< 1 Samuel 2 >

1 And Anna worschipide, and seide, Myn herte fulli ioiede in the Lord, and myn horn is reisid in my God; my mouth is alargid on myn enemyes, for Y was glad in thin helthe.
Hana aliomba akasema, “moyo wangu wamtukuza BWANA. Pembe yangu imejulikana katika BWANA. Kinywa changu kinatamba dhidi ya maadui zangu, kwa kuwa naufurahia wokovu wako.
2 Noon is hooli as the Lord is; `for noon other is, outakun thee, and noon is strong as oure God.
Hakuna aliye mtakatifu kama BWANA, kwa kuwa hakuna mwingine zaidi yako; hakuna mwamba kama Mungu wetu.
3 Nyle ye multiplie to speke hiye thingis, and haue glorie; elde thingis go awey fro youre mouth; for God is Lord of kunnyngis, and thouytis ben maad redi to hym.
Msijivune sana hivyo kwa kiburi; vinywa vyenu visitoke majivuno. Kwa kuwa BWANA ni Mungu wa maarifa; yeye huyapima matendo kwa mizani.
4 The bouwe of strong men is ouercomun, and sijk men ben gird with strengthe.
Pinde za mashujaa zimevunjika, bali wale wanaojikwaa hujivika nguvu kama mshipi.
5 Men fillid bifore settiden hem silf to hire for looues, and hungri men ben fillid; while the bareyn womman childide ful manye, and sche that hadde many sones, was sijke.
Wale walio na shibe ya kutosha wamejikodisha ili wapate chakula; wale waliokuwa na njaa hawana njaa tena. Hata yule aliye kuwa tasa amezaa watoto saba, bali mwanamke mwenye watoto wengi amenyong'onyea.
6 The Lord sleeth, and quikeneth; he ledith forth to hellis, and bryngith ayen. (Sheol h7585)
BWANA huua na huuisha. Hushusha kuzimu na huleta tena juu. (Sheol h7585)
7 The Lord makith pore, and makith riche; he makith low, and reisith.
BWANA humfanya maskini, na yeye ndiye humtajirisha mtu. Yeye hudhili, lakini pia hukweza
8 He reisith a nedi man fro poudur, and `he reisith a pore man fro dryt, that he sitte with princes, and holde the seete of glorie; for the endis of erthe ben of the Lord, and he hath set the world on tho.
Yeye humwinua juu maskini toka mavumbini: Huwainua wahitaji toka jalalani na kuwaketisha pamoja na wakuu na kuwarithisha kiti cha enzi cha utukufu. Kwa kuwa nguzo za dunia ni za BWANA na ameukalisha ulimwengu juu yake.
9 He schal kepe `the feet of hise seyntis, and wickid men schulen be stille to gidere in derknessis; for a man schal not be maad strong in his owne strengthe.
Yeye atazilinda nyayo za watu wake waaminifu, bali waovu watanyamazishwa gizani, kwa maana hakuna atayeshinda kwa nguvu zake.
10 Aduersaries of the Lord schulen drede hym, and in heuenes he schal thundre on hem; the Lord schal deme the endis of erthe, and he schal yyue lordschip to his kyng, and he schal enhaunse the horn, `that is, power, of his Crist.
Wale wampingao BWANA watavunjwa vipande vipande; atawapiga radi kutokea mbinguni. BWANA atahukumu miisho ya dunia; atampa nguvu mfalme wake na kuinua pembe ya mtiwa mafuta wake.”
11 And Helcana yede in to Ramatha, in to his hows; forsothe the child was seruaunt in the siyt of the Lord bifor the face of Ely the preest.
Nndipo Elikana akenda Rama, nyumbani kwake. Na yule mtoto akamtumikia BWANA machoni pa Eli, kuhani.
12 Forsothe the sones of Hely weren sones of Belial,
Basi, watoto wa Eli walikuwa wakorofi. Wao hawakumheshimu BWANA.
13 and knewen not the Lord, nether the office of preestis to the puple; but who euer hadde offrid sacrifice, the child of the preest cam, while the fleischis weren in sething, and he hadde a fleischhook with thre teeth in his hond;
Desturi ya makuhani na watu ilikuwa kwamba endapo mtu yeyote ametoa dhabihu, mtumishi wa kuhani angekuja akiwa na uma wa meno matatu mkononi mwake, nyama ilipokuwa inatokoswa.
14 and he sente it in to the `grete vessel of stoon, ethir in to the caudrun, ethir in to the pot, ethir in to the panne; and what euer thing the fleischhook reiside, the preest took to hym silf; so thei diden to al Israel of men comynge in to Silo.
