< Luke 1 >

1 Seeing that many have attempted to draw up a narrative of the facts which are received with full assurance among us
Wengi wamejitahidi kuweka katika mpangilio simulizi kuhusu masuala ambayo yametimizwa kati yetu,
2 on the authority of those who were from the beginning eye-witnesses and were devoted to the service of the divine Message,
kama walivyotupatia sisi, ambao tangu mwanzo ni mashahidi wa macho na watumishi wa ujumbe.
3 it has seemed right to me also, after careful investigation of the facts from their commencement, to write for you, most noble Theophilus, a connected account,
Hivyo nami pia, baada ya kuchuguza kwa uangalifu chanzo cha mambo haya yote tokea mwanzo - nimeona ni vema kwangu pia kukuandikia katika mpangilio wake - mheshimiwa sana Theofilo.
4 that you may fully know the truth of the things which you have been taught by word of mouth.
Ili kwamba uweze kujua ukweli wa mambo uliyofundishwa.
5 There was in the time of Herod, the king of Judaea, a priest of the name of Zechariah, belonging to the class of Abijah. He had a wife who was a descendant of Aaron, and her name was Elizabeth.
Katika siku za Herode, mfalme wa Yudea, palikuwa na kuhani fulani aliyeitwa Zekaria, wa ukoo wa Abiya. Mke wake alitoka kwa binti za Haruni, na jina lake aliitwa Elizabeti.
6 They were both of them upright before God, blamelessly obeying all the Lord's precepts and ordinances.
Wote walikuwa wenye haki mbele za Mungu; walitembea bila lawama katika amri zote na maagizo ya Bwana.
7 But they had no child, because Elizabeth was barren; and both of them were far advanced in life.
Lakini hawakuwa na mtoto, kwasababu Elizabethi alikuwa tasa, na kwa wakati huu wote wawili walikuwa wazee sana.
8 Now while he was doing priestly duty before God in the prescribed course of his class,
Sasa ilitokea kwamba Zakaria alikuwa katika uwepo wa Mungu, akiendelea na wajibu wa kikuhani katika utaratibu wa zamu yake.
9 it fell to his lot--according to the custom of the priesthood--to go into the Sanctuary of the Lord and burn the incense;
Kulingana na desturi ya kuchagua ni kuhani yupi atakayehudumu, alikuwa amechaguliwa kwa kura kuingia katika hekalu la Bwana na hivyo angefukiza uvumba.
10 and the whole multitude of the people were outside praying, at the hour of incense.
Kundi lote la watu lilikuwa likiomba nje wakati wa kufukizwa kwa ufumba.
11 Then there appeared to him an angel of the Lord standing on the right side of the altar of incense;
Sasa malaika wa Bwana alimtokea na kasimama upande wa kulia wa madhabahu ya kufukizia.
12 and Zechariah on seeing him was agitated and terrified.
Zakaria alitishika alipomuona; hofu ikamwangukia.
13 But the angel said to him, "Do not be afraid, Zechariah, for your petition has been heard: and your wife Elizabeth will bear you a son, and you are to call his name John.
Lakini malaika akamwambia, “Usiogope Zakaria, kwasababu maombi yako yamesikika. Mke wako Elizabeth atakuzalia mwana. Jina lake utamwita Yohana.
14 Gladness and exultant joy shall be yours, and many will rejoice over his birth.
Utakuwa na furaha na uchangamfu, na wengi watakufurahia kuzaliwa kwake.
15 For he will be great in the sight of the Lord; no wine or fermented drink shall he ever drink; but he will be filled with the Holy Spirit from the very hour of his birth.
Kwa kuwa atakuwa mkuu mbele ya macho ya Bwana. Hatakunywa divai au kinywaji kikali, na atakuwa amejazwa na Roho Mtakatifu tangu tumboni mwa mama yake.
16 Many of the descendants of Israel will he turn to the Lord their God;
Na watu wengi wa Israel watageuzwa kwa Bwana Mungu wao.
17 and he will be His forerunner in the spirit and power of Elijah, to turn fathers' hearts to the children, and cause the rebellious to walk in the wisdom of the upright, to make a people perfectly ready for the lord."
Atakwenda mbele za uso wa Bwana katika roho na nguvu ya Eliya. Atafanya hivi ili kurejesha mioyo ya baba kwa watoto, ili kwamba wasiotii wataenenda katika hekima ya wenye haki. Atafanya hivi kuweka tayari kwa Bwana watu ambao wameandaliwa kwa ajili yake.”
18 "By what proof," asked Zechariah, "shall I know this? For I am an old man, and my wife is far advanced in years."
Zakaria akamwambia malaika, “Nitawezaje kujua hili? Kwasababu mimi ni mzee na mke wangu miaka yake imekuwa mingi sana.”
