< 1 Kings 18 >
1 Aftir many daies the word of the Lord was maad to Elie, in the thridde yeer, and seide, Go, and schewe thee to Achab, that Y yyue reyn on the face of erthe.
Baada ya muda mrefu, katika mwaka wa tatu, neno la Bwana likamjia Eliya kusema, “Nenda ukajionyeshe kwa Ahabu na mimi nitanyesha mvua juu ya nchi.”
2 Therfor Elie yede to schewe hym silf to Achab; forsothe greet hungur was in Samarie.
Kwa hiyo Eliya akaenda kujionyesha kwa Ahabu. Wakati huu njaa ilikuwa kali sana katika Samaria,
3 And Achab clepide Abdie, dispendere, ether stiward, of his hows; forsothe Abdie dredde greetli the Lord God of Israel.
naye Ahabu alikuwa amemwita Obadia ambaye alikuwa msimamizi wa jumba lake la kifalme. (Obadia alimcha Bwana sana.
4 For whanne Jezabel killide the prophetis of the Lord, he took an hundrid prophetis, and hidde hem, bi fifties and fifties, in dennes, and fedde hem with breed and watir.
Wakati Yezebeli alipokuwa akiwaua manabii wa Bwana, Obadia alikuwa amewachukua manabii mia moja na kuwaficha katika mapango mawili, hamsini kwenye kila moja na akawa akiwapa chakula na maji.)
5 Therfor Achab seide to Abdie, Go thou in to the lond, to alle wellis of watris, and in to alle valeis, if in hap we moun fynde gras, and saue horsis and mulis; and werk beestis perische not outirli.
Ahabu alikuwa amemwambia Obadia, “Nenda katika nchi yote kwenye vijito vyote na mabonde. Huenda tunaweza kupata majani ya kuwalisha farasi na nyumbu wapate kuishi ili tusilazimike kuwaua hata mmoja wa wanyama wetu.”
6 Therfor thei departiden the cuntreis to hem silf, that thei schulden cumpasse tho; Achab yede bi o weye, and Abdie yede bi another weie, `bi hym silf.
Kwa hiyo wakagawanya nchi waliyokusudia kutafuta majani, Ahabu akaenda upande mmoja na Obadia upande mwingine.
7 And whanne Abdie was in the weie, Elie mette hym; and whanne he hadde knowe Elie, he felde on his face, and seide, Whethir thou art my lord Elie?
Wakati Obadia alipokuwa akitembea njiani, Eliya akakutana naye. Obadia akamtambua, akamsujudia hadi nchi na kusema, “Je, hivi kweli ni wewe, bwana wangu Eliya?”
8 To whom he answeride, Y am. And Elie seide, Go thou, and seie to thi lord, Elie is present.
Eliya akamjibu, “Ndiyo, nenda ukamwambie bwana wako Ahabu, ‘Eliya yuko hapa.’”
9 And Abdie seide, What `synnede Y, for thou bitakist me in the hond of Achab, that he sle me?
Obadia akamuuliza, “Ni kosa gani nimefanya, hata ukaamua kumkabidhi mtumishi wako mkononi mwa Ahabu ili aniue?
10 Thi Lord God lyueth, for no folk ethir rewme is, whidur my lord, sekynge thee, sente not; and whanne alle men answeriden, He is not here, he chargide greetli alle rewmes and folkis, for thou were not foundun; and now thou seist to me,
Hakika kama Bwana Mungu wako aishivyo, hakuna taifa hata moja au ufalme ambapo bwana wangu hajamtuma mtu kukutafuta. Kila wakati taifa au ufalme walipodai kwamba haupo huko, aliwafanya waape kwamba hawakuweza kukupata.
11 Go, and seie to thi lord, Elie is present.
Lakini sasa unaniambia niende kwa bwana wangu na kusema, ‘Eliya yuko hapa.’
12 And whanne Y schal departe fro thee, the Spirit of the Lord schal bere thee awey in to a place which Y knowe not; and Y schal entre, and `Y schal telle to Achab, and he schal not fynde thee, and he schal sle me; forsothe thi seruaunt dredith the Lord fro his yong childhod.
Sijui ni wapi Roho wa Bwana ataamua kukupeleka wakati nitakapokuacha. Kama nikienda kumwambia Ahabu na asikupate, ataniua. Hata hivyo mimi mtumishi wako nimemwabudu Bwana tangu ujana wangu.
