< 1 Chronicles 15 >

1 And he made to hym housis in the citee of Dauid, and he bildide `a place to the arke of the Lord, and araiede a tabernacle to it.
Baada ya Daudi kujijengea nyumba zake katika Mji wa Daudi, akatengeneza sehemu kwa ajili ya Sanduku la Mungu, kisha akasimamisha hema kwa ajili yake.
2 Thanne Dauid seide, It is vnleueful, that the arke of God be borun of `ony thing no but of the dekenes, whiche the Lord chees to bere it, and `for to mynystre to hym `til in to with outen ende.
Kisha Daudi akasema, “Hakuna mtu yeyote anayeruhusiwa kulibeba Sanduku la Mungu isipokuwa Walawi peke yao, kwa sababu Bwana aliwachagua kulibeba Sanduku la Bwana na kuhudumu mbele zake milele.”
3 And he gaderide togidere al Israel in to Jerusalem, that the arke of God schulde be brouyt in to `his place, which he hadde maad redy to it;
Daudi akawakusanya Israeli wote huko Yerusalemu ili kulipandisha Sanduku la Bwana na kulileta hadi kwenye sehemu aliyokuwa ametengeneza kwa ajili yake.
4 also and he gaderide togidere the sones of Aaron, and the dekenes;
Kisha Daudi akawakusanya pamoja wazao wa Aroni na Walawi:
5 of the sones of Caath Vriel was prince, and hise britheren two hundrid and twenti;
Kutoka wazao wa Kohathi, Urieli kiongozi na ndugu zake 120,
6 of the sones of Merari Asaya was prince, and hise britheren two hundrid and thritti;
Kutoka wazao wa Merari, Asaya kiongozi na ndugu zake 220.
7 of the sones of Gerson the prince was Johel, and hise britheren an hundrid and thretti;
Kutoka wazao wa Gershoni, Yoeli kiongozi na ndugu zake 130.
8 of the sones of Elisaphan Semei was prynce, and hise britheren two hundrid;
Kutoka wazao wa Elisafani, Shemaya kiongozi na ndugu zake 200.
9 of the sones of Ebroun Heliel was prince, and hise britheren foure score;
Kutoka wazao wa Hebroni, Elieli kiongozi na ndugu zake 80.
10 of the sones of Oziel Amynadab was prince, and hise britheren an hundrid and twelue.
Kutoka wazao wa Uzieli, Aminadabu kiongozi na ndugu zake 112.
11 And Dauid clepide Sadoch and Abiathar preestis, and the dekenes Vriel, Asaie, Johel, Semeie, Eliel, and Amynadab; and seide to hem,
Kisha Daudi akawaita makuhani Sadoki na Abiathari, pamoja na Walawi Urieli, Asaya, Yoeli, Shemaya, Elieli na Aminadabu.
12 Ye that ben princes of the meynees of Leuy, be halewid with youre britheren, and brynge ye the arke of the Lord God of Israel to the place, which is maad redi to it;
Akawaambia, “Ninyi ndio viongozi wa jamaa za Walawi. Ninyi pamoja na Walawi wenzenu inawapasa mjitakase na kulipandisha Sanduku la Bwana, Mungu wa Israeli hadi mahali ambapo nimetengeneza kwa ajili yake.
13 lest, as at the bigynnyng, for ye weren not present, the Lord smoot vs, and now it be don, if we don ony vnleueful thing.
Ilikuwa ni kwa sababu hii, ninyi Walawi, hamkulipandisha Sanduku la Bwana mara ya kwanza, hata ikasababisha Bwana Mungu wetu kuwaka hasira dhidi yetu. Hatukumuuliza jinsi ya kufanya ili tupate kulileta jinsi alivyoagiza.”
14 Therfor the preestis and dekenes weren halewid, that thei schulden bere the arke of the Lord God of Israel.
Kwa hiyo makuhani pamoja na Walawi wakajitakasa ili kulipandisha Sanduku la Bwana, Mungu wa Israeli.
15 And the sones of Leuy token the arke of God with barris on her schuldris, as Moises comaundide bi the word of the Lord.
Nao Walawi wakalichukua Sanduku la Mungu mabegani mwao wakitumia mipiko, kama vile Mose alivyoamuru sawasawa na neno la Bwana.
16 And Dauid seide to the princes of dekenes, that thei schulden ordeyne of her britheren syngeris in orguns of musikis, that is, in giternes, and harpis, and symbalis; that the sown of gladnesse schulde sowne an hiy.
Daudi akawaambia viongozi wa Walawi kuwaweka ndugu zao waimbaji ili waimbe nyimbo za shangwe, wakiwa na vyombo vya uimbaji: zeze, vinubi na matoazi.
