< 1 Corinthians 7 >
1 But of thilke thingis that ye han write to me, it is good to a man to touche not a womman.
Kuhusu mambo mliyoniandikia: Kuna wakati ambapo ni vizuri mwanaume asilale na mke wake.
2 But for fornycacioun eche man haue his owne wijf, and ech womman haue hir owne hosebonde.
Lakini kwa sababu ya majaribu mengi ya zinaa kila mwanaume awe na mkewe, na kila mwanamke awe na mmewe.
3 The hosebonde yelde dette to the wijf, and also the wijf to the hosebonde.
Mume anapaswa kumpa mke haki yake ya ndoa, na vile vile mke naye kwa mmewe.
4 The womman hath not power of hir bodi, but the hosebonde; and the hosebonde hath not power of his bodi, but the womman.
Si mke aliye na mamlaka juu ya mwili wake, ni mme. Na vile vile, mme naye hana mamlaka juu ya mwili wake, bali mke anayo.
5 Nyle ye defraude eche to othere, but perauenture of consent to a tyme, that ye yyue tent to preier; and eft turne ye ayen to the same thing, lest Sathanas tempte you for youre vncontynence.
Msinyimane mnapolala pamoja, isipokuwa mmekubaliana kwa muda maalum. Fanyeni hivyo ili kupata muda wa maombi. Kisha mnaweza kurudiana tena pamoja, Ili kwamba Shetani asije akawajaribu kwa kukosa kiasi.
6 But Y seie this thing as yyuyng leeue, not bi comaundement.
Lakini nasema haya mambo kwa hiari na si kama amri.
7 For Y wole, that alle men be as my silf. But eche man hath his propre yifte of God; oon thus, and another thus.
Natamani kila mmoja angekuwa kama mimi nilivyo. Lakini kila mmoja ana karama yake kutoka kwa Mungu. Huyu ana karama hii, na yule ana karama ile.
8 But Y seie to hem, that ben not weddid, and to widewis, it is good to hem, if thei dwellen so as Y.
Kwa wasioolewa na wajane ninasema kwamba, ni vizuri kwao kama wakibaki bila kuolewa, kama nilivyo mimi.
9 That if thei conteynen not hem silf, be thei weddid; for it is betere to be weddid, than to be brent.
Lakini kama hawawezi kujizuia, wanapaswa kuolewa. Kwa kuwa heri kwao kuolewa kuliko kuwaka tamaa.
10 But to hem that ben ioyned in matrymonye, Y comaunde, not Y, but the Lord, that the wijf departe not fro the hosebonde;
Sasa kwa wale walioolewa nawapa amri, si mimi bali ni Bwana. “Mke asitengane na mme wake.”
11 and that if sche departith, that sche dwelle vnweddid, or be recounselid to hir hosebonde; and the hosebonde forsake not the wijf.
Lakini kama akijitenga kutoka kwa mmewe, abaki hivyo bila kuolewa au vinginevyo apatane na mmewe. Na “Mme asimpe talaka mke wake.”
12 But to othere Y seie, not the Lord. If ony brother hath an vnfeithful wijf, and sche consenteth to dwelle with hym, leeue he hir not.
Lakini kwa waliobaki, nasema- mimi, si Bwana- kwamba kama ndugu yeyote ana mke asiyeamini na anaridhika kuishi naye, hapaswi kumwacha.
13 And if ony womman hath an vnfeithful hosebonde, and this consentith to dwelle with hir, leeue sche not the hosebonde.
Kama mwanamke ana mme asiyeamini, na kama anaridhika kuishi naye, asimwache.
14 For the vnfeithful hosebonde is halewid bi the feithful womman, and the vnfeithful womman is halewid bi the feithful hosebonde. Ellis youre children weren vncleene, but now thei ben hooli.
Kwa mme asiyeamini anatakaswa kwa sababu ya imani ya mkewe. Na mwanamke asiyeamini anatakaswa kwa sababu ya mmewe aaminiye. Vinginevyo watoto wenu wangekuwa si safi, lakini kwa kweli wametakaswa.
