< 2 Peter 2 >

1 But there were also false prophets among the people, as there will be teachers of falsehood among you also, who will cunningly introduce fatal divisions, disowning even the Sovereign Lord who has redeemed them, and bringing on themselves swift destruction.
Palitokea manabii wa uongo kati ya watu, na vivyo hivyo walimu wa uongo watatokea kati yenu. Watu hao wataingiza mafundisho maharibifu na kumkana Bwana aliyewakomboa, na kwa njia hiyo watasababisha ghafla maangamizi yao wenyewe.
2 And in their immoral ways they will have many eager disciples, through whom religion will be brought into disrepute.
Tena watu wengi watazifuata hizo njia zao mbaya, kwa sababu yao, wengine wataipuuza Njia ya ukweli.
3 Thirsting for riches, they will trade on you with their canting talk. From of old their judgement has been working itself out, and their destruction has not been slumbering.
Kwa tamaa yao mbaya watajipatia faida kwa kuwaambieni hadithi za uongo. Lakini kwa muda mrefu sasa Hakimu wao yu tayari, na Mwangamizi wao yu macho!
4 For God did not spare angels when they had sinned, but hurling them down to Tartarus consigned them to caves of darkness, keeping them in readiness for judgement. (Tartaroō g5020)
Malaika walipotenda dhambi, Mungu hakuwahurumia, bali aliwatupa katika moto wa Jehanamu ambako wamefungwa wakingojea Siku ile ya Hukumu. (Tartaroō g5020)
5 And He did not spare the ancient world, although He preserved Noah, a herald of righteousness, with seven others, when He brought a deluge on the world of the ungodly.
Mungu hakuihurumia dunia ya hapo kale, bali alileta gharika kuu juu ya nchi ile ya watu wasiomcha Mungu; lakini Noa ambaye alihubiri uadilifu, Mungu alimwokoa pamoja na watu wengine saba.
6 He reduced to ashes the cities of Sodom and Gomorrah, and condemned them to overthrow, making them an example to people who might in future be living godless lives.
Mungu aliadhibu miji ya Sodoma na Gomora, akaiteketeza kwa moto, akaifanya iwe mfano wa mambo yatakayowapata watu wasiomcha Mungu.
7 But when righteous Lot was sore distressed by the gross misconduct of immoral men He rescued him.
Alimwokoa Loti, mtu mwema, ambaye alisikitishwa sana na mwenendo mbaya wa watu hao waasi.
8 (For their lawless deeds were torture, day after day, to the pure soul of that righteous man--all that he saw and heard whilst living in their midst.)
Loti aliishi miongoni mwa watu hao, na kwa siku nyingi moyo wake ulikuwa katika wasiwasi mkuu aliposikia matendo yao maovu.
9 Since all this is so, the Lord knows how to rescue godly men from temptation, and on the other hand how to keep the unrighteous under punishment in readiness for the Day of Judgement,
Kwa hiyo, basi, Bwana anajua jinsi ya kuwaokoa katika majaribu watu wanaomcha Mungu, na jinsi ya kuwaweka waovu katika adhabu hadi Siku ile ya hukumu,
10 and especially those who are abandoned to sensuality--craving, as they do, for polluted things, and scorning control. Fool-hardy and self-willed, they do not tremble when speaking evil of glorious beings;
hasa wale wanaofuata tamaa mbaya za mwili na kupuuza mamlaka. Watu hao ni washupavu na wenye majivuno, huvitukana na hawaviheshimu viumbe vitukufu vya juu.
11 while angels, though greater than they in might and power, do not bring any insulting accusation against such in the presence of the Lord.
Lakini malaika, ambao wana uwezo na nguvu zaidi kuliko hao walimu wa uongo, hawawashtaki na kuwatukana hao mbele ya Bwana.
