< Ephesians 1 >
1 Paul an apostle of Jesus Christ, by the will of God, to the saints, who are at Ephesus, even the faithful in Christ Jesus;
Mimi Paulo, mtume wa Kristo Yesu kwa mapenzi ya Mungu, nawaandikia ninyi watu wa Mungu huko Efeso, mlio waaminifu katika kuungana na Kristo Yesu.
2 grace be to you and peace from God our Father, and from the Lord Jesus Christ.
Nawatakieni neema na amani kutoka kwa Mungu Baba yetu na kwa Bwana Yesu Kristo.
3 Blessed be the God and Father of our Lord Jesus Christ, who hath blessed us with all spiritual blessings in heavenly things by Christ;
Atukuzwe Mungu na Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo! Maana, katika kuungana na Kristo ametubariki kwa kutujalia zawadi zote za kiroho mbinguni.
4 according as he hath chosen us in Him before the foundation of the world, that we should be holy and unblameable before Him in love:
Kabla ya kuumbwa ulimwengu, Mungu alituteua tuwe wake katika kuungana na Kristo ili tuwe watakatifu na bila hitilafu mbele yake. Kwa sababu ya upendo wake,
5 having before appointed us unto the adoption of children by Jesus Christ unto Himself, according to the good pleasure of his will;
Mungu alikuwa ameazimia tangu zamani kutuleta kwake kama watoto wake kwa njia ya Yesu Kristo. Ndivyo alivyopenda na kunuia.
6 to the praise of his glorious grace, whereby He hath made us acceptable in the Beloved:
Basi, tumsifu Mungu kwa sababu ya neema yake tukufu katika Mwanae mpenzi!
7 in whom we have redemption through his blood, even the remission of sins, according to the riches of his grace;
Maana kwa damu yake Kristo sisi tunakombolewa, yaani dhambi zetu zinaondolewa. Ndivyo ulivyo ukuu wa neema yake
8 wherein He hath abounded towards us with the highest wisdom and prudence;
aliotukirimia bila kipimo! Kwa hekima na ujuzi wake wote
9 having made known to us the secret of his will, according to his good pleasure, which He had before purposed in Himself:
Mungu alitekeleza kile alichonuia, akatujulisha mpango wake uliofichika, ambao alikuwa ameazimia kuutekeleza kwa njia ya Kristo.
10 that in the dispensation of the fulness of times, He might reduce all things, both in heaven and on earth, under one head in Christ:
Mpango huo ambao angeutimiza wakati utimiapo ni kukusanya pamoja viumbe vyote, kila kitu mbinguni na duniani, chini ya Kristo.
11 even in Him, in whom also we have obtained an inheritance, being predestinated to it according to the purpose of Him who effecteth all things after the counsel of His own will:
Kila kitu hufanywa kufuatana na mpango na uamuzi wa Mungu; naye Mungu ametuteua sisi tuwe watu wake kwa mapenzi yake katika kuungana na Kristo, kufuatana na azimio alilofanya tangu mwanzo.
12 that we should be to the praise of his glory, who first trusted in Christ.
Basi, sisi tuliotangulia kumtumainia Kristo tunapaswa kuusifu utukufu wa Mungu!
13 In whom ye also trusted, when ye heard the word of truth, the gospel of your salvation: in whom also when ye believed, ye were sealed with the holy Spirit of promise,
Nanyi pia watu wa mataifa mengine, mliusikia ujumbe wa kweli yaani Habari Njema iliyowaletea wokovu, mkamwamini Kristo; naye Mungu, ili kuonyesha kuwa ninyi ni wake, akawapiga mhuri kwa kuwapeni yule Roho Mtakatifu aliyetuahidia.
14 who is the pledge of our inheritance, till the redemption of his purchased possession, to the praise of his glory.
Huyu Roho ni dhamana ya kurithi yote yale Mungu aliyowaahidia watu wake, na jambo hili latuhakikishia kwamba Mungu atawakomboa kabisa wote walio wake. Tuusifu utukufu wake!
15 Wherefore I also, having heard of your faith in the Lord Jesus,
Kwa sababu hiyo, tangu niliposikia juu ya imani yenu kwa Bwana Yesu na mapendo yenu kwa watu wa Mungu,
16 and your love to all the saints, cease not to give thanks for you, making mention of you in my prayers;
sijaacha kamwe kumshukuru Mungu kwa ajili yenu. Ninawakumbuka katika sala zangu
17 that the God of our Lord Jesus Christ, the Father of glory, would give you the Spirit of wisdom and revelation to the knowledge of Him,
ili Mungu wa Bwana wetu Yesu Kristo Baba mtukufu, awajalieni Roho wake atakayewapa hekima na kuwafunulieni Mungu mpate kumjua.
18 and enlighten the eyes of your understanding; that ye may know, what is the hope of his calling, and how rich the glory of his inheritance in the saints;
Namwomba Mungu aifunue mioyo yenu iweze kuuona mwanga wake, mpate kutambua lile tumaini alilowaitieni na utukufu mkuu wa zawadi alizowawekea watu wake,
19 and what the exceeding greatness of his power towards us who believe, according to the energy of his mighty strength;
mpate kutambua jinsi uwezo wake ulivyo mkuu mno kwa ajili yetu sisi tunaoamini. Uwezo huo unaofanya kazi ndani yetu, ni sawa na nguvu ile kuu mno
20 which He exerted in Christ, when He raised Him from the dead, and set Him at his own right hand in heavenly places,
aliyomfufua nayo Kristo kutoka wafu, akamketisha kulia kwake mbinguni.
21 far above all principality and power and might and dominion, and every name that is named, not only in this world, but also in that which is to come: (aiōn )
Huko, Kristo anatawala juu ya kila tawala, mamlaka, enzi na ukuu; anatawala juu ya kila cheo kiwezacho kutajwa katika ulimwengu huu na katika ulimwengu ujao. (aiōn )
22 and hath put all things under his feet, and given Him to be head over all things to the church;
Mungu ameweka vitu vyote chini ya miguu yake, akamkabidhi kwa kanisa akiwa mkuu wa vitu vyote.
23 which is his body, the complete work of Him, who filleth all in all.
Kanisa ni mwili wa Kristo, na ukamilifu wake yeye anayekamilisha vitu vyote kila mahali.