< Psalms 96 >

1 O sing to the LORD a new song: sing to the LORD, all the earth.
Mwimbieni Bwana wimbo mpya; mwimbieni Bwana dunia yote.
2 Sing to the LORD, bless his name; show forth his salvation from day to day.
Mwimbieni Bwana, lisifuni jina lake; tangazeni wokovu wake siku baada ya siku.
3 Declare his glory among the heathen, his wonders among all people.
Tangazeni utukufu wake katikati ya mataifa, matendo yake ya ajabu miongoni mwa mataifa yote.
4 For the LORD [is] great, and greatly to be praised: he [is] to be feared above all gods.
Kwa kuwa Bwana ni mkuu mwenye kustahili kusifiwa kuliko wote; yeye ni wa kuogopwa kuliko miungu yote.
5 For all the gods of the nations [are] idols: but the LORD made the heavens.
Kwa maana miungu yote ya mataifa ni sanamu, lakini Bwana aliziumba mbingu.
6 Honor and majesty [are] before him: strength and beauty [are] in his sanctuary.
Fahari na enzi viko mbele yake; nguvu na utukufu vimo patakatifu pake.
7 Give to the LORD, O ye kindreds of the people, give to the LORD glory and strength.
Mpeni Bwana, enyi jamaa za mataifa, mpeni Bwana utukufu na nguvu.
8 Give to the LORD the glory [due to] his name: bring an offering, and come into his courts.
Mpeni Bwana utukufu unaostahili jina lake; leteni sadaka na mje katika nyua zake.
9 O worship the LORD in the beauty of holiness: fear before him, all the earth.
Mwabuduni Bwana katika uzuri wa utakatifu wake; dunia yote na itetemeke mbele zake.
10 Say among the heathen [that] the LORD reigneth: the world also shall be established that it shall not be moved: he will judge the people righteously.
Katikati ya mataifa semeni, “Bwana anatawala.” Ulimwengu ameuweka imara, hauwezi kusogezwa; atawahukumu watu kwa uadilifu.
11 Let the heavens rejoice, and let the earth be glad; let the sea roar, and the fullness of it.
Mbingu na zishangilie, nchi na ifurahi; bahari na ivume, na vyote vilivyomo ndani yake;
12 Let the field be joyful, and all that [is] in it: then shall all the trees of the wood rejoice before the LORD:
mashamba na yashangilie, pamoja na vyote vilivyomo ndani yake. Kisha miti yote ya msituni itaimba kwa furaha;
13 For he cometh, for he cometh to judge the earth: he will judge the world with righteousness, and the people with his truth.
itaimba mbele za Bwana kwa maana anakuja, anakuja kuihukumu dunia. Ataihukumu dunia kwa haki, na mataifa katika kweli yake.

< Psalms 96 >