< 1 Corinthians 12 >

1 But of spiritual thingis, britheren, Y nyle that ye vnknowun.
Basi ndugu zangu, kuhusu karama za rohoni, sitaki mkose kufahamu.
2 For ye witen, that whanne ye weren hethene men, hou ye weren led goynge to doumbe maumetis.
Mnajua kwamba mlipokuwa watu wasiomjua Mungu, kwa njia moja au ingine mlishawishika na kupotoshwa mkielekezwa kwa sanamu zisizonena.
3 Therfor Y make knowun to you, that no man spekynge in the spirit of God, seith departyng fro Jhesu; and no man may seie the Lord Jhesu, but in the Hooli Goost.
Kwa hiyo nawaambieni ya kuwa hakuna mtu anayeongozwa na Roho wa Mungu anayeweza kusema, “Yesu na alaaniwe.” Pia hakuna mtu awezaye kusema, “Yesu ni Bwana,” isipokuwa ameongozwa na Roho Mtakatifu.
4 And dyuerse graces ther ben, but it is al oon Spirit;
Kuna aina mbalimbali za karama, lakini Roho ni yule yule.
5 and dyuerse seruyces ther ben, but it is al oon Lord; and dyuerse worchingis ther ben,
Kuna huduma za aina mbalimbali, lakini Bwana ni yule yule.
6 but `al is oon God, that worchith alle thingis in alle thingis.
Kisha kuna tofauti za kutenda kazi, lakini ni Mungu yule yule atendaye kazi zote kwa watu wote.
7 And to ech man the schewyng of spirit is youun to profit. The word of wisdom is youun to oon bi spirit;
Basi kila mmoja hupewa ufunuo wa Roho kwa faida ya wote.
8 to another the word of kunnyng, bi the same spirit;
Maana mtu mmoja kwa Roho hupewa neno la hekima na mwingine neno la maarifa kwa Roho huyo huyo.
9 feith to another, in the same spirit; to anothere, grace of helthis, in o spirit;
Mtu mwingine imani kwa huyo Roho na mwingine karama za kuponya kwa huyo Roho mmoja.
10 to another, the worchyng of vertues; to another, profecie; to another, very knowyng of spiritis; to another, kyndis of langagis; to another, expownyng of wordis.
Kwa mwingine matendo ya miujiza, kwa mwingine unabii kwa mwingine kupambanua roho, kwa mwingine aina mbalimbali za lugha, na kwa mwingine bado, tafsiri za lugha.
11 And oon and the same spirit worchith alle these thingis, departynge to ech bi hem silf as he wole.
Haya yote hufanywa na huyo huyo Roho mmoja, Roho naye humgawia kila mtu, kama apendavyo.
12 For as ther is o body, and hath many membris, and alle the membris of the bodi whanne tho ben manye, ben o bodi, so also Crist.
Kama vile mwili ulivyo mmoja nao una viungo vingi, navyo viungo vyote vya mwili ingawa ni vingi, ni mwili mmoja, vivyo hivyo na Kristo.
13 For in o spirit alle we ben baptisid `in to o bodi, ether Jewis, ether hethene, ether seruauntis, ether free; and alle we ben fillid with drink in o spirit.
Kwa maana katika Roho mmoja wote tulibatizwa katika mwili mmoja, kama ni Wayahudi au Wayunani, kama ni watumwa au watu huru, nasi sote tulinyweshwa Roho mmoja.
14 For the bodi is not o membre, but manye.
Basi mwili si kiungo kimoja, bali ni viungo vingi.
15 If the foot seith, For Y am not the hoond, Y am not of the bodi; not therfor it is not of the bodi.
Kama mguu ungesema, “Kwa kuwa mimi si mkono basi mimi si wa mwili,” hiyo isingefanya huo mguu usiwe sehemu ya mwili.
