< 1 Chronicles 12 >

1 Also these camen to Dauid in Sichelech, whanne he fledde yit fro Saul, the sone of Cys; whiche weren strongeste men and noble fiyterys,
Hawa ndio watu waliomjia Daudi huko Siklagi, wakati alikuwa amefukuzwa mbele ya Sauli mwana wa Kishi (walikuwa miongoni mwa mashujaa waliomsaidia Daudi vitani,
2 beendynge bouwe, and castynge stoonys with slyngis with euer either hond, and dressynge arowis; of the britheren of Saul of Beniamyn,
walikuwa na pinde na walikuwa na uwezo wa kupiga mishale au kutupa mawe kwa kombeo wakitumia mkono wa kushoto au wa kulia; hawa walikuwa ndugu zake Sauli kutoka kabila la Benyamini):
3 the prince Achieser, and Joas, the sones of Samaa of Gabaath, and Jazachel, and Phallech, the sones of Azmod, and Barachie, and Jehu of Anathot;
Mkuu wao alikuwa Ahiezeri, na wa pili Yoashi, wote wana wa Shemaa Mgibeathi; pia Yezieli na Peleti wana wa Azmawethi; Beraka, Yehu Mwanathothi,
4 also Samay of Gabaon was the strongeste among thretti and aboue thretti; Jeremy, and Jezihel, and Johannan, and Zebadga Zerothites,
na Ishmaya Mgibeoni, shujaa miongoni mwa wale Thelathini, ambaye alikuwa kiongozi wa wale Thelathini; Yeremia, Yahazieli, Yohanani, Yozabadi, Mgederathi,
5 Elusay, and Jerymoth, and Baalia, and Samaria, and Saphia Araphites,
Eluzai, Yeremothi, Bealia, Shemaria, Shefatia, Mharufi;
6 Elchana, and Jesia, and Azrahel, and Jezer, and Jesbaam of Taremy,
Elikana, Ishia, Azareli, Yoezeri na Yashobeamu, wana wa Kora;
7 and Joelam, and Sabadia, the sones of Jeroam of Jedor.
Yoela na Zebadia, wana wa Yerohamu, kutoka Gedori.
8 But also of Gaddi strongeste men, and beste fiyteris, holdynge scheld and spere, fledden ouer to Dauid, whanne he was hid in deseert; the faces of hem as the face of a lioun, and thei weren swift as capretis in hillis.
Baadhi ya Wagadi wakajitenga na kujiunga na Daudi katika ngome yake huko jangwani. Walikuwa mashujaa hodari, waliokuwa tayari kwa vita na wenye uwezo wa kutumia ngao na mkuki. Nyuso zao zilikuwa nyuso za simba na walikuwa na wepesi kama paa milimani.
9 Ozer was the prince, Obdias the secounde, Eliab the thridde,
Ezeri alikuwa mkuu wao, Obadia alikuwa wa pili katika uongozi, Eliabu wa tatu,
10 Masmana the fourthe, Jeremye the fyuethe,
Mishmana wa nne, Yeremia wa tano,
11 Becchi the sixte, Heliel the seuenthe,
Atai wa sita, Elieli wa saba,
12 Johannan the eiythe, Helzedad the nynthe,
Yohanani wa nane, Elzabadi wa tisa,
13 Jeremye the tenthe, Bachana the euleuenthe;
Yeremia wa kumi, na Makbanai wa kumi na moja.
14 these of the sones of Gad weren princes of the oost; the laste was souereyn ouer an hundrid knyytis, and the moost was souereyn ouer a thousynde.
Hawa Wagadi walikuwa majemadari. Aliyekuwa wa mwisho kuliko wote aliweza kuongoza askari 100, na aliyekuwa na uweza zaidi ya wote aliongoza 1,000.
15 These it ben that passiden ouer Jordan in the firste monethe, whanne it was wont to flowe ouer hise brynkis; and thei dryueden awei alle men that dwelliden in the valeis at the eest coost and west coost.
Wao ndio walivuka Mto Yordani katika mwezi wa kwanza ukiwa umefurika hadi kwenye kingo zake zote na kusababisha watu wote waliokuwa wanaishi kwenye mabonde kukimbilia mashariki na wengine magharibi.
16 Sotheli also men of Beniamyn and of Juda camen to the stronge hoold, whereyn Dauid dwellide.
Wabenyamini wengine na baadhi ya watu kutoka Yuda pia walikuja kwa Daudi katika ngome yake.
