< Psalms 71 >

1 In thee, O LORD, do I put my trust: let me never be put to confusion.
Ee Bwana, nimekukimbilia wewe, usiache nikaaibika kamwe.
2 Deliver me in thy righteousness, and cause me to escape: incline thy ear to me, and save me.
Kwa haki yako uniponye na kuniokoa, unitegee sikio lako uniokoe.
3 Be thou my strong habitation, to which I may continually resort: thou hast given commandment to save me; for thou [art] my rock and my fortress.
Uwe kwangu mwamba wa kimbilio, mahali nitakapokimbilia kila wakati; toa amri ya kuniokoa, kwa kuwa wewe ni mwamba wangu na ngome yangu.
4 Deliver me, O my God, from the hand of the wicked, from the hand of the unrighteous and cruel man.
Ee Mungu wangu uniokoe kutoka kwenye mkono wa mwovu, kutoka kwenye makucha ya watu wabaya na wakatili.
5 For thou [art] my hope, O LORD God: [thou art] my trust from my youth.
Kwa kuwa umekuwa tumaini langu, Ee Bwana Mwenyezi, tegemeo langu tangu ujana wangu.
6 By thee have I been sustained from my birth: thou art he that brought me into life: my praise [shall be] continually of thee.
Tangu kuzaliwa nimekutegemea wewe, ulinitoa tumboni mwa mama yangu. Nitakusifu wewe daima.
7 I am as a wonder to many; but thou [art] my strong refuge.
Nimekuwa kama kioja kwa wengi, lakini wewe ni kimbilio langu imara.
8 Let my mouth be filled [with] thy praise [and with] thy honor all the day.
Kinywa changu kimejazwa sifa zako, nikitangaza utukufu wako mchana kutwa.
9 Cast me not off in the time of old age; forsake me not when my strength faileth.
Usinitupe wakati wa uzee, wala usiniache nguvu zangu zinapopungua.
10 For my enemies speak against me; and they that lay wait for my soul take counsel together,
Kwa maana adui zangu wananisengenya, wale wanaonivizia kuniua wafanya hila.
11 Saying, God hath forsaken him: persecute and take him; for [there is] none to deliver [him].
Wanasema, “Mungu amemwacha, mkimbilieni mkamkamate, kwani hakuna wa kumwokoa.”
12 O God, be not far from me: O my God, make haste for my help.
Ee Mungu, usiwe mbali nami, njoo haraka kunisaidia, Ee Mungu wangu.
13 Let them be confounded [and] consumed that are adversaries to my soul; let them be covered [with] reproach and dishonor that seek my hurt.
Washtaki wangu na waangamie kwa aibu, wale wanaotaka kunidhuru na wafunikwe kwa dharau na fedheha.
14 But I will hope continually, and will yet praise thee more and more.
Lakini mimi, nitatumaini siku zote, nitakusifu zaidi na zaidi.
15 My mouth shall show forth thy righteousness [and] thy salvation all the day; for I know not the numbers [thereof].
Kinywa changu kitasimulia haki yako, wokovu wako mchana kutwa, ingawa sifahamu kipimo chake.
16 I will go in the strength of the Lord GOD: I will make mention of thy righteousness, [even] of thine only.
Ee Bwana Mwenyezi, nitakuja na kutangaza matendo yako makuu, nitatangaza haki yako, yako peke yako.
17 O God, thou hast taught me from my youth: and hitherto have I declared thy wondrous works.
Ee Mungu, umenifundisha tangu ujana wangu, hadi leo ninatangaza matendo yako ya ajabu.
18 Now also when I am old and gray-headed, O God, forsake me not; until I have shown thy strength to [this] generation, [and] thy power to every one [that] is to come.
Ee Mungu, usiniache, hata niwapo mzee wa mvi, mpaka nitangaze uwezo wako kwa kizazi kijacho, nguvu zako kwa wote watakaokuja baadaye.
19 Thy righteousness also, O God, [is] very high, who hast done great things: O God, who [is] like to thee!
Ee Mungu, haki yako imefika juu katika mbingu, wewe ambaye umefanya mambo makuu. Ee Mungu, ni nani aliye kama wewe?
20 [Thou], who hast shown me great and severe troubles, wilt revive me again, and wilt bring me again from the depths of the earth.
Ingawa umenifanya nipate taabu, nyingi na chungu, utanihuisha tena, kutoka vilindi vya dunia utaniinua tena.
21 Thou wilt increase my greatness, and comfort me on every side.
Utaongeza heshima yangu na kunifariji tena.
22 I will also praise thee with the psaltery, [even] thy truth, O my God: to thee will I sing with the harp, O thou Holy One of Israel.
Ee Mungu wangu, nitakusifu kwa kinubi kwa ajili ya uaminifu wako; Ee Uliye Mtakatifu wa Israeli, nitakuimbia sifa kwa zeze.
23 My lips shall greatly rejoice when I sing to thee; and my soul, which thou hast redeemed.
Midomo yangu itapaza sauti kwa furaha ninapokuimbia sifa, mimi, ambaye umenikomboa.
24 My tongue also shall talk of thy righteousness all the day long: for they are confounded, for they are brought to shame, that seek my hurt.
Ulimi wangu utasimulia matendo yako ya haki mchana kutwa, kwa maana wale waliotaka kunidhuru, wameaibishwa na kufadhaishwa.

< Psalms 71 >