12 But these men, like brute beasts, created (with their natural instincts) only to be captured or destroyed, are abusive in matters of which they are ignorant, and in their corruption will perish,
Watu hao ambao hutukana chochote kile wasichoelewa, ni sawa na wanyama wasio na akili, ambao huzaliwa na baadaye hukamatwa na kuchinjwa! Wataangamizwa kutokana na uharibifu wao wenyewe,
13 being doomed to receive a requital for their guilt. They reckon it pleasure to feast daintily in broad daylight. They are spots and blemishes, while feeding luxuriously at their love-feasts, and banqueting with you.
na watalipwa mateso kwa mateso ambayo wameyasababisha. Furaha yao ni kufanya, tena mchana kabisa, chochote kinachotosheleza anasa zao za mwili. Hao ni fedheha na aibu tupu kwa jumuiya yenu wakati wanapojiunga nanyi katika karamu zenu, bali wakifurahia njia zao za udanganyifu.
14 Their very eyes are full of adultery--being eyes which never cease from sin. These men set traps to catch unstedfast souls, their own hearts being well trained in greed. They are fore-doomed to God's curse!
Macho yao yamejaa uzinzi na uwezo wao wa kutenda dhambi hauna kikomo. Huwaongoza watu walio dhaifu mpaka mitegoni. Mioyo yao imezoea kuwa na tamaa ya mali. Wapo chini ya laana ya Mungu!
15 Forsaking the straight road, they have gone astray, having eagerly followed in the steps of Balaam, the son of Beor, who was bent on securing the wages of unrighteousness.
Wameiacha njia iliyonyoka, wakapotoka na kuifuata njia aliyofuata Balaamu, mwana wa Beori, ambaye alipendelea kupata faida kwa kufanya udanganyifu,
16 But he was rebuked for his transgression: a dumb ass spoke with a human voice and checked the madness of the Prophet.
akakaripiwa kwa ajili ya uovu wake. Punda ambaye hasemi alinena kwa sauti ya binadamu, akaukomesha wazimu wa huyo nabii.
17 These people are wells without water, mists driven along by a storm, men for whom the dense darkness has been reserved.
Watu hao ni kama chemchemi zilizokauka, kama mawingu yanayopeperushwa na tufani; makao yao waliyowekewa ni mahali pa giza kuu.
18 For, while they pour out their frivolous and arrogant talk, they use earthly cravings--every kind of immorality--as a bait to entrap men who are just escaping from the influence of those who live in error.
Husema maneno ya majivuno na yasiyo na maana, na kutumia tamaa zao mbaya za kimwili kuwatega wale ambao wamejitenga hivi karibuni na watu waishio katika udanganyifu.
19 And they promise them freedom, although they are themselves the slaves of what is corrupt. For a man is the slave of any one by whom he has been worsted in fight.
Huwaahidi watu wengine eti watakuwa huru, kumbe wao wenyewe ni watumwa wa upotovu—maana mtu ni mtumwa wa chochote kile kinachomtawala.
20 For if, after escaping from the pollutions of the world through a full knowledge of our Lord and Saviour Jesus Christ, people are once more entangled in these pollutions and are overcome, their last state has become worse than their first.
Watu waliokwisha ponyoka katika upotovu wa ulimwengu kwa kupata kumjua Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo, kisha wakakubali kunaswa na kutawaliwa tena na upotovu huo, hali yao itakuwa mbaya zaidi kuliko awali.
21 For it would have been better for them not to have fully known the way of righteousness, than, after knowing it, to turn back from the holy commandments in which they were instructed.
Ingalikuwa afadhali kwao kama wasingalijua kamwe njia hiyo ya uadilifu kuliko kujua na kisha kuiacha na kupoteza amri takatifu waliyopokea.
22 Their case is that described in the true proverb, "A dog returns to what he has vomited," and also in the other proverb, "The sow has washed itself and now goes back to roll in its filth."
Ipo mithali isemayo: “Mbwa huyarudia matapishi yake mwenyewe,” na nyingine isemayo: “Nguruwe aliyekwisha oshwa hugaagaa tena katika matope!” Ndivyo ilivyo kwao sasa.

< 2 Peter 2 >