< Romans 1 >
1 Paul a servant of Jesus Christ, called to be an apostle,
Kutoka kwangu mimi Paulo, mtumishi wa Kristo Yesu, na mtume niliyeteuliwa na kuitwa kwa ajili ya kuhubiri Habari Njema ya Mungu.
2 separated unto the gospel of God, (which He had promised before by his prophets in the holy scriptures) concerning his Son,
Hapo kale, Mungu aliwaahidia watu hii Habari Njema kwa njia ya manabii wake katika Maandiko Matakatifu.
3 who was of the seed of David according to the flesh,
Hii Habari Njema inamhusu Mwana wa Mungu, Bwana wetu Yesu Kristo, ambaye mintarafu ubinadamu wake, alikuwa mzawa wa Daudi;
4 but powerfully declared to be the Son of God, according to the spirit of holiness, by his resurrection from the dead, even Jesus Christ our Lord;
mintarafu utakatifu wake wa kimungu, alithibitishwa kwa uwezo mkuu kwamba ni Mwana wa Mungu kwa kufufuliwa kutoka wafu.
5 by whom we have received grace and apostleship to preach the obedience of faith for his name's sake, to all nations;
Kwa njia yake, mimi nimepewa neema ya kuwa mtume, ili kwa ajili yake niwaongoze watu wa mataifa yote wapate kuamini na kutii.
6 among whom are ye also the called of Jesus Christ;
Ninyi ni miongoni mwa watu hao; mmeitwa muwe watu wake Yesu Kristo.
7 to all that are in Rome beloved of God, called and holy: grace be to you, and peace from God our Father, and from the Lord Jesus Christ.
Basi, ninawaandikia ninyi nyote mlioko Roma ambao Mungu anawapenda, akawateua muwe watu wake. Nawatakieni neema na amani kutoka kwa Mungu Baba yetu na Bwana Yesu Kristo.
8 And first I thank my God through Jesus Christ for you all, that your faith is celebrated through the whole world:
Awali ya yote, namshukuru Mungu wangu kwa njia ya Yesu Kristo kwa ajili yenu nyote, kwa sababu imani yenu inasikika duniani kote.
9 for God is my witness, whom I serve with my spirit in the gospel of his Son, how incessantly I make mention of you always in my prayers,
Mungu, ambaye ninamtumikia kwa moyo wangu wote katika kuhubiri Habari Njema ya Mwanae, ni shahidi wangu kwamba ninawakumbukeni
10 intreating if I may now at length have a prosperous journey by the will of God, to come unto you.
daima katika sala zangu. Namwomba Mungu akipenda, anipatie nafasi nzuri ya kuja kwenu sasa.
11 For I long to see you, that I may impart to you some spiritual gift, that you may be established:
Kwa maana ninatamani sana kuwaoneni ili nipate kuwagawieni zawadi ya kiroho na kuwaimarisha.
12 that is to say, that being among you we may be comforted together by the faith of each, both yours and mine.
Ndiyo kusema, tutaimarishana: imani yenu itaniimarisha mimi, na yangu itawaimarisha ninyi.
13 And I would not have you ignorant, brethren, that I often purposed to come unto you, (but have been hindered hitherto) that I might have some fruit among you also, even as among the other Gentiles.
Ndugu zangu, nataka mjue kwamba mara nyingi nilikusudia kuwatembeleeni, lakini mpaka sasa nimezuiwa. Ningependa kupata mafanikio mema kati yenu kama nilivyopata kati ya watu wa mataifa mengine.
14 For I am a debtor both to Greeks and barbarians, both to the learned and the unlearned:
Ninalo jukumu kwa watu wote, waliostaarabika na wasiostaarabika, wenye elimu na wasio na elimu.
15 therefore am I ready, as much as in me lies, to preach the gospel to you also that are at Rome.
Ndiyo maana ninatamani pia kuihubiri Habari Njema kwenu ninyi mlioko huko Roma.
16 For I am not ashamed of the gospel of Christ; for it is the power of God unto salvation to every one that believeth, both Jew and Greek:
Sioni aibu kutangaza Habari Njema; yenyewe ni nguvu ya Mungu inayowaokoa wote wanaoamini: Wayahudi kwanza, na wasio Wayahudi pia.
17 for the righteousness of God is therein revealed from faith to faith; as it is written, "The just shall live by faith."
Kwa maana Habari Njema inaonyesha wazi jinsi Mungu anavyowakubali watu kuwa waadilifu; jambo hili hufanyika kwa imani, tangu mwanzo mpaka mwisho. Kama ilivyoandikwa: “Mwadilifu kwa imani ataishi.”
