< 1 Kings 15 >

1 Therfor in the eiytenthe yeer of the rewme of Jeroboam, sone of Nabath, Abia regnede on Juda.
Katika mwaka wa kumi na nane wa utawala wa Yeroboamu mwana wa Nebati, Abiya akawa mfalme wa Yuda,
2 Thre yeer he regnede in Jerusalem; the name of his modir was Maacha, douyter of Abessalon.
naye akatawala huko Yerusalemu miaka mitatu. Mama yake aliitwa Maaka binti Abishalomu.
3 And he yede in alle the synnes of his fadir, which he dide bifor hym; and his herte was not perfit with his Lord God, as the herte of Dauid, his fadir, `was perfit.
Alitenda dhambi zote baba yake alizotenda kabla yake; moyo wake haukuwa mkamilifu kwa Bwana Mungu wake kama moyo wa Daudi baba yake ulivyokuwa.
4 But for Dauid his Lord God yaf to hym a lanterne in Jerusalem, that he schulde reise his sone after hym, and that he schulde stonde in Jerusalem;
Pamoja na hayo, kwa ajili ya Daudi, Bwana Mungu wake akampa taa katika Yerusalemu kwa kumwinua mwana atawale badala yake na kwa kuifanya Yerusalemu kuwa imara.
5 for Dauid hadde do riytfulnesse in the iyen of the Lord, and hadde not bowid fro alle thingis whiche the Lord hadde comaundid to him, in alle the daies of his lijf, outakun the word of Urie Ethei.
Kwa kuwa Daudi alifanya yaliyo mema machoni pa Bwana na hakushindwa kushika maagizo yote ya Bwana siku zote za uhai wake, isipokuwa katika habari ya Uria, Mhiti.
6 Netheles batel was bitwix Abia and Jeroboam, in al the tyme of his lijf.
Kulikuwa na vita kati ya Rehoboamu na Yeroboamu wakati wote wa maisha ya Abiya.
7 Sotheli the residue of wordis of Abia, and alle thinges whiche he dide, whether these ben not writun in the book of wordis of daies of the kyngys of Juda? And batel was bitwixe Abia and Jeroboam.
Kwa habari ya matukio mengine ya utawala wa Abiya na yote aliyofanya, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Yuda? Kulikuwa na vita kati ya Abiya na Yeroboamu.
8 And Abia slepte with his fadris; and thei birieden hym in the citee of Dauid; and Asa, his sone, regnede for hym.
Naye Abiya akalala na baba zake akazikwa katika Mji wa Daudi. Asa mwanawe akawa mfalme baada yake.
9 Sotheli Asa, king of Jude, regnede in the twentithe yeer of Jeroboam, kyng of Israel;
Katika mwaka wa ishirini wa utawala wa Yeroboamu mfalme wa Israeli, Asa akawa mfalme wa Yuda,
10 and Asa regnede oon and fourti yeer in Jerusalem. The name of his modir was Maacha, douyter of Abessalon.
naye akatawala katika Yerusalemu miaka arobaini na mmoja. Bibi yake aliitwa Maaka binti Abishalomu.
11 And Asa dide riytfulnesse in the siyt of the Lord, as Dauid, his fadir, dide;
Asa akatenda yaliyo mema machoni mwa Bwana, kama alivyokuwa ametenda Daudi baba yake.
12 and he took awey fro the loond men of wymmens condiciouns, and he purgide alle the filthis of idols, whiche his fadris maden.
Akawafukuza mahanithi wa mahali pa kuabudia miungu kutoka nchi na kuondoa sanamu zote ambazo baba zake walikuwa wametengeneza.
13 Ferthermore and he remouyde Maacha, his modir, that sche schulde not be princesse in the solempne thingis of Priapus, and in his wode which sche hadde halewid; and he distriede the denne of hym, and he brak the foulest symylacre, and brente in the stronde of Cedron;
Hata akamwondoa bibi yake Maaka kwenye wadhifa wake kama mama malkia, kwa sababu alikuwa ametengeneza nguzo ya Ashera ya kuchukiza. Asa akaikata hiyo nguzo na kuiteketeza kwa moto katika Bonde la Kidroni.