Naye angeutia uma huo sufuriani, au birikani au chomboni au chunguni; nyama yote ambayo ingeinuliwa na uma huo ingetwaliwa na kuhani mwenyewe. Ndivyo walivyofanya huko Shilo kwa Waisraeli wote waliokwenda huko.
15 Yhe bifor that `the sones of Hely brenten the ynnere fatnesse, the `child of the preest cam, and seyde to the offerere, Yyue `thou fleisch to me, that Y sethe to the preest; for Y schal not take of thee sodun fleisch, but raw.
Tena, kabla ya kuteketeza mafuta, mtumishi wa kuhani alikuja, na kumwambia aliyekuwa akitoa dhabihu, “Tenga nyama ya kuchoma kwa ajili ya kuhani; kwa sababu hataikubali ile ya kutokosa kutoka kwako, bali tu ile mbichi.”
16 And `the offrere seide to hym, The ynnere fatnesse be brent first to day bi the custom, and take thou to thee hou myche euer thi soule desirith. Whiche answeride, and seide to hym, Nay, for thou schalt yyue now; ellis Y schal take bi violence.
Ikiwa mtu atamwambia, “Wachome mafuta kwanza, na kisha uchukue kiasi utakacho.” Ndipo angesema, “Hapana, utanipatia sasa hivi; la sivyo; Nitaichukua kwa lazima.”
17 Therfor the synne of the children was ful greuouse bifor the Lord; for thei withdrowen men fro the `sacrifice of the Lord.
Dhambi ya vijana hawa ilikuwa mbaya sana mbele za BWANA, kwa sababu waliidharau dhabihu ya BWANA.
18 `Forsothe Samuel, a child gird with a lynnun clooth, mynystride bifor the face of the Lord.
Lakini Samweli alimtumikia BWANA akiwa mdogo akivaa nguo ya naivera ya kitani.
19 And his moder made to hym a litil coote, which sche brouyte in daies ordeyned, and stiede with hir hosebonde, that he schulde offre a solempne offryng, and his auow.
Kila mwaka mama yake alimtengenezea kanzu dogo na kumletea, wakati wakija na mmewe kutoa dhabihu ya kila mwaka.
20 And Heli blesside Helcana and his wijf; and Heli seide `to hym, The Lord yelde to thee seed of this womman, for the yifte which thou hast youe to the Lord. And thei yeden in to her place.
Eli aliwabariki Elikana na mke wake na kusema, “BWANA akupatie watoto zaidi kwa mwanamke huyu kwa sababu ya ahadi yake aliyoitoa kwa BWANA.” Baadaye walirudi nyumbani kwao.
21 Therfor the Lord visitide Anna, and sche conseyuede, and childide thre sones and twei douytris. And the child Samuel was `magnyfied at the Lord.
BWANA alimsaidia tena Hana, akawa amebeba mimba nyingine. Akazaa watoto watatu wa kiume na wa kike wawili. Wakati huo huo mtoto Samweli akakua akiwa mbele za BWANA.
22 Forsothe Hely was ful eld, and he herde alle `thingis whiche hise sones diden in al Israel, and hou thei slepten with wymmen, that awaitiden at the dore of the tabernacle.
Basi Eli alikuwa mzee sana, akayasikia yote ambayo watoto wake walikuwa wakiwafanyia Waisraeli wote, na jinsi walivyotembea na mwanamke aliyekuwa akitumika katika lango la hema ya kukutania.
23 And he seide to hem, Whi doen ye siche thingis, the worste thingis whiche Y here of al the puple?
Akawaambia, “Kwa nini mnafanya mambo hayo? Kwa maana nasikia matendo yenu maovu kutoka kwa watu hawa wote.”
24 Nyle ye, my sones; it is not good fame, which Y here, that ye make the `puple of the Lord to do trespas.
Sivyo hivyo, watoto wangu, maana hii ninayoisikia siyo taarifa njema. Mnawakosesha watu wa BWANA.
25 If a man synneth ayens a man, God may be plesid to him; forsothe if a man synneth ayens the Lord, who schal preye for hym? And thei herden not the vois of her fadir, for God wolde sle hem.
“Kama mtu mmoja akimkosea mwenzake, Mungu atamhukumu; Lakini mtu akimkosea BWANA, ni nani atakayemtetea mtu huyo?” Lakini hawakuitii sauti ya baba yao, sababu BWANA alinuia kuwaua.
26 Forsothe the child Samuel profitide, and encreessyde, and pleside bothe God and men.
Yule mtoto Samweli aliongezeka umri, na kupata kibali kwa BWANA na kwa watu pia.
