< Psalms 113 >

1 Praise the LORD! Praise, you servants of the LORD, praise the LORD’s name.
Msifuni Bwana. Enyi watumishi wa Bwana msifuni, lisifuni jina la Bwana.
2 Blessed be the LORD’s name, from this time forward and forever more.
Jina la Bwana na lisifiwe, sasa na hata milele.
3 From the rising of the sun to its going down, the LORD’s name is to be praised.
Kuanzia mawio ya jua hadi machweo yake, jina la Bwana linapaswa kusifiwa.
4 The LORD is high above all nations, his glory above the heavens.
Bwana ametukuka juu ya mataifa yote, utukufu wake juu ya mbingu.
5 Who is like the LORD, our God, who has his seat on high,
Ni nani aliye kama Bwana Mungu wetu, Yeye ambaye ameketi juu kwenye kiti cha enzi,
6 who stoops down to see in heaven and in the earth?
ambaye huinama atazame chini aone mbingu na nchi?
7 He raises up the poor out of the dust, and lifts up the needy from the ash heap,
Huwainua maskini kutoka mavumbini, na kuwanyanyua wahitaji kutoka kwenye jalala,
8 that he may set him with princes, even with the princes of his people.
huwaketisha pamoja na wakuu, pamoja na wakuu wa watu wake.
9 He settles the barren woman in her home as a joyful mother of children. Praise the LORD!
Humjalia mwanamke tasa kutulia nyumbani mwake, akiwa mama watoto mwenye furaha. Msifuni Bwana.

< Psalms 113 >