13 Whether it is not schewid to thee, my lord, what Y dide, whanne Jesabel killide the prophetis of the Lord, that Y hidde of the prophetis of the Lord an hundrid men, bi fifty and bi fifti, in dennes, and Y fedde hem with breed and watir?
Je, hukusikia, bwana wangu, nilifanya nini wakati Yezebeli alipokuwa akiua manabii wa Bwana? Niliwaficha manabii wa Bwana mia moja katika mapango mawili, hamsini katika kila moja, nami nikawapatia chakula na maji.
14 And now thou seist, Go, and seie to thi lord, Elie is present, that he sle me.
Nawe sasa unaniambia niende kwa bwana wangu na kumwambia, ‘Eliya yuko hapa.’ Yeye ataniua!”
15 And Elie seide, The Lord of oostis lyueth, bifor whos siyt Y stonde, for to dai Y schal appere to hym.
Eliya akasema, “Kama Bwana Mwenye Nguvu Zote aishivyo, yeye ninayemtumikia, hakika nitajionyesha kwa Ahabu leo.”
16 Therfor Abdie yede in to the metyng of Achab, and schewide to hym; and Achab cam in to the meetyng of Elie.
Basi Obadia akaenda kukutana na Ahabu na kumwambia, naye Ahabu akaenda kukutana na Eliya.
17 And whanne he hadde seyn Elie, he seide, Whether thou art he, that disturblist Israel?
Ahabu alipomwona Eliya, akamwambia, “Je, ni wewe, mtaabishaji wa Israeli?”
18 And he seide, Not Y disturble Israel, but thou, and the hows of thi fadir, whiche han forsake the comaundementis of the Lord, and sueden Baalym, `disturbliden Israel.
Eliya akamjibu, “Mimi sijaitaabisha Israeli. Lakini wewe na jamaa ya baba yako ndio mnaofanya hivyo. Mmeziacha amri za Bwana na mkafuata Mabaali.
19 Netheles now sende thou, and gadere to me al Israel, in the hil of Carmele, and foure hundrid and fifti prophetis of Baal, and foure hundrid prophetis of woodis, that eten of the table of Jezabel.
Sasa waite watu kutoka Israeli yote tukutane nao juu ya Mlima Karmeli. Nawe uwalete hao manabii wa Baali mia nne na hamsini na hao manabii mia nne wa Ashera, walao chakula mezani mwa Yezebeli.”
20 Achab sente to alle the sones of Israel, and gaderide prophetis in the hil of Carmele.
Ndipo Ahabu akatuma ujumbe katika Israeli yote na kuwakusanya manabii hao juu ya mlima Karmeli.
21 Forsothe Elie neiyede to al the puple of Israel, and seide, Hou long halten ye in to twey partis? If the Lord is God, sue ye hym; forsothe if Baal is God, sue ye hym. And the puple answeride not o word to hym.
Eliya akasimama mbele ya watu na kusema, “Mtasitasita katika mawazo mawili hadi lini? Ikiwa Bwana ndiye Mungu, mfuateni yeye; lakini ikiwa Baali ni Mungu, basi mfuateni yeye.” Lakini watu hawakusema kitu.
22 And Elie seide eft to the puple, Y dwellide aloone a prophete of the Lord; sotheli the prophetis of Baal ben foure hundrid and fifti, and the prophetis of woodis ben foure hundrid men.
Kisha Eliya akawaambia, “Ni mimi peke yangu nabii wa Bwana aliyebaki, lakini Baali ana manabii mia nne na hamsini.
23 Tweyne oxis be youun to us; and chese thei oon oxe, and thei schulen kitte in to gobetis, and schulen putte on trees, but putte thei not fier vndur; and Y schal make the tother oxe in to sacrifice, and Y schal putte on the trees, and Y schal not putte fier vnder.
Leteni mafahali wawili. Wao na wajichagulie mmoja, wamkate vipande vipande na waweke juu ya kuni lakini wasiiwashie moto. Nitamwandaa huyo fahali mwingine na kumweka juu ya kuni lakini sitawasha moto.
24 Clepe ye the name of youre goddis, and Y schal clepe the name of my God; and the God that herith bi fier, be he God. And al the puple answeride, and seide, The resoun is best, `which resoun Elie spak.
Kisha mliitie jina la mungu wenu, nami nitaliitia jina la Bwana Mungu yule ambaye atajibu kwa moto, huyo ndiye Mungu.” Kisha watu wote wakasema, “Hilo unalosema ni jema.”
