< Luke 24 >

1 But on the first day of the week, at early dawn, they and some others came to the tomb, bringing the spices which they had prepared.
Mnamo siku ya kwanza ya juma, alfajiri na mapema, wale wanawake walichukua yale manukato waliyokuwa wameyaandaa, wakaenda kaburini.
2 They found the stone rolled away from the tomb.
Wakakuta lile jiwe limevingirishwa kutoka kwenye kaburi,
3 They entered in, and didn’t find the Lord Jesus’ body.
lakini walipoingia ndani, hawakuuona mwili wa Bwana Yesu.
4 While they were greatly perplexed about this, behold, two men stood by them in dazzling clothing.
Walipokuwa wanashangaa juu ya jambo hili, ghafula watu wawili waliokuwa wamevaa mavazi yanayongʼaa kama umeme wakasimama karibu nao.
5 Becoming terrified, they bowed their faces down to the earth. The men said to them, “Why do you seek the living among the dead?
Wale wanawake, wakiwa na hofu, wakainamisha nyuso zao mpaka chini. Lakini wale watu wakawaambia, “Kwa nini mnamtafuta aliye hai miongoni mwa wafu?
6 He isn’t here, but is risen. Remember what he told you when he was still in Galilee,
Hayuko hapa; amefufuka! Kumbukeni alivyowaambia alipokuwa bado yuko pamoja nanyi huko Galilaya kwamba:
7 saying that the Son of Man must be delivered up into the hands of sinful men and be crucified, and the third day rise again?”
‘Ilikuwa lazima Mwana wa Adamu atiwe mikononi mwa watu wenye dhambi na waovu ili asulubiwe, na siku ya tatu afufuke.’”
8 They remembered his words,
Ndipo wakayakumbuka maneno ya Yesu.
9 returned from the tomb, and told all these things to the eleven and to all the rest.
Waliporudi kutoka huko kaburini, wakawaeleza wale wanafunzi kumi na mmoja pamoja na wengine wote mambo haya yote.
10 Now they were Mary Magdalene, Joanna, and Mary the mother of James. The other women with them told these things to the apostles.
Basi Maria Magdalene, Yoana, na Maria mama yake Yakobo, pamoja na wanawake wengine waliofuatana nao ndio waliwaelezea mitume habari hizi.
11 These words seemed to them to be nonsense, and they didn’t believe them.
Lakini hawakuwasadiki hao wanawake, kwa sababu maneno yao yalionekana kama upuzi.
12 But Peter got up and ran to the tomb. Stooping and looking in, he saw the strips of linen lying by themselves, and he departed to his home, wondering what had happened.
Hata hivyo, Petro akainuka na kukimbia kwenda kule kaburini. Alipoinama kuchungulia, akaona vile vitambaa vya kitani, ila hakuona kitu kingine. Naye akaenda zake akijiuliza nini kilichotokea.
13 Behold, two of them were going that very day to a village named Emmaus, which was sixty stadia from Jerusalem.
Ikawa siku iyo hiyo, wanafunzi wawili wa Yesu walikuwa njiani wakienda kijiji kilichoitwa Emau, yapata maili saba kutoka Yerusalemu.
14 They talked with each other about all of these things which had happened.
Walikuwa wakizungumza wao kwa wao kuhusu mambo yote yaliyotukia.
15 While they talked and questioned together, Jesus himself came near, and went with them.
Walipokuwa wakizungumza na kujadiliana, Yesu mwenyewe akaja akatembea pamoja nao,
16 But their eyes were kept from recognizing him.
lakini macho yao yakazuiliwa ili wasimtambue.
17 He said to them, “What are you talking about as you walk, and are sad?”
Akawauliza, “Ni mambo gani haya mnayozungumza wakati mnatembea?” Wakasimama, nyuso zao zikionyesha huzuni.
18 One of them, named Cleopas, answered him, “Are you the only stranger in Jerusalem who doesn’t know the things which have happened there in these days?”
