< Yochanan 11 >

1 Now a certain man was sick, Lazarus from Bethany, of the village of Miriam and her sister, Martha.
Basi mtu mmoja jina lake Lazaro alikuwa mgonjwa. Alitokea Bethania, kijiji cha Mariamu na dada yake Martha.
2 It was that Miriam who had anointed the Lord with ointment and wiped his feet with her hair, whose brother Lazarus was sick.
Alikuwa ni Mariamu yule yule aliyempaka Bwana Marhamu na kumfuta miguu yake kwa nywele zake, ambaye ndugu yake Lazaro alikuwa ni mgonjwa.
3 The sisters therefore sent to him, saying, “Lord, behold, he for whom you have great affection is sick.”
Ndipo dada hawa walituma ujumbe kwa Yesu na kusema, “Bwana, angalia yule umpendaye anaumwa.”
4 But when Yeshua heard it, he said, “This sickness is not to death, but for the glory of God, that God’s Son may be glorified by it.”
Yesu aliposikia alisema, “Ugonjwa huu si wa mauti, lakini, badala yake ni kwa ajili ya utukufu wa Mungu ili kwamba Mwana wa Mungu apate kutukuzwa katika huo Ugonjwa.”
5 Now Yeshua loved Martha, and her sister, and Lazarus.
Yesu alimpenda Martha na dada yake na Lazaro.
6 When therefore he heard that he was sick, he stayed two days in the place where he was.
Aliposikia kuwa Lazaro ni mgonjwa, Yesu alikaa siku mbili zaidi mahali alipokuwa.
7 Then after this he said to the disciples, “Let’s go into Judea again.”
Ndipo baada ya hili aliwaambia wanafunzi wake, “Twendeni Uyahudi tena.”
8 The disciples asked him, “Rabbi, the Judeans were just trying to stone you. Are you going there again?”
Wanafunzi wakamwambia, “Rabi, Wayahudi walikuwa wakijaribu kukuponda mawe, na wewe unataka kurudi huko tena?”
9 Yeshua answered, “Aren’t there twelve hours of daylight? If a man walks in the day, he doesn’t stumble, because he sees the light of this world.
Yesu akawajibu, “Saa za mchana si kumi na mbili? Mtu anapotembea mchana hawezi kujikwaa, kwa sababu anaona kwa nuru ya mchana.
10 But if a man walks in the night, he stumbles, because the light isn’t in him.”
Hata hivyo, ikiwa atatembea usiku, atajikwaa kwa sababu nuru haiko ndani yake.”
11 He said these things, and after that, he said to them, “Our friend Lazarus has fallen asleep, but I am going so that I may awake him out of sleep.”
Yesu akasema mambo haya, na baada ya mambo haya, akawaambia, “Rafiki yetu Lazaro amelala, lakini ninakwenda ili kwamba nipate kumuamsha kutoka usingizini.”
12 The disciples therefore said, “Lord, if he has fallen asleep, he will recover.”
Ndipo wanafunzi wakamwambia, “Bwana, kama amelala, ataamka.
13 Now Yeshua had spoken of his death, but they thought that he spoke of taking rest in sleep.
Wakati huu Yesu alikuwa akizungumza habari za kifo cha Lazaro, lakini wao walidhani anazungumza juu ya kulala usingizi.
14 So Yeshua said to them plainly then, “Lazarus is dead.
Ndipo Yesu akazungumza nao wazi wazi, “Lazaro amekufa.
15 I am glad for your sakes that I was not there, so that you may believe. Nevertheless, let’s go to him.”
Nina furaha kwa ajili yenu, kwamba sikuwepo kule ili kwamba mpate kuamini. Twendeni kwake.”
16 Thomas therefore, who is called Didymus, said to his fellow disciples, “Let’s also go, that we may die with him.”
Basi Tomaso, aliyeitwa Pacha, aliwaambia wanafunzi wenzake, “Nasi twendeni pia tukafe pamoja na Yesu.”
17 So when Yeshua came, he found that he had been in the tomb four days already.
Wakati Yesu alipokuja, alikuta kwamba Lazaro tayari amekwishakuwa kaburini siku nne.
18 Now Bethany was near Jerusalem, about fifteen stadia away.
Nayo Bethania ilikuwa karibu na Yerusalemu kama kilomita arobaini na tano hivi.
19 Many of the Judeans had joined the women around Martha and Miriam, to console them concerning their brother.
Wengi kati ya Wayahudi wakaja kwa Martha na Mariamu kuwafariji kwa ajili ya ndugu yao.
20 Then when Martha heard that Yeshua was coming, she went and met him, but Miriam stayed in the house.
Ndipo Martha aliposikia kuwa Yesu anakuja, alienda kukutana naye, lakini Mariamu aliendelea kukaa nyumbani.
