< Matthew 16 >

1 And the pharisees and sadducees came to Him, and captiously asked Him to shew them a sign from heaven.
Mafarisayo na Masadukayo wakamjia Yesu na kumjaribu kwa kumwomba awaonyeshe ishara kutoka mbinguni.
2 But He answered them, In the evening ye say, It will be fair weather, for the sky is red:
Yesu akawajibu, “Ifikapo jioni, mnasema, ‘Hali ya hewa itakuwa nzuri, kwa kuwa anga ni nyekundu.’
3 and in the morning, It will be foul weather to-day, for the sky is red and lowring. Ye hypocrites, can ye distinguish the appearance of the sky, and not discern the signs of these times?
Nanyi wakati wa asubuhi mnasema, ‘Leo kutakuwa na dhoruba, kwa sababu anga ni nyekundu na mawingu yametanda.’ Mnajua jinsi ya kupambanua kule kuonekana kwa anga, lakini hamwezi kupambanua dalili za nyakati.
4 This wicked and degenerate race demand a sign; but no sign shall be given them, except that of the prophet Jonah. And so He left them and went away.
Kizazi kiovu na cha uzinzi kinatafuta ishara, lakini hakitapewa ishara yoyote isipokuwa ishara ya Yona.” Yesu akawaacha, akaenda zake.
5 Now when his disciples departed to the other side, they forgot to take bread with them:
Wanafunzi wake walipofika ngʼambo ya bahari, walikuwa wamesahau kuchukua mikate.
6 and therefore when Jesus said to them, Take heed and beware of the leaven of the pharisees and of the sadducees,
Yesu akawaambia, “Jihadharini. Jilindeni na chachu ya Mafarisayo na ya Masadukayo.”
7 they said one to another, It is because we have taken no bread.
Wakajadiliana wao kwa wao, wakisema, “Ni kwa sababu hatukuleta mikate.”
8 And Jesus knowing their thoughts said to them, O ye of little faith, why do ye argue among yourselves, because ye have brought no bread?
Yesu, akifahamu majadiliano yao, akauliza, “Enyi wa imani haba! Mbona mnajadiliana miongoni mwenu kuhusu kutokuwa na mikate?
9 Do ye not yet understand, nor remember the five loaves divided among five thousand, and how many baskets ye took up?
Je, bado hamwelewi? Je, hamkumbuki ile mikate mitano iliyolisha watu 5,000 na idadi ya vikapu vingapi vya mabaki mlivyokusanya?
10 nor the seven loaves among four thousand, and how many baskets-full ye took away?
Au ile mikate saba iliyolisha watu 4,000 na idadi ya vikapu vingapi vya mabaki mlivyokusanya?
11 How is it then that ye do not understand that I did not speak to you concerning bread, when I bid you to beware of the leaven of the pharisees and of the sadducees?
Inakuwaje mnashindwa kuelewa kwamba nilikuwa sisemi nanyi habari za mikate? Jilindeni na chachu ya Mafarisayo na Masadukayo.”
12 Then they understood, that He did not bid them beware of the leaven of bread, but of the doctrine of the pharisees and of the sadducees.
Ndipo wakaelewa kwamba alikuwa hasemi juu ya chachu ya kutengeneza mikate, bali juu ya mafundisho ya Mafarisayo na Masadukayo.
13 And when Jesus came into the parts of Cesarea Philippi, He asked his disciples, saying, Whom do men say that I, the Son of man, am?
Basi Yesu alipofika katika eneo la Kaisaria-Filipi, akawauliza wanafunzi wake, “Watu husema kwamba mimi Mwana wa Adamu ni nani?”
14 And they answered, Some say thou art John the Baptist, others Elias, and others Jeremias, or one of the prophets.
Wakamjibu, “Baadhi husema ni Yohana Mbatizaji; wengine husema ni Eliya; na bado wengine husema ni Yeremia au mmojawapo wa manabii.”
15 But, saith He unto them, whom do ye say that I am?
Akawauliza, “Je, ninyi mnasema mimi ni nani?”