14 sotheli he dide not awei hiy thingis; netheles the herte of Asa was perfit with hys Lord God, in alle hise daies.
Ijapokuwa hakuondoa mahali pa juu pa kuabudia miungu, moyo wa Asa ulikuwa umejiweka kwa Bwana kikamilifu maisha yake yote.
15 And he brouyte in to the hous of the Lord tho thingis, whiche his fadir hadde halewid and auowid, siluer, and gold, and vessel.
Akaleta ndani ya Hekalu la Bwana fedha na dhahabu na vile vyombo ambavyo yeye na baba yake walikuwa wameviweka wakfu.
16 Forsothe batel was bitwixe Asa and Baasa, kyng of Israel, in alle the daies of hem.
Kulikuwa na vita kati ya Asa na Baasha mfalme wa Israeli siku zote za utawala wao.
17 And Baasa, kyng of Israel, stiede in to Juda, and bildide Rama, that no man of the part of Aza, kyng of Juda, myyte go out, ether go yn.
Mfalme Baasha wa Israeli akashambulia Yuda na kuweka ngome mji wa Rama ili kumzuia yeyote asitoke wala kuingia nchi ya Mfalme Asa wa Yuda.
18 Therfor Asa took al the siluer and gold, that lefte in the tresouris of the hows of the Lord, and in the tresouris of the kyngis hows, and yaf it in to the hondis of hise seruauntis; and sente to Benadab, sone of Tabrennon, sone of Ozion, the kyng of Sirie, that dwellide in Damask, and seide,
Kisha Asa akachukua fedha yote na dhahabu iliyokuwa imeachwa katika hazina za Hekalu la Bwana na za jumba lake mwenyewe la kifalme. Akawakabidhi maafisa wake na kuwatuma kwa Ben-Hadadi mwana wa Tabrimoni, mwana wa Hezioni, mfalme wa Aramu, aliyekuwa akitawala Dameski.
19 Boond of pees is bitwixe me and thee, and bitwixe my fadir and thi fadir, and therfor Y sente to thee yiftis, gold, and siluer; and Y axe, that thou come, and make voide the boond of pees, which thou hast with Baasa, kyng of Israel, and that he go awey fro me.
“Akasema na pawepo mkataba kati yangu na wewe, kama ulivyokuwepo kati ya baba yangu na baba yako. Tazama, nimekuletea zawadi ya fedha na dhahabu. Sasa vunja mkataba wako na Baasha mfalme wa Israeli ili aniondokee mimi.”
20 Benadab assentide to kyng Asa, and sente the princes of his oost in to the citees of Israel; and thei smytiden Ahion, and Dan, and Abel, the hows of Maacha, and al Cenoroth, that is, al the lond of Neptalym.
Ben-Hadadi akakubaliana na Mfalme Asa na kutuma majemadari wa majeshi yake dhidi ya miji ya Israeli. Akaishinda miji ya Iyoni, Dani, Abel-Beth-Maaka na Kinerethi yote, pamoja na Naftali.
21 And whanne Baasa hadde herd this thing, he lefte to bilde Rama, and turnede ayen in to Thersa.
Wakati Baasha aliposikia hili, akaacha kuijenga Rama na akaenda kuishi Tirsa.
22 Forsothe kyng Asa sente message in to al Juda, and seide, No man be excusid. And thei token the stoonys of Rama, and the trees therof, bi whiche Baasa hadde bildid; and kyng Asa bildide of the same `stoonys and trees Gabaa of Beniamyn, and Maspha.
Kisha Mfalme Asa akatoa amri kwa Yuda yote, pasipo kumbagua hata mmoja, kubeba mawe na mbao kutoka Rama, ambazo Baasha alikuwa akitumia huko. Mfalme Asa akazitumia kujengea Geba iliyoko Benyamini na Mispa pia.
23 Sotheli the residue of alle wordis of Asa, and of al his strengthe, and alle thingis whiche he dide, and the citees whiche he bildide, whether these ben not writun in the book of wordis of daies of kingis of Juda? Netheles Asa hadde ache in feet, in the tyme of his eelde.
