< Mark 15 >
1 Immediately in the morning the chief priests, with the elders, scribes, and the whole council, held a consultation, bound Jesus, carried him away, and delivered him up to Pilate.
Asubuhi na mapema, viongozi wa makuhani, pamoja na wazee, walimu wa sheria na Baraza lote, wakafikia uamuzi. Wakamfunga Yesu, wakamchukua na kumkabidhi kwa Pilato.
2 Pilate asked him, “Are you the King of the Jews?” He answered, “So you say.”
Pilato akamuuliza, “Je, wewe ndiye Mfalme wa Wayahudi?” Yesu akajibu, “Wewe umesema.”
3 The chief priests accused him of many things.
Viongozi wa makuhani wakamshtaki kwa mambo mengi.
4 Pilate again asked him, “Have you no answer? See how many things they testify against you!”
Pilato akamuuliza tena, “Je, huna la kujibu? Tazama ni mashtaka mangapi wanayaleta juu yako.”
5 But Jesus made no further answer, so that Pilate marveled.
Lakini Yesu hakujibu lolote, hivyo Pilato akashangaa.
6 Now at the feast he used to release to them one prisoner, whomever they asked of him.
Ilikuwa desturi wakati wa Sikukuu ya Pasaka kumfungulia mfungwa yeyote ambaye watu wangemtaka.
7 There was one called Barabbas, bound with his fellow insurgents, men who in the insurrection had committed murder.
Wakati huo, mtu aliyeitwa Baraba alikuwa amefungwa gerezani pamoja na waasi wengine waliokuwa wametekeleza uuaji wakati wa maasi.
8 The multitude, crying aloud, began to ask him to do as he always did for them.
Ule umati wa watu ukamjia Pilato na kumwomba awafanyie kama ilivyokuwa desturi yake.
9 Pilate answered them, saying, “Do you want me to release to you the King of the Jews?”
Pilato akawauliza, “Mnataka niwafungulie huyu Mfalme wa Wayahudi?”
10 For he perceived that for envy the chief priests had delivered him up.
Kwa maana yeye alitambua kuwa viongozi wa makuhani walikuwa wamemtia Yesu mikononi mwake kwa ajili ya wivu.
11 But the chief priests stirred up the multitude, that he should release Barabbas to them instead.
Lakini viongozi wa makuhani wakauchochea ule umati wa watu wamwombe awafungulie Baraba badala yake.
12 Pilate again asked them, “What then should I do to him whom you call the King of the Jews?”
Pilato akawauliza tena, “Basi mnataka nifanye nini na huyu mtu mnayemwita Mfalme wa Wayahudi?”
13 They cried out again, “Crucify him!”
Wakapiga kelele wakisema, “Msulubishe!”
14 Pilate said to them, “Why, what evil has he done?” But they cried out exceedingly, “Crucify him!”
Pilato akawauliza, “Kwa nini? Amefanya kosa gani?” Lakini wao wakapiga kelele kwa nguvu zaidi, wakisema, “Msulubishe!”
15 Pilate, wishing to please the multitude, released Barabbas to them, and handed over Jesus, when he had flogged him, to be crucified.
Pilato, akitaka kuuridhisha ule umati wa watu, akawafungulia Baraba. Naye baada ya kuamuru Yesu achapwe mijeledi, akamtoa ili asulubishwe.
16 The soldiers led him away within the court, which is the Praetorium; and they called together the whole cohort.
Askari wakampeleka Yesu hadi kwenye ukumbi wa ndani wa jumba la kifalme, ndio Praitorio, wakakusanya kikosi kizima cha askari.
17 They clothed him with purple; and weaving a crown of thorns, they put it on him.
Wakamvalisha Yesu joho la zambarau, wakasokota taji ya miiba, wakamvika kichwani.
18 They began to salute him, “Hail, King of the Jews!”
Wakaanza kumsalimu kwa dhihaka, “Salamu, mfalme wa Wayahudi!”