21 Therefore Martha said to Yeshua, “Lord, if you would have been here, my brother wouldn’t have died.
Ndipo Martha akamwambia Yesu, “Bwana, kama ungelikuwa hapa, kaka yangu asingelikufa.
22 Even now I know that whatever you ask of God, God will give you.”
Hata sasa, najua ya kuwa lolote utakaloomba kutoka kwa Mungu, atakupatia.”
23 Yeshua said to her, “Your brother will rise again.”
Yesu akamwambia, kaka yako atafufuka tena.”
24 Martha said to him, “I know that he will rise again in the resurrection at the last day.”
Martha akamwambia, najua kwamba atafufuka katika ufufuo siku ya mwisho.”
25 Yeshua said to her, “I am the resurrection and the life. He who believes in me will still live, even if he dies.
Yesu akamwambia, “Mimi ni ufufuo na uzima; yeye aniaminiye, ingawa atakufa, hata hivyo atakuwa anaishi;
26 Whoever lives and believes in me will never die. Do you believe this?” (aiōn g165)
na yeye aishiye na kuniamini mimi hatakufa. Unaamini hili?” (aiōn g165)
27 She said to him, “Yes, Lord. I have come to believe that you are the Messiah, God’s Son, he who comes into the world.”
Akamwambia, “Ndiyo, Bwana naamini kwamba wewe ni Kristo, Mwana wa Mungu, yeye ajaye katika ulimwengu.”
28 When she had said this, she went away and called Miriam, her sister, secretly, saying, “The Rabbi is here and is calling you.”
Alipokwisha kusema hili, alienda zake na kumwita dada yake Mariamu faraghani. Akasema, “Mwalimu yuko hapa na anakuita.”
29 When she heard this, she arose quickly and went to him.
Mariamu aliposikia haya, aliinuka kwa haraka na kwenda kwa Yesu.
30 Now Yeshua had not yet come into the village, but was in the place where Martha met him.
Naye Yesu alikuwa hajaja bado ndani ya kijiji, bali alikuwa bado mahali alipokutana na Martha.
31 Then the Judeans who were with her in the house and were consoling her, when they saw Miriam, that she rose up quickly and went out, followed her, saying, “She is going to the tomb to weep there.”
Ndipo Wayahudi waliokuwa na Mariamu katika nyumba na wale waliokuwa wakimfariji, walipomuona akiinuka haraka na kutoka nje, walimfuata; walidhani kuwa anaenda kaburini ili akalie huko.
32 Therefore when Miriam came to where Yeshua was and saw him, she fell down at his feet, saying to him, “Lord, if you would have been here, my brother wouldn’t have died.”
Ndipo Mariamu, alipofika pale Yesu alipokuwa alimuona na, alianguka chini ya miguu yake na kumwambia, “Bwana, kama ungelikuwa hapa, ndugu yangu asingelikufa.”
33 When Yeshua therefore saw her weeping, and the Judeans weeping who came with her, he groaned in the spirit and was troubled,
Yesu alipomuona analia, na Wayahudi waliokuja pamoja naye walikuwa wakilia pia, aliomboleza katika roho na kufadhaika;
34 and said, “Where have you laid him?” They told him, “Lord, come and see.”
akasema, “Mmemlaza wapi? wakamwambia, Bwana, njoo utazame.”
35 Yeshua wept.
Yesu akalia.
36 The Judeans therefore said, “See how much affection he had for him!”
Ndipo Wayahudi wakasema, “Angalia alivyompenda Lazaro!”
37 Some of them said, “Couldn’t this man, who opened the eyes of him who was blind, have also kept this man from dying?”
Lakini wengine kati yao wakasema, “Siyo huyu, mtu aliyeyafumbua macho ya yule aliyekuwa kipofu, hakuweza kumfanya huyu mtu asife?”
38 Yeshua therefore, again groaning in himself, came to the tomb. Now it was a cave, and a stone lay against it.
Ndipo Yesu, hali akiomboleza nafsini mwake tena, alienda kwenye kaburi. Sasa lilikuwa pango, na jiwe limewekwa juu yake.
39 Yeshua said, “Take away the stone.” Martha, the sister of him who was dead, said to him, “Lord, by this time there is a stench, for he has been dead four days.”
Yesu akasema, “Liondoweni jiwe.” Martha, dada yake na Lazaro, yeye aliyekufa, akamwambia Yesu, “Bwana, kwa muda huu, mwili utakuwa umeoza, kwa sababu amekwishakuwa maiti kwa siku nne.”
40 Yeshua said to her, “Didn’t I tell you that if you believed, you would see God’s glory?”
Yesu akamwambia, “Mimi sikukuwaambia ya kwamba, kama ukiamini, utauona utukufu wa Mungu?”
