< Leviticus 18 >

1 Yahweh said to Moses,
Yahweh akazungumza na Musa, akisema,
2 “Speak to the children of Israel, and say to them, ‘I am Yahweh your God.
“Zungumza na watu wa Israeli na uwaambie, “Mimi ndimi Yahweh Mungu wenu.
3 You shall not do as they do in the land of Egypt, where you lived. You shall not do as they do in the land of Canaan, where I am bringing you. You shall not follow their statutes.
Msitende mambo ambayo watu wa Misri huyatenda, mahali mlikokuwa mkiishi awali. Na ni lazima msitende mambo yale wanayoyatenda watu wa Kanaani, nchi ambayo ninawapeleka nyinyi. Msifuate desturi zao.
4 You shall do my ordinances. You shall keep my statutes and walk in them. I am Yahweh your God.
Sheria zangu ndizo mtakazozitenda, na amri zangu ndizo mtakazozishika, kwa sababu Mimi ndimi Yahweh Mungu wenu.
5 You shall therefore keep my statutes and my ordinances, which if a man does, he shall live in them. I am Yahweh.
Kwa hiyo ni lazima mzitunze hukumu zangu na sheria zangu. Ikiwa mtu amezitii, ataishi kwa sababu ya hizo. Mimi Ndimi Yahweh.
6 “‘None of you shall approach any close relatives, to uncover their nakedness: I am Yahweh.
Pasiwepo kwenu atakayelala na yeyote aliye na uhusiano wa karibu naye. Mimi ndimi Yahweh.
7 “‘You shall not uncover the nakedness of your father, nor the nakedness of your mother: she is your mother. You shall not uncover her nakedness.
Usimfedheheshe baba yako kwa kulala na mama yako. Yeye ni mama yako! Haikupasi kumfedhehesha yeye.
8 “‘You shall not uncover the nakedness of your father’s wife. It is your father’s nakedness.
Usilale na yeyote wa wake za baba yako; Usimfedheheshe namna hiyo baba yako.
9 “‘You shall not uncover the nakedness of your sister, the daughter of your father, or the daughter of your mother, whether born at home or born abroad.
Usilale na yeyote aliye mmoja miongoni mwa dada zako, ama ni binti ya baba yako au ni binti ya mama yako, ama aliyelelewa nyumbani mwenu au mbali nawe. Usilale na dada zako.
10 “‘You shall not uncover the nakedness of your son’s daughter, or of your daughter’s daughter, even their nakedness; for theirs is your own nakedness.
Usilale na binti ya mwanao, au binti ya binti yako. Hiyo ingekuwa aibu yako mwenyewe.
11 “‘You shall not uncover the nakedness of your father’s wife’s daughter, conceived by your father, since she is your sister.
Usilale na binti ya mke wa baba yako, aliyezaliwa kwa baba yako, yeye ni dada yako, na usilale naye.
12 “‘You shall not uncover the nakedness of your father’s sister. She is your father’s near kinswoman.
Usilale na dada ya baba yako. Yeye ni ndugu wa karibu kwa baba yako.
13 “‘You shall not uncover the nakedness of your mother’s sister, for she is your mother’s near kinswoman.
Usilale na dada ya mama yako. Yeye ni ndugu wa mama yako.
14 “‘You shall not uncover the nakedness of your father’s brother. You shall not approach his wife. She is your aunt.
Usimfedheheshe ndug wa baba yako kwa kulala na mke wake. Usimkaribie kwa kusudi hilo; yeye ni shangazi yako.
15 “‘You shall not uncover the nakedness of your daughter-in-law. She is your son’s wife. You shall not uncover her nakedness.
Usilale na binti- mkwe wako, Yeye ni mke wa mwanao; usilale naye.
16 “‘You shall not uncover the nakedness of your brother’s wife. It is your brother’s nakedness.
Usilale na mke wa kaka yako; usije ukamfedhesha yeye katika njia hii.