Mmoja wao, aliyeitwa Kleopa, akamuuliza, “Je, wewe ndiye peke yako mgeni huku Yerusalemu ambaye hufahamu mambo yaliyotukia humo siku hizi?”
19 He said to them, “What things?” They said to him, “The things concerning Jesus the Nazarene, who was a prophet mighty in deed and word before God and all the people;
Akawauliza, “Mambo gani?” Wakamjibu, “Mambo ya Yesu wa Nazareti. Yeye alikuwa nabii, mwenye uwezo mkuu katika maneno yake na matendo yake, mbele za Mungu na mbele ya wanadamu wote.
20 and how the chief priests and our rulers delivered him up to be condemned to death, and crucified him.
Viongozi wa makuhani na viongozi wetu walimtoa ahukumiwe kufa, nao wakamsulubisha.
21 But we were hoping that it was he who would redeem Israel. Yes, and besides all this, it is now the third day since these things happened.
Lakini tulikuwa tumetegemea kwamba yeye ndiye angelikomboa Israeli. Zaidi ya hayo, leo ni siku ya tatu tangu mambo haya yatokee.
22 Also, certain women of our company amazed us, having arrived early at the tomb;
Isitoshe, baadhi ya wanawake katika kundi letu wametushtusha. Walikwenda kaburini leo alfajiri,
23 and when they didn’t find his body, they came saying that they had also seen a vision of angels, who said that he was alive.
lakini hawakuukuta mwili wake. Walirudi wakasema wameona maono ya malaika ambao waliwaambia kwamba Yesu yu hai.
24 Some of us went to the tomb and found it just like the women had said, but they didn’t see him.”
Kisha baadhi ya wenzetu walikwenda kaburini wakalikuta kama vile wale wanawake walivyokuwa wamesema, lakini yeye hawakumwona.”
25 He said to them, “Foolish people, and slow of heart to believe in all that the prophets have spoken!
Yesu akawaambia, “Ninyi ni wajinga kiasi gani, nanyi ni wazito mioyoni mwenu kuamini mambo yote yaliyonenwa na manabii!
26 Didn’t the Christ have to suffer these things and to enter into his glory?”
Je, haikumpasa Kristokuteswa kwa njia hiyo na kisha aingie katika utukufu wake?”
27 Beginning from Moses and from all the prophets, he explained to them in all the Scriptures the things concerning himself.
Naye akianzia na Sheria ya Mose na Manabii wote, akawafafanulia jinsi Maandiko yalivyosema kumhusu yeye.
28 They came near to the village where they were going, and he acted like he would go further.
Nao walipokaribia kile kijiji walichokuwa wakienda, Yesu akawa kama anaendelea mbele.
29 They urged him, saying, “Stay with us, for it is almost evening, and the day is almost over.” He went in to stay with them.
Lakini wao wakamsihi sana akae nao, wakisema, “Kaa hapa nasi, kwa maana sasa ni jioni na usiku unaingia.” Basi akaingia ndani kukaa nao.
30 When he had sat down at the table with them, he took the bread and gave thanks. Breaking it, he gave it to them.
Alipokuwa mezani pamoja nao, akachukua mkate, akashukuru, akaumega, akaanza kuwagawia.
31 Their eyes were opened and they recognized him; then he vanished out of their sight.
Ndipo macho yao yakafumbuliwa, nao wakamtambua, naye akatoweka machoni pao. Hawakumwona tena.
32 They said to one another, “Weren’t our hearts burning within us while he spoke to us along the way, and while he opened the Scriptures to us?”
Wakaulizana wao kwa wao, “Je, mioyo yetu haikuwakawaka kwa furaha ndani yetu alipokuwa anazungumza nasi njiani na kutufafanulia Maandiko?”
33 They rose up that very hour, returned to Jerusalem, and found the eleven gathered together, and those who were with them,
Wakaondoka mara, wakarudi Yerusalemu. Wakawakuta wale wanafunzi kumi na mmoja na wale waliokuwa pamoja nao, wamekusanyika
34 saying, “The Lord is risen indeed, and has appeared to Simon!”
wakisema, “Ni kweli! Bwana amefufuka, naye amemtokea Simoni.”
