< 1 Corinthians 15 >

1 Moreover, brethren, I declare unto you the gospel which I preached to you at first, which ye received, and wherein ye stand.
Sasa ndugu, napenda kuwakumbusha ile Habari Njema niliyowahubirieni nanyi mkaipokea na kusimama imara ndani yake.
2 By which also ye are saved, if ye retain it as I preached it to you: unless indeed ye have believed in vain.
Kwa njia yake mnaokolewa, ikiwa mnayazingatia maneno niliyowahubirieni, na kama kuamini kwenu hakukuwa bure.
3 For in the first place I delivered to you, that which I also received, to wit, that Christ died for our sins, according to the scriptures:
Mimi niliwakabidhi ninyi mambo muhimu sana ambayo mimi niliyapokea: kwamba Kristo alikufa kwa ajili ya dhambi zetu kufuatana na Maandiko Matakatifu;
4 and that He was buried, and that He rose again the third day, according to the scriptures.
kwamba alizikwa, akafufuka siku ya tatu kama ilivyoandikwa;
5 And that he was seen by Cephas, then by the twelve:
kwamba alimtokea Kefa, na baadaye aliwatokea wale kumi na wawili.
6 after that He appeared to above five hundred brethren at once, of whom the greater part remain yet alive, but some are fallen asleep.
Kisha aliwatokea ndugu zaidi ya mia tano kwa mara moja; wengi wao wanaishi bado, lakini baadhi yao wamekwisha kufa.
7 Afterwards He was seen by James, then by all the apostles.
Baadaye alimtokea Yakobo kisha akawatokea mitume wote.
8 And last of all He appeared to me also, as one born out of due time: for I am the lest of the apostles,
Baada ya wote, akanitokea hata mimi, mimi niliyekuwa kama mtu aliyezaliwa kabla ya wakati.
9 not worthy to be called an apostle, because I persecuted the church of God.
Maana mimi ni mdogo kabisa miongoni mwa mitume na wala sistahili kuitwa mtume, kwa sababu nililidhulumu kanisa la Mungu.
10 But by the grace of God I am what I am: and his favor to me was not in vain; but I laboured more abundantly than they all; yet not I, but the grace of God that was with me.
Lakini, kwa neema yake Mungu, nimekuwa kama nilivyo. Na neema yake kwangu haikuwa bure. Mimi nimefanya kazi kuliko wote; si mimi hasa, ila ni neema ya Mungu ifanyayo kazi pamoja nami.
11 Whether therefore I or they laboured most, thus we preach, and thus ye believed.
Lakini hata hivyo, iwe wao ndio wahubirio au mimi nihubiriye, haidhuru, hiki ndicho tunachuhubiri, na hiki ndicho mnachoamini.
12 Now if it be preached that Christ is risen from the dead, how say some among you, that there is no resurrection of the dead?
Sasa, maadam inahubiriwa kwamba Kristo amefufuliwa kutoka wafu, baadhi yenu wanawezaje kusema kwamba hakuna ufufuo wa wafu?
13 for if there be no resurrection of the dead, then Christ is not risen.
Kama hakuna ufufuo wa wafu, basi, Kristo naye hakufufuka;
14 And if Christ be not risen, then is our preaching vain, and your faith is also vain.
na kama Kristo hakufufuka, basi mahubiri yetu hayana maana na imani yenu haina maana.
15 Yea, and we are found false witnesses concerning God, for we have testified of God, that He raised up Christ; whom He did not raise up, if indeed the dead do not rise.
Zaidi ya hayo sisi tungekuwa mashahidi wa uongo mbele ya Mungu, maana tulisema kwamba Mungu alimfufua Kristo kutoka wafu na kumbe yeye hakumfufua—kama ni kweli kwamba wafu hawafufuliwi.
16 For if the dead rise not, then Christ is not raised:
Maana, ikiwa ni kweli kwamba wafu hawafufuki, basi naye Kristo hakufufuka.
17 and if Christ be not risen, your faith is vain; ye are yet in your sins.
Na kama Kristo hakufufuliwa, basi, imani yenu ni ya bure; mngali bado katika dhambi zenu.
18 Then they also that sleep in Christ, are perished.
Zaidi ya hayo, wale wote waliokufa wakiwa wameungana na Kristo wamepotea kabisa.
19 If in this life only we have hope in Christ, we are of all men most miserable.
Kama matumaini yetu katika Kristo yanahusu tu maisha haya ya sasa, basi, sisi ni watu wa kusikitikiwa zaidi kuliko wengine wote duniani.
20 But now Christ is risen from the dead, and is become the first-fruits of them that slept:
Lakini ukweli ni kwamba Kristo amefufuliwa kutoka wafu, limbuko lao wale waliolala katika kifo.
21 for as by man came death, by man cometh also the resurrection of the dead.
Maana kama vile kifo kilivyoletwa duniani na mtu mmoja, vivyo hivyo nako kufufuka kutoka wafu kumesababishwa na mtu mmoja.
