< Acts 21 >
1 When, at last, we had torn ourselves away and had set sail, we ran in a straight course to Cos; the next day to Rhodes, and from there to Patara.
Wakati tulipokua tumeachana nao, na tunasafiri baharini, tukafika moja kwa moja kwenye mji wa Kosi, na kesho yake tukafika mji wa Rodo, na kutoka huko tukafika mji wa Patara.
2 Finding a ship bound for Phoenicia, we went on board and put to sea.
Tulipopata meli inayovuka kwenda Foinike, tulipanda tukasafiri.
3 After sighting Cyprus and leaving that island on our left, we continued our voyage to Syria and put in at Tyre; for there the ship was to unload her cargo.
Tulipofika mbele ya kisiwa cha Kipro, tukaiacha upande wa kushoto, tukasafiri hadi Siria, tukaweka nanga katika mji wa Tiro, kwa sababu huko ndiko meli ilikuwa ipakuliwe shehena yake.
4 Having searched for the disciples and found them, we stayed at Tyre for seven days; and, taught by the Spirit, they repeatedly urged Paul not to proceed to Jerusalem.
Baada ya kuwaona wanafunzi, tukakaa huko siku saba. Wanafunzi hawa wakamwambia Paulo kupitia kwa Roho kwamba yeye asikanyage Yerusalemu.
5 When, however, our time was up, we left and went on our way, all the disciples and their wives and children coming to see us off. Then, after kneeling down on the beach and praying,
Hata tulipotimiza siku zile, sisi tukaondoka tukaenda zetu. Wote pamoja, na wanawake zao na watoto wao, walitusindikiza katika njia zetu hadi tulipotoka nje ya mji. Kisha tukapiga magoti pwani, tukaomba, tukaagana kila mmoja.
6 we took leave of one another; and we went on board, while they returned home.
Tukapanda meli, huku nao wakarudi nyumbani kwao tena.
7 As for us, our voyage was over when having sailed from Tyre we reached Ptolemais. here we inquired after the welfare of the brethren, and remained a day with them.
Hata tulipomaliza safari yetu kutoka Tiro, tukafika Tolemai. Pale tulisalimia ndugu, na kukakaa nao kwa siku moja.
8 On the morrow we left Ptolemais and went on to Caesarea, where we came to the house of Philip the Evangelist, who was one of the seven, and stayed with him.
Kesho yake tuliondoka tukaenda Kaisaria. Sisi tukaingia nyumbani mwa Filipo, mhubiri wa injili, aliyekuwa mmoja wa wale saba, nasi tukakaa pamoja naye.
9 Now Philip had four unmarried daughters who were prophetesses;
Mtu huyu alikuwa na mabinti wanne mabikira ambao walitabiri.
10 and during our somewhat lengthy stay a Prophet of the name of Agabus came down from Judaea.
Baada ya kukaa huko kwa siku kadhaa, akashuka kutoka Uyahudi nabii mmoja aitwaye Agabo.
11 When he arrived he took Paul's loincloth, and bound his own feet and arms with it, and said, "Thus says the Holy Spirit, 'So will the Jews in Jerusalem bind the owner of this loincloth, and will hand him over to the Gentiles.'"
Yeye alikuja kwetu na akautwaa mkanda wa Paulo. kwa huo alijifunga miguu na mikono yake mwenyewe na kusema, “Roho Mtakatifu asema hivi,” “Wayahudi wa Yerusalemu watamfunga mtu anayemiliki mkanda huu, nao watamkabidhi mikononi mwa watu wa mataifa.”
12 As soon as we heard these words, both we and the brethren at Caesarea entreated Paul not to go up to Jerusalem.
Tuliposikia mambo hayo, sisi na watu waliokuwa wakiishi mahali pale tulimsihi Paulo asipande kwende Yerusalemu.
13 His reply was, "What can you mean by thus breaking my heart with your grief? Why, as for me, I am ready not only to go to Jerusalem and be put in chains, but even to die there for the sake of the Lord Jesus."
Ndipo Paulo alijibu, “Mnafanya nini, mnalia na kunivunja moyo wangu? Kwa maana niko tayari, siyo tu kufungwa, lakini pia kufia huko Yerusalemu kwa ajili ya jina la Bwana Yesu.”
