< 2 Corinthians 2 >
1 But I determined with myself, not to come to you again in grief:
Basi nimeamua nisiwatembelee tena kuwatia huzuni.
2 for if I grieve you, who is it that maketh me glad, but he that is grieved by me?
Maana nikiwahuzunisha ninyi, basi, ni nani atakayenifariji? Ni walewale niliowahuzunisha!
3 And I wrote this to you, that when I come I may not have grief from those of whom I ought to receive joy, being persuaded concerning all of you, that my joy is the joy of you all.
Ndiyo maana niliwaandikia—sikutaka kuja kwenu na kuhuzunishwa na ninyi ambao ndio mngepaswa kuwa furaha yangu. Nina hakika kwamba, mimi nikifurahi, ninyi nyote pia mnafurahi.
4 For through much affliction and distress of heart I wrote to you with many tears; not that ye might be grieved, but that ye might know the love with which I abound towards you.
Nilipowaandikia hapo awali katika hali ya huzuni na sikitiko moyoni na kwa machozi mengi, haikuwa kwa ajili ya kuwahuzunisha ninyi, bali kwa ajili ya kuwaonyesheni kwamba nawapenda mno.
5 And if any one hath caused grief, it hath grieved me only as to part of you, (that I may not overcharge you
Ikiwa kuna mtu aliyemhuzunisha mwingine, hakunihuzunisha mimi—ila amewahuzunisha ninyi nyote, na sipendi kuwa mkali zaidi.
6 all) though sufficient to such a one is the censure passed on him by many.
Adhabu aliyokwisha pata kutoka kwa wengi wenu inamtosha.
7 So that on the contrary, ye ought rather to forgive and comfort him, least such a one should be swallowed up with excessive sorrow.
Iliyobakia ni afadhali kwenu kumsamehe mtu huyo na kumpa moyo ili asije akahuzunika mno na kukata tamaa kabisa.
8 Wherefore I beseech you to confirm your love to him.
Kwa hiyo nawasihi: mwonyesheni kwamba mnampenda.
9 For to this end also did I write, that I might have proof of you, whether ye are obedient in all things.
Madhumuni yangu kuandika ile barua yalikuwa kutaka kujua kama mko tayari kutii katika kila jambo.
10 And to whom ye forgive any thing, I also forgive it: for if I have forgiven any thing, I forgave it him, to whom I did forgive it, for your sakes, in the person of Christ; that we might not be foiled by Satan:
Mkimsamehe mtu, nami pia ninamsamehe. Maana ninaposamehe—kama kweli ninacho cha kusamehe—nasamehe mbele ya Kristo kwa ajili yenu,
11 for we are not ignorant of his devices.
ili tusimpe nafasi Shetani atudanganye; maana twaijua mipango yake ilivyo.
12 So that when I came to Troas on account of the gospel of Christ, and a door was opened to me in the Lord,
Nilipofika Troa kuhubiri Habari Njema ya Kristo, nilikuta mlango u wazi kwa ajili ya kazi ya Bwana.
13 yet I had no rest in my spirit, because I found not Titus my brother there; but taking my leave of them, I went away into Macedonia.
Lakini nilifadhaika sana kwa kutomkuta ndugu yetu Tito. Ndiyo maana niliwaaga wote pale nikaenda Makedonia.
14 But thanks be to God, who always causeth us to triumph in Christ, and spreadeth the odor of his knowledge by us in every place.
Lakini, shukrani kwa Mungu anayetuongoza daima katika msafara wa ushindi wa Kristo. Yeye hutufanya tuueneze ukweli wa Kristo kama harufu nzuri, kila mahali.
15 For we are the sweet odor of Christ unto God, in them that are saved, yea and in them that perish:
Maana sisi ni kama harufu nzuri ya ubani ambayo Kristo anamtolea Mungu, harufu nzuri inayofikia wote wanaookolewa na wanaopotea.
16 to these indeed we are an odor of death to death; to those an odor of life unto life. And who is sufficient for these things?
Kwa wale wanaopotea, harufu hiyo ni kifo; lakini kwa wale wanaookolewa, harufu hiyo ni uhai. Nani basi, awezaye kushiriki katika kazi ya namna hiyo?
17 For we are not like many who adulterate the word of God: but as with sincerity, but as from God, and in the sight of God, we speak concerning Christ.
Sisi si kama wengine ambao hufanya biashara na ujumbe wa Mungu; sisi tunahubiri kwa unyofu mbele ya Mungu, kama watu tuliotumwa na Mungu, tukiwa tumeungana na Kristo.