22 For as in Adam all die, so also in Christ shall all be made alive.
Kama vile watu wote wanavyokufa kwa kujiunga na Adamu, vivyo hivyo wote watafufuliwa kwa kuungana na Kristo.
23 But each in their proper order: the first-fruits, Christ; afterwards they that are Christ's, at his coming.
Lakini kila mmoja kwa mpango wake: Kristo kwanza, halafu wale walio wake Kristo wakati Kristo atakapokuja.
24 Then will be the end, when He shall have delivered up the kingdom to God even the Father; when He shall have abolished all rule, and all authority, and power.
Baada ya hayo, mwisho utafika wakati ambapo Kristo atamkabidhi Mungu Baba Utawala, baada ya kufutilia mbali kila tawala na mamlaka na nguvu.
25 For he must reign till He hath put all his enemies under his feet.
Maana Kristo sharti atawale mpaka Mungu atakapowashinda adui zake na kuwaweka chini ya miguu yake.
26 The last enemy that is destroyed is death:
Adui wa mwisho atakayeangamizwa ni kifo.
27 for He hath put all things under his feet. But when He saith that all things are put under Him, it is plain that we are to except Him who put all things under Him.
Maana, Maandiko yasema: “Mungu ameweka vitu vyote chini ya miguu yake.” Lakini, Maandiko yanaposema: “Vitu vyote vimewekwa chini ya miguu yake avitawale” ni dhahiri kwamba Mungu haingii katika kundi hilo la vitu, maana yeye ndiye anayeviweka vitu hivyo chini ya Kristo.
28 And when all things shall be subjected to Him, then shall the Son also himself be subject to Him, that put all things under Him, that God may be all in all.
Lakini vitu vyote vitakapowekwa chini ya Utawala wa Kristo, ndipo naye Mwana atakapojiweka chini ya Mungu, aliyeweka vyote chini ya Utawala wake; ili Mungu atawale juu ya vyote.
29 Besides, what shall they do who are baptized for the dead, if the dead rise not at all? why then are they baptized for the dead?
Kama hakuna ufufuo, je watu wale wanaobatizwa kwa ajili ya wafu wanatumainia kupata nini? Kama wafu hawafufuliwi, ya nini kubatizwa kwa ajili yao?
30 And why are we in danger every hour?
Na sisi, ya nini kujitia hatarini kila saa?
31 I protest by your rejoicing, which I have in Christ Jesus our Lord, that I am even dying daily.
Ndugu, mimi nakikabili kifo kila siku! Fahari niliyo nayo juu yenu katika kuungana na Kristo Yesu Bwana wetu inanifanya nitangaze jambo hili.
32 If, to speak as a man, I fought with beasts at Ephesus, what advantage have I, if the dead rise not? Let us eat and drink, for to-morrow we die. ---
Kama kusudi langu lingalikuwa la kibinadamu tu, kule kupigana kwangu na wanyama wakali hapa Efeso kungalinifaa kitu gani? Kama wafu hawafufuki, basi, “Tule na tunywe, maana kesho tutakufa.”
33 Be not deceived, bad conversations corrupt good morals.
Msidanganyike! Urafiki mbaya huharibu tabia njema.
34 Behave soberly, as ye ought to do, and sin not: for some of you have not the knowledge of God; to your shame I speak it.
Amkeni! Anzeni kuishi vema, na acheni kutenda dhambi. Baadhi yenu hawamjui Mungu kabisa. Hii nawaambieni, ni aibu kubwa kwenu!
35 But some will say, How are the dead raised, and with what body do they come?
Lakini mtu anaweza kuuliza: “Wafu watafufuliwaje? Watakuwa na mwili wa namna gani wakati watakapokuja tena?”
36 Silly creature! that which thou sowest, is not quickened, except it die first.
Hayo ni maswali ya kijinga! Ukipanda mbegu, isipokufa kwanza haitaota.
37 And as to what thou sowest, thou sowest not the very body that shall be produced, but a bare grain, it may be, of wheat, or any other corn:
Unachopanda ni mbegu tu, labda ya ngano au nafaka nyingine, na si mmea mzima ambao hutokea baadaye.
38 and God giveth it a body as He pleaseth, and to every one of the seeds it's own body.
Mungu huipa hiyo mbegu mwili anaoutaka mwenyewe; kila mbegu hupata mwili wake wa pekee.
39 All flesh is not the same kind of flesh: but there is one flesh of men, and another of beasts, another of fishes, and another of birds.
Miili ya viumbe vyote si sawa. Miili ya binadamu ni ya namna moja, ya wanyama ni ya namna nyingine, ya ndege ni ya namna nyingine na miili ya samaki pia ni ya namna nyingine.
40 There are also celestial bodies, and terrestrial bodies: but there is one glory of the celestial, and another of the terrestrial.
Iko miili ya mbinguni na miili ya duniani; uzuri wa miili ya mbinguni ni mwingine, na na uzuri wa miili ya duniani ni mwingine.