17 And thei ordeyneden dekenes, Heman, the sone of Johel, and of hise britheren, Asaph, the sone of Barachie; sotheli of the sones of Merary, britheren of hem, thei ordeyneden Ethan,
Basi Walawi wakawaweka Hemani mwana wa Yoeli; kutoka miongoni mwa ndugu zake, Asafu mwana wa Berekia; kutoka miongoni mwa ndugu zao Wamerari, Ethani mwana wa Kushaiya;
18 the sone of Casaye, and the britheren of hem with hem; in the secunde ordre `thei ordeyneden Zacarie, and Ben, and Jazihel, and Semyramoth, and Jahiel, `and Am, Heliab, and Benaye, and Maasie, and Mathathie, and Eliphalu, and Mathenye, and Obededon, and Jehiel, porteris;
hawa ndio waliochaguliwa kuwa wasaidizi wao: Zekaria, Yaazieli, Shemiramothi, Yehieli, Uni, Eliabu, Benaya, Maaseya, Matithia, Elifelehu, Mikneya, pamoja na mabawabu Obed-Edomu na Yehieli.
19 forsothe `thei ordeyneden the syngeris Eman, Asaph, and Ethan, sownynge in brasun cymbalis;
Waimbaji Hemani, Asafu na Ethani walichaguliwa kupiga matoazi ya shaba;
20 sotheli Zacarie, and Oziel, and Semyramoth, and Jahihel, and Ham, and Eliab, and Maasie, and Banaie, sungun pryuetees in giternes; forsothe Mathathie,
Zekaria, Azieli, Shemiramothi, Yehieli, Uni, Eliabu, Maaseya na Benaya walikuwa wapiga zeze kufuatana na sauti ya alamothi,
21 and Eliphalu, and Mathenye, and Obededom, and Jehiel, and Ozazym, sungen in harpis for the eiytithe, and epynychion, `that is, victorie `be to God ouercomere;
na Matithia, Elifelehu, Mikneya, Obed-Edomu, Yehieli na Azazia walikuwa wapiga vinubi, wakiongozwa kwa kufuata sauti ya sheminithi.
22 forsothe Chinonye, the prince of dekenes, and of profecie, was souereyn to biforsynge melodie, for he was ful wijs;
Kenania kiongozi wa Walawi alikuwa msimamizi wa uimbaji; huu ndio uliokuwa wajibu wake kwa sababu alikuwa stadi katika hilo.
23 and Barachie, and Elchana, weren porters of the arke; forsothe Sebenye,
Berekia na Elikana walikuwa mabawabu kwa ajili ya Sanduku.
24 and Josaphath, and Mathanael, and Amasaye, and Zacarie, and Banaye, and Eliezer, preestis, sowneden with trumpis bifor the arke of the Lord; and Obededom, and Achymaas, weren porteris of the arke.
Shebania, Yoshafati, Nethaneli, Amasai, Zekaria, Benaya na Eliezeri, makuhani, walikuwa wapiga tarumbeta mbele ya Sanduku la Mungu. Obed-Edomu na Yehiya waliwekwa pia kuwa mabawabu wa Sanduku.
25 Therfor Dauid, and the grettere men in birthe of Israel, and the tribunes, yeden to brynge the arke of boond of pees of the Lord fro the hows of Obededom with gladnesse.
Basi Daudi pamoja na wazee wa Israeli na majemadari wa vikosi vya elfu wakaenda ili kulipandisha Sanduku la Agano la Bwana kutoka nyumba ya Obed-Edomu kwa shangwe.
26 And whanne God hadde helpid the dekenes that baren the arke of boond of pees of the Lord, seuene bolis and seuene rammes weren offrid.
Kwa sababu Mungu alikuwa amewasaidia Walawi waliokuwa wanalichukua Sanduku la Agano la Bwana, mafahali saba na kondoo dume saba walitolewa dhabihu.
27 Forsothe Dauid was clothid with a white stole, and alle the dekenes that baren the arke, and the syngeris, and Chononye, the prince of profecie among syngeris, weren clothid in white stolis; forsothe also Dauid was clothid with a lynun surplijs.
Basi Daudi alikuwa amevaa joho la kitani safi, kama walivyokuwa wamevaa Walawi wote waliokuwa wanalichukua lile Sanduku, waimbaji nao walivaa vivyo hivyo, pamoja na Kenania aliyekuwa anaongoza nyimbo za waimbaji. Daudi alivaa pia kisibau cha kitani safi.
28 And al Israel ledden forth the arke of boond of pees of the Lord, and sowneden in ioiful song, and in sown of clariouns, and in trumpis, and cymbalis, and giternis, and harpis.
Hivyo Israeli wote wakalipandisha Sanduku la Agano la Bwana kwa shangwe, wakipiga pembe za kondoo dume, tarumbeta, matoazi, wakipiga zeze na vinubi.
29 And whanne the arke of boond of pees of the Lord hadde come to the citee of Dauid, Mychol, the douytir of Saul, bihelde forth bi a wyndowe, and sche siy king Dauyd daunsynge and pleiynge; and sche dispiside hym in hir herte.
Sanduku la Agano la Bwana lilipokuwa linaingia katika Mji wa Daudi, Mikali binti Sauli akachungulia dirishani. Naye alipomwona Mfalme Daudi akicheza na kusherehekea, akamdharau moyoni mwake.

< 1 Chronicles 15 >