< Revelation 1 >
1 The Revelation of Jesus Christ, which God gave unto Him, to shew to his servants things which must shortly come to pass; and He sent and signified it by his angel to his servant John,
Hizi ni habari za mambo ambayo yalifunuliwa na Yesu Kristo. Mungu alimpa Kristo ufunuo huu ili awaonyeshe watumishi wake mambo ambayo yanapaswa kutukia karibuni. Kristo alimtuma malaika wake amjulishe Yohane, mtumishi wake, mambo hayo,
2 who bare witness to the word of God and the testimony of Jesus Christ, and to whatever He saw.
naye Yohane, ameyasema yote aliyoyaona. Na hii ndio taarifa yake kuhusu ujumbe wa Mungu na ukweli uliofunuliwa na Yesu Kristo.
3 Happy is he that readeth, and those that hear the words of the prophecy, and keep the things that are written therein: for the time is near.
Heri yake mtu anayesoma kitabu hiki; heri yao wale wanaosikiliza maneno ya ujumbe huu wa kinabii na kushika yaliyoandikwa humu, maana wakati umekaribia ambapo mambo haya yatatukia.
4 John to the seven churches in Asia---Grace and peace be to you, from Him who is, and who was, and who is to come; and from the seven Spirits which are before his throne;
Mimi Yohane nayaandikia makanisa yaliyoko mkoani Asia. Nawatakieni neema na amani kutoka kwake yeye aliyeko, aliyekuwako na anayekuja; na kutoka kwa roho saba walio mbele ya kiti chake cha enzi,
5 and from Jesus Christ, who is the faithful witness, the first-born from the dead, and the ruler of the kings of the earth. To Him that loved us, and washed us from our sins in his own blood,
na kutoka kwa Yesu Kristo, shahidi mwaminifu, wa kwanza kufufuliwa kutoka wafu, na ambaye ni mtawala wa wafalme wa dunia. Yeye anatupenda, na kwa damu yake ametufungua kutoka vifungo vya dhambi zetu,
6 and hath made us kings and priests to his God and Father, to Him be glory and dominion for ever and ever. Amen. (aiōn )
akatufanya sisi kuwa ufalme wa makuhani, tumtumikie Mungu, Baba yake. Kwake Yesu Kristo uwe utukufu na nguvu, milele na milele! Amina. (aiōn )
7 Behold, He is coming with the clouds, and every eye shall see Him, even they that pierced Him: and all the tribes of the earth shall lament before Him. Even so, Amen!
Tazama! Anakuja katika mawingu! Kila mtu atamwona, hata wale waliomchoma. Makabila yote duniani yataomboleza juu yake. Naam! Amina.
8 I am the Alpha and the Omega, the beginning and the end, saith the Lord, who is, and who was, and who is to come, the Almighty.
“Mimi ni Alfa na Omega,” asema Bwana Mungu Mwenye Uwezo, aliyeko, aliyekuwako na anayekuja.
9 I John, who am also your brother, and companion in the affliction, and in the kingdom and patience of Jesus Christ, was in the island called Patmos, for the sake of the word of God, and for the testimony of Jesus Christ.
Mimi ni Yohane, ndugu yenu; na kwa kuungana na Kristo nashiriki pamoja nanyi katika kustahimili mateso yanayowapata wale walio wa Utawala wake. Mimi nilikuwa kisiwani Patmo kwa sababu ya kuhubiri ujumbe wa Mungu na ukweli wa Yesu.
10 Here I was in the Spirit on the Lord's-day: and heard behind me a loud voice, as of a trumpet,
Basi, wakati mmoja, siku ya Bwana, nilikumbwa na Roho, nikasikia nyuma yangu sauti kubwa kama sauti ya tarumbeta.
11 saying, I am the Alpha and the Omega, the first and the last; and, What thou seest write in a book, and send it to the seven churches in Asia, to Ephesus, and to Smyrna, and to Pergamos, and to Thyatira, and to Sardis, and to Philadelphia, and to Laodicea.
Nayo ilisema, “Andika katika kitabu yote unayoyaona, ukipeleke kwa makanisa haya saba: Efeso, Smurna, Pergamoni, Thuatira, Sarde, Filadelfia na Laodikea.”
12 And I turned to see the voice that spake to me: and when I turned, I saw seven golden candlesticks;
Basi, nikageuka nimwone huyo aliyesema nami, nikaona vinara vya taa saba vya dhahabu,
13 and in the midst of the seven candlesticks one like the Son of man, clothed with a long robe, and girded about the breasts with a golden girdle.
na katikati yake kulikuwa na kitu kama mtu, naye alikuwa amevaa kanzu ndefu na ukanda wa dhahabu kifuani.
14 His head and his hairs were white like white wool, as white as snow; and his eyes as a flame of fire;
Nywele zake zilikuwa nyeupe kama pamba safi, kama theluji; macho yake yalimetameta kama moto;
15 and his feet like fine brass, as if they were glowing in a furnace: and his voice as the sound of many waters:
miguu yake iling'aa kama shaba iliyosafishwa katika tanuru ya moto na kusuguliwa, na sauti yake ilikuwa, kama sauti ya poromoko la maji.
16 and He had in his right hand seven stars, and out of his mouth went a sharp two-edged sword: and his countenance was as the sun when he shineth in his strength.
Katika mkono wake wa kulia, alikuwa na nyota saba, na kinywani mwake mlitoka upanga wenye makali kuwili. Uso wake uling'aa kama jua kali.
17 And when I saw Him, I fell at his feet as dead; and He laid his right hand upon me, and said to me, "Fear not,
Basi, nilipomwona tu, nilianguka mbele ya miguu yake kama maiti. Lakini yeye akaweka mkono wake wa kulia juu yangu, akasema, “Usiogope! Mimi ni wa kwanza na wa mwisho.
18 I am the first and the last, who live, though I was dead; and behold, I am alive for ever and ever, Amen, and have the keys of hades and of death. (aiōn , Hadēs )
Mimi ni yeye aliye hai! Nilikuwa nimekufa, lakini, tazama, sasa ni mzima milele na milele. Ninazo funguo za kifo na Kuzimu. (aiōn , Hadēs )
19 Write what thou hast seen, the things which are, and which are to be hereafter."
Basi, sasa andika mambo haya unayoyaona, mambo yanayotukia sasa na yale yatakayotukia baadaye.
20 As to the mystery of the seven stars which thou sawest in my right hand, and the seven golden candlesticks; the seven stars are the angels of the seven churches, and the seven candlesticks which thou sawest are the seven churches.
Siri ya nyota zile saba ulizoziona katika mkono wangu wa kulia, na siri ya vile vinara saba vya taa hii: zile nyota saba ni malaika wa makanisa; na vile vinara saba vya taa ni makanisa saba.