< 1 Chronicles 22 >

1 And Dauid seide, This is the hows of God, and this auter is in to brent sacrifice of Israel.
Kisha Daudi akasema, “Hapo ndipo nyumba ya Yahweh Mungu itakuwepo, na madhabahu ya sadaka za kuteketezwa za Israeli.”
2 And he comaundide that alle conuersis fro hethenesse to the lawe of Israel `schulden be gaderid `of the lond of Israel; and he ordeynede of hem masouns for to kytte stoonys and for to polische, that the hows of the Lord schulde be bildid;
Hivyo Daudi akaagiza watumishi wake wawakusanye pamoja wageni wote wanao ishi katika nchi ya Israeli. Aliwapangia kuwa wachonga mawe, kuchonga matofali ya mawe, ilikuweza kujenga nyumba ya Mungu.
3 also Dauid made redy ful myche yrun to the nailes of the yatis, and to the medlyngis and ioyntouris, and vnnoumbrable weiyte of bras;
Daudi alisambaza idadi kubwa ya chuma kwa ajili ya misumari na vitasa vya kuweka kwenye malango. Pia alitoa shaba zaidi kushinda kipimo,
4 also the trees of cedre myyten not be gessid, whiche the men of Sidonye and the men of Tyre brouyten to Dauid.
na miti ya mierezi zaidi ya kipimo. (Wasidoni na Watiria walileta mboa nyingi za mierezi kwa Daudi azihesabu.)
5 And Dauid seide, Salomon, my sone, is a litil child and delicat; sotheli the hows, which Y wole be bildid to the Lord, owith to be sich, that it be named in alle cuntrees; therfor Y schal make redi necessaries to hym. And for this cause Dauid bifor his deeth made redi alle costis.
Daudi akasema, “Mwanangu Sulemani ni mdogo na hana uzoefu, na nyumba itayo jengwa kwa Yahweh lazima iwe maridadi, ilikwamba iwe maarufu na ya utukufu kwa nchi zingine. Hivyo nitaanda ujenzi wake.” Hivyo Daudi akafanya maandalizi ya kina kabla ya mauti yake.
6 And he clepide Salomon, his sone, and comaundide to hym, that he schulde bilde an hows to the Lord God of Israel.
Akaagiza Sulemani mwanae kuitwa na kumuamuru ajenge nyumba ya Yahweh, Mungu wa Israeli.
7 And Dauid seide to Salomon, My sone, it was my wille to bilde an hows to the name of `my Lord God;
Daudi akasema kwa Sulemani, “Mwanangu, ilikuwa dhamira yangu kujenga nyumba mwenyewe, kwa ajili ya jina la Yahweh Mungu wangu.
8 but the word of the Lord was made to me, and seide, Thou hast sched out myche blood, and thou hast fouyt ful many batels; thou mayst not bilde an hows to my name, for thou hast sched out so myche blood bifor me;
Lakini Yahweh alikuja kwangu na kusema, 'Wewe umemwaga damu nyingi na umepigana mapambono mengi. Hauta jenga nyumba kwa jina langu, kwasababu umemwaga damu nyingi kwenye ardhi machoni pangu.
9 the sone that schal be borun to thee, schal be a man most pesible, for Y schal make hym to haue reste of alle hise enemyes bi cumpas, and for this cause he schal be clepid pesible, and Y schal yyue pees and reste in Israel in alle hise daies.
Walakini, utapata mwana ambaye atakuwa mtu wa amani. Nitampa kupumzika na maadui zake kwa kila upande. Kwa kuwa jina lake litaitwa Sulemani, na nitatoa amani na utulivu kwa Israeli katika siku zake.
10 He schal bilde an hows to my name; he schal be to me in to a sone, and Y schal be to hym in to a fadir, and Y schal make stidefast the seete of his rewme on Israel withouten ende.
Ata jenga nyumba kwa jina langu. Ata kuwa mwana wangu, na nitakuwa baba yake. Nitaimarisha kiti cha enzi cha ufalme wake juu ya Israeli.
11 Now therfor, my sone, the Lord be with thee, and haue thou prosperite, and bilde thou an hows to `thi Lord God, as he spak of thee.
Sasa, mwanangu, Yahweh awe nawe na kukuwezesha kufanikiwa. Uweze kujenga nyumba ya Yahweh Mungu wako, kama alivyo sema utajenga.
12 And the Lord yyue to thee prudence and wit, that thou mow gouerne Israel, and kepe the lawe of `thi Lord God.
Yahweh tu akupe uwelewa na ufahamu, ili utii sheria ya Yahweh Mungu wako, ata kapokuweka kiongozi juu ya Israeli.
13 For thanne thou maist profite, if thou kepist the comaundementis and domes, whiche the Lord comaundide to Moises, that he schulde teche Israel; be thou coumfortid, and do manli, drede thou not `with outforth, nether drede thou `with ynne.
Kisha utafanikiwa, kama tu ukitii maagizo na amri Yahweh alizo mpa Musa kuhusu Israeli. Kuwa hodari na mshujaa. Usiogope wala kufadhaika.
14 Lo! in my pouert Y haue maad redi the costis of the hows of the Lord; an hundrid thousinde talentis of gold, and a thousynde thousynde talentis of siluer; sotheli of bras and irun is no weiyte, for the noumbre is ouercomun bi greetnesse; Y haue maad redi trees and stoonys to alle costis.
Sasa, ona, kwa bidii kubwa nimeandaa kwa ajili ya nyumba ya Yahweh talanta 100, 000 za dhahabu, talanta milioni moja za fedha, na shaba na chuma katika idadi kubwa. Pia nimetoa mbao na mawe. Lazima uongeze zaidi katika haya.
15 Also thou hast ful many crafti men, masouns, and leggeris of stonys, and crafti men of trees, and of alle craftis,
Una wafanya kazi wengi: wachonga mawe, maseremala, wanaume wenye ujuzi mbali mbali,
16 most prudent to make werk, in gold, and siluer, and bras, and in yrun, of which is no noumbre; therfor rise thou, and make, and the Lord schal be with thee.
wenye uwezo wa kufanya kazi na dhahabu, fedha, shaba, na nishati. Hivyo anza kufanya kazi, na Yahweh awe nawe.
17 Also Dauid comaundide to alle the princis of Israel, that thei schulden helpe Salomon,
Daudi akawaagiza viongozi wote Waisraeli wamsaidie Sulemani mwanae, akisema,
18 his sone, and seide, Ye seen, that `youre Lord God is with you, and hath youe to you reste `by cumpas, and hath bitake alle enemyes in youre hoond, and the erthe is suget bifor the Lord, and bifor his puple.
“Yahweh Mungu wenu yupo nanyi na amewapa amani kila pande. Amewakabidhi mikononi mwangu wenyeji wote mkoa. Mkoa umetiishwa mbele za Yahweh na watu wake.
19 Therfor yyue youre hertis and youre soulis, that ye seke `youre Lord God; and rise ye togidere, and bilde ye a seyntuarie to `youre Lord God, that the arke of boond of pees of the Lord be brouyt in, and that vessels halewid to the Lord be brouyt in to the hows, which is bildid to the name of the Lord.
Sasa mtafuteni Yahweh Mungu wenu kwa moyo wenu wote na nafsi. Simameni na mjenge sehemu takatifu ya Yahweh Mungu. Kisha mwaweza kuleta sanduku la agano la Yahweh na vitu vya Mungu ndani ya nyumba iliyo jengwa kwa ajili ya jina la Yahweh.

< 1 Chronicles 22 >