14 So when he was not to be dissuaded, we ceased remonstrating with him and said, "The Lord's will be done!"
Kwa vile Paulo hakutaka kushawishiwa, tuliacha na kusema, “Basi mapenzi ya Bwana yafanyike.”
15 A few days afterwards we loaded our baggage-cattle and continued our journey to Jerusalem.
Baada ya siku hizi, tulichukua mifuko yetu na tukapanda Yerusalemu.
16 Some of the disciples from Caesarea also joined our party, and brought with them Mnason, a Cyprian, one of the early disciples, at whose house we were to lodge.
Baadhi ya wanafunzi kutoka Kaisaria pia walifuatana nasi. Wakamleta mtu mmoja aitwaye Mnasoni, mtu wa Kipro, mwanafunzi wa zamani, ambaye tulikaa naye.
17 At length we reached Jerusalem, and there the brethren gave us a hearty welcome.
Tulipofika Yerusalemu, ndugu walitukaribisha kwa furaha.
18 On the following day we went with Paul to call on James, and all the Elders of the Church came also.
Kesho yake Paulo alienda pamoja nasi kwa Yakobo, na wazee wote walikuwepo.
19 After exchanging friendly greetings, Paul told in detail all that God had done among the Gentiles through his instrumentality.
Baada ya kuwasalimu, aliwapa taarifa moja baada ya nyingine ya mambo ambayo Mungu aliyotenda miongoni mwa mataifa kwa kupitia huduma yake.
20 And they, when they had heard his statement, gave the glory to God. Then they said, "You see, brother, how many tens of thousands of Jews there are among those who have accepted the faith, and they are all zealous upholders of the Law.
Wakati waliposikia hayo, wakamsifu Mungu, na wakamwambia, “Unaona, ndugu, kuna maelfu wangapi wameamini miongoni mwa Wayahudi. Wao wote wana nia ya kushika sheria.
21 Now what they have been repeatedly told about you is that you teach all the Jews among the Gentiles to abandon Moses, and that you forbid them to circumcise their children or observe old-established customs.
Wameambiwa kuhusu wewe, kwamba unafundisha Wayahudi wanaoishi kati ya mataifa kuachana na Musa, na kwamba unawaambia wasiwatahiri watoto wao, na wasifuate desturi za zamani.
22 What then ought you to do? They are sure to hear that you have come to Jerusalem;
Tunapaswa tufanye nini? Bila shaka watasikia kwamba wewe umekuja.
23 so do this which we now tell you. We have four men here who have a vow resting on them.
Hivyo fanya kile sisi tunachokuambia sasa: tunao watu wanne ambao wameweka nadhiri.
24 Associate with these men and purify yourself with them, and pay their expenses so that they can shave their heads. Then everybody will know that there is no truth in these stories about you, but that in your own actions you yourself scrupulously obey the Law.
Wachukue watu hawa na ujitakase mwenyewe pamoja nao, na uwalipie gharama zao, ili waweze kunyoa vichwa vyao. Hivyo kila mmoja apate kujua kwamba mambo waliyoambiwa kuhusu wewe ni ya uongo. Watajifunza kwamba wewe pia unafuata sheria.
25 But as for the Gentiles who have accepted the faith, we have communicated to them our decision that they are carefully to abstain from anything sacrificed to an idol, from blood, from what is strangled, and from fornication."
Lakini kwa habari za mataifa ambao wamekuwa waumini, tuliandika na kutoa maagizo kwamba wanapaswa kujiepusha na vitu vilivyotolewa dhabihu kwa sanamu, na damu, kutokana na kile kilichonyongwa, na wajiepushe na uasherati.”
26 So Paul associated with the men; and the next day, having purified himself with them, he went into the Temple, giving every one to understand that the days of their purification were finished, and there he remained until the sacrifice for each of them was offered.
Ndipo, Paulo aliwatwaa wanaume, na siku ya pili, akajitakasa mwenyewe pamoja nao, akaingia Hekaluni, kutangaza kipindi cha siku za kujitakasa, hadi sadaka itolewa kwa ajili ya kila mmoja wao.
27 But, when the seven days were nearly over, the Jews from the province of Asia, having seen Paul in the Temple, set about rousing the fury of all the people against him.
Siku hizo saba zilipokaribia kumalizika, baadhi ya Wayahudi kutoka Asia wakamuona Paulo Hekaluni, na makutano wakakasirika, na wakamnyoshea mikono.
