< 1 Samuel 24 >

1 And whanne Saul turnede ayen, aftir that he pursuede Filisteis, thei telden to hym, and seiden, Lo! Dauid is in the deseert of Engaddi.
Sauli aliporudi kuwafukuza Wafilisti, akaambiwa kwamba, “Daudi yuko katika jangwa la Engedi.”
2 Therfor Saul took three thousinde of chosun men of al Israel, and yede to seke Dauid and hise men, yhe on moost brokun rochis, that ben `able to weie to wield geet aloone.
Ndipo Sauli akachukua watu elfu tatu waliochaguliwa kutoka Iraeli yote, wakaenda kumtafuta Daudi na watu wake katika miamba ya Mbuzi Mwitu.
3 And he cam to the fooldis of scheep, that offriden hem silf to the wei goere. And there was a denne, in to which denne Saul entride, that he schulde purge the wombe; forsothe Dauid and hise men weren hid in the ynnere part of the denne.
Akafika penye mazizi ya kondoo kando ya njia, mahali palipokuwa na pango. Sauli akaingia ndani yake kujisaidia. Wakati huo Daudi na watu wake walikuwa wamekaa mbali zaidi ndani ya pango lilelile.
4 And the seruauntis of Dauid seiden to hym, Lo! the dai of which the Lord spak to the, Y schal bitake to thee thin enemy, that thou do to hym as it plesith in thin iyen. Therfor Dauid roos, and kittide the hemme of the mentil of Saul priuely.
Watu wake Daudi wakamwambia, “Hii ndiyo siku ambayo BWANA aliisema akikuambia, 'Nitamweka adui wako mkononi mwako, ili umtendee kama unavyotaka.”' Kisha Daudi akainuka na kumnyemelea kwa mbele kimya kimya na kulikata pindo la kanzu ya Sauli.
5 Aftir these thingis Dauid smoot his herte, for he hadde kit awei the hemme of the mentil of Saul.
Baadaye moyo wa Daudi ukamchoma kwa sababu alilikata pindo la kanzu ya Sauli.
6 And Dauid seide to hise men, The Lord be merciful to me, lest Y do this thing to my lord, the crist of the Lord, that Y sende myn hond `in to hym, for he is the crist of the Lord. The Lord lyueth, for no but the Lord smyte hym, ether his dai come, that he die, ether he go doun in to batel and perische, the Lord be merciful to me, that Y sende not myn hond in to the crist of the Lord.
Akawaambia watu wake, “BWANA anisamehe, sikupaswa kumtendea jambo hili bwana wangu, Mtiwa mafuta wa BWANA, kwa kunyoosha mkono wangu juu yake, maana yeye ni masihi wa BWANA.”
7 Forsothe Saul roos out of the denne, and yede in the weie bigunnun.
Hivyo Daudi akawakemea watu wake kwa maneno haya, na kuwazuia wasimpige Sauli. Sauli akasimama, akatoka pangoni, na kwenda zake.
8 Sotheli Dauid roos aftir hym, and he yede out of the denne, and criede aftir the bak of Saul, and seide, My lord, the kyng! And Saul bihelde bihinde him silf; and Dauid bowide hym silf lowe to the erthe, and worschipide.
Baadaye tena, Daudi akasimama juu, akatoka pangoni, na kumwita Sauli: “Bwana wangu mfalme.” Sauli alipotazama nyuma, Daudi akasujudu hadi chini na kuonyesha heshima.
9 And he seide to Saul, Whi herist thou the wordis of men spekynge, Dauid sekith yuel ayens thee?
Daudi akamwambia Sauli, “Kwa nini unawasikiliza watu ambao wanasema, “Angalia, Daudi anatafuta kukudhuru?'
10 Lo! to dai thin iyen siyen, that the Lord bitook thee in myn hond in the denne, and Y thouyte that Y wolde sle thee, but myn iye sparide thee; for Y seide, Y schal not holde forth myn hond in to my lord, which is the crist, `that is, anoyntid, of the Lord.
