< 1 Chronicles 14 >
1 And Iram, the kyng of Tyre, sente messageris to Dauid, and `he sente trees of cedre, and werk men of wallis and of trees, that thei schulden bilde to hym an hows.
Basi Hiramu mfalme wa Tiro akawatuma wajumbe kwa Daudi, wakiwa na magogo ya mierezi, waashi na maseremala ili kumjengea jumba la kifalme.
2 And Dauid knewe that the Lord hadde confermyd hym in to kyng on Israel; and that his rewme was reisid on his puple Israel.
Naye Daudi akatambua kwamba Bwana amemwimarisha kuwa mfalme juu ya Israeli na kwamba ufalme wake umetukuzwa kwa ajili ya Israeli, watu wake.
3 And Dauid took othere wyues in Jerusalem, and gendride sones and douytris.
Huko Yerusalemu Daudi akaoa wake wengine zaidi na akawa baba wa wana na mabinti wengi.
4 And these ben the names of hem that weren borun to hym in Jerusalem; Sammu, and Sobab, Nathan, and Salomon,
Haya ndiyo majina ya watoto waliozaliwa kwake huko: Shamua, Shobabu, Nathani, Solomoni,
5 Jeber, and Elisu, and Heli, and Eliphalech,
Ibihari, Elishua, Elpeleti,
6 and Noga, and Napheg, and Japhie,
Noga, Nefegi, Yafia,
7 and Elisama, and Baliada, and Eliphelech.
Elishama, Beeliada na Elifeleti.
8 Forsothe the Filisteis herden that Dauid was anoyntid `in to kyng on al Israel, and alle stieden to seke Dauid. And whanne Dauid hadde herd this thing, he yede out ayens hem.
Wafilisti waliposikia kuwa Daudi ametiwa mafuta kuwa mfalme wa Israeli yote, wakapanda na jeshi lao lote kwenda kumsaka, lakini Daudi akapata habari hizo, naye akatoka ili kwenda kukabiliana nao.
9 Forsothe Filisteis camen, and weren spred abrood in the valey of Raphaym;
Basi Wafilisti walikuwa wameingia na kushambulia Bonde la Warefai,
10 and Dauid counselide the Lord, and seide, Whether Y schal stie to Filisteis? and whether thou schalt bitake hem in to myn hondis? And the Lord seide to hym, Stie thou, and Y schal bitake hem in thin hond.
Hivyo Daudi akamuuliza Mungu: “Je, niende kuwashambulia hao Wafilisti? Je, utawatia mikononi mwangu?” Bwana akamjibu, “Nenda, nitawatia mikononi mwako.”
11 And whanne thei hadden styed in to Baal Pharasym, Dauid smoot hem there, and seide, God hath departid myn enemyes bi myn hond, as watris ben departid. And therfor the name of that place was clepid Baal Pharasym; and thei leften there her goddis,
Hivyo Daudi pamoja na watu wake wakakwea mpaka Baal-Perasimu, akawashinda huko. Akasema, “Kama maji yafurikavyo, Mungu amewafurikia adui zangu kwa kutumia mkono wangu.” Kwa hiyo mahali pale pakaitwa Baal-Perasimu.
12 which Dauid comaundide to be brent.
Wafilisti walikuwa wameacha miungu yao huko, Daudi akaamuru iteketezwe kwa moto.
13 Forsothe another tyme Filisteis felden in, and weren spred abrood in the valei;
Kwa mara nyingine Wafilisti wakavamia lile bonde;
14 and eft Dauid counseilide the Lord, and the Lord seide to hym, Thou schalt not stie aftir hem; go awei fro hem, and thou schalt come ayens hem euen ayens the pere trees.
hivyo Daudi akamuuliza Mungu tena, naye Mungu akamjibu, “Usiwapandie moja kwa moja, bali wazungukie na uwashambulie kutoka mbele ya hiyo miti ya miforosadi.
15 And whanne thou schalt here the sowun of a goere in the cop of the pere trees, thanne thou schalt go out to batel; for the Lord is go out byfor thee, to smyte the castels of Filisteis.
Mara usikiapo sauti ya kwenda juu ya hiyo miti ya miforosadi, hapo ndipo utoke upigane vita, kwa sababu hiyo itaonyesha kwamba Mungu amekutangulia ili kupiga jeshi la Wafilisti.”
16 Therfor Dauid dide as God comaundide to hym, and he smoot the castels of Filisteis fro Gabaon `til to Gazara.
Kwa hiyo Daudi akafanya kama alivyoagizwa na Mungu, wakalipiga jeshi la Wafilisti kuanzia Gibeoni hadi Gezeri.
17 And the name of Dauid was puplischid in alle cuntreis, and the Lord yaf his drede on alle folkis.
Hivyo umaarufu wa Daudi ukaenea katika kila nchi, naye Bwana akayafanya mataifa yote kumwogopa Daudi.