< 2 Samuel 22 >

1 David spoke to the LORD the words of this song in the day that the LORD delivered him out of the hand of all his enemies, and out of the hand of Saul,
Daudi alimwimbia Bwana maneno ya wimbo huu wakati Bwana alipomwokoa mikononi mwa adui zake wote, na pia mkononi mwa Sauli.
2 and he said: “The LORD is my rock, my fortress, and my deliverer, even mine;
Akasema: “Bwana ni mwamba wangu, ngome yangu na mwokozi wangu,
3 God is my rock in whom I take refuge; my shield, and the horn of my salvation, my high tower, and my refuge. My saviour, you save me from violence.
Mungu wangu ni mwamba wangu, ambaye kwake ninakimbilia, ngao yangu na pembe ya wokovu wangu. Yeye ni ngome yangu, kimbilio langu na mwokozi wangu, huniokoa kutoka kwa watu wenye jeuri.
4 I call on the LORD, who is worthy to be praised; So shall I be saved from my enemies.
Ninamwita Bwana, anayestahili kusifiwa, nami ninaokolewa kutoka kwa adui zangu.
5 For the waves of death surrounded me. The floods of ungodliness made me afraid.
“Mawimbi ya mauti yalinizunguka, mafuriko ya maangamizi yalinilemea.
6 The cords of Sheol were around me. The snares of death caught me. (Sheol h7585)
Kamba za kuzimu zilinizunguka, mitego ya mauti ilinikabili. (Sheol h7585)
7 In my distress, I called on the LORD. Yes, I called to my God. He heard my voice out of his temple. My cry came into his ears.
Katika shida yangu nalimwita Bwana, nilimlilia Mungu wangu. Kutoka Hekaluni mwake alisikia sauti yangu, kilio changu kikafika masikioni mwake.
8 Then the earth shook and trembled. The foundations of heaven quaked and were shaken, because he was angry.
“Dunia ilitetemeka na kutikisika, misingi ya mbingu ikatikisika, vilitetemeka kwa sababu alikuwa amekasirika.
9 Smoke went up out of his nostrils. Consuming fire came out of his mouth. Coals were kindled by it.
Moshi ukapanda kutoka puani mwake, moto uteketezao ukatoka kinywani mwake, makaa ya moto yawakayo yakatoka ndani mwake.
10 He bowed the heavens also, and came down. Thick darkness was under his feet.
Akazipasua mbingu akashuka chini, mawingu meusi yalikuwa chini ya miguu yake.
11 He rode on a cherub, and flew. Yes, he was seen on the wings of the wind.
Alipanda juu ya kerubi akaruka, akapaa juu kwa mbawa za upepo.
12 He made darkness a shelter around himself, gathering of waters, and thick clouds of the skies.
Alifanya giza hema lake la kujifunika: mawingu meusi ya mvua ya angani.
13 At the brightness before him, coals of fire were kindled.
Kutokana na mwanga wa uwepo wake mawingu yalisogea, ikanyesha mvua ya mawe na umeme wa radi.
14 The LORD thundered from heaven. The Most High uttered his voice.
Bwana alinguruma kutoka mbinguni, sauti ya Aliye Juu Sana ilisikika.
15 He sent out arrows and scattered them, lightning and confused them.
Aliipiga mishale na kutawanya adui, umeme wa radi na kuwafukuza.
16 Then the channels of the sea appeared. The foundations of the world were laid bare by the LORD’s rebuke, at the blast of the breath of his nostrils.
Mabonde ya bahari yalifunuliwa, na misingi ya dunia ikawa wazi kwa kukaripia kwake Bwana, kwa uvumi wa pumzi kutoka puani mwake.
17 He sent from on high and he took me. He drew me out of many waters.
“Alinyoosha mkono kutoka juu na kunishika; alinitoa kutoka kilindi cha maji makuu.
18 He delivered me from my strong enemy, from those who hated me, for they were too mighty for me.
Aliniokoa kutoka adui wangu mwenye nguvu nyingi, kutoka adui zangu waliokuwa na nguvu nyingi kuliko mimi.
19 They came on me in the day of my calamity, but the LORD was my support.
Walinikabili siku ya msiba wangu, lakini Bwana alikuwa msaada wangu.
20 He also brought me out into a large place. He delivered me, because he delighted in me.
Alinileta nje mahali penye nafasi tele, akaniokoa kwa kuwa alipendezwa nami.
21 The LORD rewarded me according to my righteousness. He rewarded me according to the cleanness of my hands.
“Bwana alinitendea sawasawa na uadilifu wangu; sawasawa na usafi wa mikono yangu amenilipa.
22 For I have kept the LORD’s ways, and have not wickedly departed from my God.
Kwa maana nimezishika njia za Bwana; sijatenda ubaya nikamwacha Mungu wangu.
23 For all his ordinances were before me. As for his statutes, I didn’t depart from them.
Sheria zake zote zi mbele yangu, wala sijayaacha maagizo yake.
24 I was also perfect towards him. I kept myself from my iniquity.
Nimekuwa sina hatia mbele zake, nami nimejilinda nisitende dhambi.
25 Therefore the LORD has rewarded me according to my righteousness, According to my cleanness in his eyesight.
Bwana amenilipa sawasawa na uadilifu wangu, sawasawa na usafi wangu machoni pake.