41 There is one glory of the sun, and another glory of the moon, and another glory of the stars: and one star differeth from another star in glory.
Uko uzuri wa jua, wa mwezi na wa nyota; hata nyota nazo huhitilafiana kwa uzuri.
42 So also will be the resurrection of the dead. Our body is sown in corruption, it is raised incorruptible: it is sown in dishonor, it is raised in glory:
Ndivyo ilivyo kuhusu ufufuo wa wafu. Kama vile mbegu, mwili huzikwa ardhini ukiwa katika hali ya kuharibika, lakini hufufuliwa katika hali ya kutoharibika.
43 it is sown in weakness, it is raised in power;
Huzikwa katika hali duni, hufufuliwa katika hali tukufu; huzikwa katika hali dhaifu, hufufuliwa ukiwa wenye nguvu.
44 it is sown an animal body, it is raised a spiritual body: for there is an animal body, and there is a spiritual body.
Unapozikwa ni mwili wa kawaida, unapofufuliwa ni mwili wa kiroho. Kuna mwili wa kawaida na kutakuwa na mwili wa kiroho.
45 And so it is written, "The first man Adam was made a living soul." But the last Adam is an enlivening spirit.
Maana Maandiko yasema: “Mtu wa kwanza, Adamu, alikuwa kiumbe mwenye uhai;” lakini adamu wa mwisho ni Roho awapaye watu uzima.
46 However, the spiritual is not first, but the animal; and afterwards the spiritual.
Lakini unaotangulia kuwako si ule mwili wa kiroho, ila ule mwili wa kawaida kisha ule mwili wa kiroho.
47 The first man being made out of the earth, was earthy: the second man is the Lord from heaven.
Adamu wa kwanza aliumbwa kwa udongo, alitoka ardhini; mtu wa pili alitoka mbinguni.
48 Such as the earthy was, such are they also that are earthy: and such, as is the heavenly, are they also that are heavenly.
Wote walio wa dunia wako kama huyo mtu aliyeumbwa kwa udongo; wale walio wa mbinguni wako kama yule aliyetoka mbinguni.
49 And as we have borne the image of the earthy, we shall also bear the image of the heavenly.
Kama vile tulivyofanana na yule aliyeumbwa kwa udongo, vivyo hivyo tutafanana na huyohuyo aliyetoka mbinguni.
50 But this I say, brethren, that flesh and blood cannot inherit the kingdom of God; nor doth what is corruptible inherit incorruption.
Basi, ndugu, nasema hivi: kile kilichofanywa kwa mwili na damu hakiwezi kuushiriki Ufalme wa Mungu; na chenye kuharibika hakiwezi kuwa na hali ya kutoharibika.
51 Behold, I tell you a mystery: we shall not all sleep; but we shall all be changed in a moment,
Sikilizeni, nawaambieni siri: sisi hatutakufa sote, ila sote tutageuzwa
52 in the twinkling of an eye, at the sound of the last trumpet (for the trumpet shall sound) and the dead shall be raised incorruptible, and we shall be changed:
wakati wa mbiu ya mwisho, kwa nukta moja, kufumba na kufumbua. Maana mbiu itakapolia, wafu watafufuliwa katika hali ya kutoweza kufa tena, na sisi tutageuzwa.
53 for this corruptible body must put on incorruption, and this mortal body must be clothed with immortality.
Maana ni lazima kila kiharibikacho kijivalie hali ya kutoharibika, mwili uwezao kufa ujivalie hali ya kutokufa.
54 And when this corruptible shall be clothed with incorruption, and this mortal shall have put on immortality, then shall come to pass the word that is written, "Death is swallowed up in victory."
Basi, mwili huu wenye kuharibika utakapojivalia hali ya kutoharibika, na kile chenye kufa kitakapojivalia hali ya kutokufa, hapo ndipo litakapotimia lile neno lililoandikwa: “Kifo kimeangamizwa ushindi umekamilika!”
55 O death, where is thy sting? O grave, where is thy victory? (Hadēs g86)
“Kifo, ushindi wako uko wapi? Uwezo wako wa kuumiza uko wapi?” (Hadēs g86)
56 the sting of death is sin; and the strength of sin is the law:
Ukali wa kifo hutokana na dhambi, nayo dhambi hupata nguvu yake katika Sheria.
57 but thanks be to God, who giveth us the victory through our Lord Jesus Christ.
Lakini tumshukuru Mungu anayetupatia ushindi kwa njia ya Bwana wetu Yesu Kristo.
58 Wherefore, my beloved brethren, be stedfast, unmoveable, always abounding in the work of the Lord, since ye know that your labor is not in vain in the Lord.
Basi, ndugu zangu wapenzi, simameni imara na thabiti. Endeleeni daima kuwa na bidii katika kazi ya Bwana, mkijua kwamba kazi mnayofanya katika utumishi wa Bwana haitapotea bure.

< 1 Corinthians 15 >