< Hebrews 4 >
1 Let us therefore fear least a promise being left us of entering into his rest, any of us should seem to fall short of it:
Mungu alituahidia kwamba tutaweza kupata pumziko hilo alilosema. Basi, na tuogope ili yeyote kati yenu asije akashindwa kupata pumziko hilo.
2 for we are graciously offered it, as they also were. But the word, which they heard, did not profit them, not being mixed with faith in them that heard it.
Maana Habari Njema imehubiriwa kwetu kama vile ilivyohubiriwa kwa hao watu wa kale. Lakini ujumbe huo haukuwafaa chochote, maana waliusikia lakini hawakuupokea kwa imani.
3 For we who believe shall enter into rest, as He said above, "So I sware in my wrath, they shall not enter into my rest:" though the works of creation were finished from the foundation of the world:
Basi, sisi tunaoamini tunapata pumziko hilo aliloahidi Mungu. Kama alivyosema: “Nilikasirika, nikaapa: Hawataingia huko ambako ningewapa pumziko.” Mungu alisema hayo ingawa kazi yake ilikuwa imekwisha malizika tangu alipoumba ulimwengu.
4 for it is thus said concerning the seventh day, "And God rested the seventh day from all his works."
Maana Maandiko yasema mahali fulani kuhusu siku ya saba: “Mungu alipumzika siku ya saba, akaacha kazi zake zote.”
5 And yet in this place, "They shall not enter into my rest."
Tena jambo hili lasemwa pia: “Hawataingia huko ambako ningewapa pumziko.”
6 Seeing therefore it remaineth that some are to enter into it, and they to whom it was at first offered did not enter because of their unbelief,
Wale waliotangulia kuhubiriwa Habari Njema hawakupata pumziko hilo kwa sababu hawakuamini. Wapo, basi, wengine ambao wangejaliwa kulipata.
7 He appoints a certain day, called To-day, saying by David so long after, (as it is recorded) "To-day if ye will hear his voice, harden not your hearts."
Jambo hili ni wazi, kwani Mungu aliweka siku nyingine ambayo inaitwa “Leo”. Miaka mingi baadaye Mungu alisema juu ya hiyo siku kwa maneno ya Daudi katika Maandiko yaliyokwisha tajwa: “Kama mkisikia sauti ya Mungu leo, msiifanye mioyo yenu kuwa migumu.”
8 For if Joshua had given them the rest, He would not afterwards have spoken of another day.
Kama Yoshua angaliwapa watu hao hilo pumziko, Mungu hangalisema baadaye juu ya siku nyingine.
9 There remaineth therefore a rest for the people of God:
Kwa hiyo, basi, bado lipo pumziko kwa watu wa Mungu kama kule kupumzika kwake Mungu siku ya saba.
10 for he that is entered into his rest, hath also himself ceased from his works, as God did from his.
Maana, kila anayepata pumziko aliloahidi Mungu atapumzika baada ya kazi yake kama vile pia Mungu alivyopumzika baada ya yake.
11 Let us labour therefore to enter into that rest, least any one fall after the same example of unbelief.
Basi, tujitahidi kupata pumziko hilo, ili asiwepo yeyote miongoni mwenu atakayeshindwa, kama walivyofanya wao kwa sababu ya ukosefu wao wa imani.
12 For the word of God is lively and efficacious, and sharper than any two-edged sword, piercing even to the dividing of soul and spirit, and of the very joints and marrow, and judging the thoughts and intentions of the heart.
Neno la Mungu ni hai na lina nguvu; ni kali zaidi kuliko upanga wenye makali kuwili. Hukata kabisa mpaka mahali ambapo moyo na roho hukutana, mpaka pale vikutanapo viungo vya mwili na mafuta. Neno hilo huchambua nia na fikira za mioyo ya watu.
13 And there is no creature concealed from his sight: but all things are naked and open to the eyes of Him, to whom we are to give an account.
Hakuna kiumbe chochote kilichofichika mbele ya Mungu; kila kitu kimefunuliwa wazi mbele ya macho yake. Kwake, sisi sote tutapaswa kutoa hoja ya matendo yetu.
14 Having therefore a great high-priest, that is passed into the heavens, even Jesus the Son of God, let us hold fast our profession:
Basi, tunapaswa kuzingatia kwa uthabiti imani tunayoiungama. Maana tunaye Kuhani Mkuu aliyeingia mpaka kwa Mungu mwenyewe—Yesu, Mwana wa Mungu.
15 for we have not an high-priest who cannot sympathize with our infirmities, but was in all respects tempted in like manner with us, yet without sin.
Huyu Kuhani Mkuu wetu si mmoja ambaye hawezi kutuunga mkono katika unyonge wetu, ila ni Kuhani Mkuu ambaye alijaribiwa kama sisi kwa kila namna lakini hakutenda dhambi.
16 Let us therefore come with freedom to the throne of grace, that we may obtain mercy and find grace for our seasonable help.
Basi, na tukikaribie bila hofu kiti cha enzi cha Mungu, palipo na neema, ili tukajipatie huruma na neema ya kutusaidia wakati wa lazima.