro euentid `til to euentid of the tothir dai, and not ony of hem escapide, no but foure hundrid yonge men, that stieden on camels, and fledden.
Daudi akapigana nao kuanzia machweo ya jua hadi kesho yake jioni, na hakuna yeyote miongoni mwao aliyetoroka, isipokuwa vijana wanaume 400 waliopanda ngamia na kutoroka.
18 Forsothe Dauid delyuerede alle thingis whiche the men of Amalech token, and he delyuerede hise twei wyues;
Daudi akarudisha kila kitu Waamaleki walikuwa wamechukua, pamoja na wake zake wawili.
19 nether ony of hem failide fro litil `til to greet, as wel of sones as of douytris, and of spuylis; and what euer thingis thei hadden rauyschid, Dauid ledde ayen alle thingis;
Hakuna chochote kilichopotea: kijana au mzee, mvulana au msichana, nyara au kitu kingine chochote walichokuwa wamechukua. Daudi akarudisha kila kitu.
20 and he took alle flockis and grete beestis, and droof bifor his face. And thei seiden, This is the prey of Dauid.
Akachukua makundi yote ya kondoo, mbuzi na ngʼombe, nao watu wake wakawaswaga wanyama hao mbele ya wanyama wengine wa kufugwa, wakisema, “Hizi ni nyara za Daudi.”
21 Forsothe Dauid cam to twei hundrid men, that weren weeri, and abididen, and myyten not sue Dauid; and he hadde comaundid hem to sitte in the stronde of Besor; whiche yeden out ayens Dauid, and the puple that was with hym. Forsothe Dauid neiyede to the puple, and grette it pesibli.
Kisha Daudi akafika kwa wale watu 200 waliokuwa wamechoka sana kumfuata na ambao waliachwa nyuma kwenye Bonde la Besori. Wakatoka kwenda kumlaki Daudi na wale watu aliokuwa nao. Daudi na watu wake walipowakaribia, akawasalimu.
22 And o man, the werste and vniust of the men that weren with Dauid, answeride, and seide, For thei camen not with vs, we schulen not yyue to hem ony thing of the prey, which we rauyschiden, but his wijf and children `suffice to ech man; and whanne thei han take hem, go thei awei.
Lakini watu wote waovu na wakorofi miongoni mwa wafuasi wa Daudi wakasema, “Kwa sababu hawakwenda pamoja nasi, hatutagawana nao nyara tulizorudisha. Lakini, kila mtu aweza kuchukua mkewe na watoto wake na kuondoka.”
23 Forsothe Dauid seide, My britheren, ye schulen not do so of these thingis, whiche the Lord yaf to vs, and kepte vs, and yaf the theues, that braken out ayens vs, in to oure hondis;
Daudi akajibu, “La hasha, ndugu zangu, kamwe hamwezi kufanya hivyo kwa kile ambacho Bwana ametupatia. Yeye ametulinda na kuweka mikononi mwetu majeshi yale yaliyokuja kupigana dhidi yetu.
24 nether ony man schal here vs on this word. For euene part schal be of him that goith doun to batel, and of hym that dwellith at the fardelis; and in lijk maner thei schulen departe.
Ni nani atasikiliza yale mnayosema? Fungu la mtu aliyekaa na vyombo litakuwa sawa na la yule aliyekwenda vitani. Wote watashiriki sawa.”
25 And this was maad a constitucioun and doom fro that dai and afterward, and as a lawe in Israel til in to this dai.
Daudi akafanya hili liwe amri na agizo kwa Israeli kutoka siku ile hata leo.
26 Therfor Dauid cam in to Sichelech, and sente yiftis of the prey to the eldere men of Juda, hise neiyboris, and seide, Take ye blessyng of the prey of enemyes of the Lord;
Daudi alipofika Siklagi, akatuma baadhi ya nyara kwa wazee wa Yuda, waliokuwa rafiki zake, akasema, “Tazama, hapa kuna zawadi kwa ajili yenu kutoka nyara za adui za Bwana.”
27 to hem that weren in Bethel, and that weren in Ramoth, at the south,
Akazituma kwa wale waliokuwa Betheli, Ramoth-Negebu na Yatiri;
28 and that weren in Jether, and that weren in Aroer, and that weren in Sephamoth, and that weren in Escama, and that weren in Rethala,
kwa wale walioko Aroeri, Sifmothi, Eshtemoa
29 and that weren in the citees of Jeramel, and that weren in the citees of Ceny,
na Rakali; kwa wale waliokuwa katika miji ya Wayerameeli na ya Wakeni;
30 and that weren in Arama, and that weren in Lautuasam, and that weren in Athec,
na kwa wale walioko Horma, Bori-Ashani, Athaki,
31 and that weren in Ebron, and to othere men, that weren in these places, in whiche Dauid dwellide and hise men.
na kwa wakazi wa Hebroni; na kwa wale waliokuwa mahali pengine pote ambako Daudi na watu wake walitembelea.

< 1 Samuel 30 >