15 That if the vnfeithful departith, departe he. For whi the brother or sistir is not suget to seruage in siche; for God hath clepid vs in pees.
Lakini mwenzi asiyeamini akiondoka na aende. Kwa namna hiyo, kaka au dada hafungwi na viapo vyao. Mungu ametuita tuishi kwa amani.
16 And wherof wost thou, womman, if thou schalt make the man saaf; or wherof wost thou, man, if thou schalt make the womman saaf?
Unajuaje kama mwanamke, huenda utamwokoa mmeo? Au unajuaje kama mwanaume, huenda utamwokoa mkeo?
17 But as the Lord hath departid to ech, and as God hath clepid ech man, so go he, as Y teche in alle chirchis.
Kila mmoja tu aishi maisha kama Bwana alivyowagawia, kila mmoja kama Mungu alivyowaita wao. Huu ni mwongozo wangu kwa makanisa yote.
18 A man circumcidid is clepid, brynge he not to the prepucie. A man is clepid in prepucie, be he not circumcidid.
Yupo aliyekuwa ametahiriwa alipoitwa kuamini? Asijaribu kuondoa alama ya tohara yake. Yupo yeyote aliyeitwa katika imani hajatahiriwa? Hapaswi kutahiriwa.
19 Circumcisioun is nouyt, and prepucie is nouyt, but the kepyng of the maundementis of God.
Kwa hili aidha ametahiriwa wala asiye tahiriwa hakuna matatizo. Chenye matatizo ni kutii amri za Mungu.
20 Ech man in what clepyng he is clepid, in that dwelle he.
Kila mmoja abaki katika wito alivyokuwa alipoitwa na Mungu kuamini.
21 Thou seruaunt art clepid, be it no charge to thee; but if thou maist be fre, `the rather vse thou.
Ulikuwa mtumwa wakati Mungu alipokuita? Usijali kuhusu hiyo. Lakini kama unaweza kuwa huru, fanya hivyo.
22 He that is a seruaunt, and is clepid in the Lord, is a freman of the Lord. Also he that is a freman, and is clepid, is the seruaunt of Crist.
Kwa mmoja aliyeitwa na Bwana kama mtumwa ni mtu huru katika Bwana. Kama vile, mmoja aliye huru alipoitwa kuamini ni mtumwa wa Kristo.
23 With prijs ye ben bouyt; nyle ye be maad seruauntis of men.
Mmekwisha nunuliwa kwa thamani, hivyo msiwe watumwa wa wanadamu.
24 Therfor ech man in what thing he is clepid a brothir, dwelle he in this anentis God.
Kaka na dada zangu, katika maisha yoyote kila mmoja wetu tulipoitwa kuamini, tubaki kama vile.
25 But of virgyns Y haue no comaundement of God; but Y yyue counseil, as he that hath mercy of the Lord, that Y be trewe.
Sasa, wale wote ambao hawajaoa kamwe, sina amri kutoka kwa Bwana. Lakini nawapa maoni yangu kama nilivyo. Kwa huruma za Bwana, zinazo aminika
26 Therfor Y gesse, that this thing is good for the present nede; for it is good to a man to be so.
Kwa hiyo, ninafikiri hivyo kwa sababu ya usumbufu, ni vyema mwanaume abaki kama alivyo.
27 Thou art boundun to a wijf, nyle thou seke vnbyndyng; thou art vnboundun fro a wijf, nyle thou seke a wijf.
Umefungwa kwa mwanamke na kiapo cha ndoa? Usitake uhuru kutoka kwa hiyo. Una uhuru kutoka kwa mke au hujaolewa? Usitafute mke.
28 But if thou hast takun a wijf, thou hast not synned; and if a maidun is weddid, sche synnede not; nethelesse siche schulen haue tribulacioun of fleisch.
Lakini kama ukioa, hujafanya dhambi. Na kama mwanamke hajolewa akiolewa, hajafanya dhambi. Bado wale wanaoana wanapata masumbufu ya aina mbalimbali. Nami nataka niwaepushe hayo.