16 And if the ere seith, For Y am not the iye, Y am not of the bodi; not therfor it is not of the bodi.
Na kama sikio lingesema, “Kwa kuwa mimi si jicho, basi mimi si wa mwili,” hiyo isingefanya hilo sikio lisiwe sehemu ya mwili.
17 If al the bodi is the iye, where is heryng? and if al the bodi is heryng, where is smellyng?
Kama mwili wote ungelikuwa jicho, kusikia kungekuwa wapi? Au kama mwili wote ungelikuwa sikio, kunusa kungekuwa wapi?
18 But now God hath set membris, and ech of hem in the bodi, as he wolde.
Lakini kama ilivyo, Mungu ameweka viungo katika mwili, kila kimoja kama alivyopenda.
19 That if alle weren o membre, where were the bodi?
Kama vyote vingekuwa kiungo kimoja, mwili ungekuwa wapi?
20 But now ther ben many membris, but o bodi.
Kama ulivyo, una viungo vingi, lakini mwili ni mmoja.
21 And the iye may not seie to the hond, Y haue no nede to thi werkis; or eft the heed to the feet, Ye ben not necessarie to me.
Jicho haliwezi kuuambia mkono, “Sina haja nawe!” Wala kichwa hakiwezi kuiambia miguu, “Sina haja na ninyi!”
22 But myche more tho that ben seyn to be the lowere membris of the bodi, ben more nedeful;
Lakini badala yake, vile viungo vya mwili vinavyoonekana kuwa dhaifu, ndivyo ambavyo ni vya muhimu sana.
23 and thilke that we gessen to be the vnworthier membris of the bodi, we yyuen more honour `to hem; and tho membris that ben vnonest, han more oneste.
Navyo vile viungo tunavyoviona havina heshima, ndivyo tunavipa heshima maalum. Vile viungo vya mwili ambavyo havina uzuri, tunavipa heshima ya pekee;
24 For oure oneste membris han nede of noon; but God tempride the bodi, yyuynge more worschip to it, to whom it failide,
wakati vile viungo vyenye uzuri havihitaji utunzaji wa pekee. Lakini Mungu ameviweka pamoja viungo vya mwili na akavipa heshima zaidi vile vilivyopungukiwa,
25 that debate be not in the bodi, but that the membris be bisi in to the same thing ech for othere.
ili pasiwe na mafarakano katika mwili, bali viungo vyote vihudumiane kwa usawa kila kimoja na mwenzake.
26 And if o membre suffrith ony thing, alle membris suffren therwith; ethir if o membre ioieth, alle membris ioien togidere.
Kama kiungo kimoja kikiumia, viungo vyote huumia pamoja nacho, kama kiungo kimoja kikipewa heshima, viungo vyote hufurahi pamoja nacho.
27 And ye ben the bodi of Crist, and membris of membre.
Sasa ninyi ni mwili wa Kristo na kila mmoja wenu ni sehemu ya huo mwili.
28 But God sette sum men in the chirche, fyrst apostlis, the secunde tyme prophetis, the thridde techeris, aftirward vertues, aftirward graces of heelyngis, helpyngis, gouernails, kyndis of langagis, interpretaciouns of wordis.
Mungu ameweka katika kanisa, kwanza mitume, pili manabii, tatu walimu, kisha watenda miujiza, pia karama za kuponya, karama za kusaidiana, karama za uongozi, aina mbalimbali za lugha.
29 Whether alle apostlis? whethir alle prophetis? whether alle techeris? whether alle vertues?
Je, wote ni mitume? Je, wote ni manabii? Je, wote ni walimu? Je, wote wanatenda miujiza?
30 whether alle men han grace of heelyngis? whether alle speken with langagis? whether alle expownen?
Je, wote wana karama ya kuponya? Je, wote hunena kwa lugha mpya? Je, wote wanatafsiri?
31 But sue ye the betere goostli yiftis. And yit Y schewe to you a more exellent weye.
Basi tamanini sana karama zilizo kuu. Nami nitawaonyesha njia iliyo bora zaidi.

< 1 Corinthians 12 >