26 With the merciful you will show yourself merciful. With the perfect man you will show yourself perfect.
“Kwa yeye aliye mwaminifu unajionyesha kuwa mwaminifu, kwa asiye na hatia unajionyesha kutokuwa na hatia,
27 With the pure you will show yourself pure. With the crooked you will show yourself shrewd.
kwa aliye mtakatifu unajionyesha kuwa mtakatifu, lakini kwa aliyepotoka unajionyesha kuwa mkaidi.
28 You will save the afflicted people, but your eyes are on the arrogant, that you may bring them down.
Wewe huwaokoa wanyenyekevu, lakini macho yako ni juu ya wenye kiburi ili uwashushe.
29 For you are my lamp, LORD. The LORD will light up my darkness.
Wewe ni taa yangu, Ee Bwana. Bwana hulifanya giza langu kuwa mwanga.
30 For by you, I run against a troop. By my God, I leap over a wall.
Kwa msaada wako naweza kushinda jeshi, nikiwa pamoja na Mungu wangu nitaweza kuruka ukuta.
31 As for God, his way is perfect. The LORD’s word is tested. He is a shield to all those who take refuge in him.
“Kuhusu Mungu, njia yake ni kamilifu; neno la Bwana halina dosari. Yeye ni ngao kwa wote wanaokimbilia kwake.
32 For who is God, besides the LORD? Who is a rock, besides our God?
Kwa maana ni nani aliye Mungu zaidi ya Bwana? Ni nani aliye Mwamba isipokuwa Mungu wetu?
33 God is my strong fortress. He makes my way perfect.
Mungu ndiye anivikaye nguvu na kufanya njia yangu kuwa kamilifu.
34 He makes his feet like hinds’ feet, and sets me on my high places.
Huifanya miguu yangu kama miguu ya kulungu, huniwezesha kusimama mahali palipo juu.
35 He teaches my hands to war, so that my arms bend a bow of bronze.
Huifundisha mikono yangu kupigana vita; mikono yangu inaweza kupinda upinde wa shaba.
36 You have also given me the shield of your salvation. Your gentleness has made me great.
Hunipa ngao yako ya ushindi, unajishusha chini ili kuniinua.
37 You have enlarged my steps under me. My feet have not slipped.
Huyapanua mapito yangu, ili miguu yangu isiteleze.
38 I have pursued my enemies and destroyed them. I didn’t turn again until they were consumed.
“Niliwafuatia adui zangu na nikawaseta, sikurudi nyuma mpaka walipoangamizwa.
39 I have consumed them, and struck them through, so that they can’t arise. Yes, they have fallen under my feet.
Niliwaseta kabisa, nao hawakuweza kuinuka tena; walianguka chini ya miguu yangu.
40 For you have armed me with strength for the battle. You have subdued under me those who rose up against me.
Ulinivika nguvu kwa ajili ya kupigana vita; uliwafanya adui zangu wasujudu miguuni pangu.
41 You have also made my enemies turn their backs to me, that I might cut off those who hate me.
Uliwafanya adui zangu wageuke na kukimbia, nami nikawaangamiza adui zangu.
42 They looked, but there was no one to save; even to the LORD, but he didn’t answer them.
Walipiga yowe, lakini hapakuwepo na yeyote wa kuwaokoa; walimlilia Bwana, lakini hakuwajibu.
43 Then I beat them as small as the dust of the earth. I crushed them as the mire of the streets, and spread them abroad.
Niliwaponda kama mavumbi ya nchi; niliwaponda na kuwakanyaga kama tope barabarani.
44 You also have delivered me from the strivings of my people. You have kept me to be the head of the nations. A people whom I have not known will serve me.
“Umeniokoa kutokana na mashambulizi ya watu wangu; umenihifadhi mimi kama kiongozi wa mataifa. Watu ambao sikuwajua wananitumikia,
45 The foreigners will submit themselves to me. As soon as they hear of me, they will obey me.
nao wageni huja wakininyenyekea, mara wanisikiapo, hunitii.
46 The foreigners will fade away, and will come trembling out of their close places.
Wote wanalegea, wanatoka katika ngome zao wakitetemeka.
47 The LORD lives! Blessed be my rock! Exalted be God, the rock of my salvation,
“Bwana yu hai! Sifa ni kwa Mwamba wangu! Atukuzwe Mungu, Mwamba, Mwokozi wangu!
48 even the God who executes vengeance for me, who brings down peoples under me,
Yeye ndiye Mungu anilipiziaye kisasi, ayawekaye mataifa chini yangu,
49 who brings me away from my enemies. Yes, you lift me up above those who rise up against me. You deliver me from the violent man.
aniwekaye huru toka kwa adui zangu. Uliniinua juu ya adui zangu; uliniokoa toka kwa watu wajeuri.
50 Therefore I will give thanks to you, LORD, amongst the nations, and will sing praises to your name.
Kwa hiyo nitakusifu, Ee Bwana, katikati ya mataifa; nitaliimbia sifa jina lako.
51 He gives great deliverance to his king, and shows loving kindness to his anointed, to David and to his offspring, forever more.”
Humpa mfalme wake ushindi mkuu; huonyesha fadhili zake kwa mpakwa mafuta wake, kwa Daudi na wazao wake milele.”

< 2 Samuel 22 >