17 And Dauid yede out ayens hem, and seide, If ye `ben comyn pesible to me, for to helpe me, myn herte be ioyned to you; forsothe if ye setten aspies to me for myn aduersaries, sithen Y haue not wickidnesse in the hondis, God of our fadris se and deme.
Daudi akatoka nje kuwalaki na akawaambia, “Kama mmekuja kwangu kwa amani, kunisaidia, mimi niko tayari kuwaruhusu ninyi kuungana nami. Lakini kama mmekuja ili kunisaliti kwa adui zangu wakati mimi mikono yangu haina hatia, basi Mungu wa baba zetu aone na awahukumu.”
18 Forsothe the spirit clothide Amasay, the prynce among thritti, and he seide, A! Dauid, we ben thin, and thou, sone of Ysai, we schulen be with thee; pees, pees to thee, and pees to thin helperis, for thi Lord God helpith thee. Therfor Dauid resseyuede hem, and made princes of the cumpeny.
Kisha Roho akaja juu ya Amasai, mkuu wa wale Thelathini, naye akasema: “Sisi tu watu wako, ee Daudi! Nasi tuko pamoja na wewe, ee mwana wa Yese! Ushindi, naam, ushindi uwe kwako, pia ushindi kwa wale walio upande wako, kwa kuwa Mungu wako atakusaidia.” Kwa hiyo Daudi akawapokea na kuwafanya viongozi wa vikosi vyake vya uvamizi.
19 Forsothe men of Manasses fledden ouer to Dauid, whanne he cam with Filisteis to fiyte ayens Saul, and he fauyte not with hem, for after that the princes of Filisteis hadden take counsel, thei senten hym ayen, and seiden, With perel of oure heed he schal turne ayen to Saul his lord.
Baadhi ya watu kutoka kabila la Manase wakajiunga na Daudi wakati alikwenda pamoja na Wafilisti, kupigana na Sauli. (Daudi na watu wake hawakuwasaidia Wafilisti kwa sababu, baada ya ushauri, watawala wao walimrudisha. Wakasema, “Itatugharimu vichwa vyetu kama Daudi atatuasi na kurudi kwa Sauli bwana wake.”)
20 Therfor whanne Dauid turnede ayen in to Sichelech, men of Manasses fledden ouer to hym, Eduas, and Jozabad, Jedihel, and Mychael, and Naas, and Jozabath, and Helyu, and Salathi, princes of knyytis in Manasses.
Daudi alipokwenda Siklagi, hawa ndio watu wa kabila la Manase waliojiunga naye: Adna, Yozabadi, Yediaeli, Mikaeli, Yozabadi, Elihu na Silethai, viongozi wa vikosi vya watu 1,000 katika kabila la Manase.
21 These men yauen help to Dauid ayens theues; for alle weren strongeste men, and thei weren maad prynces in the oost.
Walimsaidia Daudi dhidi ya makundi ya uvamizi, kwa kuwa wote walikuwa mashujaa hodari na walikuwa majemadari katika jeshi lake.
22 But also bi ech dai men camen to Dauid, for to helpe hym, til that the noumbre was maad greet as the oost of God.
Siku baada ya siku watu walikuja kumsaidia Daudi, mpaka akawa na jeshi kubwa, kama jeshi la Mungu.
23 Also this is the noumbre of princes of the oost that camen to Dauid, whanne he was in Ebron, that thei schulden translate the rewme of Saul to hym, bi the word of the Lord; the sones of Juda,
Hawa ndio watu waliojiandaa kwa ajili ya vita waliokuja kwa Daudi huko Hebroni ili kumtwalia ufalme kutoka kwa Sauli, kama Bwana alivyokuwa amesema:
24 berynge scheeld and spere, sixe thousynde and eiyte hundrid, redi to batel;
watu wa Yuda, wanaochukua ngao na mikuki walikuwa 6,800 wote wakiwa tayari kwa vita.
25 of the sones of Simeon, seuene thousinde and an hundrid, of strongeste men to fiyte;
Watu wa Simeoni, mashujaa waliokuwa tayari kwa vita walikuwa 7,100.
26 of the sones of Leuy, foure thousynde and sixe hundrid;
Watu wa Lawi walikuwa 4,600,
27 also Joiada, prince of the generacioun of Aaron, and thre thousynd and seuene hundrid with hym;
pamoja na Yehoyada, kiongozi wa jamaa ya Aroni, aliyekuwa pamoja na watu 3,700,
28 also Sadoch, a child of noble wit, and the hows of his fadir, twei and twenti princes;
na Sadoki, kijana shujaa na hodari, aliyekuwa pamoja na maafisa ishirini na wawili kutoka jamaa yake.