29 But Y spare you. Therfor, britheren, Y seie this thing, The tyme is schort. Another is this, that thei that han wyues, be as thouy thei hadden noon;
Lakini nasema hivi, kaka na dada zangu, muda ni mfupi. Tangu sasa na kuendelea, wale walio na wake waishi kama hawana.
30 and thei that wepen, as thei wepten not; and thei that ioien, as thei ioieden not; and thei that bien, as thei hadden not;
Wote walio na huzuni wajifanye kama walikuwa hawana huzuni, na wote wanaofurahi, kama walikuwa hawafurahi, na wote wanaonunua kitu chochote, kama hawakumiliki chochote.
31 and thei that vsen this world, as thei that vsen not. For whi the figure of this world passith.
Na wote wanaoshughulika na ulimwengu, wawe kama hawakushughulika nao. Kwa kuwa mitindo ya dunia inafikia mwisho wake.
32 But Y wole, that ye be without bisynesse, for he that is without wijf, is bisi what thingis ben of the Lord, hou he schal plese God.
Ninataka muwe huru kwa masumbufu yote. Mwanaume asiyeoa anajihusisha na vitu vinavyo mhusu Bwana, namna ya kumpendeza yeye.
33 But he that is with a wijf, is bysy what thingis ben of the world, hou he schal plese the wijf, and he is departid.
Lakini mwanaume aliyeoa hujihusisha na mambo ya dunia, namna ya kumpendeza mkewe,
34 And a womman vnweddid and maidun thenkith what thingis ben of the Lord, that sche be hooli in bodi and spirit. But sche that is weddid, thenkith what thingis ben of the world, hou sche schal plese the hosebonde.
amegawanyika. Mwanawake asiyeolewa au bikira hujihusisha na vitu kuhusu Bwana, namna ya kujitenga katika mwili na katika roho. Lakini mwanamke aliyeolewa hujihusisha kuhusu vitu dunia, namna ya kumfurahisha mme wake.
35 And Y seie these thingis to youre profit, not that Y caste to you a snare, but to that that is onest, and that yyueth esynesse, with outen lettyng to make preieris to the Lord.
Nasema hivi kwa faida yenu wenyewe, na siweki mtego kwenu. Nasema hivi kwa vile ni haki, ili kwamba mnaweza kujiweka wakfu kwa Bwana bila kikwazo chochote.
36 And if ony man gessith hym silf to be seyn foule on his virgyn, that sche is ful woxun, and so it bihoueth to be doon, do sche that that sche wole; sche synneth not, if sche be weddid.
Lakini kama mtu anafikiri hawezi kumtendea kwa heshima mwanawali wake, kwa sababu ya hisia zake zina nguvu sana, acha aoane naye kama apendavyo. Siyo dhambi.
37 For he that ordeynede stabli in his herte, not hauynge nede, but hauynge power of his wille, and hath demed in his herte this thing, to kepe his virgyn, doith wel.
Lakini kama amefanya maamuzi kutokuoa, na hakuna haja ya lazima, na kama anaweza kutawala hamu yake, atafanya vyema kama hatamwoa.
38 Therfore he that ioyneth his virgyn in matrymonye, doith wel; and he that ioyneth not, doith betere.
Hivyo, anayemwoa mwanamwali wake afanya vyema, na yeyote ambaye anachagua kutooa atafanya vyema zaidi.
39 The womman is boundun to the lawe, as longe tyme as hir hosebonde lyueth; and if hir hosebonde is deed, sche is delyuered fro the lawe of the hosebonde, be sche weddid to whom sche wole, oneli in the Lord.
Mwanamke amefungwa na mmewe wakati yu hai. Lakini kama mmewe akifa, yuko huru kuolewa na yeyote ampendaye, lakini katika Bwana tu.
40 But sche schal be more blessid, if sche dwellith thus, aftir my counsel; and Y wene, that Y haue the Spirit of God.
Bado katika maamuzi yangu, atakuwa na furaha zaidi kama akiishi kama alivyo. Na ninafikiri kuwa nami pia nina Roho wa Mungu.