< Proverbs 16 >

1 The plans of the heart belong to man, but the answer of the tongue is from the LORD.
Mipango ya moyo ni ya mtu, bali Yehova hutoa jawabu kutoka kwenye ulimi wake.
2 All the ways of a man are clean in his own eyes, but the LORD weighs the motives.
Njia zote za mtu ni safi kwenye macho yake mwenyewe, bali Yehova huipima mioyo.
3 Commit your deeds to the LORD, and your plans shall succeed.
Kabidhi kwa Yehova kazi zako zote na mipango yako itafanikiwa.
4 The LORD has made everything for its own end— yes, even the wicked for the day of evil.
Yehova alifanya kila kitu kwa kusudi lake, hata waovu kwa ajili ya siku ya taabu.
5 Everyone who is proud in heart is an abomination to the LORD; they shall certainly not be unpunished.
Yehova anamchukia kila mtu mwenye moyo wa majivuno, ingawa wanasimama imara, hawakosi kupata adhabu.
6 By mercy and truth iniquity is atoned for. By the fear of the LORD men depart from evil.
Kwa agano la uaminifu na udhamini uovu husafishwa na kwa kumcha Yehova watu hujitenga na ubaya.
7 When a man’s ways please the LORD, he makes even his enemies to be at peace with him.
Njia za mtu zinapompendeza Yehova, huwafanya hata adui zake huyo mtu wawe na amani naye.
8 Better is a little with righteousness, than great revenues with injustice.
Bora kitu kidogo pamoja na haki, kuliko mapato makubwa pamoja na udhalimu.
9 A man’s heart plans his course, but the LORD directs his steps.
Katika moyo wake mtu hunuia njia yake, bali Yehova huziongoza hatua zake.
10 Inspired judgements are on the lips of the king. He shall not betray his mouth.
Mshauri yupo katika midimo ya mfalme, katika hukumu kinywa chake hakisemi kwa udanganyifu.
11 Honest balances and scales are the LORD’s; all the weights in the bag are his work.
Vipimo vya kweli hutoka kwa Yehova; uzito wote kwenye gunia ni kazi yake.
12 It is an abomination for kings to do wrong, for the throne is established by righteousness.
Wafalme wanapofanya mambo maovu, hicho ni kitu cha kudharauliwa, kwa maana utawala huimarishwa kwa kutenda haki.
13 Righteous lips are the delight of kings. They value one who speaks the truth.
Mfalme hufurahia midomo ambayo husema haki na anampenda mwenye kusema waziwazi.
14 The king’s wrath is a messenger of death, but a wise man will pacify it.
Hasira ya mfalme ni mjumbe wa mauti lakini mtu mwenye busara atajaribu kutuliza hasira yake.
15 In the light of the king’s face is life. His favour is like a cloud of the spring rain.
Katika nuru ya uso wa mfalme ni uzima na fadhila yake ni kama wingu linaloleta mvua ya masika.
16 How much better it is to get wisdom than gold! Yes, to get understanding is to be chosen rather than silver.
Ni bora kiasi gani kupata hekima kuliko dhahabu. Kuchagua kupata ufahamu ni zaidi kuliko fedha.
17 The highway of the upright is to depart from evil. He who keeps his way preserves his soul.
Njia kuu ya watu waadilifu hujitenga na ubaya; mwenye kuyahifadhi maisha yake huilinda njia yake.
18 Pride goes before destruction, and an arrogant spirit before a fall.
Kiburi hutangulia kabla ya uharibifu na moyo wa kujivuna kabla ya maangamizi.
19 It is better to be of a lowly spirit with the poor, than to divide the plunder with the proud.
Ni bora kunyenyekea miongoni mwa watu masikini kuliko kugawana ngawira pamoja watu wenye kiburi.
20 He who heeds the Word finds prosperity. Whoever trusts in the LORD is blessed.
Mwenye kutafakari yaliyofundishwa hupata kilicho chema na wenye kumtumaini Yehova watafurahi.
21 The wise in heart shall be called prudent. Pleasantness of the lips promotes instruction.
Mwenye hekima moyoni anaitwa ufuhamu na utamu wa hotuba huongeza uwezo wa kufundisha.
22 Understanding is a fountain of life to one who has it, but the punishment of fools is their folly.
Ufahamu ni chemchemi ya uzima kwake ambaye nayo, bali adhabu ya wapumbavu ni upumbavu wao.
23 The heart of the wise instructs his mouth, and adds learning to his lips.
Moyo wa mtu mwenye hekima hutoa busara katika kinywa chake na huongeza ushawishi katika midomo yake.
24 Pleasant words are a honeycomb, sweet to the soul, and health to the bones.
Maneno yenye kufaa ni sega la asali -matamu kwenye nafsi na huponya mifupa.
25 There is a way which seems right to a man, but in the end it leads to death.
Kuna njia ambayo huonekana sawa kwa mtu, bali mwisho wake ni njia ya mauti.
26 The appetite of the labouring man labours for him, for his mouth urges him on.
Hamu ya kibarua humfanyia kazi; njaa yake humsihi kuendelea.
27 A worthless man devises mischief. His speech is like a scorching fire.
Mtu duni huchimba madhara na usemi wake ni kama moto unaounguza.
28 A perverse man stirs up strife. A whisperer separates close friends.
Mtu mkaidi huchochea mafarakano na umbeya huwafarakanisha marafiki.
29 A man of violence entices his neighbour, and leads him in a way that is not good.
Mtu wa vurugu humdanganya jirani yake na kumwongoza kwenye mapito ambayo si mema.
30 One who winks his eyes to plot perversities, one who compresses his lips, is bent on evil.
Yule anayekonyeza kwa jicho anapanga njama za mambo ya ukaidi; wenye kuandama midomo yao watapitisha mabaya.
31 Grey hair is a crown of glory. It is attained by a life of righteousness.
Mvi ni taji ya utukufu; hupatikana kwa kuishi katika njia ya haki.
32 One who is slow to anger is better than the mighty; one who rules his spirit, than he who takes a city.
Ni bora kukawia kuwa na hasira kuliko kuwa shujaa na mwenye kutawala roho yake ni imara zaidi kuliko yule anayeuteka mji.
33 The lot is cast into the lap, but its every decision is from the LORD.
Kura hurushwa kwenye mkunjo, bali maamuzi hutoka kwa Yehova.

< Proverbs 16 >