< 2 Corinthians 6 >

1 Working together, we entreat also that you do not receive the grace of God in vain.
Na kwa hiyo, kufanya kazi pamoja, tunawasihi ninyi msiipokee neema ya Mungu pasipo matokeo.
2 For he says, “At an acceptable time I listened to you. In a day of salvation I helped you.” Behold, now is the acceptable time. Behold, now is the day of salvation.
Kwa kuwa anasema, “Wakati uliokubalika nilikuwa makini kwenu, na katika siku ya wokovu niliwasaidia.” Tazama, sasa ni wakati uliokubalika. Tazama, sasa ni siku ya wokovu.
3 We give no occasion of stumbling in anything, that our service may not be blamed,
Hatuweki jiwe la kizuizi mbele ya mtu yeyote, kwa kuwa hatuitakii huduma yetu iletwe katika sifa mbaya.
4 but in everything commending ourselves as servants of God: in great endurance, in afflictions, in hardships, in distresses,
Badala yake, tunajihakiki wenyewe kwa matendo yetu yote, kwamba tu watumishi wa Mungu. Tu watumishi wake katika wingi wa ustahimilivu, mateso, dhiki, ugumu wa maisha,
5 in beatings, in imprisonments, in riots, in labours, in watchings, in fastings,
kupigwa, vifungo, ghasia, katika kufanya kazi kwa bidii, katika kukosa usingizi usiku, katika njaa,
6 in pureness, in knowledge, in perseverance, in kindness, in the Holy Spirit, in sincere love,
katika usafi, maarifa, uvumilivu, wema, katika Roho Mtakatifu, katika upendo halisi.
7 in the word of truth, in the power of God, by the armour of righteousness on the right hand and on the left,
Tu watumishi wake katika neno la kweli, katika nguvu ya Mungu. Tuna silaha ya haki kwa ajili ya mkono wa kuuume na wa kushoto.
8 by glory and dishonour, by evil report and good report, as deceivers and yet true,
Tunafanya kazi katika heshima na kudharauliwa, katika kashfa na sifa. Tunatuhumiwa kuwa wadanganyifu na wakati tu wakweli.
9 as unknown and yet well known, as dying and behold—we live, as punished and not killed,
Tunafanya kazi kana kwamba hatujulikani na bado tunajulikana vizuri. Tunafanya kazi kama wanaokufa na -Tazama! - bado tunaishi. Tunafanya kazi kama tunaoadhibiwa kwa ajili ya matendo yetu lakini sio kama waliohukumiwa hata kufa.
10 as sorrowful yet always rejoicing, as poor yet making many rich, as having nothing and yet possessing all things.
Tunafanya kazi kama wenye masikitiko, lakini siku zote tuna furaha. Tunafanya kazi kama maskini, lakini tunatajirisha wengi. Tunafanya kazi kana kwamba hatupati kitu bali kama tunaomiliki kila kitu.
11 Our mouth is open to you, Corinthians. Our heart is enlarged.
Tumezungumza ukweli wote kwenu, Wakorintho, na mioyo yetu imefunguka kwa upana.
12 You are not restricted by us, but you are restricted by your own affections.
mioyo yenu haizuiliwi na sisi, bali mnazuiliwa na hisia zenu wenyewe.
13 Now in return—I speak as to my children—you also open your hearts.
Sasa katika kubadilishana kwa haki - ninaongea kama kwa watoto - fungueni mioyo yenu kwa upana.
14 Don’t be unequally yoked with unbelievers, for what fellowship do righteousness and iniquity have? Or what fellowship does light have with darkness?
Msifungamanishwe pamoja na wasioamini. Kwa kuwa kuna uhusiano gani kati ya haki na uasi? Na kuna ushirika gani kati ya nuru na giza?
15 What agreement does Messiah have with Belial? Or what portion does a believer have with an unbeliever?
Ni makubaliano gani Kristo anaweza kuwa nayo na Beliari? Au yeye aaminiye ana sehemu gani pamoja na asiyeamini?
16 What agreement does a temple of God have with idols? For you are a temple of the living God. Even as God said, “I will dwell in them and walk in them. I will be their God and they will be my people.”
Na kuna makubaliano gani yapo kati ya hekalu la Mungu na sanamu? Kwa kuwa sisi ni hekalu la Mungu aliye hai, kama ambavyo Mungu alisema: “Nitakaa kati yao na kutembea kati yao. Nitakuwa Mungu wao, nao watakuwa watu wangu.”
17 Therefore “‘Come out from amongst them, and be separate,’ says the Lord. ‘Touch no unclean thing. I will receive you.
Kwa hiyo, “Tokeni kati yao, na mkatengwe nao,” asema Bwana. “Msiguse kitu kichafu, na nitawakaribisha ninyi.
18 I will be to you a Father. You will be to me sons and daughters,’ says the Lord Almighty.”
Nitakuwa Baba kwenu, nanyi mtakuwa wanangu wa kiume na wa kike,” asema Bwana Mwenyezi.

< 2 Corinthians 6 >