< Psalms 88 >

1 A Song. A Psalm by the sons of Korah. For the Chief Musician. To the tune of “The Suffering of Affliction.” A contemplation by Heman, the Ezrahite. Yahweh, the God of my salvation, I have cried day and night before you.
Yahwe, Mungu wa wokovu wangu, ninalia mchana na usiku mbele zako.
2 Let my prayer enter into your presence. Turn your ear to my cry.
Sikiliza maombi yangu; utazame kulia kwangu.
3 For my soul is full of troubles. My life draws near to Sheol. (Sheol h7585)
Maana nimejawa taabu, na uhai wangu umefika kuzimuni. (Sheol h7585)
4 I am counted among those who go down into the pit. I am like a man who has no help,
Watu hunichukulia kama wale waendao chini shimoni; mimi ni mtu asiye na nguvu.
5 set apart among the dead, like the slain who lie in the grave, whom you remember no more. They are cut off from your hand.
Nimetelekezwa miongoni mwa wafu; niko kama mfu alalaye katika kaburi, wao ambao wewe huwajari tena kwa sababu wametengwa mbali na nguvu zako.
6 You have laid me in the lowest pit, in the darkest depths.
Wewe umeniweka katika sehemu ya chini kabisa ya shimo, sehemu yenye giza na kilindini.
7 Your wrath lies heavily on me. You have afflicted me with all your waves. (Selah)
Gadhabu yako yanielemea, na mawimbi yako yote yanatua juu yangu. (Selah)
8 You have taken my friends from me. You have made me an abomination to them. I am confined, and I can’t escape.
Kwa sababu yako, wale wanijuao wote hunikwepa. Umenifanya wakutisha machoni pao. Nimefungwa na siwezi kutoroka.
9 My eyes are dim from grief. I have called on you daily, Yahweh. I have spread out my hands to you.
Macho yangu yamefifia kutokana na shida; kila siku nakuita wewe, Yahwe; ninakunyoshea wewe mikono yangu.
10 Do you show wonders to the dead? Do the departed spirits rise up and praise you? (Selah)
Je! utafanya miujiza kwa ajili ya wafu? Wale waliokufa watafufuka na kukusifu wewe? (Selah)
11 Is your loving kindness declared in the grave? Or your faithfulness in Destruction?
Uaminifu wa agano lako utatangazwa kaburini? au uaminifu wako mahali pa wafu?
12 Are your wonders made known in the dark? Or your righteousness in the land of forgetfulness?
Matendo yako ya ajabu yatajulikana gizani? au haki yako katika mahali pa usahaulifu?
13 But to you, Yahweh, I have cried. In the morning, my prayer comes before you.
Lakini ninakulilia wewe, Yahwe; wakati wa asubuhi maombi yangu huja kwako.
14 Yahweh, why do you reject my soul? Why do you hide your face from me?
Yahwe, kwa nini unanikataa? Kwa nini unauficha uso wako mbali nami?
15 I am afflicted and ready to die from my youth up. While I suffer your terrors, I am distracted.
Nimekuwa nikiteswa kila siku na hatihati ya kifo tangu ujana wangu. Nimeteseka dhidi ya hofu yako kuu; ninakata tamaa.
16 Your fierce wrath has gone over me. Your terrors have cut me off.
Matendo yako ya hasira yamepita juu yangu, na matendo yako ya kutisha yameniangamiza.
17 They came around me like water all day long. They completely engulfed me.
Siku zote yananizingira mimi kama maji; yote yamenizunguka mimi.
18 You have put lover and friend far from me, and my friends into darkness.
Wewe umemuondoa kwangu kila rafiki na anijuaye. Na sasa anijuaye pekee ni giza.

< Psalms 88 >