< Psalms 63 >

1 A Psalm of David, when he was in the wilderness of Judah. O God, thou [art] my God; early will I seek thee: my soul thirsteth for thee, my flesh longeth for thee in a dry and thirsty land, where no water is;
Mungu, wewe ni Mungu wangu! Ninakutafuta wewe kwa bidii, moyo wangu unakiu yako, mwili wangu unakutamani sana wewe, katika ukame na nchi iliyochoka mahali ambapo hakuna maji.
2 To see thy power and thy glory, so [as] I have seen thee in the sanctuary.
Hivyo nimekutafuta wewe katika watu watakatifu kuona nguvu zako na utukufu wako.
3 Because thy loving-kindness [is] better than life, my lips shall praise thee.
Kwa sababu uaminifu wa agano lako ni bora kuliko uhai, midomo yangu itakusifu wewe.
4 Thus will I bless thee while I live: I will lift up my hands in thy name.
Hivyo nitakutukuza wewe niwapo hai; kwa jina lako nitainua mikono yangu juu.
5 My soul shall be satisfied as [with] marrow and fatness; and my mouth shall praise [thee] with joyful lips:
Itakuwa kana kwamba nilikula mlo wa mafuta na wenye kunona, kwa midomo ya furaha kinywa changu kitakusifu wewe,
6 When I remember thee upon my bed, [and] meditate on thee in the [night] watches.
nikufikiripo kitandani mwangu na kukutafakari wewe wakati wa saa za usiku.
7 Because thou hast been my help, therefore in the shadow of thy wings will I rejoice.
Kwa maana umekuwa msaada wangu, na katika uvuli wa mbawa zako ninafurahia.
8 My soul followeth hard after thee: thy right hand upholdeth me.
Ninashikamana nawe; mkono wako wa kuume unanisaidia.
9 But those [that] seek my soul to destroy [it], shall go into the lower parts of the earth.
Lakini wale watafutao kuuharibu uhai wangu wataenda chini kwenye sehemu ya chini kabisa ya nchi;
10 They shall fall by the sword: they shall be a portion for foxes.
watakabidhiwa kwa wale ambao mikono yao hutumia upanga, nao watakuwa chakula cha mbweha.
11 But the king shall rejoice in God; every one that sweareth by him shall glory: but the mouth of them that speak lies shall be stopped.
Bali mfalme atashangilia katika Mungu; yeyote anaye apa kupitia yeye atajivunia yeye, lakini vinywa ya wale wasemao uongo watanyamazishwa.

< Psalms 63 >