19 "I am Gabriel, who stand in the presence of God," answered the angel, "and I have been sent to talk with you and tell you this good news.
Malaika akajibu na kumwambia, “Mimi ni Gabrieli, ambaye husimama mbele za Mungu. Nilitumwa kukwambia, kukuletea habari hii njema.
20 And now you will be dumb and unable to speak until the day when this has taken place; because you did not believe my words--words which will be fulfilled at their appointed time."
Na tazama, hutaongea, utakuwa kimya, hutaweza kuongea mpaka siku ile mambo haya yatakapotokea. Hii ni kwasababu ulishindwa kuamini maneno yangu ambayo yatatimizwa kwa wakati mwafaka.”
21 Meanwhile the people were waiting for Zechariah, and were surprised that he stayed so long in the Sanctuary.
Sasa watu walikuwa wakimsubiri Zakaria. Walishangazwa kwamba alikuwa anatumia muda mwingi hekaluni.
22 When, however, he came out, he was unable to speak to them; and they knew that he must have seen a vision in the Sanctuary; but he kept making signs to them and continued dumb.
Lakini alipotoka nje, hakuweza kuongea nao. Wakatambua kwamba alikuwa amepata maono alipokuwa hekaluni. Aliendelea kuonesha ishara na alibaki kimya.
23 When his days of service were at an end, he went to his home;
Ikatokea kwamba siku za huduma yake zilipokwisha aliondoka kurudi nyumbani kwake.
24 and in course of time his wife Elizabeth conceived, and kept herself secluded five months.
Baada ya Zakaria kurudi nyumbani kutoka kwenye huduma yake hekaluni, mke wake akawa mjamzito. Naye hakutoka nyumbani mwake kwa muda wa miezi mitano. Akasema,
25 "Thus has the Lord dealt with me," she said, "now that He has graciously taken away my reproach among men."
“Hili ndilo amabalo Bwana amefanya kwangu aliponitazama kwa upendeleo ili kuiondoa aibu yangu mbele za watu.”
26 Now in the sixth month the angel Gabriel was sent from God to a town in Galilee called Nazareth,
Sasa, katika mwezi wa sita wa mimba ya Elizabeti, Mungu alimwambia malaika Gabrieli kwenda kwenye mji wa Galilaya uitwao Nazareti,
27 to a maiden betrothed to a man of the name of Joseph, a descendant of David. The maiden's name was Mary.
kwa bikra aliyekuwa ameposwa na mwanaume ambaye jina lake lilikuwa Yusufu. Yeye alikuwa wa ukoo wa Daudi, na jina la bikra huyo lilikuwa Mariamu.
28 So Gabriel went into the house and said to her, "Joy be to you, favoured one! the Lord is with you."
Akaja kwake na akasema, “Salaam, wewe uliyepokea neema kuu! Bwana amependezwa nawe.”
29 She was greatly agitated at his words, and wondered what such a greeting meant.
Lakini maneno ya malaika yalimchanganya na hakuelewa kwa nini malaika alisema salaam hii ya ajabu kwake.
30 But the angel said, "Do not be frightened, Mary, for you have found favour with God.
Malaika akamwambia, “Usiogope, Mariamu, maana umepata neema kutoka kwa Mungu.
31 You will conceive in your womb and bear a son; and you are to call His name JESUS.
Na tazama, utabeba mimba katika tumbo lako na utazaa mwana. Nawe utamwita jina lake 'Yesu.'
32 He will be great and He will be called 'Son of the Most High.' And the Lord God will give Him the throne of His forefather David;
Atakuwa mkuu na ataitwa Mwana wa Aliye Juu Sana. Bwana Mungu atampa kiti cha enzi cha Daudi baba yake.
33 and He will be King over the House of Jacob for the Ages, and of His Kingdom there will be no end." (aiōn g165)
Atatawala juu ya ukoo wa Yakobo milele na ufalme wake hautakuwa na mwisho. (aiōn g165)
34 "How can this be," Mary replied, "seeing that I have no husband?"
Mariamu akamwambia malaika, hili litatokea kwa namna gani, maana sijawahi kulala na mwanaume yeyote?
35 The angel answered, "The Holy Spirit will come upon you, and the power of the Most High will overshadow you; and for this reason your holy offspring will be called 'the Son of God.'
Malaika akajibu na akamwambia, “Roho Mtakatifu atakujia juu yako, na nguvu ya Aliye Juu Sana itakuja juu yako. Kwa hiyo, mtakatifu atakayezaliwa ataitwa Mwana wa Mungu.
36 And see, your relative Elizabeth--she also has conceived a son in her old age; and this is the sixth month with her who was called barren.