28 They laid hands on him, crying out, "Men of Israel, help! help! This is the man who goes everywhere preaching to everybody against the Jewish people and the Law and this place. And besides, he has even brought Gentiles into the Temple and has desecrated this holy place."
Walikuwa wanapiga kelele, “Watu wa Israeli, tusaidieni. Huyu ni yule mtu anayewafundisha watu kila mahali mambo ambayo ni kinyume na watu, sheria, na mahali hapa. Pia amewaleta Wayunani katika Hekalu na kupanajisi mahali hapa patakatifu.”
29 (For they had previously seen Trophimus the Ephesian with him in the city, and imagined that Paul had brought him into the Temple.)
Kwa kuwa mwanzoni walikuwa wamemwona Trofimo Muefeso akiwa pamoja naye mjini, nao walidhani kwamba Paulo alimleta hekaluni.
30 The excitement spread through the whole city, and the people rushed in crowds to the Temple, and there laid hold of Paul and began to drag him out; and the Temple gates were immediately closed.
Mji wote ulikuwa na taharuki, na watu wakakimbia pamoja na kumkamata Paulo. Wakamtoa nje ya Hekalu, na milango mara ikafungwa.
31 But while they were trying to kill Paul, word was taken up to the Tribune in command of the battalion, that all Jerusalem was in a ferment.
Walipokuwa wakijaribu kumuua, habari zilimfikia mkuu wa jeshi la walinzi kuwa Yerusalemu yote ilikuwa imejaa ghasia.
32 He instantly sent for a few soldiers and their officers, and came down among the people with all speed. At the sight of the Tribune and the troops they ceased beating Paul.
Mara hiyo akawachukua askari na jemadari akaukimbilia umati. Wakati Watu walipomwona mkuu wa jeshi na askari, wakaacha kumpiga Paulo.
33 Then the Tribune, making his way to him, arrested him, and, having ordered him to be secured with two chains, proceeded to ask who he was and what he had been doing.
Kisha mkuu wa jeshi alimkaribia na akamshika Paulo, na akaamuru afungwe minyororo miwili. Akamuuliza yeye ni nani na amefanya nini.
34 Some of the crowd shouted one accusation against Paul and some another, until, as the uproar made it impossible for the truth to be ascertained with certainty, the Tribune ordered him to be brought into the barracks.
Baadhi ya watu kwenye umati walikuwa wanapayuka kitu hiki na wengine kingine. Kwa kuwa jemadari hakuweza kuwaambia chochote kwa sababu ya zile kelele, akaamuru Paulo aletwe ndani ya ngome.
35 When Paul was going up the steps, he had to be carried by the soldiers because of the violence of the mob;
Basi alipofika kwenye ngazi, akachukuliwa na askari kwa sababu ya ghasia za umati.
36 for the whole mass of the people pressed on in the rear, shouting, "Away with him!"
Maana umati wa watu walimfuata na waliendelea kupiga kelele, “Mwondoeni huyu!”
37 When he was about to be taken into the barracks, Paul said to the Tribune, "May I speak to you?" "Do you know Greek?" the Tribune asked.
Paulo alipokuwa analetwa ndani ya ngome, alimwambia mkuu wa jeshi, “Naweza kukwambia kitu?” Yule mkuu wa jeshi akasema, “Je unaongea Kiyunani?
38 "Are you not the Egyptian who some years ago excited the riot of the 4,000 cut-throats, and led them out into the Desert?"
Je, wewe si yule Mmisri ambaye awali aliongoza uasi na alichukua magaidi elfu nne nyikani?”
39 "I am a Jew," replied Paul, "belonging to Tarsus in Cilicia, and am a citizen of no unimportant city. Give me leave, I pray you, to speak to the people."
Paulo akasema, “Mimi ni Myahudi, kutoka mji wa Tarso ya Kilikia. Mimi ni raia wa mji maarufu. Nawaomba, mniruhusu nizungumze na watu.”
40 So with his permission Paul stood on the steps and motioned with his hand to the people to be quiet; and when there was perfect silence he addressed them in Hebrew.
Wakati jemadari alipompa ruhusa, Paulo akasimama penye ngazi na akatoa ishara kwa watu kwa mkono wake. Wakati kulipokuwa na ukimya sana, akaongea nao kwa Kihebrania. Akasema,