Leo macho yako yameona jinsi BWANA alivyokuweka mkononi mwangu tulipokuwa ndani ya pango. Wengine waliniambia nikuuwe, lakini nilikuacha hai. Nikasema, 'Sitanyoosha mkono wangu juu ya bwana wangu; kwa kuwa ni masihi wa BWANA.'
11 But rathere, my fadir, se thou, and knowe the hemme of thi mentil in myn hond, for whanne Y kittide aweie the hemme of thi mentil, Y nolde holde forth myn hond in thee; perseyue thou, and see, for nether yuel nether wickidnesse is in myn hond, nether Y synnede ayens thee; but thou aspiest my lijf, that thou do it awei.
Tazama, baba yangu, angalia pindo la kanzu yako mkononi mwangu. Kwa maana kama nilikata pindo la kanzu yako na sikukuua, basi ujuwe na uone kwamba sina uovu au kosa katika mkono wangu, na sijafanya dhambi juu yako, ingawa unawinda kuutoa uhai wangu.
12 The Lord deme bitwixe me and thee, and the Lord venge me of thee; but myn hond be not in thee,
BWANA aamue kati yangu na wewe, na BWANA anilipizie kisasi juu yako, lakini mkono wangu kamwe hautakuwa juu yako.
13 as it is seid also in eld prouerbe, Wickidnesse schal go out of wickid men; therfor myn hond be not in thee.
Kama mithali ya wazee isemavyo, 'Katika waovu hutoka uovu.' Lakini mkono wangu hautakuwa juu yako.
14 `Whom pursuest thou, kyng of Israel, whom pursuest thou? Thou pursuest a deed hound, and a quyk fle.
Mfalme wa Israeli ametoka kumuandama nani? Unamsaka nani? Unasaka mzoga wa mbwa! Unasaka kiroboto!
15 The Lord be iuge, and the Lord deme bitwixe me and thee, and se, and deme my cause, and delyuere me fro thin hond.
BWANA na awe mwamuzi na atoe hukumu kati yangu na wewe, na akaione, na akatetee sababu yangu na aniruhusu kuepuka mkono wako.”
16 Sotheli whanne Dauid hadde fillid spekynge siche wordis to Saul, Saul seide, Whether this is thi vois, my sone Dauid? And Saul reiside his vois, and wepte.
Daudi alipomaliza kuongea maneno haya kwa Sauli, Sauli akasema, “Hii ni sauti yako, mwanangu Daudi?” Sauli alinyanyua sauti yake akalia.
17 And he seide to Dauid, Thou art more iust than Y; for thou yauest goodis to me; forsothe Y yeldide yuelis to thee.
Akamwambia Daudi, “Wewe ni mwenye haki kuliko mimi. Kwa sababu umenilipa mazuri, wakati mimi nimekulipa maovu.
18 And thou schewidist to me to dai, what goodis thou hast do to me, how the Lord bitook me in thin hond, and thou killidist not me.
Leo umetangaza jinsi ulivyonitendea mazuri, kwa sababu hukuniua wakati BWANA aliponiweka katika rehema yako.
19 For who, `whanne he fyndith his enemy, schal delyuere hym in good weie? But the Lord yelde to thee this while, for that, that thou wrouytist to dai in me.
Kwa kuwa mtu akimpata adui yake, atamwacha aende zake salama? Na BWANA akuzawadie mema kwa kile ulichonifanyia leo.
20 And now, for Y woot, that thou schalt regne moost certeynli, and schalt haue in thin hond the rewme of Israel, swere thou to me in the Lord,
Basi, najua kwa hakika kwamba utakuwa mfalme na kwamba ufalme wa Israeli utaimarika katika mkono wako.
21 that thou do not a wei my seed aftir me, nether take a wey my name fro the hows of my fadir.
Niapie kwa BWANA kwamba baada yangu hautawakatilia mbali uzao wangu, na kwamba hautaliharibu jina langu katika nyumba ya baba yangu.”
22 And Dauid swoor to Saul. Therfor Saul yede in to his hows, and Dauid and hise men stieden to sikire placis.
Hivyo Daudi akamwapia Sauli kiapo. Kisha Sauli akaenda nyumbani, lakini Daudi na watu wake wakapanda kwenda ngomeni.

< 1 Samuel 24 >