Na tazama, ndugu yako Elizabeti anaujauzito wa mwana kwenye umri wake wa uzee. Huu ni mwezi wa sita kwake, ambaye alikuwa anaitwa mgumba.
37 For no promise from God will be impossible of fulfilment."
Maana hakuna lisilowezekana kwa Mungu.”
38 "I am the Lord's maidservant," Mary replied; "may it be with me in accordance with your words!" And then the angel left her.
Mariamu akasema, “Tazama, mimi ni mtumishi wa kike wa Bwana. Acha iwe hivyo kwangu sawa sawa na ujumbe wako.” Kisha malaika akamwacha.
39 Not long after this, Mary rose up and went in haste into the hill country to a town in Judah.
Ndipo katika siku hizo Mariamu aliondoka na kwa haraka alikwenda katika nchi ya vilima, kwenye mji katika nchi ya Yudea.
40 Here she came to the house of Zechariah and greeted Elizabeth;
Alikwenda nyumbani mwa Zekaria na akamsalimia Elizabeti.
41 and as soon as Elizabeth heard Mary's greeting, the babe leapt within her. And Elizabeth was filled with the Holy Spirit,
Sasa, ilitokea kwamba Elizabeti aliposikia salamu ya Mariamu, mtoto tumboni mwake akaruka, na Elizabeti akajazwa na Roho Mtakatifu.
42 and uttered a loud cry of joy. "Blest among women are you," she said, "and the offspring of your body is blest!
Akapaza sauti yake na kusema kwa sauti kuu, “umebarikiwa wewe zaidi miongoni mwa wanawake, na mtoto aliyemo tumboni mwako amebarikiwa.
43 But why is this honour done me, that the mother of my Lord should come to me?
Na imekuwaje kwangu kwamba, mama wa Bwana wangu ilipasa aje kwangu?
44 For, the moment your greeting reached my ears, the babe within me leapt for joy.
Kwa kuwa tazama, iliposikika masikoni mwangu sauti ya kusalimia kwako, mtoto tumboni mwangu akaruka kwa furaha.
45 And blessed is she who has believed, for the word spoken to her from the Lord shall be fulfilled."
Na amebarikiwe mwanamke yule ambaye aliamini ya kwamba ungetokea ukamilifu wa mambo yale aliyoambiwa kutoka kwa Bwana.”
46 Then Mary said: "My soul extols the Lord,
Mariamu akasema, nafsi yangu inamsifu Bwana,
47 And my spirit triumphs in God my Saviour;
na roho yangu imefurahi katika Mungu Mwokozi wangu.
48 Because He has not turned from His maidservant in her lowly position; For from this time forward all generations will account me happy,
Kwa maana ameiangalia hali ya chini ya mtumishi wake wa kike. Tazama, tangu sasa katika vizazi vyote wataniita mbarikiwa.
49 Because the mighty One has done great things for me--Holy is His name!--
Kwa maana yeye aliyemweza amefanya mambo makubwa kwangu, na jina lake ni takatifu.
50 And His compassion is, generation after generation, Upon those who fear Him.
Rehema yake inadumu toka kizazi hata kizazi kwa wale wanao mheshimu yeye.
51 He has manifested His supreme strength. He has scattered those who were haughty in the thoughts of their hearts.
Ameonesha nguvu kwa mkono wake; amewatawanya wale ambao walijivuna juu ya mawazo ya mioyo yao.
52 He has cast monarchs down from their thrones, And exalted men of low estate.
Amewashusha chini wana wa wafalme toka katika viti vyao vya enzi na kuwainua juu walio na hali ya chini.
53 The hungry He has satisfied with choice gifts, But the rich He has sent empty-handed away.
Aliwashibisha wenye njaa kwa vitu vizuri, bali matajiri amewafukuza mikono mitupu.
54 His servant Israel He has helped, Remembering His compassion--
Ametoa msaada kwa Israeli mtumishi wake, ili kukumbuka kuonesha rehema
55 In fulfillment of His promises to our forefathers--For Abraham and his posterity for ever." (aiōn g165)
(kama alivyosema kwa baba zetu) kwa Abrahamu na uzao wake milele.” (aiōn g165)
56 So Mary stayed with Elizabeth about three months, and then returned home.
Mariamu alikaa na Elizabeti yapata miezi mitatu hivi ndipo akarudi nyumbani kwake.
57 Now when Elizabeth's full time was come, she gave birth to a son;
Sasa wakati ulikuwa umewadia kwa Elizabeti kujifungua mtoto wake na akajifungua mtoto wa kiume.
58 and her neighbours and relatives heard how the Lord had had great compassion on her; and they rejoiced with her.
Jirani zake na ndugu zake walisikia jinsi Bwana alivyoikuza rehema kwake, na wakafurahi pamoja naye.
