< Jonah 2 >

1 Then Jonah prayed to the LORD, his God, out of the fish’s belly.
Akiwa ndani ya tumbo la nyangumi, Yona alimwomba Bwana Mungu wake.
2 He said, “I called because of my affliction to the LORD. He answered me. Out of the belly of Sheol I cried. You heard my voice. (Sheol h7585)
Akasema: “Katika shida yangu nalimwita Bwana, naye akanijibu. Kutoka kina cha kaburi niliomba msaada, nawe ukasikiliza kilio changu. (Sheol h7585)
3 For you threw me into the depths, in the heart of the seas. The flood was all around me. All your waves and your billows passed over me.
Ulinitupa kwenye kilindi, ndani kabisa ya moyo wa bahari, mikondo ya maji ilinizunguka, mawimbi yako yote na viwimbi vilipita juu yangu.
4 I said, ‘I have been banished from your sight; yet I will look again towards your holy temple.’
Nikasema, ‘Nimefukuziwa mbali na uso wako, hata hivyo nitatazama tena kuelekea Hekalu lako takatifu.’
5 The waters surrounded me, even to the soul. The deep was around me. The weeds were wrapped around my head.
Maji yaliyonimeza yalinitisha, kilindi kilinizunguka; mwani ulijisokota kichwani pangu.
6 I went down to the bottoms of the mountains. The earth barred me in forever; yet you have brought my life up from the pit, LORD my God.
Nilizama chini sana mpaka pande za mwisho za milima, makomeo ya hiyo nchi yalinifungia hata milele. Lakini uliuleta uhai wangu kutoka shimoni, Ee Bwana Mungu wangu.
7 “When my soul fainted within me, I remembered the LORD. My prayer came in to you, into your holy temple.
“Wakati uhai wangu ulipokuwa unatoka, nilikukumbuka wewe, Bwana, nayo maombi yangu yalikufikia wewe, katika Hekalu lako takatifu.
8 Those who regard vain idols forsake their own mercy.
“Wale watu wanaongʼangʼana na sanamu zisizofaa hupoteza neema ile ambayo ingekuwa yao.
9 But I will sacrifice to you with the voice of thanksgiving. I will pay that which I have vowed. Salvation belongs to the LORD.”
Lakini mimi, kwa wimbo wa shukrani, nitakutolea dhabihu. Lile nililowekea nadhiri nitalitimiza. Wokovu watoka kwa Bwana.”
10 Then the LORD spoke to the fish, and it vomited out Jonah on the dry land.
Basi Bwana akamwamuru yule nyangumi, naye akamtapika Yona katika nchi kavu.

< Jonah 2 >