< Psalms 115 >
1 Not to us, Yahweh, not to us, but to your name give glory, for your loving kindness, and for your truth’s sake.
Sio kwetu, Yahwe, sio kwetu, bali kwa jina lako ulete heshima, kwa ajili ya uaminifu wa agano lako na uaminifu wako.
2 Why should the nations say, “Where is their God, now?”
Kwa nini mataifa yalazimike kusema, “Yuko wapi Mungu wako?”
3 But our God is in the heavens. He does whatever he pleases.
Mungu wetu aliye mbinguni; hufanya chochote apendacho.
4 Their idols are silver and gold, the work of men’s hands.
Sanamu za mataifa ni fedha na dhahabu, kazi ya mikono ya wanadamu.
5 They have mouths, but they don’t speak. They have eyes, but they don’t see.
Sanamu hizo zina vinywa, lakini haziongei; zina macho, lakini hazioni;
6 They have ears, but they don’t hear. They have noses, but they don’t smell.
zina masikio, lakini hazisikii; zina pua lakini hazinusi.
7 They have hands, but they don’t feel. They have feet, but they don’t walk, neither do they speak through their throat.
Sanamu hizo zina mikono, lakini hazishiki; zina miguu, lakini haziwezi kutembea; wala haziongei kutoka viywani mwao.
8 Those who make them will be like them; yes, everyone who trusts in them.
Wale wanao zitengeneza wanafanana nazo, vile vile yeyote anaye amini katika hizo.
9 Israel, trust in Yahweh! He is their help and their shield.
Israeli, amini katika Yahwe; yeye ni msaada wako na ngao yako.
10 House of Aaron, trust in Yahweh! He is their help and their shield.
Nyumba ya Haruni, amini katika Yahwe; yeye ni msaada wako na ngao yako.
11 You who fear Yahweh, trust in Yahweh! He is their help and their shield.
Ninyi mnao mheshumu Yahwe, mwamini yeye; yeye ni msaada wenu na ngao yenu.
12 Yahweh remembers us. He will bless us. He will bless the house of Israel. He will bless the house of Aaron.
Yahwe hutukumbuka sisi na atatubariki; ataibariki familia ya Israeli; atabariki familia ya Haruni.
13 He will bless those who fear Yahweh, both small and great.
Atawabariki wale wanao muheshimu yeye, wote vijana na wazee.
14 May Yahweh increase you more and more, you and your children.
Yahwe na awaongeze ninyi zaidi na zaidi, ninyi pamoja na watoto wenu.
15 Blessed are you by Yahweh, who made heaven and earth.
Yahwe na awabariki, aliyeziumba mbingu na nchi.
16 The heavens are Yahweh’s heavens, but he has given the earth to the children of men.
Mbingu ni za Yahwe; lakini nchi amewapa wanadamu.
17 The dead don’t praise Yah, nor any who go down into silence,
Wafu hawamsifu Yahwe, wala wote washukao chini kwenye ukimya;
18 but we will bless Yah, from this time forward and forever more. Praise Yah!
bali tutamtukuza Yahwe sasa na hata milele. Msifuni Yahwe.