19 They struck his head with a reed and spat on him, and bowing their knees, did homage to him.
Wakampiga kwa fimbo ya mwanzi tena na tena kichwani na kumtemea mate. Wakapiga magoti mbele yake, wakamsujudia kwa kumdhihaki.
20 When they had mocked him, they took the purple cloak off him, and put his own garments on him. They led him out to crucify him.
Walipokwisha kumdhihaki, wakamvua lile joho la zambarau, wakamvika tena nguo zake. Kisha wakamtoa nje ili wakamsulubishe.
21 They compelled one passing by, coming from the country, Simon of Cyrene, the father of Alexander and Rufus, to go with them that he might bear his cross.
Mtu mmoja kutoka Kirene, jina lake Simoni, baba yao Aleksanda na Rufo, alikuwa anapita zake kuingia mjini kutoka shamba, nao wakamlazimisha kuubeba ule msalaba.
22 They brought him to the place called Golgotha, which is, being interpreted, “The place of a skull.”
Kisha wakampeleka Yesu mpaka mahali palipoitwa Golgotha (maana yake ni Mahali pa Fuvu la Kichwa).
23 They offered him wine mixed with myrrh to drink, but he didn’t take it.
Nao wakampa divai iliyochanganywa na manemane, lakini hakuinywa.
24 Crucifying him, they parted his garments among them, casting lots on them, what each should take.
Basi wakamsulubisha, nazo nguo zake wakagawana miongoni mwao kwa kuzipigia kura ili kuamua ni gani kila mtu ataichukua.
25 It was the third hour when they crucified him.
Ilikuwa yapata saa tatu asubuhi walipomsulubisha.
26 The superscription of his accusation was written over him: “THE KING OF THE JEWS.”
Tangazo likaandikwa la mashtaka dhidi yake lenye maneno haya: “Mfalme wa Wayahudi.”
27 With him they crucified two robbers, one on his right hand, and one on his left.
Pamoja naye walisulubiwa wanyangʼanyi wawili, mmoja upande wake wa kuume na mwingine upande wa kushoto. [
28 The Scripture was fulfilled which says, “He was counted with transgressors.”
Nayo maandiko yakatimizwa, yale yasemayo, “Alihesabiwa pamoja na watenda dhambi.]”
29 Those who passed by blasphemed him, wagging their heads and saying, “Ha! You who destroy the temple and build it in three days,
Watu waliokuwa wakipita njiani wakamtukana huku wakitikisa vichwa vyao na kusema, “Aha! Wewe ambaye utalivunja Hekalu na kulijenga kwa siku tatu,
30 save yourself, and come down from the cross!”
basi shuka kutoka msalabani na ujiokoe mwenyewe!”
31 Likewise, also the chief priests mocking among themselves with the scribes said, “He saved others. He can’t save himself.
Vivyo hivyo, viongozi wa makuhani pamoja na walimu wa sheria wakamdhihaki miongoni mwao wakisema, “Aliwaokoa wengine, lakini hawezi kujiokoa mwenyewe!
32 Let the Christ, the King of Israel, now come down from the cross, that we may see and believe him.” Those who were crucified with him also insulted him.
Basi huyu Kristo, huyu Mfalme wa Israeli, ashuke sasa kutoka msalabani, ili tupate kuona na kuamini.” Wale waliosulubiwa pamoja naye pia wakamtukana.
33 When the sixth hour had come, there was darkness over the whole land until the ninth hour.
Ilipofika saa sita, giza liliifunika nchi yote hadi saa tisa.
34 At the ninth hour Jesus cried with a loud voice, saying, “Eloi, Eloi, lama sabachthani?” which is, being interpreted, “My God, my God, why have you forsaken me?”
Mnamo saa tisa, Yesu akapaza sauti, akalia, “Eloi, Eloi, lama sabakthani?” (maana yake, “Mungu wangu, Mungu wangu, mbona umeniacha?”)