17 “‘You shall not uncover the nakedness of a woman and her daughter. You shall not take her son’s daughter, or her daughter’s daughter, to uncover her nakedness. They are near kinswomen. It is wickedness.
Usilale na mwanamke kisha na binti yake, au binti wa mwanawe au binti wa binti yake. Hao ni ndugu zake wa karibu, na kulala nao lingekuwa ni uovu.
18 “‘You shall not take a wife in addition to her sister, to be a rival, to uncover her nakedness, while her sister is still alive.
Usimwoe dada ya mke wako kuwa mke wako wa pili na kulala naye wakati bado mke wako wa kwanza angali hai.
19 “‘You shall not approach a woman to uncover her nakedness, as long as she is impure by her uncleanness.
Usilale na mwanamke wakati wake wa hedhi.
20 “‘You shall not lie carnally with your neighbor’s wife, and defile yourself with her.
Yeye ni najisi kwa wakati huo. Usilale na mke wa jilani yako na kujichafua mwenyewe kwake katika njia hii.
21 “‘You shall not give any of your children as a sacrifice to Molech. You shall not profane the name of your God. I am Yahweh.
Msiwatoe watoto wenu ili kuwapitisha kwenye moto, ili kwamba muwatoe sadaka kwa Moleki, kwa sababu msije mkalinajisi jina la Mungu wenu. Mimi ndimi Yahweh.
22 “‘You shall not lie with a man as with a woman. That is detestable.
Usilale na mwanaume mwingine kama ulalavyo na mwanamke. Jambo hili lingekuwa uovu.
23 “‘You shall not lie with any animal to defile yourself with it. No woman may give herself to an animal, to lie down with it: it is a perversion.
Usilale na myama yeyote na kujitia unajisi kwake. Haimpasi mwanamke kufikiria kulala na mnyama ye yote. Huo ungekuwa upotovu.
24 “‘Don’t defile yourselves in any of these things; for in all these the nations which I am casting out before you were defiled.
Msijichafue wenyewe katika njia hizi, kwa kuwa katika njia hizi mataifa yamechafuliwa, mataifa ambayo Nitayafukuza yatoke kwa ajili yenu.
25 The land was defiled. Therefore I punished its iniquity, and the land vomited out her inhabitants.
Ni kwa sababu nchi imenajisiwa, hivyo niliiadhibu dhambi yao, nayo nchi ikawatapika wakazi wake
26 You therefore shall keep my statutes and my ordinances, and shall not do any of these abominations; neither the native-born, nor the stranger who lives as a foreigner among you
Kwa hiyo, yawapasa kuzishika amri zangu na maagiza yangu, na msifanye aina yoyote ya mambo haya ya machukizo, wala Mwisraeli mzaliwa au Mgeni aishie miongoni mwenu.
27 (for the men of the land that were before you had done all these abominations, and the land became defiled),
Kwa kuwa ni uovu huu ambao watu wametenda, wale ambao waliishi hapa kabla yenu, na sasa nchi imenajisiwa.
28 that the land not vomit you out also, when you defile it, as it vomited out the nation that was before you.
Kwa hiyo, muwe waangalifu ili kwamba nchi isiwatapike nyinyi baada ya kuwa mmeinajisi, kama ilivyowatapika wale watu waliokuwako kabla yenu.
29 “‘For whoever shall do any of these abominations, even the souls that do them shall be cut off from among their people.
Yeyote anayefanya mambo haya ya kuchukiza, watu wafanyao mambo hayo ya kuchukiza lazima watakatiliwa mbali kutoka miongoni mwa watu wao.
30 Therefore you shall keep my requirements, that you do not practice any of these abominable customs which were practiced before you, and that you do not defile yourselves with them. I am Yahweh your God.’”
Kw a hiyo inawapasa kuzishika amri zangu na sitende mojawapo ya desturi hizi zenyekuchukiza ambazo zilitendwa hapo kabla yenu, ili msijinajisi wenyewe kwa hizo. Mimi ndimi Yahweh Mungu wenu.

< Leviticus 18 >