25 Therfor Elie seide to the prophetis of Baal, Chese ye oon oxe to you, and make ye first, for ye ben the mo; and clepe ye the names of youre goddis, and putte ye not fier vnder.
Eliya akawaambia manabii wa Baali, “Chagueni mmoja kati ya hawa mafahali na mwe wa kwanza kumwandaa, kwa kuwa ninyi mko wengi sana. Liitieni jina la mungu wenu, lakini msiwashe moto.”
26 And whanne thei hadden take the oxe, whom Elie yaf to hem, thei maden sacrifice, and clepiden the name of Baal, fro the morewtid `til to myddai, and seiden, Baal, here vs! And no vois was, nether ony that answerd; and thei skippiden ouer the auter, which thei hadden maad.
Kwa hiyo wakamchukua yule fahali waliyepewa, nao wakamwandaa. Kisha wakaliitia jina la Baali kutoka asubuhi hadi adhuhuri, wakapiga kelele, “Ee Baali, utujibu!” Lakini hapakuwa na jibu; hakuna aliyejibu. Nao wakacheza kuizunguka madhabahu waliyoijenga.
27 And whanne it was thanne myddai, Elie scornede hem, and seide, Crie ye with gretter vois, for Baal is youre god, and in hap he spekith with an other, ethir he is in a herborgerie, ether in weie, ether certis he slepith, that he be reisid.
Wakati wa adhuhuri, Eliya akaanza kuwadhihaki, akisema, “Pigeni kelele zaidi! Hakika yeye ni mungu! Labda amezama katika mawazo mazito, au ana shughuli nyingi, au amesafiri. Labda amelala usingizi mzito, naye ni lazima aamshwe.”
28 Therfor thei crieden with greet vois, and thei kerueden hem silf with knyues and launcetis, bi her custom, til thei weren bisched with blood.
Kwa hiyo wakapiga kelele zaidi na kama ilivyokuwa desturi yao wakajichanja wenyewe kwa visu na vyembe, mpaka damu ikachuruzika.
29 Sotheli after that mydday passide, and while thei prophesieden, the tyme cam, in which the sacrifice is wont to be offrid, nether vois was herd `of her goddis, nether ony answeride, nether perceyuede hem preiynge.
Adhuhuri ikapita, nao wakaendelea na utabiri wao wa kiwazimu mpaka wakati wa dhabihu ya jioni. Lakini hapakuwa na jibu, hakuna aliyejibu, hakuna aliyeangalia.
30 Elie seide to al the puple, Come ye to me. And whanne the puple cam to him, he arrayede the auter of the Lord, that was distried.
Kisha Eliya akawaambia watu wote, “Sogeeni karibu nami.” Watu wote wakamkaribia, naye akakarabati madhabahu ya Bwana, ambayo ilikuwa imevunjwa.
31 And he took twelue stonys, bi the noumbre of lynagis of sones of Jacob, to which Jacob the word of the Lord was maad, and seide, Israel schal be thi name.
Eliya akachukua mawe kumi na mawili, moja kwa ajili ya kila kabila la wana wa Yakobo, ambaye neno la Bwana lilimjia, likisema, “Jina lako litakuwa Israeli.”
32 And he bildide an auter of stonys, in the name of the Lord, and he made a ledyng to of watir, `ether a dich, as bi twei litle dichis in the cumpas of the auter.
Kwa mawe hayo, akajenga madhabahu katika jina la Bwana, na akachimba handaki kuizunguka, ukubwa wa kutosha vipimo viwili vya mbegu.
33 And he dresside trees, and he departide the oxe bi membris, and puttide on the trees,
Akapanga kuni, akamkata yule fahali vipande vipande na kuvipanga juu ya kuni. Kisha akawaambia, “Jazeni mapipa manne maji na kuyamwaga juu ya sadaka ya kuteketezwa na juu ya kuni.”
34 and seide, Fille ye foure pottis with watir, and schede ye on the brent sacrifice, and on the trees. And eft he seide, Also the secounde tyme do ye this. `And thei diden the secounde tyme. And he seide, Do ye the same thing the thridde tyme; and thei diden the thridde tyme.
Akawaambia, “Fanyeni hivyo tena.” Nao wakafanya hivyo tena. Akaagiza, “Fanyeni kwa mara ya tatu.” Nao wakafanya hivyo kwa mara ya tatu.
35 And the watris runnen aboute the auter, and the dich of ledyng to `of watir was fillid.
Maji yakatiririka kuizunguka madhabahu na hata kujaza lile handaki.