59 And on the eighth day they came to circumcise the child, and were going to call him Zechariah, after his father.
Sasa ilitokea siku ya nane kwamnba walikuja kumtahiri mtoto. Ingewapasa kumwita jina lake, “Zekaria,” kwa kuzingatia jina la baba yake,
60 His mother, however, said, "No, he is to be called John."
Lakini mama yake akajibu na kusema, “Hapana; ataitwa Yohana.”
61 "There is not one of your family," they said, "who has that name."
Wakamwambia, hakuna hata mmoja katika ndugu zako anayeitwa kwa jina hili.”
62 They asked his father by signs what he wished him to be called.
Wakamfanyia ishara baba yake kuashiria yeye alitaka jina aitwe nani.
63 So he asked for a writing-tablet, and wrote, "His name is John." And they all wondered.
Baba yake akahitaji kibao cha kuandikia, na akaandika, “Jina lake ni Yohana.” Wote wakashangazwa na hili.
64 Instantly his mouth and his tongue were set free, and he began to speak and bless God.
Ghafla mdomo wake ukafunguliwa na ulimi wake ukawa huru. Akaongea na kumsifu Mungu.
65 And all who lived round about them were filled with awe, and throughout the hill country of Judaea reports of all these things were spread abroad.
Hofu ikawajia wote walioishi karibu nao. Mambo haya yakaenea katika nchi yote ya vilima vya Yudea.
66 All who heard the story treasured it in their memories. "What then will this child be?" they said. For the lord's hand was indeed with him.
Na wote walioyasikia wakayatunza mioyoni mwao, wakisema, “Mtoto huyu kuwa wa namna gani?” Kwasababu mkono wa Bwana ulikuwa pamoja naye.
67 And Zechariah his father was filled with the Holy Spirit, and spoke in a rapture of praise.
Baba yake Zekaria alijazwa na Roho Mtakatifu na akatoa unabii, akisema,
68 "Blessed be the Lord, the God of Israel," he said, "Because He has not forgotten His people but has effected redemption for them,
“Asifiwe Bwana, Mungu wa Israeli, kwa sababu amesaidia na alishughulikia wokovu kwa watu wake.
69 And has raised up a mighty Deliverer for us In the house of David His servant--
Ametuinulia pembe ya wokovu katika nyumba ya mtumishi wake Daudi, kutoka miongoi mwa mwa ukoo wa mtumishi wake Daudi,
70 As He has spoken from all time by the lips of His holy Prophets-- (aiōn g165)
kama alivyosema kwa kinywa cha manabii wake waliokuweko katika nyakati za kale. (aiōn g165)
71 To deliver us from our foes and from the power of all who hate us.
Atatuoka kutoka kwa adui zetu na kutoka mikononi mwa wote wanaotuchukia.
72 He dealt pitifully with our forefathers, And remembered His holy covenant,
Atafanya hivi kuonesha rehema kwa baba zetu, na kukumbuka agano lake takatifu,
73 The oath which He swore to Abraham our forefather,
kiapo alichokisema kwa Abrahamu baba yetu.
74 To grant us to be rescued from the power of our foes And so render worship to Him free from fear,
Aliapa kuthibitha kwamba ingewezekana kumtumikia Yeye bila hofu, baada ya kuokolewa kutoka katika mikononi ya adui zetu.
75 In piety and uprightness before Him all our days.
katika utakatifu na haki mbele zake siku zetu zote.
76 And you moreover, O child, shall be called Prophet of the Most High; For you shall go on in front before the Lord to prepare the way for Him,
Ndiyo, na wewe mtoto, utaitwa nabii wa Aliye Juu Sana, kwa kuwa utaenenda mbele za uso wa Bwana ili kumwandalia njia, kuwaandaa watu kwa ajili ya ujio wake,
77 To give to His People a knowledge of salvation In the forgiveness of their sins,
kuwafahamisha watu wake kwamba, wataokolewa kwa njia ya kusamehewa dhambi zao.
78 Through the tender compassion of our God, Through which the daybreak from on high will come to us,
Hili litatokea kwa sababu ya huruma ya Mungu wetu, sababu ambayo jua tokea juu litatujia,
79 Dawning on those who now dwell in the darkness and shadow of death--To direct our feet into the path of peace."
kuangaza kwao wakaao gizani na katika uvuli wa mauti. Atafanya hivi kuiongoza miguu yetu kwenye njia ya amani.”
80 And the child grew and became strong in character, and lived in the Desert till the time came for him to appear publicly to Israel.
Sasa, yule mtoto akakua na kuwa mwenye nguvu rohoni na alikaa nyikani mpaka siku ya kujitokeza kwake kwa Israeli.

< Luke 1 >