29 forsothe of the sones of Beniamyn, britheren of Saul, thre thousynde; for a greet part of hem suede yit the hows of Saul;
Watu wa Benyamini, ndugu zake Sauli, walikuwa 3,000; wengi wao walikuwa wameendelea kuwa waaminifu kwa Sauli mpaka wakati huo.
30 forsothe of the sones of Effraym, twenti thousynde and eiyte hundrid, strongeste men in bodili myyt, men named in her meynees;
Watu wa Efraimu, mashujaa hodari 20,800, watu waliokuwa maarufu katika koo zao.
31 and of the half part of the lynage of Manasses, eiytene thousynde; alle camen bi her names, to make Dauid kyng;
Watu wa nusu ya kabila la Manase, waliotajwa kwa majina ili waje kumweka Daudi kuwa mfalme, watu 18,000.
32 also of the sones of Ysacar, two hundrid princes, lernd men, that knewen ech tyme to comaunde what the puple of Israel ouyt to do; sotheli al the residue lynage suede the counseils of hem;
Watu wa Isakari, waliofahamu majira na kujua kile ambacho Israeli inapasa kufanya, walikuwa viongozi 200, pamoja na jamaa zao wote chini ya uongozi wao.
33 forsothe of Zabulon camen fifti thousynde in to helpe, not in double herte, which yeden out to batel, and stoden in the scheltrun, and weren maad redi with armuris of batel;
Watu wa Zabuloni, askari wenye uzoefu mkubwa walioandaliwa tayari kwa vita wakiwa na silaha za kila aina, ili kumsaidia Daudi kwa uaminifu thabiti, walikuwa 50,000.
34 and of Neptalym a thousynde prynces, and with hem camen seuene and thritti thousynde men, arayed with scheeld and speere;
Watu wa Naftali, maafisa 1,000, pamoja na watu 37,000 waliochukua ngao na mikuki.
35 also of Dan, eiyte and twenti thousynde and sixe hundrid men, maad redi to batel;
Watu wa Dani 28,600 waliokuwa tayari kwa vita.
36 and of Aser fourti thousynde men, goynge out to batel, and stirynge to batel in the scheltrun.
Watu wa Asheri, askari 40,000 wenye uzoefu mkubwa waliondaliwa kwa ajili ya vita.
37 Forsothe biyende Jordan, of the sones of Ruben, and of Gad, and of the half part of the lynage of Manasses, sixe scoore thousynde men, araied with armuris of batel.
Na pia watu kutoka mashariki ya Yordani, watu wa Reubeni, Gadi na nusu ya kabila la Manase, wakiwa na kila aina ya silaha, watu 120,000.
38 Alle these men werriouris and redi to batel camen with perfit herte in to Ebron, to make Dauid kyng on al Israel; but also alle the residue of Israel weren of oon herte, that Dauid schulde be maad king on al Israel.
Wote hawa walikuwa watu wapiganaji waliojitolea kutumika katika safu zao. Walikuja Hebroni wakiwa wameamua kikamilifu kumfanya Daudi mfalme juu ya Israeli yote. Waisraeli wengine wote walikuwa pia na nia hiyo moja ya kumfanya Daudi kuwa mfalme.
39 And thei weren ther at Dauid thre daies, and eten and drunken; for her britheren hadden maad redi to hem;
Watu hawa wakakaa huko na Daudi siku tatu, wakila na kunywa, kwa sababu jamaa zao zilikuwa zimewapatia mahitaji yao.
40 but also thei that weren niy hem, til to Isacar and Zabulon and Neptalym, brouyten looues on assis, and camelis, and mulis, and oxis, for to ete; mele, bundelis of pressid figis, dried grapis, wyn, oile, oxis and wetheres, to al plentee; for ioy was in Israel.
Pia, majirani zao hata wale walio mbali hadi Isakari, Zabuloni na Naftali, walikuja wakiwaletea vyakula walivyovibeba kwa punda, ngamia, nyumbu na maksai. Kulikuwepo na wingi wa unga, maandazi ya tini, maandazi ya zabibu kavu, divai, mafuta, ngʼombe na kondoo, kwa maana kulikuwa na furaha katika Israeli.

< 1 Chronicles 12 >