27 Sotheli a man of God cam to Hely, and seide to hym, The Lord seith these thingis, Whether Y was not schewid apertli to the hows of thi fadir, whanne he was in Egipt, in the hows of Farao?
Kisha mtu wa Mungu akamwendea Eli na kumwambia, “BWANA asema, 'Je, sikujifunua mwenyewe kwa nyumba ya baba zako, walipokuwa Misri utumwani nyumbani mwa Farao?
28 And Y chees hym of alle lynagis of Israel `in to preest to me, that he schulde stie to myn auter, and schulde brenne encense to me, and that he schulde bere bifor me preestis cloth; and Y yaf to `the hows of thi fadir alle thingis of the sacrifices of the sones of Israel.
Mimi nilimchagua yeye kutoka makabila yote ya Israeli awe kuhani wangu, apande madhabahuni kwangu, na kufukiza uvumba, na kuvaa kanzu ya naivera mbele yangu. Niliwapa nyumba ya baba zako dhabihu zote za wana wa Israeli zilizotolewa kwa moto.
29 Whi hast thou cast awey with the heele my sacrifice, and my yiftis, whiche Y comaundide to be offrid in the temple; and thou onouridst more thi sones than me, that ye eeten the principal partis of ech sacrifice of `Israel, my puple?
Kwanini basi, unaidharau dhabihu yangu na sadaka ambazo ninazitaka mahali ninapoishi? Kwanini unawaheshimu watoto wako kuliko mimi, kwa kujinenepesha ninyi wenyewe kwa uzuri wa kila sadaka ya watu wangu Israeli?'
30 Therfor the Lord God of Israel seith these thingis, Y spekynge spak, that thin hows and `the hows of thi fadir schulde mynystre in my siyt til in to with outen ende; `now forsothe the Lord seith, Fer be this fro me; but who euere onourith me, Y schal glorifie hym; forsothe thei that dispisen me, schulen be vnnoble.
Maana, BWANA, Mungu wa Isareli, asema, niliahidi kwamba nyumba yako, na nyumba ya baba yako, yawapasa kwenda mbele zangu milele,' Lakini sasa BWANA asema. 'Mambo haya yapishe mbali. nami nisifanye hivi, maana nitawaheshimu wanaoniheshimu, bali wanaonidharau mimi hawatakuwa na thamani.
31 Lo! daies comen, and Y schal kitte awei thin arm, and the arm of the hows of thi fadir, that an eld man be not in thin hows.
Tazama, siku zinakuja nitakapoondoa nguvu zako na nguvu za nyumba za baba yako, ili kwamba pasije kuwepo mtu mzee katika nyumba yako.
32 And thou schalt se thin enemy in the temple, in alle prosperitees of Israel; and an eld man schal not be in thin hows in alle daies.
Nawe utalitazama hangaiko katika makao yangu. Ingawa Israeli watapewa jambo jema, hapatakuwapo tena mtu yeyote mzee katika nyumba yako.
33 Netheles Y schal not outerli take awei of thee a man fro myn auter, but that thin iyen faile, and thi soule faile; and greet part of thin hows schal die, whanne it schal come to mannus age.
Yeyote miongoni mwenu nisiye mwondoa kutoka madhabahuni pangu, Nitasababisha macho yenu yaanguke, na ita nitasababisha huzuni maishani mwenu. Wanaume wote waliozaliwa katika familia yako watakufa.
34 Forsothe this schal be signe, that schal come to thi twei sones Ophym and Fynees, bothe schulen die in o dai.
Hii ndiyo itakuwa ishara kwako ambayo itawaijia watoto wako wakiume wawili, juu ya Hofni na Finehasi: Wote wawili watakufa siku moja.
35 And Y schal reise to me a feithful preest, that schal do bi myn herte and my soule; and Y schal bilde to hym a feithful hows, and he schal go bifore my Crist in alle daies.
Nami nitamwinua juu kuhani wangu mwaminifu atakaye fanya kile kilichomo moyoni mwangu na nafisini mwangu. Nami nitamjengea nyumba madhubuti; naye atakwenda mbele ya mfalme wangu mbarikiwa milele.
36 Forsothe it schal come, that who euer dwellith in thin hows, he come that `me preie for him, and that he offre a peny of siluer, and a cake of breed, and seie, Y biseche, suffre thou me to o `part of the preest, that Y ete a mussel of breed.
Kila mmoja aliyebakia nyumbani mwako atakuja na kusujudu mbele ya mtu huyo, akiomba kipande cha fedha na mkate mmoja, naye atasema, “Tafadhali uniajiri katika moja ya nafasi za kuhani ili niweze kula kipande cha mkate'”'

< 1 Samuel 2 >