16 And Simon Peter answered and said, Thou art the Christ the Son of the living God.
Simoni Petro akamjibu, “Wewe ndiwe Kristo, Mwana wa Mungu aliye hai.”
17 And Jesus replied and said unto him, Blessed art thou Simon son of Jonas, for flesh and blood hath not revealed it unto thee, but my Father who is in heaven.
Naye Yesu akamwambia, “Heri wewe, Simoni Bar-Yona, kwa maana hili halikufunuliwa kwako na mwanadamu, bali na Baba yangu aliye mbinguni.
18 And I also say unto thee, as thou art called Peter, so upon this rock, which thou hast confessed, will I build my church, and the gates of death shall not prevail against it. (Hadēs g86)
Nami nakuambia, wewe ndiwe Petro na juu ya mwamba huu nitalijenga kanisa langu, hata malango ya Kuzimu hayataweza kulishinda. (Hadēs g86)
19 And I will give thee the keys of the kingdom of heaven, and whatsoever thou shalt bind on earth shall be bound in heaven, and whatsoever thou shalt loose on earth shall be loosed in heaven.
Nitakupa funguo za Ufalme wa mbinguni, na lolote utakalolifunga duniani litakuwa limefungwa Mbinguni, nalo lolote utakalofungua duniani litakuwa limefunguliwa mbinguni.”
20 Then charged He his disciples that they should tell no one that He was the Messiah.
Kisha akawakataza wanafunzi wake wasimwambie mtu yeyote kwamba yeye ndiye Kristo.
21 And from that time began Jesus to acquaint his disciples, that He must go to Jerusalem and suffer many things from the elders, and chief priests, and scribes; and be put to death, and be raised again on the third day.
Tangu wakati huo, Yesu alianza kuwaeleza wanafunzi wake kwamba hana budi kwenda Yerusalemu na kupata mateso mengi mikononi mwa wazee, viongozi wa makuhani, na walimu wa sheria, na kwamba itampasa auawe lakini siku ya tatu kufufuliwa.
22 Then Peter took Him and began to expostulate with Him, saying, Be it far from thee, Lord: may this never be unto thee.
Petro akamchukua kando, akaanza kumkemea akisema, “Haiwezekani, Bwana! Jambo hili kamwe halitakupata!”
23 But He turned and said unto Peter, Get thee behind me, Satan, thou art an offence to me; for thou regardest not the things of God, but those that be of men.
Lakini Yesu akageuka na kumwambia Petro, “Rudi nyuma yangu, Shetani! Wewe ni kikwazo kwangu. Moyo wako hauwazi yaliyo ya Mungu, bali ya wanadamu.”
24 Then said Jesus to his disciples, If any one is willing to come after me, let him deny himself, and take up his cross, and follow me:
Ndipo Yesu akawaambia wanafunzi wake, “Mtu yeyote akitaka kunifuata, ni lazima ajikane mwenyewe, auchukue msalaba wake, anifuate.
25 for he that would save his life shall lose it; but he that would lose his life for my sake shall find it.
Kwa maana yeyote anayetaka kuyaokoa maisha yake atayapoteza, lakini yeyote atakayeyapoteza maisha yake kwa ajili yangu atayapata.
26 For what is a man profited, if he gain the whole world, and lose his own soul? or what shall a man give as a ransom for his soul?
Kwa maana, je, itamfaidi nini mtu kuupata ulimwengu wote, lakini akayapoteza maisha yake? Au mtu atatoa nini badala ya nafsi yake?
27 For the Son of man will come in the glory of his father, with his angels, and then he will recompense every one according to his practice.
Kwa maana Mwana wa Adamu atakuja katika utukufu wa Baba yake pamoja na malaika zake, naye ndipo atakapomlipa kila mtu kwa kadiri ya matendo yake.
28 And I tell you of a truth, there be some of those standing here, who shall not taste of death, till they have seen the Son of man coming in his kingdom.
Nawaambia kweli, baadhi yenu hapa hawataonja mauti kabla ya kumwona Mwana wa Adamu akija katika Ufalme wake.”

< Matthew 16 >