18 For the wrath of God is revealed from heaven against all ungodliness and unrighteousness of men, who withhold the truth in unrighteousness;
Ghadhabu ya Mungu imedhihirishwa kutoka mbinguni dhidi ya uasi na uovu wote wa binadamu ambao kwa njia zao mbaya wanaupinga ukweli usijulikane.
19 for what is to be known of God is manifest among them, for God hath manifested it to them.
Kwa maana, yote yanayoweza kujulikana juu ya Mungu ni wazi kwao; maana Mungu mwenyewe ameyadhirisha.
20 Inasmuch as from the first creation of the world, the invisible things of Him, even his eternal power and Godhead, are, if attended to, clearly seen in his works: (aïdios )
Tangu Mungu alipoumba ulimwengu, uwezo wake wa milele na uungu wake, ingawa havionekani kwa macho, vinafahamika wazi. Watu wanaweza kuyajua mambo hayo kutokana na vitu hivyo alivyoumba Mungu. Kwa hiyo hawana njia yoyote ya kujitetea! (aïdios )
21 so that they are inexcusable; because having thus known God they glorified Him not as God, neither were they thankful; but were infatuated by their own reasonings, and their heart being void of understanding was darkened.
Ingawa wanajua kuna Mungu, lakini hawampi heshima anayostahili, wala hawamshukuru. Badala yake, fikira zao zimekuwa batili na akili zao tupu zimejaa giza.
22 Pretending to be wise they Became fools:
Wanajidai kuwa wenye hekima, kumbe ni wapumbavu.
23 and changed the glory of the incorruptible God for an image like to corruptible man, and birds, and beasts, and reptiles.
Wanaacha kumwabudu Mungu aishiye milele, na badala yake, wanaabudu sanamu zilizo mfano wa binadamu ambaye hufa, mfano wa wanyama, ndege, au wanyama watambaao.
24 Wherefore God also gave them up to impurity, in the lusts of their own hearts, to dishonour their own bodies among themselves;
Kwa sababu hiyo, Mungu amewaacha wafuate tamaa mbaya za mioyo yao na kufanyiana mambo ya aibu kwa miili yao.
25 who changed the truth of God into a lie, and worshipped and served the creature instead of the Creator, who is blessed for ever. Amen. (aiōn )
Wanaubadili ukweli juu ya Mungu kwa uongo; wanaheshimu na kuabudu kiumbe badala ya Muumba mwenyewe, ambaye ndiye astahiliye sifa milele! Amina. (aiōn )
26 Therefore God gave them up to infamous passions: for even their women changed the natural use into that which is unnatural,
Kwa hiyo, Mungu amewaacha wafuate tamaa mbaya. Hata wanawake wanabadili matumizi yanayopatana na maumbile.
27 and the men likewise, leaving the natural use of the woman, burned in their lust to one another, men with men committing shame, and receiving in themselves the recompence of their error which they deserved.
Nao wanaume hali kadhalika, wanaacha kufuata matumizi ya maumbile ya mume na mke wakawakiana tamaa wao kwa wao. Wanaume wanafanyiana mambo ya aibu, na hivyo wanajiletea wenyewe adhabu wanayostahili kwa vitendo vyao viovu.
28 And as they were not careful to acknowledge God, God gave them up to an undiscerning mind to do things that were not fit to be done:
Kwa vile watu walikataa kumtambua Mungu, Mungu amewaacha katika fikira zao potovu, wakafanya yale ambayo hawangestahili kufanya.
29 being filled with all injustice, lewdness, wickedness, covetousness, malignity; full of envy, murder, strife, deceit, and every evil habit; whisperers,
Wamejaa kila aina ya uovu, dhuluma, ulafi na ufisadi. Wamejaa wivu, uuaji, ugomvi, udanganyifu na nia mbaya; husengenya,
30 slanderers, haters of God, injurious, haughty, proud, inventers of mischief, undutiful to parents, void of understanding,
na kusingiziana; ni watu wa kuchukiza kwa Mungu, wafidhuli, wenye kiburi na majivuno; hodari sana katika kutenda mabaya, na hawawatii wazazi wao;
31 covenant-breakers, without natural affection, implacable, and unmerciful:
hawana dhamiri, hawatimizi ahadi zao, hawana wema wala huruma kwa wengine.
32 who though they knew the just judgement of God, (that they who commit such practises are worthy of death) yet not only do these very things, but also countenance and encourage others in the practice of them.
Wanajua kwamba Sheria ya Mungu yasema kwamba watu wanaoishi mithili hiyo, wanastahili kifo. Zaidi ya hayo, siyo tu kwamba wanafanya mambo hayo wao wenyewe, bali hata huwapongeza wale wanaofanya mambo hayohayo.