36 And whanne the tyme was thanne, that the brent sacrifice schulde be offrid, Elye the prophete neiyede, and seide, Lord God of Abraham, of Isaac, and of Israel, schewe thou to dai that thou art God of Israel, and that Y am thi seruaunt, and haue do alle these wordis bi thi comaundement.
Wakati wa kutoa dhabihu ya jioni, nabii Eliya akasogea mbele na kuomba, akisema: “Ee Bwana, Mungu wa Abrahamu, na Isaki na Israeli, ijulikane leo kwamba wewe ndiye Mungu katika Israeli na ya kwamba mimi ni mtumishi wako na nimefanya mambo haya yote kwa neno lako.
37 Lord, here thou me; Lord, here thou me; that this puple lerne, that thou art the Lord God, and that thou hast conuertid eft the herte of hem.
Unijibu mimi, Ee Bwana, nijibu mimi, ili watu hawa wajue kwamba wewe, Ee Bwana, ndiwe Mungu, na kwamba unaigeuza mioyo yao ikurudie tena.”
38 Sotheli fier of the Lord felde doun, and deuouride brent sacrifice, and trees, and stonus, and lickide vp also the poudre, and the water that was in the `leding of water.
Kisha moto wa Bwana ukashuka na kuiteketeza ile dhabihu, zile kuni, yale mawe, ule udongo, na pia kuramba yale maji yaliyokuwa ndani ya handaki.
39 And whanne al the puple hadde seyn this, it felde in to his face, and seide, The Lord he is God; the Lord he is God.
Wakati watu wote walipoona hili, wakaanguka kifudifudi na kulia, “Bwana: yeye ndiye Mungu! Bwana: yeye ndiye Mungu!”
40 And Elie seide to hem, Take ye the prophetis of Baal; not oon sotheli ascape of hem. And whanne thei hadden take hem, Elie ledde hem to the stronde of Cison, and killide hem there.
Kisha Eliya akawaamuru, “Wakamateni hao manabii wa Baali. Msimwache hata mmoja atoroke!” Wakawakamata, naye Eliya akawaleta mpaka Bonde la Kishoni na kuwachinja huko.
41 And Elie seide to Achab, Stie thou, ete, and drynke, for the sown of myche reyn is.
Eliya akamwambia Ahabu, “Nenda, ukale na kunywa, kwa kuwa kuna sauti ya mvua kubwa.”
42 Achab stiede to ete and drynke; forsothe Elie stiede in to the hil of Carmele, and he settide lowli his face to the erthe, bitwixe hise knees;
Hivyo Ahabu akaondoka ili kula na kunywa. Lakini Eliya akapanda kileleni mwa Karmeli, akasujudu na akaweka kichwa chake katikati ya magoti yake.
43 and seide to his child, Stie thou, and biholde ayens the see. And whanne he hadde stied, and hadde biholde, he seide, No thing is. And eft Elie seide to hym, Turne thou ayen bi seuene tymes.
Akamwambia mtumishi wake, “Nenda ukatazame kuelekea bahari.” Akaenda na kutazama. Akasema, “Hakuna kitu chochote huko.” Mara saba Eliya akasema, “Nenda tena.”
44 Sotheli in the seuenthe tyme, lo! a litil cloude as the step of a man stiede fro the see. And Elie seide, Stie thou, and seie to Achab, Ioyne thi chare, and go doun, lest the reyn byfor ocupie thee.
Mara ya saba, mtumishi akaleta taarifa, “Wingu dogo kama mkono wa mwanadamu linainuka kutoka baharini.” Hivyo Eliya akasema, “Nenda ukamwambie Ahabu, ‘Tandika gari lako na ushuke kabla mvua haijakuzuia.’”
45 And whanne thei turneden hem hidur and thidur, lo! heuenes weren maad derk, and cloud, and wynd, and greet reyn was maad. Therfor Achab stiede, and yede in to Jezrael;
Wakati ule ule anga likawa jeusi kwa mawingu, upepo ukainuka na mvua kubwa ikanyesha, naye Ahabu akaenda zake Yezreeli.
46 and the hond of the Lord was maad on Elie, and whanne the leendis weren gird, he ran bifor Achab, til he cam in to Jezrael.
Nguvu za Bwana zikamjia Eliya, naye akajikaza viuno, akakimbia mbele ya Ahabu njia yote hadi maingilio ya Yezreeli.