35 Some of those who stood by, when they heard it, said, “Behold, he is calling Elijah.”
Baadhi ya watu waliokuwa wamesimama karibu waliposikia hayo, wakasema, “Msikieni, anamwita Eliya.”
36 One ran, and filling a sponge full of vinegar, put it on a reed and gave it to him to drink, saying, “Let him be. Let’s see whether Elijah comes to take him down.”
Mtu mmoja akaenda mbio, akachovya sifongo kwenye siki, akaiweka kwenye mwanzi na akampa Yesu ili anywe, akisema, “Basi mwacheni. Hebu tuone kama Eliya atakuja kumshusha kutoka hapo msalabani.”
37 Jesus cried out with a loud voice, and gave up the spirit.
Kisha Yesu akatoa sauti kuu, akakata roho.
38 The veil of the temple was torn in two from the top to the bottom.
Pazia la Hekalu likachanika vipande viwili kuanzia juu hadi chini.
39 When the centurion, who stood by opposite him, saw that he cried out like this and breathed his last, he said, “Truly this man was the Son of God!”
Basi yule jemadari aliyekuwa amesimama hapo mbele ya msalaba wa Yesu aliposikia ile sauti yake na kuona jinsi alivyokata roho, akasema, “Hakika mtu huyu alikuwa Mwana wa Mungu!”
40 There were also women watching from afar, among whom were both Mary Magdalene and Mary the mother of James the less and of Joses, and Salome;
Walikuwepo pia wanawake waliokuwa wakiangalia kwa mbali. Miongoni mwao walikuwepo Maria Magdalene, na Maria mama yao Yakobo mdogo na Yose, pia na Salome.
41 who, when he was in Galilee, followed him and served him; and many other women who came up with him to Jerusalem.
Hawa walifuatana na Yesu na kushughulikia mahitaji yake alipokuwa Galilaya. Pia walikuwepo wanawake wengine wengi waliokuwa wamekuja pamoja naye Yerusalemu.
42 When evening had now come, because it was the Preparation Day, that is, the day before the Sabbath,
Ilipofika jioni, kwa kuwa ilikuwa Siku ya Maandalizi, yaani siku moja kabla ya Sabato,
43 Joseph of Arimathaea, a prominent council member who also himself was looking for God’s Kingdom, came. He boldly went in to Pilate, and asked for Jesus’ body.
Yosefu wa Arimathaya, mtu aliyeheshimiwa katika Baraza, na ambaye alikuwa anautarajia Ufalme wa Mungu, akamwendea Pilato kwa ujasiri na kumwomba mwili wa Yesu.
44 Pilate was surprised to hear that he was already dead; and summoning the centurion, he asked him whether he had been dead long.
Pilato alikuwa akijiuliza kama Yesu alikuwa amekwisha kufa. Hivyo akamwita yule jemadari, akamuuliza iwapo Yesu alikuwa amekwisha kufa.
45 When he found out from the centurion, he granted the body to Joseph.
Baada ya kupata habari kutoka kwa yule jemadari kwamba kweli amekwisha kufa, Pilato akampa Yosefu ruhusa ya kuuchukua huo mwili.
46 He bought a linen cloth, and taking him down, wound him in the linen cloth and laid him in a tomb which had been cut out of a rock. He rolled a stone against the door of the tomb.
Hivyo Yosefu akanunua kitambaa cha kitani safi, akaushusha mwili kutoka msalabani, akaufunga katika kile kitambaa cha kitani, na kuuweka ndani ya kaburi lililochongwa kwenye mwamba. Kisha akavingirisha jiwe kwenye ingilio la kaburi.
47 Mary Magdalene and Mary the mother of Joses, saw where he was laid.
Maria Magdalene na Maria mamaye Yose walipaona mahali pale alipolazwa.