35 They related the things that happened along the way, and how he was recognized by them in the breaking of the bread.
Kisha wale wanafunzi wawili wakaeleza yaliyotukia njiani na jinsi walivyomtambua Yesu alipoumega mkate.
36 As they said these things, Jesus himself stood among them, and said to them, “Peace be to you.”
Walipokuwa bado wanazungumza hayo, Yesu mwenyewe akasimama katikati yao, akasema, “Amani iwe nanyi!”
37 But they were terrified and filled with fear, and supposed that they had seen a spirit.
Wakashtuka na kuogopa wakidhani kwamba wameona mzuka.
38 He said to them, “Why are you troubled? Why do doubts arise in your hearts?
Lakini Yesu akawauliza, “Kwa nini mnaogopa? Kwa nini mna shaka mioyoni mwenu?
39 See my hands and my feet, that it is truly me. Touch me and see, for a spirit doesn’t have flesh and bones, as you see that I have.”
Tazameni mikono yangu na miguu yangu, mwone kuwa ni mimi hasa. Niguseni mwone; kwa maana mzuka hauna nyama na mifupa, kama mnionavyo kuwa navyo.”
40 When he had said this, he showed them his hands and his feet.
Aliposema haya, akawaonyesha mikono na miguu yake.
41 While they still didn’t believe for joy, and wondered, he said to them, “Do you have anything here to eat?”
Wakashindwa kuamini kwa ajili ya furaha na mshangao waliokuwa nao. Akawauliza, “Mna chakula chochote hapa?”
42 They gave him a piece of a broiled fish and some honeycomb.
Wakampa kipande cha samaki aliyeokwa,
43 He took them, and ate in front of them.
naye akakichukua na kukila mbele yao.
44 He said to them, “This is what I told you while I was still with you, that all things which are written in the law of Moses, the prophets, and the psalms concerning me must be fulfilled.”
Akawaambia, “Haya ndiyo yale niliyowaambia nilipokuwa bado niko pamoja nanyi, kwamba yote yaliyoandikwa kunihusu mimi katika Sheria ya Mose, Manabii na Zaburi hayana budi kutimizwa.”
45 Then he opened their minds, that they might understand the Scriptures.
Ndipo akafungua fahamu zao ili waweze kuyaelewa Maandiko.
46 He said to them, “Thus it is written, and thus it was necessary for the Christ to suffer and to rise from the dead the third day,
Akawaambia, “Haya ndiyo yaliyoandikwa: Kristo atateswa na siku ya tatu atafufuka kutoka kwa wafu.
47 and that repentance and remission of sins should be preached in his name to all the nations, beginning at Jerusalem.
Toba na msamaha wa dhambi zitatangaziwa mataifa yote kupitia jina lake kuanzia Yerusalemu.
48 You are witnesses of these things.
Ninyi ni mashahidi wa mambo haya.
49 Behold, I send out the promise of my Father on you. But wait in the city of Jerusalem until you are clothed with power from on high.”
“Tazama nitawatumia ahadi ya Baba yangu; lakini kaeni humu mjini hadi mtakapovikwa uwezo utokao juu.”
50 He led them out as far as Bethany, and he lifted up his hands and blessed them.
Akiisha kuwaongoza mpaka kwenye viunga vya Bethania, akainua mikono yake juu na kuwabariki.
51 While he blessed them, he withdrew from them and was carried up into heaven.
Alipokuwa anawabariki, akawaacha, akachukuliwa mbinguni.
52 They worshiped him and returned to Jerusalem with great joy,
Kisha wakamwabudu na kurudi Yerusalemu wakiwa wamejawa na furaha kuu.
53 and were continually in the temple, praising and blessing God. Amen.
Nao wakadumu ndani ya Hekalu wakimtukuza Mungu. Amen.

< Luke 24 >