< 1 Kings 5 >

1 Also Hiram, kyng of Tire, sente hise seruauntis to Salomon; for he herde that thei hadden anoyntide hym kyng for his fadir; for Hiram was frend of Dauid in al time.
Hiramu mfalme wa Tiro aliposikia kuwa Solomoni ametiwa mafuta awe mfalme mahali pa Daudi baba yake, akatuma wajumbe kwa Solomoni, kwa sababu Hiramu siku zote alikuwa na uhusiano mzuri wa kirafiki na Daudi.
2 Sotheli also Salomon sente to Hiram,
Solomoni akapeleka ujumbe huu kwa Hiramu:
3 and seide, Thou knowist the wille of Dauid, my fadir, and for he miyte not bilde an hows to the name of his God, for batels neiyynge bi cumpas, til the Lord yaf hem vndur the step of hise feet.
“Unajua kwamba kwa sababu ya vita vilivyopiganwa dhidi ya baba yangu Daudi kutoka pande zote, hakuweza kujenga Hekalu kwa ajili ya Jina la Bwana Mungu wake, hadi Bwana alipowaweka adui zake chini ya miguu yake.
4 Now forsothe my Lord God yaf reste to me bi cumpas, and noon aduersarie is, nethir yuel asailyng;
Lakini sasa Bwana Mungu wangu amenipa utulivu kila upande hakuna adui wala maafa.
5 wherfor Y thenke to buylde a temple to the name of my Lord God, as God spak to Dauid, my fadir, and seide, Thi sone, whom Y schal yyue to thee for thee on thi trone, he schal bilde an hows to my name.
Kwa hiyo, ninakusudia kujenga Hekalu kwa ajili ya Jina la Bwana, Mungu wangu, kama Bwana alivyomwambia baba yangu Daudi, wakati aliposema, ‘Mwanao nitakayemweka kwenye kiti cha ufalme mahali pako, ndiye atajenga Hekalu kwa ajili ya Jina langu.’
6 Therfor comaunde thou, that thi seruauntis hewe doun to me cedris of the Liban; and my seruauntis be with thi seruauntis; sotheli Y schal yyue to thee the meede of thi seruauntis, what euere meede thou schalt axe; for thou woost, that in my puple is not a man that kan hewe trees, as Sidonyes kunnen.
“Hivyo toa amri ili mierezi ya Lebanoni ikatwe kwa ajili yangu. Watu wangu watafanya kazi na watu wako, nami nitawalipa watu wako kwa ujira wowote utakaoupanga. Unajua kwamba hatuna mtu yeyote mwenye ustadi katika kukata miti kama Wasidoni.”
7 Therfor whanne Hiram hadde herde the wordis of Salomon, he was ful glad, and seide, Blessid be the Lord God to dai, that yaf to Dauid a sone moost wijs on this puple ful myche.
Hiramu aliposikia ujumbe wa Solomoni, akafurahishwa sana akasema, “Ahimidiwe Bwana leo, kwa kuwa amempa Daudi mwana mwenye hekima kutawala juu ya taifa hili kubwa.”
8 And Hiram sente to Salomon, and seide, Y haue herde what euer thingis thou sentist to me; Y schal do al thi wille, in trees of cedres, and of beechis.
Hiramu akatuma neno kwa Solomoni: “Nimepokea ujumbe ulionipelekea na nitafanya yote unayohitaji katika kukupatia magogo ya mierezi na misunobari.
9 My seruauntis schulen putte doun tho trees fro the Liban to the see, and Y schal araye tho trees in schippis in the see, `til to the place which thou schalt signyfie to me; and Y schal dresse tho there, that thou take tho; and thou schalt yyue necessaries to me, that mete be youun to myn hows.
Watu wangu watayakokota kutoka Lebanoni hadi kwenye bahari, nami nitayafunga mafungu mafungu yaelee juu ya maji hadi utakapoelekeza. Huko nitayatenganisha, nawe utaweza kuyachukua. Wewe utakidhi haja yangu kwa kunipatia chakula kwa ajili ya watu wa nyumbani mwangu.”
10 Therfor Hiram yaf to Salomon `trees of cedres, and `trees of beechis, bi al his wille;
Kwa njia hii Hiramu akampa Solomoni miti yote ya mierezi na magogo ya misunobari kama alivyohitaji,
11 forsothe Salomon yaf to Hiram twenti thousynde chorus of wheete, in to meete to his hows, and twenti chorus of pureste oile; Salomon yaf these thingis to Hiram bi alle yeeris.
naye Solomoni akampa Hiramu kori 20,000 za ngano kama chakula kwa ajili ya watu wa nyumbani mwake, pamoja na mafuta safi ya zeituni yaliyokamuliwa bathi 20,000. Solomoni aliendelea kumfanyia Hiramu hivyo mwaka baada ya mwaka.
12 Also the Lord yaf wisdom to Salomon, as he spak to hym; and pees was bitwixe Hiram and Salomon, and bothe smytiden boond of pees.
Bwana akampa Solomoni hekima, kama alivyomwahidi. Palikuwepo na uhusiano wa amani kati ya Hiramu na Solomoni, na wote wawili wakafanya mkataba.
13 And kyng Salomon chees werk men of al Israel; and the summe was thretti thousynde of men.
Mfalme Solomoni akakusanya wafanyakazi 30,000 kutoka Israeli yote.
14 And `Salomon sente hem in to the Liban, ten thousynde bi ech monethe bi whilis, so that in twei monethis bi whilis thei weren in her howsis; and Adonyram was on sich a summe.
Akawapeleka Lebanoni kwa zamu za watu 10,000 kwa mwezi, hivyo walikaa Lebanoni kwa mwezi mmoja na miezi miwili nyumbani. Adoniramu ndiye alikuwa kiongozi wa shokoa.
15 Therfor seuenti thousynde of hem, that baren burthuns, weren to Salomon, and foure score thousynde of masouns in the hil, with out the souereyns,
Solomoni alikuwa na wachukuzi wa mizigo 70,000 na wachonga mawe 80,000 huko vilimani,
16 that weren maistris of alle werkis, bi the noumbre of thre thousynde and thre hundrid, comaundynge to the puple, and to hem that maden werk.
pamoja na wasimamizi 3,300 ambao walisimamia kazi hiyo na kuwaongoza wafanyakazi.
17 And the kyng comaundide, that thei schulden take greete stonys, `and preciouse stonys, in to the foundement of the temple, and that thei schulden make tho square;
Kwa amri ya mfalme walitoa kwenye machimbo ya mawe, mawe makubwa, yaliyo bora kwa kujengea msingi wa nyumba yaliyochongwa kwa ajili ya Hekalu.
18 whiche stoonys the masouns of Salomon, and the masouns of Hyram, hewiden. Forsothe Biblies maden redi trees and stonus, to the hows to be bildid.
Mafundi wa Solomoni, wa Hiramu na watu wa Gebali walikata na kuandaa mbao na mawe kwa ajili ya ujenzi wa Hekalu.

< 1 Kings 5 >