< 1 Timothy 6 >

1 Let as many as are servants under the yoke account their own masters worthy of all honor; that the name of God and his doctrine may not be blasphemed:
Watumwa wote wanapaswa kuwaheshimu wakuu wao ili kusiwe na sababu ya watu kulitukana jina la Mungu na mafundisho yetu.
2 and let not those who have believing masters, despise them, because they are brethren; but serve them more readily, because they are faithful and beloved by God, partakers of his grace.
Watumwa ambao wakuu wao ni Wakristo wasiwadharau kwani ni ndugu zao. Badala yake, wanapaswa kuwatumikia hata vizuri zaidi, maana hao wanaopata faida kutokana na kazi yao ni waumini ambao wanawapenda. Unapaswa kufundisha na kuhubiri mambo haya.
3 These things teach and exhort. If any one teach otherwise, and adhere not to the sound words of our Lord Jesus Christ, and the doctrine which is according to godliness;
Mtu yeyote anayefundisha kinyume cha mambo haya, na ambaye hakubaliani na maneno ya kweli ya Bwana wetu Yesu Kristo na mafundisho ya dini,
4 he is proud, knowing nothing, but is delirious about questions and strifes of words: from which cometh envy, contention, calumnies, wicked suspicions, perverse debates of men corrupted in mind,
huyo amejaa majivuno na wala hajui chochote. Ni mtu wa kupenda ubishi na magombano juu ya maneno matupu, na hiyo husababisha wivu, ugomvi, matusi, shuku mbaya,
5 and void of truth, accounting gain to be godliness: from such withdraw thyself.
na ubishi usio na kikomo kutoka kwa watu ambao akili zao zimeharibika, na ambao hawana tena ukweli. Wanadhani dini ni njia ya kujipatia utajiri.
6 But godliness with contentment is great gain.
Kweli dini humfanya mtu awe tajiri sana, ikiwa anatosheka na vitu alivyo navyo.
7 For we brought nothing into the world, and it is certain that we can carry nothing out:
Maana hatukuleta kitu chochote hapa duniani, wala hatutachukua chochote.
8 having therefore food and raiment, let us be herewith content.
Kwa hiyo basi, kama tunacho chakula na mavazi, tunapaswa kuridhika navyo.
9 But they, that will be rich, fall into temptation and a snare, and into many foolish and hurtful lusts, which plunge men into ruin and perdition.
Lakini wale wanaotaka kutajirika huanguka katika majaribu, na kunaswa katika mtego wa tamaa nyingi mbaya za kipumbavu, ambazo huwavuta mpaka kwenye uharibifu na maangamizi.
10 For the love of money is the root of all evils, which some coveting after have been led astray from the faith, and pierced themselves through with many sorrows.
Kwa maana kupenda sana fedha ni chanzo cha uovu wote. Watu wengine wametamani sana kupata fedha hata wakatangatanga mbali na imani, na wameivunja mioyo yao kwa huzuni nyingi.
11 But do thou, O man of God, flee these things, and follow after righteousness, piety, fidelity, love, patience, meekness.
Lakini wewe, mtu wa Mungu, jiepushe na mambo hayo. Zingatia uadilifu, uchaji wa Mungu, imani, mapendo, subira na unyenyekevu.
12 Maintain the glorious combat of faith, lay hold on eternal life, to which thou hast been called, and hast made a good profession before many witnesses. (aiōnios g166)
Piga mbio kadiri uwezavyo katika shindano la mbio za imani, ukajipatie tuzo la uzima wa milele, uliloitiwa wakati ulipokiri imani yako mbele ya mashahidi wengi. (aiōnios g166)
13 I charge thee before God, who giveth life to all, and before Christ Jesus who witnessed a good confession before Pontius Pilate,
Mbele ya Mungu anayevipa vitu vyote uhai, na mbele ya Yesu Kristo aliyetoa ushahidi na kukiri ukweli mbele ya Pontio Pilato,
14 that thou keep this commandment, unspotted and blameless, till the appearance of our Lord Jesus Christ;
nakuamuru ushike maagizo yako na kuyatii kwa uaminifu mpaka Siku ile atakapotokea Bwana wetu Yesu Kristo.
15 which He will manifest in his own times, who is the blessed and only potentate, the King of kings, and Lord of lords,
Kutokea kwake kutafanyika wakati ufaao uliopangwa na Mungu mwenye heri na aliye Mtawala pekee, Mfalme wa wafalme, na Bwana wa mabwana.
16 who alone hath immortality, dwelling in light inaccessible, whom no man hath seen, nor can see: to whom be honor and power everlasting. Amen. (aiōnios g166)
Yeye peke yake anaishi milele, katika mwanga usioweza kukaribiwa na mtu. Hakuna mtu aliyepata kumwona au awezaye kumwona. Kwake iwe heshima na uwezo wa milele! Amina. (aiōnios g166)
17 Charge them, that are rich in this world, not to be high-minded nor trust in uncertain riches, but in the living God, who richly affords us all things for enjoyment: charge them to do good, (aiōn g165)
Waamuru watu walio matajiri katika mambo ya maisha ya sasa, wasijivune, wasiweke tumaini lao katika mali isiyoweza kutegemewa; bali wamtegemee Mungu, ambaye kwa ukarimu hutupatia vitu vyote tuvifurahie. (aiōn g165)
18 to be rich in good works, to be ready to distribute, willing to communicate;
Waamuru watende mema, wawe matajiri katika matendo mema, na wawe wakarimu na walio tayari kuwashirikisha wengine mali zao.
19 treasuring up to themselves a good foundation for the future, that they may obtain eternal life.
Kwa namna hiyo watajiwekea hazina ambayo itakuwa kwao msingi imara kwa wakati ujao. Hapo wataweza kujipatia uzima ambao ni uzima wa kweli.
20 O Timothy, keep that with which thou art entrusted, avoiding profane empty babblings, and the oppositions of science falsely so called:
Timotheo, tunza salama yote yale uliyokabidhiwa. Jiepushe na majadiliano ya kidunia na ubishi wa kipumbavu juu ya kile wanachokiita watu wengine: “Elimu”.
21 which some pretending to, have erred from the faith. Grace be with thee. Amen.
Maana wengine wamejidai kuwa na hiyo elimu, na matokeo yake wamepoteza imani. Nawatakieni nyote neema!

< 1 Timothy 6 >