41 So they took away the stone from the place where the dead man was lying. Yeshua lifted up his eyes and said, “Father, I thank you that you listened to me.
Kwa hiyo wakaliondoa jiwe. Yesu akainua macho yake juu na kusema, “Baba, nakushukuru kwa kuwa unanisikiliza.
42 I know that you always listen to me, but because of the multitude standing around I said this, that they may believe that you sent me.”
Nilijua kwamba unanisikia mara zote, lakini ni kwa sababu ya kusanyiko ambalo limesimama kunizunguka kwamba nimesema haya, ili kwamba wapate kuamini kuwa wewe umenituma.”
43 When he had said this, he cried with a loud voice, “Lazarus, come out!”
Baada ya kusema haya, alilia kwa sauti kubwa, “Lazaro, toka nje!”
44 He who was dead came out, bound hand and foot with wrappings, and his face was wrapped around with a cloth. Yeshua said to them, “Free him, and let him go.”
Mfu alitoka nje amefungwa mikono na miguu kwa sanda za kuzikia, na uso wake ulifungwa na kitambaa.” Yesu akawaambia, “Mfungueni mkamwache aende.”
45 Therefore many of the Judeans who came to Miriam and saw what Yeshua did believed in him.
Ndipo Wayahudi wengi waliokuja kwa Mariamu na kuona Yesu alichofanya, walimwamini;
46 But some of them went away to the Pharisees and told them the things which Yeshua had done.
lakini baadhi yao walienda kwa Mafarisayo na kuwaambia mambo aliyoyafanya Yesu.
47 The chief priests therefore and the Pharisees gathered a council, and said, “What are we doing? For this man does many signs.
Ndipo wakuu wa Makuhani na Mafarisayo wakakusanyika pamoja katika baraza na kusema, “Tutafanya nini? Mtu huyu anafanya ishara nyingi.
48 If we leave him alone like this, everyone will believe in him, and the Romans will come and take away both our place and our nation.”
Ikiwa tutamwacha hivi peke yake, wote watamwamini; Warumi watakuja na kuchukua vyote mahali petu na taifa letu.”
49 But a certain one of them, Caiaphas, being high priest that year, said to them, “You know nothing at all,
Hata hivyo, mtu mmoja kati yao, Kayafa, aliyekuwa kuhani Mkuu mwaka huo, akawaambia, “Hamjui chochote kabisa.
50 nor do you consider that it is advantageous for us that one man should die for the people, and that the whole nation not perish.”
Hamfikirii kwamba yafaa kwa ajili yenu kwamba mtu mmoja yapasa kufa kwa ajili ya watu kuliko taifa lote kuangamia.”
51 Now he didn’t say this of himself, but being high priest that year, he prophesied that Yeshua would die for the nation,
Haya hakuyasema kwa sababu yake mwenyewe, badala yake, kwa kuwa alikuwa kuhani mkuu mwaka ule, alitabiri kwamba Yesu atakufa kwa ajili ya taifa;
52 and not for the nation only, but that he might also gather together into one the children of God who are scattered abroad.
na si kwa taifa peke yake, bali Yesu apate vile vile kuwakusanya watoto wa Mungu ambao wametawanyika sehemu mbali mbali.
53 So from that day forward they took counsel that they might put him to death.
Kwa hiyo kuanzia siku hiyo na kuendelea wakapanga namna ya kumwua Yesu.
54 Yeshua therefore walked no more openly amongst the Judeans, but departed from there into the country near the wilderness, to a city called Ephraim. He stayed there with his disciples.
Yesu hakutembea tena wazi wazi kati ya Wayahudi, bali aliondoka hapo na kwenda nchi iliyo karibu na jangwa katika mji uitwao Efraimu. Hapo alikaa na wanafunzi.
55 Now the Passover in Judea was at hand. Many went up from the country to Jerusalem before the Passover, to purify themselves.
Basi Pasaka ya Wayahudi ilikuwa karibu, na wengi wakapanda kwenda Yerusalemu nje ya mji kabla ya Pasaka ili wapate kujitakasa wenyewe.
56 Then they sought for Yeshua and spoke with one another as they stood in the temple, “What do you think—that he isn’t coming to the feast at all?”
Walikuwa wakimtafuta Yesu, na kuzungumza kila mmoja walipokuwa wamesimama hekaluni, “Mnafikiri nini? Kwamba hatakuja katika sikukuu?”
57 Now the chief priests and the Pharisees had commanded that if anyone knew where he was, he should report it, that they might seize him.
Wakati huu wakuu wa makuhani na Mafarisayo walikuwa wametoa amri kwamba ikiwa mmoja atajua Yesu alipo, anapaswa kutoa taarifa ili kwamba wapate kumkamata.

< Yochanan 11 >