Kwa matukio yote ya utawala wa Asa, mafanikio yake yote, yote aliyofanya na miji aliyoijenga, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Yuda? Katika uzee wake, hata hivyo, alipata ugonjwa wa miguu.
24 And Asa slepte with hise fadris, and he was biried with hem in the citee of Dauid, his fader; and Josophat, his sone, regnede for him.
Kisha Asa akalala pamoja na baba zake na kuzikwa pamoja nao katika mji wa Daudi baba yake. Naye Yehoshafati mwanawe akawa mfalme baada yake.
25 Forsothe Nadab, the sone of Jeroboam, regnede on Israel, in the secunde yeer of Asa, king of Juda; and he regnede on Israel two yeer.
Nadabu mwana wa Yeroboamu akawa mfalme wa Israeli katika mwaka wa pili wa utawala wa Mfalme Asa wa Yuda, naye akatawala Israeli kwa miaka miwili.
26 And he dide that, that was yuel in the siyt of the Lord, and he yede in the weies of his fadir, and in the synnes of hym, in whiche he made Israel to do synne.
Akafanya maovu machoni pa Bwana, akienenda katika njia za baba yake na katika dhambi yake, ambayo alisababisha Israeli kuifanya.
27 Forsothe Baasa, the sone of Ahia, of the hows of Ysachar, settide tresoun to hym, and smoot him in Gebethon, which is a citee of Filisteis; sothely Nadab and al Israel bisegiden Gebethon.
Baasha mwana wa Ahiya wa nyumba ya Isakari akafanya shauri baya dhidi yake, naye akamuua huko Gibethoni, mji wa Wafilisti, wakati Nadabu na Israeli yote walipokuwa wameuzingira.
28 Therfor Baasa killide hym, in the thridde yeer of Asa, king of Juda, and regnede for hym.
Baasha akamuua Nadabu katika mwaka wa tatu wa utawala wa Asa mfalme wa Yuda, naye Baasha akaingia mahali pake kuwa mfalme.
29 And whanne he hadde regnede, he smoot al the hows of Jeroboam; he lefte not sotheli not o man of his seed, til he dide awei hym, bi the word of the Lord, which he spak in the hond of his seruaunt, Ahia of Silo, a profete,
Mara tu alipoanza kutawala, aliua jamaa yote ya Yeroboamu. Hakumwachia Yeroboamu yeyote aliyekuwa hai, bali aliwaangamiza wote, kulingana na neno la Bwana lililotolewa kupitia kwa mtumishi wake Ahiya Mshiloni,
30 for the synnes of Jeroboam whiche he synnede, and in whiche he made Israel to do synne, and for the trespas, bi which he wraththide the Lord God of Israel.
kwa sababu ya dhambi alizokuwa amezitenda Yeroboamu na kusababisha Israeli kuzitenda, tena kwa sababu alimkasirisha Bwana, Mungu wa Israeli.
31 Sotheli the residue of wordis of Nadab, and alle thingis whiche he wrouyte, whether these ben not writun in the book of wordis of daies of the kyngis of Israel?
Kwa matukio mengine ya utawala wa Nadabu na yote aliyofanya, je hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli?
32 And batel was bitwixe Asa and Baasa, kyng of Israel, in al the daies of hem.
Kulikuwa na vita kati ya Asa na Baasha mfalme wa Israeli wakati wote wa utawala wao.
33 In the thridde yeer of Asa, kyng of Juda, Baasa, sone of Ahia, regnede on al Israel, in Thersa, foure and twenti yeer.
Katika mwaka wa tatu wa utawala wa Asa mfalme wa Yuda, Baasha mwana wa Ahiya akawa mfalme wa Israeli yote huko Tirsa, naye akatawala kwa miaka ishirini na minne.
34 And he dide yuel bifor the Lord, and he yede in the weies of Jeroboam, and in hise synnes, bi whiche he made Israel to do synne.
Akatenda maovu machoni pa Bwana, akienenda katika njia za Yeroboamu na dhambi yake, ambayo alikuwa amesababisha Israeli kuitenda.

< 1 Kings 15 >